Kazi ya udalali inalipa sana kiukweli siwezi kuiacha hii kazi

Manfried

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2024
Posts
1,288
Reaction score
4,074
Wakuu katika Kazi ambazo zinalipa ni pamoja na udalali.

Hii inakuhitaji uwe at least unajua kiingereza , mwandiko mzuri na kuwa na ushawishi wa kuongea vyema.

Kiufupi njia ambazo natumia kufanya hii biashara ni kuwa na smartphone nzuri , laptop kali .

Kisha naaanza kutangaza bidhaa mbalimbali .

Sasa wakati naanza hii Kazi sikutegemea kuwa itanipa pesa.

Mimi bidhaa ninazouza ni slow moving Ila siku nikitusua natusua kweli kweli.

Wiki iliingia simu ya Kazi , ghafla nikaambiwa nipokee na kufanya mazungumzo .

Sasa tayari nimeshapiga 6 Million

Hapa nilipo najua hii million sita ni mshahara wa mtu wa mwaka mzima .

Leo huko kijijini nimewapa jumla laki nane nimewanunulia gas na jiko lake.

Nimewavutia Maji.

Wakuu tuendelee kupambania
 
Dalali ni kupe dalali ni shetani dalali nawachukia Sanaa.

Sipendagi ma middle manπŸ‘ž

Yaan anagawana na mkulima 50% 50% inauma Sanaa

Nenda kwenye kuuza au kupangisha nyumba anataka Kodi ya mwezi Bure bureee 🧐

Wapuuzi Sana na muda wote wanatafuna tafuna Kama mbuzi...( Washirikina Sana)
 
Aaah
 
Sio inalipa mkuu usichokielewa ni kwamba ww u naona hujawekeza chochote na unatengeneza pesa ila kumbukuka kunamda inakushukua mda gan mpaka kumpata mteja naizitoshe unakuwa haupo pekeyako mfana laki nane unaweza mkakuta mpo sita au wanne na unachokisahau ni ule mda unaopoteza kumsubili mteja ipo siku utaugharamia mkuu kwa kujutia
 
Ni kazi moja ngumu sana inahitaji uwe na moyo wa chuma kufanya na ndio maana wengi wanaloga ili mambo yaende. Hebu fikiria mteja anakuja na hela alafu huyo anapotea mazima.
 
πŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“ŒThadi wadi a.k.a shithole country a.k.a Banana republic kila kitu kinajiendea hovyohovyo, ni huzuni!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…