Kauli ya Chongolo ni ufedhuli kwa wasomi wa vyuo vikuu. Ipingwe!

Kauli ya Chongolo ni ufedhuli kwa wasomi wa vyuo vikuu. Ipingwe!

Elimu haina Mwisho.
Chongolo kaongea fact tupu.
Vijana wengi wanaotoka vyuoni wanajua white collar jobs, Wakati vijana wengi wanaotoka Veta ndiyo washika spana, ndiyo wanaojua kushika chepe, nyundo, grisi, kunyoosha ukuta, kurepair simu, computer etc.

Kiufupi vijana wengi wanaotoka vyuoni wana matheory mengi kichwani ambayo hata hayo nayo wanayasahau wakishagraduate, Ila vijana wa Veta wana skills za kufanya vitu vitokee

Siku hizi elimu inadharaulika kuliko maelezo kisa ajira. Wapo wengi tu wanaelimu ya chuo kikuu wamejiajiri na wengine wameajiriwa, tusidanganyane kwa mifano midogo, wakati serikali ndio chanzo Cha yote haya.
 
Weka ushabiki wa kivyama pembeni, utaona mantiki halisi ya aliyoysema Katibu Mkuu huyo.

Kuwa na digrii si hoja, hoja ni kuwa na uwezo wa kujiajiri.

Mtu mwenye ujuzi wake toka Veta wa kuunganisha mabomba ya maji taka, na mtu aliye na digrii ya political sayansi ni yupi aliye na urahisi wa kujiajiri mwenyewe?

Na itanoga zaidi, kama huyu msomi wa political sayansi akawa na ujuzi wa kutengeneza vitu na kuitumia kwa upana zaidi hiyo digrii yake, badala ya kukaa nayo tu akiilea huku akiwa tegemezi kwa wengine.

Digrii kwa siku hizi siyo nyenzo tena ya kupatia kazi.
Nimewatungia kitabu cha ujasiriamali cha kimombo ambacho unakisoma unaweka kwapani na kuanza kufanya biashara kwa mafaniko changamoto itakuwa mazingira ya kufanyaji bisahara yamedumazwa kila mtu anapambana kivyake
 
Mimi ningeshauri serikali kwa vile vyuo vyetu vingi havina sehemu za kufanyia tafiti (research centers) basi watu waliokaa kwenye kazi (field) kwa muda mrefu sana ndo warusishwe vyuoni wakafundishe siyo mtu amebakishwa tutorial..within 5years tayari ni lecture kisa amechukua masters na phd tayari. mfano. Akina Kibatara and likes wakatoe elimu ya sheria huko chuo kikuu..

Wale wataalam wanaotengeneza mitambo ya gesi pale kinyerezi na waotengeneza and the likes wakafundishe chuo kikuu.

Wale wahasibu wabobezi warudi wakafundishe.
Wale wataalam wa mabarabara na ujenzi walioko kwenye field muda mrefu wakafundishe.

Wale miners wabobezi kule GGM na Nyamongo warudishwe wakafundishe...

Tuachaneni na Hao wahadhiri ambao vichwa vyao vimeota kutu na hawafanyi vitu kwa vitendo kwasababu hawaoni vitu katika uhalisia...tuchukue watu waliopo kwenye field. Haiwezekani mwanafunzi amemaliza chuo lakini akipewa mtihani kwa vitendo anaonekana kichekesho..

Please, kwani hao wanaotengeneza gesi walifundishwa wapi Kama sio vyuoni? Acheni kushusha elimu ya chuo kikuu.
 
Chongolo nae fala tu. Hajui anachokisema huwezi kumwambia mtu mwenye degree ya uhasibu au manunuzi ajiajiri. Serikali iweke mpango madhubuti kusaidia watakaokosa ajira mana mfumo unaotumika kuajir watu utatoa watakaokosa kila mwaka mpaka dunia iishe. Aache ufala wake na yeye kama hajui cha kuongea asiongee
Huu ni kuonyesha uduni wa upeo ulionao kuhusu mambo haya.

Ndiyo maana unatumia maneno ya kipumbavu kujibu hoja usiyo na uwezo wa kuijibu.

Kwa hiyo wewe hapo unaona "uhasibu au ununuzi" ni fani za kipekee sana kwamba walio na digrii hizo hawawezi kufanya kazi nyingine nje ya kuajiriwa?

Hii inaonyesha hata kama una digrii katika maeneo hayo hiyo digrii haikukusaidia kitu chochote. Hujawahi kuona wahitimu wa eneo hilo waliojiajiri badala ya kuajiriwa?

Halafu unajipachika u-'Sir' kuonyesha ujinga mkubwa unaokusumbua.
 
