Kauli ya Chongolo ni ufedhuli kwa wasomi wa vyuo vikuu. Ipingwe!

Kauli ya Chongolo ni ufedhuli kwa wasomi wa vyuo vikuu. Ipingwe!

Chongolo amewataka wasomi wa vyuo vikuu kwenda veta ili wakapate uwezo wa kujiajiri.

Kauli hii inatoa tafsiri hasi nyingi sana dhidi ya wasomi wa vyuo vikuu na vyuo vikuu vyenyewe.

Mosi, inatoa tafsiri kwamba elimu ya vyuo vikuu ni dhaifu ukilinganisha na ile ya veta. Kama hivi ndivyo. Je, malengo ya utoaji wa elimu ya vyuo vikuu yamefikiwa? Ikiwa bado hayajafikiwa ni nani wa kulaumiwa, kama siyo CCM na wanaccm?

Pili, inatoa tafsiri kwamba waliohitimu veta wana uwezo wa kujiajiri kuliko waliohitimu vyuo vikuul. Binafsi naona kuwa haya ni madhara ya kusema kabla ya kufanya utafiti. Huku mitaani tunaona watu wengi waliojiri ni wale ambao hawajaenda veta wala vyuo vikuu.

Sasa Chongolo atuambie hawa waliupata wapi uwezo huu? Je, ni shule ya msingi? Kama ndivyo atoe kauli nyingine.

Natoa wito kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vyote nchini kuandaa maandamano kupinga kauli hii inayotweza na kuidhalilisha elimu ya daraja la juu kabisa duniani. Mkikaa kimya CCM haikawii kuwafanya muonekane kama wahitimu wa darasa la saba.

Yaani Chongolo anawafanya ninyi wasomi wenye madigrii kuwa ni mbumbumbu kuliko kijana wa darasa la nne aliyehitimu ufundi uashi?

MSIKUBALI!
Isomi wako usio na Tija una manufaa gani Kwako na jamii zaidi ya kuwa mzigo?
 
Unaweza kutaja japo nchi moja tu duniani iliyojitosheleza kiajira kwa raia wake wote?.
Wana private sectors, na foreign investors.
Tatizo la CCM wamerundika makodi mpaka makampuni ya nje yanaogopa kuja kuinvest hapa.
 
Isomi wako usio na Tija una manufaa gani Kwako na jamii zaidi ya kuwa mzigo?
Kwanini wameweka vyuo vikuu kama wataproduce wasomi wasio na tija?
Hapa wa kuilaumu ni CCM, CCM wamefanya makosa alaf wanataka wananchi wasolve makosa ambayo wao hawakuyafanya.
 
Kwanini wameweka vyuo vikuu kama wataproduce wasomi wasio na tija?
Hapa wa kuilaumu ni CCM, CCM wamefanya makosa alaf wanataka wananchi wasolve makosa ambayo wao hawakuyafanya.
Ccm ndio Huwa inafundisha watu huko vyuoni? Kwanza ni kazi ya mhitumu kuonesha Tija ya Elimu yake
 
Tunaongozwa na Serikali ya watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri, wangetumia akili, wasingeweka vyuo vikuu, wangebadilisha mfumo wa elimu wakaweka VETA kama sehemu ya kupitia baada ya secondary level of education.
1677908334970.jpg
 
Wewe uliyesomea MAENDELEO YA JAMII,nje ya kuajiriwa unaweza kujiajiri kufanya kipi?.
Kwani unadhani wanaotoa ushauri kuhusiana na unyanyasaji wa kijinsia pamoja na kusaidia jamii namna bora ya kfungua na kuanzisha miradi ya kujikwamua kama vile kuanzisha vikundi, namna ya kupata mikopo kwa ajili ya makundi, kuandika andiko ili waweze kusajiliwa, kuandika katiba pamoja na kujisajili.

kazi ni nyingi sana...sema mnajua kazi za ki ufundi.
 
Mjumbe anatapika halafu anayala tena. Chongolo kasema nenda VETA jifunze umekanika ujiajiri. Wewe una BSc Mechanical Engineering unajisikia vibaya kuambiwa kwenda VETA? Ni kwa sababu digrii yako ni feki. Mtu mwenye digrii ya kweli ya umekanika hawezi kwenda VETA vile yote yaliyoko VETA anayajua. Shida ni kiburi kuwa ni msomi na kutojituma. Kuna imani potofu kuwa Jamii inatakiwa ikupe kazi. Serkali haina ajira zaidi ya watumishi wake wachache, haina gereji, shamba, nini kinakufanya udhani kuwa inawajibika kukuajiri? Vijana wapuuzi wanadanganywa na CHADEMA kuitukana CCM mbowe kasema tatizo ni tumehuru. Si nendeni kutafuta tumehuru iwape ajira kwenye gereji ya tume?
Mkuu siyo kwamba ni yeye hataki tu kufanya bali ni hajui kabisa kutenda.Mimi nimefanya kazi na wahandisi wa umeme miaka ya 2000 huko,yaani muhandi hajua jinsi ya kubadili ballistic chock katika tubelight flame!?.
Mwengini alishindwa kupima ufanisi wa three phase earthing katika project yake.Baada ya kangaika kwa muda mrefu bila mafanikio,ndiyo akaelekezwa kuja katika ofisi yetu ili kumpa msaada.
Kifipu mambo bado ni magumu kwa wasome wetu.
 
