Kawe leo hii kuanzia Saa 1 hadi Saa 3 Usiku kulitokea nini hadi MP wa JWTZ Kufurika, Kukamata Watu, Kutembeza Kichapo na Kuzua taharuki?

Kawe leo hii kuanzia Saa 1 hadi Saa 3 Usiku kulitokea nini hadi MP wa JWTZ Kufurika, Kukamata Watu, Kutembeza Kichapo na Kuzua taharuki?

Mbona watu wengine ni washamba sana? Wanafanya kazi bure? Si ni kazi waliyoichagua na wanalipwa? Hujui kuna mgawanyo wa kazi? Unajua watu wanaokulisha wewe? Unajua watu wanaokutibu? Unajua watu wanaosafisha takataka? Una maana kwa vile mtu analinda ndiyo apige raia bila kufuata sheria?
Majitu majinga sana ,na hii mada ndio inapima akili ya Watanzania walio wengi ,sijui ni mtindio wa akili ?
 
Soma CPA kasome defensive factors ambazo zinaweza kukulinda usiwe liable.Utaelewa.
Zipo kwenye PENAL CODE hizo (zinazotumika hapa)
Kuna defense of Provocation and Self defense and if this successful pleaded it would help to exonerate an accused person from murder to manslaughter or it might acquit him
 
Definitely, na amepata anachostahili. Hata kama wenzake wakifanya fujo kuanzia kawe mpaka bagamoyo bado hawawezi kurudisha uhai wa mwenzao, Point blank!


Kunguru muhoga anaishi miaka mingi
Hivi Mtu ukila mshahara wako na Familia yako na ku-play low key utapungukiwa Nini

Uku Tz Mtu akiwa mwanajeshi basi anaamini yeye anajua kila kitu na anaweza mpiga raia

Kuna siku nimeona jamaa wanampiga dereva wa daladala viboko vya usoni na wakampasua jicho akiwa amekaa katika usikani wake nilihisi uchungu Sana maana jamaa hakuweza kuendelea na safari tena huku jamaa aliyempiga aliendelea kula jogging as if he did the right thing.

Ebu waza kuhusu Familia ya yule dereva ?
So nadhani tusipojitambua na kuamini sisi ni Bora na wengine sio bora litatukuta Jambo

Pia na kuwa na Elimu ndogo bila personal growth hiyo nayo inachangia ushamba wa vyeo , kutafuta attention , social proof lazima utaishia kuimuza famlia yako

We need to fuckky our Ego
 
Wewe utakuwa ni mmoja wao. Unatetea ujinga. Mimi nashauri busara itumike
Sasa hapo nani katiwa adabu?
Acheni ufala wenu. Ninyi ni watu kama sisi na hamna uwezo huo mnaojidai nao tukiwa mmoja mmoja.
Mimi labda mje wengi. Nikiwa peke yangu nawe uko mwenyewe ntakupasua ukigusa mwili wangu. Huwezi kunionea kijinga jinga. Pelekeni ubabe wenu huko kwa wake zenu.
Na kwa wake zao wasipeleke ubabe maana watalishwa sumu waishe familia zikose wababa. 😆😆😆

Kikubwa ubabe wao wasubiri kibiti panuke waupeleke huko 😅
 
Mzee ukicheka na nyani siku zote utavuna mabua ukiwachekea waliofanya tukio matukio hayatoisha nishakutana na muuza chips mmoja anatamba kwamba yeye haogopi mwanajeshi mwanajeshi akimletea anampoteza na usisahau wale wana taratibu zao hawajafanya bila kufuata utaratibu, raia mnawadharau sana na kuwachukulia poa ndio maana wanatia adabu
Huyu wa kwenye stori ametumia utaratibu upi?

Wanajeshi wana kero sana
Shule flani palikuwa na huyo mwanajeshi, tulikuwa tunamuogopa.
Alikuwa hatufundishi, ila anakuja class. Anajisikia tu kukwambia usimame ucheze kiduku.. sasa kataa uone.
 
Unaeleza ujinga tu,namna ya mwanajeshi kuendelea kumlinda mwananchi,yaani kutimiza majukumu yake,mwananchi anapaswa alipe kodi ili pesa zipatikane za kumlipa huyo(mwanajeshi),ili atimize majukumu yake kwa uweledi.Katika majukumu yake,kupiga raia siyo jukumu lake,na kama siyo jukumu lake,raia anatakiwa ajilinde dhidi ya huyo askari ambaye amelishwa na raia,akagharamiwa mavazi,mafunzo na mpaka malazi na raia.Raia hatakiwi kutwndewa ndivyo sivyo,ilhali anatakiwa alindwe ili afanye kazi mfano za kuendesha bajaji,bodaboda,ualimu n.k ili pesa ya kodi ipatikane,ambayo itaenda kwa mwanajeshi kama posho na mshahara.
 
Inasemekana ( kwa aliyenipa Taarifa Kamili kuwa ) Dereva Bajaji jana Usiku katika Baa Moja maarufu iliyo kwa ndani ( Mafichoni kidogo ) mkabala na Petro Station ya PUMA Kawe alipishana Kauli na Mwanajeshi ( tena Mkubwa wa Cheo cha Kanali ) kuhusu Kuzibiana njia ya kupita.