Yaani watanzania tuna Shida, watu wanadhani Chongolo amekosea lakini mimi sioni jipya huko vyuo vikuu haswa Kwa baadhi ya kozi maana ziko ki nadharia tu Wala hazina mchango wa maana . Mtu aliyeenda Veta ni Bora zaidi kuliko KWENDA ELIMU ya juu haswa Tanzania
Siyo Tanzania pekee mkuu, ni dunia nzima.
Huko nchi zilizoendelea kuwa na digrii hakumfanyi mtu awe wa kipekee kuliko wengine..
 
Unataka mtu aliyesoma Political science, Medicine, au Accounting akafanye kazi za fundi bomba au fundi ujenzi?
Kama hakuna ajira kwenye maeneo ya alikosomea, 'why not'?

Hivi watu mbona hizi digrii mnaziona kuwa za ajabu sana? Kuwa na digrii yoyote, maana yake ni kumpa uwezo zaidi aliyo nayo, ili kuweza kutatua matatizo yake kwa kutumia elimu hiyo aliyonayo, hata katika maeneo mengine yasiyohusika na digrii yake.

Ulaya tumeona watu wakiendesha taxi na digrii zao. Hapa kwetu bado ni kasumba tu ndiyo imajaa vichwani.

Lakini nikuulize. Ni kipi cha maana zaidi, kuwa na digrii halafu huna kazi, au unayo digrii na unao ujuzi nje ya digrii yako unaokuwezesha kuendesha maisha yako?

Hapa si swala la kuwa na digrii, bali ni swala la kuwa na ajira, iwe ni yako mwenyewe kwa kujiajiri au uwe umeajiriwa.

Daktari, Mhasibu au mwenye digrii nyine yoyote kama hana ajira kwenye fani yake, na wala hakuna uwezo wa kufungua ofisi yake katika eneo hilo analolijua na kujiajiri, lakini eneo la fundi bomba au ujenzi kuna kazi kuajiriwa au kujiajiri, kwa nini asiifanye, kwa vile tu kasomea udaktari au uhasibu?
 
Mtoa mada nahisi uelewa wako ni mdogo na unapenda kukurupuka.Punguza mhemko na papara.Bandiko lako lote limekosa mantiki.

Kupata ajira kwa miaka ya hivi karibuni imekuwa changamoto karibu dunia nzima!!!!!!!!!!Kwa utamaduni wa elimu yetu humuandaa mwanafunzi kuajiriwa, kwamba ukimaliza masomo yako utakutana na ajira!!!!!!!!!! Hizi zama zimepita na hazitarudi tena!!!!!!!!!!!

Ajira zimekuwa ngumu lakini shughuli za kufanya ziko nyingi!!!!!!!!!!!!!!! Huko vyuo vikuu asilimia kubwa ya mafunzo hasa wanaochukua masomo ya sanaa na hata sayansi hakuna ujuzi wa mikono unaofundishwa zaidi ya kukariri vitini!!!!!!!!!!!!!

Huyu mhitimu akitoka huko hatakuwa na uwezo mkubwa wa kujishughulisha na shughuli mbalimbali ambazo nyingi hutumia ujuzi wa mikono!!!!!!!!!!!

Veta kuna mafunzo mbalimbali ya muda mfupi sana na muda mrefu ambayo kwa kiasi kikubwa hutumia ujuzi wa mikono ambao haupatikani kwa wanafunzi wengi huko vyuoni. Mfano wa mafunzo hayo ni:

Masonry & Bricklaying (MB)

Carpentry & Joinery (CJ)

Road Construction & Maintenance (RCM)

Civil Draughting (CD)

Painting & Sign writing (PS)

Welding & Fabrication (WF)

Fitter Mechanics (FM)

Meat Processing Technology (MPT)

Electronics (ELEC)

Motor Vehicle Mechanics (MVM)

Electrical Installation (EL)

Food Production (FP)

Food & Beverage Services & Sales (FBSS)

Front Office Operations (FO)

Plumbing & Pipe fitting (PPF).

Ukipata haya mafunzo ambayo huchukua muda mfupi utakuwa na uwanda mpana wa kujishughulisha wakati unasubiria muujiza wa ajira!!!!!!!!!!!

Nb 1: Zama zimebadilika. Tujifunze kubadilika!!!!!!!!!

Nb 2: Maarifa ya darasani hutumika kidogo sana mtaani!!!!!!!!!!!!!!

Nb 3: Mtaa una kanuni, sheria na taratibu zake ambazo hutafundishwa chuoni!!!!!!!!!!

Ni mtazamo!!!!!!!!!!!!!!!!
Huko kote ni mwendo wa "What is the........"