Veta Kuna Kozi nyingi.
Kwani.

Kwani kuendesha basi la Mwendo Kasi unaweza kuipata chuo kikuu.?

Kuendesha mitambo kule migodini, kuendesha madumper na exavetor,ni kazi zenye maslahi mazuri kuliko kukaa na Cheti Cha digrii bila ujuzi Wowote ZAIDI ya theories tu na kukariri hotuba za watu mashuhuri tu. Umejaza kichwani hotuba na falsafa za Pilato ambazo hazina Mchango Wowote kwenye uzalishaji unapokosa Ajira.

Veta Kuna Kozi nyingi ambazo msomi Wa chuo Kikuu angeweza kuzipata angeweza kuajiri watu wengine kutokana na KUWA na Upeo Mkubwa ZAIDI .
Mfano ufundi Wa kuchomelea mageti na kutengeneza vitanda n.k . Ni Ajira KUBWA sana na imeajiri watu wengi tatizo unafanywa Kienyeji sana ,uchochoroni, hakuna ofisi za maana n.k lakini wasomi wangeteka fani hizo zinagekua na ushindani na kuua vitu dhaifu kutoka nje.

Hivi unategemea viatu kutoka itali vinatengenezwa na watu wasio na Elimu kubwa ?
Wasomi ni wakati Sasa wa kujiajiri bila kuchagua kazi.

Nenda Moshi Kuna madereva na makondakta Wana digrii. Hata ukiwaangalia wanavyojiheshimu utaona tofauti na wengine. Wana Bima ya Afya ,NSSF ,free lunch n.k. Madereva Wengi Sasa Wana miliki fuso zao. Wasomi wanaona kusafrisha abiria au mizigo Kwa Ndege au Meli ni jambo la hadhi sana kuliko magari lakini vyote ni vyombo vya usafririshaji. Mmoja ameitwa rubani ,Mwingine Dereva ,Mwingine nahodha au captain .

Wasomi wengi wa vyuo vikuu vya Tanzania wanataka pesa za haraka haraka ndio maana wengi wamekimbilia kwenye bodaboda.
Wasomi wengi wa vyuo vikuu vya Tanzania wanataka pesa za haraka haraka ndio maana wengi wamekimbilia kwenye bodaboda.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Yaani na bachelor yake akaanze kusoma tena kupiga rangi sijui kuunganisha umeme?

Halafu hata hizo kazi za ufundi zenyewe zitawasaidia hao vijana kupata hela ya kula tu hakuna la maana watafanya.

Nachukia sana watu wanaorahisisha vitu wakati mfumo wa elimu wametengeneza wao. Like seriously, uanze tena kusoma kuunganisha mabomba?

Halafu hivi yeye amewahi kujiajiri hata kidogo, kama hajui kujiajiri ni moja ya kazi ngumu sana, yaani anakuwa na maisha ambayo uncertainly hana tofauti na "deiwaka" ukiamka mpaka mtu awaze kuja kwako kupata huduma.
Mkuu!Ndiyo endelea kusugua gaga huku ukiwa umekaa kwa dadako, ukila ugali alotafuta shemeji yako fundi bomba![emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mkuu!Ndiyo endelea kusugua gaga huku ukiwa umekaa kwa dadako, ukila ugali alotafuta shemeji yako fundi bomba![emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
naona fundi bomba imekugusa sana. Ahahahaah pole mkuu sitakudharau sababu hiyo ni kazi halali.
 
Umeshaoma matangazo ya Utumishi kuhusina na walimu wa kwenda kufundisha VETA?
Mkuu Veta wana masomo ambayo haya husu ufundi kama English,Entrepreneurship,Computer,Life skills Engineering Science,TD haya husiani na ufundi walimu wa secondary wanaundisha..Lakini mwalimu wa ufundi lazima awe fundi ana ujua ufundi na wana chuo chao pale Morogoro la sivyo Veta wangezalisha mafundi wa ajabu..
 
Mtoa mada nahisi uelewa wako ni mdogo na unapenda kukurupuka.Punguza mhemko na papara.Bandiko lako lote limekosa mantiki.

Kupata ajira kwa miaka ya hivi karibuni imekuwa changamoto karibu dunia nzima!!!!!!!!!!Kwa utamaduni wa elimu yetu humuandaa mwanafunzi kuajiriwa, kwamba ukimaliza masomo yako utakutana na ajira!!!!!!!!!! Hizi zama zimepita na hazitarudi tena!!!!!!!!!!!