Ambapo Afande Kanali alikuwa Kapaki Gari lake lililokuwa limezuia njia kwa mbele na Dogo ( Dereva Bajaji ) kuhoji kwanini Afande aliziba njia hali iliyomkwaza Afande ( wa Cheo cha Kanali Muro kama sijalikosea Jina lake ) ambapo Afande Kanali akatoka ndani ya Gari lake na Kumzaba Makofi Dereva Bajaji huyo.

Kisha nae ( Dereva Bajaji ) kwa Hasira akaamua kwenda kuchukua Bisibisi Bajajini Kwake na kuja Kumchoma nayo Afande Kanali upande wa Moyo hali iliyomfanya akimbizwe Lugalo Hospital kwa Matibabu na Umauti kumkuta huko huko Wodini.
Mama weee yan uyo dogo atateswaaa weee na atauawa bila kupelekwa popote na vyombo vingine vya usalama havutafanya lolote mind my words
 
Kwa hio wanajeshi wote unaowana ni sawa na kuanza kuwavimbia na kuwatukana unavyojisikia na kutaka kupimana nao nguvu si ndio?
Labda sisi wengine tunaoishi huku Nkome hatujui kinachoendelea huko Kawe, Kwani ni Kweli ninyi maaskari mkipita mnatukanwa tu na raia?

Binafsi sijawahi shuhudia askari anapita zake raia wakaanza kumtukana, nchi hii bado haijatokea acha kukuza mambo, na wala hatuwachukii maaskari wetu kama unavyojaribu kuaminisha umma hapa.
 
Kuna wanajeshi wawili walizoea kuendekeza ubabe kwenye baba moja Sinza. Kuna siku waliingia cha kike kwa black belt mmoja ambae kwa muonekano walidhani wanammudu.
Jamaa aliwanyoosha wote wawili halafu akaondoka zake mdogo mdogo hata hakimbii.
Wajeda kwa aibu wakainuana pale wakaita bajaji wakaondoka kwa aibu.
Dolphin bila shaka. Nakumbuka huo mkasa.
 
Inasemekana ( kwa aliyenipa Taarifa Kamili kuwa ) Dereva Bajaji jana Usiku katika Baa Moja maarufu iliyo kwa ndani ( Mafichoni kidogo ) mkabala na Petro Station ya PUMA Kawe alipishana Kauli na Mwanajeshi ( tena Mkubwa wa Cheo cha Kanali ) kuhusu Kuzibiana njia ya kupita.

Ambapo Afande Kanali alikuwa Kapaki Gari lake lililokuwa limezuia njia kwa mbele na Dogo ( Dereva Bajaji ) kuhoji kwanini Afande aliziba njia hali iliyomkwaza Afande ( wa Cheo cha Kanali Muro kama sijalikosea Jina lake ) ambapo Afande Kanali akatoka ndani ya Gari lake na Kumzaba Makofi Dereva Bajaji huyo.

Kisha nae ( Dereva Bajaji ) kwa Hasira akaamua kwenda kuchukua Bisibisi Bajajini Kwake na kuja Kumchoma nayo Afande Kanali upande wa Moyo hali iliyomfanya akimbizwe Lugalo Hospital kwa Matibabu na Umauti kumkuta huko huko Wodini.
Hapo unaweza kuta jamaa wa Bajaj alianza kuongea shit!
Unajua vijana wa bodaboda au Bajaj unaweza kuta anafosi kupita ukimkazia akikupita atakutukana au kukuonyeshea ishara ya kidole cha kati wengi sio wastaarabu.[emoji23]
Akikukwangua rangi anakimbia ila yeye ukimkwangua au kumpushi kidogo anakomaa umlipe tena varangati kubwa na watajaa hapo as if kuna tafrani kubwa wote wakimtetea mwenzao.
 
Kawe ni eneo lenye wahuni wengi kupindukia kusafisha na kuleta ustaarabu ni suala la LAZIMA.
Kawe uswahili kinoma kuanzia ukwamani mpaka maringo ukiingia kule ndani ndani kuna tisha, nyumba hazina mpangilio vichochoro sasa, vibaka wa kukata madirisha wako tele, watoto wasela wamama wasela wababa nao wasela pamoja na dada poa kibao wachafu wachafu, mitaro ya maji machafu sasa daah tabu tupu kule magonjwa ya mlipuko nje nje!

Wauza vitumbua, mamalishe wachafu wachafu na wauza samaki wa kukaanga vumbi kibao, kule wachawi watakuwa wengi sana, waganga wa kienyeji tele!

Wamama/wadada wasio na shughuli za kufanya wanaongoza kwa kukopa kausha damu [emoji23]
 
Kuna mwanajeshi mkubwa nimekutana nae asubuhi hii yupo very frustrated how come raia mnakua na uadui na wanajeshi wa Nchi yenu why muwadharau watu wanaowalinda why mnawaonyesha dharau kiasi cha kuanza kuwaua wakianza kujibu mapigo mtaanza kulialia maana hawashindwi Ila taratibu na kanuni zao zinawabana, sio fair hata kidogo kwanini usimsikilize hata km kablock njia na mmepishana kauli ndio uchukue maamuzi ya kumuua?
Acheni kuwajaza kichwa wajione wana jua sana .ni mapimbi tu hawa wenye elimu ndogo wengi wao na ubabe wa kijinga
 
Back
Top Bottom