Hakuna vitendo
 
Kwahiyo Chongolo anataka vijana wote wa vyuo vikuu wawe mafundi mchundo ??

Muwe mnaangalia mantiki ya hoja iliyotolewa kwanza kabla ya kukimbilia kuunga mkono hoja mfu.

Daniel Chongolo anapowaambia vijana wa vyuo vikuu waende veta wawe na uwezo wa kujiajiri maana yake elimu yao ya chuo kikuu haina maana yoyote isipokuwa elimu ya veta na kwamba chuo kikuu wamepoteza muda wao bure.

Kuna la maana hapo ??
Ni wapi aliposema "Anataka vijana wote wa vyuo vikuu wawe mafundi mchundo"
Maneno hayo pekee yanakufanya uonekane kutokuwa mtu makini katika kufikiri kwako

Hiyo 'mantiki' ya hoja uliyoiona wewe ni ipi hasa, mbona ni kama unajisemea tu maneno bila ya kujua maana yake ni nini?

Mkuu 'DEJAN7, sijui kama kweli nawe unayo digrii katika eneo lolote, na kama unayo, na umeajiriwa kutokana na hiyo digrii, basi hizi digrii hazina maana tena.
 
Wewe ndio unapotosha. Tofautisha employment opportunities na academic opportunities. Huwezi kumdhihaki mtu aliyesoma political science kisa hawezi kujiajiri, unatakiwa kujiuliza aliposoma political science alikuwa na lengo la kujiajiri au kuajiriwa?. Kama kuajiriwa achana naye. Huwezi kucheka academic opportunities kwa sababu ya employment opportunity ya plumbing.
Sasa kama wewe uko huko na ki-digrii chako ka 'political science, lakini huna ajira, utamvimbia nani? Si mwisho wa siku utamtegemea huyo fundi wa Veta akulishe?
Hizi digrii watu bado mnayo kasumba ya ajabu sana juu yake.

Sawa, pata digrii yako, kama inakuwezesha kupata ajira hakuna atakayekuuliza.
Lakini huku unayo digrii, unailea tu miaka minne au zaidi huna kazi, unatembea nayo tu digrii yako mitaani. Hiyo digrii inakusaidia kitu gani?
Kwa nini upoteze muda wako wote huo, ambao ujuzi wa Veta ungekuwezesha kujifanyia shughuli zako mwenyewe na hata kupanua wigo wako wa akili kutazama fursa zaidi ya hiyo inayokuwezesha kuishi kwa heshima.
 
Hao VETA wanafundishwa na wahitimu wa vyuo vikuu, sasa sijui unongea Nini. Tatizo mnashabikia kauli za wanasiasa bila kufanya utafiti.
Tatizo haujenda shule unaongea mambo ya mitaani, pia haujawahi kuajiriwa viwandani ambako ungeona kama kuna mhitimu wa chuo kikuu anayeshika spana na nyundo.
 
Sina uhakika kama unaelewa hata maana ya private "sector" ni nini, Maana naona hapa unaongelea mtu akaanzishe private sector!
What is the Private Sector?

The private sector is the part of the economy that is run by individuals and companies for profit and is not state controlled.

Types of Private Sector Businesses

The private sector is a very diverse sector and makes up a big part of many economies. It is based on many different individuals, partnerships, and groups.

Kati ya mimi na wewe sijui ni nani sasa hajui maana.[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hao watu wanahusika katika kuandaa na kushauri kuhusu miradi mbali mbali, kwahiyo, watu wa fani hiyo wanaweza kujiajiri kwa njia hiyo ya kutoa ushauri.
[emoji23][emoji23][emoji23] Kwa hiyo wanaweza kuandaa maandiko ya miradi na kuwauzia watu siyo!?.
 
Huu ni kuonyesha uduni wa upeo ulionao kuhusu mambo haya.

Ndiyo maana unatumia maneno ya kipumbavu kujibu hoja usiyo na uwezo wa kuijibu.

Kwa hiyo wewe hapo unaona "uhasibu au ununuzi" ni fani za kipekee sana kwamba walio na digrii hizo hawawezi kufanya kazi nyingine nje ya kuajiriwa?

Hii inaonyesha hata kama una digrii katika maeneo hayo hiyo digrii haikukusaidia kitu chochote. Hujawahi kuona wahitimu wa eneo hilo waliojiajiri badala ya kuajiriwa?

Halafu unajipachika u-'Sir' kuonyesha ujinga mkubwa unaokusumbua.
Oke twende taratib Kwa hoja. Tatizo la ajira ni tatizo la jamii au la mtu binafsi?
 
Back
Top Bottom