Ajira zimekuwa ngumu lakini shughuli za kufanya ziko nyingi!!!!!!!!!!!!!!! Huko vyuo vikuu asilimia kubwa ya mafunzo hasa wanaochukua masomo ya sanaa na hata sayansi hakuna ujuzi wa mikono unaofundishwa zaidi ya kukariri vitini!!!!!!!!!!!!!

Huyu mhitimu akitoka huko hatakuwa na uwezo mkubwa wa kujishughulisha na shughuli mbalimbali ambazo nyingi hutumia ujuzi wa mikono!!!!!!!!!!!

Veta kuna mafunzo mbalimbali ya muda mfupi sana na muda mrefu ambayo kwa kiasi kikubwa hutumia ujuzi wa mikono ambao haupatikani kwa wanafunzi wengi huko vyuoni. Mfano wa mafunzo hayo ni:

Masonry & Bricklaying (MB)

Carpentry & Joinery (CJ)

Road Construction & Maintenance (RCM)

Civil Draughting (CD)

Painting & Sign writing (PS)

Welding & Fabrication (WF)

Fitter Mechanics (FM)

Meat Processing Technology (MPT)

Electronics (ELEC)

Motor Vehicle Mechanics (MVM)

Electrical Installation (EL)

Food Production (FP)

Food & Beverage Services & Sales (FBSS)

Front Office Operations (FO)

Plumbing & Pipe fitting (PPF).

Ukipata haya mafunzo ambayo huchukua muda mfupi utakuwa na uwanda mpana wa kujishughulisha wakati unasubiria muujiza wa ajira!!!!!!!!!!!

Nb 1: Zama zimebadilika. Tujifunze kubadilika!!!!!!!!!

Nb 2: Maarifa ya darasani hutumika kidogo sana mtaani!!!!!!!!!!!!!!

Nb 3: Mtaa una kanuni, sheria na taratibu zake ambazo hutafundishwa chuoni!!!!!!!!!!


Ni mtazamo!!!!!!!!!!!!!!!!
Thread closed
 
Chongolo amewataka wasomi wa vyuo vikuu kwenda veta ili wakapate uwezo wa kujiajiri.

Kauli hii inatoa tafsiri hasi nyingi sana dhidi ya wasomi wa vyuo vikuu na vyuo vikuu vyenyewe.

Mosi, inatoa tafsiri kwamba elimu ya vyuo vikuu ni dhaifu ukilinganisha na ile ya veta. Kama hivi ndivyo. Je, malengo ya utoaji wa elimu ya vyuo vikuu yamefikiwa? Ikiwa bado hayajafikiwa ni nani wa kulaumiwa, kama siyo CCM na wanaccm?

Pili, inatoa tafsiri kwamba waliohitimu veta wana uwezo wa kujiajiri kuliko waliohitimu vyuo vikuul. Binafsi naona kuwa haya ni madhara ya kusema kabla ya kufanya utafiti. Huku mitaani tunaona watu wengi waliojiri ni wale ambao hawajaenda veta wala vyuo vikuu.

Sasa Chongolo atuambie hawa waliupata wapi uwezo huu? Je, ni shule ya msingi? Kama ndivyo atoe kauli nyingine.

Natoa wito kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vyote nchini kuandaa maandamano kupinga kauli hii inayotweza na kuidhalilisha elimu ya daraja la juu kabisa duniani. Mkikaa kimya CCM haikawii kuwafanya muonekane kama wahitimu wa darasa la saba.

Yaani Chongolo anawafanya ninyi wasomi wenye madigrii kuwa ni mbumbumbu kuliko kijana wa darasa la nne aliyehitimu ufundi uashi?

MSIKUBALI!
Ndiyo. Elimu ya Chuo.Kikuu ni dhaifu dhidhi ya elimu ya VETA na vyuo vya NACTE.
 
Wana private sectors, na foreign investors.
Tatizo la CCM wamerundika makodi mpaka makampuni ya nje yanaogopa kuja kuinvest hapa.
PRIVATE SECTORS ina anzishwa na nani?.Ujui kuwa hizo PRIVATE SECTORS zinabuniwa na kuanzishwa na raia wenyewe?.
 
Wana private sectors, na foreign investors.
Tatizo la CCM wamerundika makodi mpaka makampuni ya nje yanaogopa kuja kuinvest hapa.
Msomi ndiyo ulipaswa utengeneze PRIVATE SECTOR ndani ya nchi na nje ya nchi,lakini eti wewe unawaza watu waje toka nje ya nchi ndiyo wa anzishe PRIVATE SECTOR ndiyo wewe uajiriwe!.Aisee!Hii ni aibu kwa msomi kuwa na mawazo ya aina hii.
 
Back
Top Bottom