Kauli za jeuri na dharau za viongozi wetu kwa wananchi ni matokeo ya Katiba yetu mbovu

Kauli za jeuri na dharau za viongozi wetu kwa wananchi ni matokeo ya Katiba yetu mbovu

Kuendelea kumlaumu Nyerere asiyekuwepo haisaidii kitu, muhimu ni kuchukua hatua za kuimarisha hiyo demokrasia mnayoitaka.

Hatua gani unataka zichukuliwe? Unaona vyama vya upinzani vinasambaratishwa, uchaguzi unavurugwa mchana kweupee, ukiatandamana wanakupa vilema halafu wewe unasema tuimarishe demokrasia. Kazi kweli.
 
Hatua gani unataka zichukuliwe? Unaona vyama vya upinzani vinasambaratishwa, uchaguzi unavurugwa mchana kweupee, ukiatandamana wanakupa vilema halafu wewe unasema tuimarishe demokrasia. Kazi kweli.
Tatizo huo mzigo wa kupigania demokrasia wameachiwa wapinzani pekee, raia wengine wapo bize wanatafuta maisha.
 
Kupaza sauti za kudai demokrasia pale inapokiukwa kwa makusudi.

Wapaze sauti wapi? Wakiingia barabarani kuandamana wanapigwa. Hao wapinzani wanavurugwa mpaka wanakimbia nchi. Hakuna demokrasia kwa sababu Nyerere aliikataa.
 
Kuhoji idadi ya safari ni uzwazwa, anaenda kufanya nini nje na matokeo ya safari hizo je tunayaona?
Hakuna dharau ama lugha mbaya ametumia ila katumia lugha ile ile mtumiayo ikija kwenye kumsema kuhusu safari, mkuki kwa nguruwe kwa binadamu.................
Wananchi wamepokwa madaraka yao ndiyo maana anakuwa na uthubutu wa kutoa majibu ya karaha kiasi hicho.

Yaani wenye nchi (wananchi) wanataka apunguze safari za nje halafu jibu lake linakuwa mkaa??
 
Wananchi wamepokwa madaraka yao ndiyo maana anakuwa na uthubutu wa kutoa majibu ya karaha kiasi hicho.

Yaani wenye nchi (wananchi) wanataka apunguze safari za nje halafu jibu lake linakuwa mkaa??
Wamepokwa vipi wakati yupo kwa mujibu wa sheria pale alipo?
Na wewe ama wananchi wenzio,nini kinawaumiza ama kinakwama akitoka?
 
Na wewe ama wananchi wenzio,nini kinawaumiza ama kinakwama akitoka?
Hujui? Ama kweli watanzania walio wengi ni wajinga. Rais anaposafiri kwenda nje ya nchi mamilioni ya shiling yanatupotea kulipia nauli na posho. Fedha hizi zingeweza kufanyia Jambo lingine kubwa lenye maslahi mapana kwa taifa.

Ndiyo maana tunataka rais apunguze idadi ya safari zake za kwenda nje ya nchi.
 
Back
Top Bottom