Kelele zikiwa nyingi na kuwazomoea Bodi Kwa Maamuzi ya Kijinga, msije kushangaa Yanga anapewa Point 3 maana washaanza kuraruana tayar.

Kelele zikiwa nyingi na kuwazomoea Bodi Kwa Maamuzi ya Kijinga, msije kushangaa Yanga anapewa Point 3 maana washaanza kuraruana tayar.

Ameandika kujitetea tu hakuna kanuni rasmi ya utoaji taarifa hata pale alipopigiwa simu kuwa simba wapo getini na kwamba ni ndani ya muda wa kikanuni alipaswa kuruhusu waingie. Suala hili likiisha huyo naye kibarua chake kwisha.
Huyo ndo wa kumshikia bango sio yanga sasa.
 
kwani mazoezi kabla ya mechi wamepanga simba au kanuni za bodi ya ligi?.sasa kwanini useme sio sababu ya timu kususia mechi?.kwani mlipogoma nyie siku ile mlitumia kanuni gani kugoma?
Kwasababu kabla ya hapo mechi zilipigwa licha ya kukataliwa kufanya mazoezi kabla ya mechi..
Na timu mwenyeji kama ndio sababu basi anakula rungu na sio mchezo kuahirishwa, hiyo ni sababu nyepesi ila ni nzito ikifanywa na hivi vilabu viwili.
 
Kwasababu kabla ya hapo mechi zilipigwa licha ya kukataliwa kufanya mazoezi kabla ya mechi..
Na timu mwenyeji kama ndio sababu basi anakula rungu na sio mchezo kuahirishwa, hiyo ni sababu nyepesi ila ni nzito ikifanywa na hivi vilabu viwili.
unajua simba imeathirika kiasi gani kukatazwa kufanya mazoezi
 
Hapa ni haki ya simba ipatikane kama ni viongozi wa tff walifanya uzembe na uhuni wawajibishwe sasa kama kulikuwa na mkono wa yanga kupitia mabaunsa itajulikana.
Hamna haki hapo ni "busara" hilo zaga washalivagaa tff wenyewe hamna mwenye kosa sio simba wala yanga, wao ndo wana sababu zao za kuahirisha game
 
Hamna haki hapo ni "busara" hilo zaga washalivagaa tff wenyewe hamna mwenye kosa sio simba wala yanga, wao ndo wana sababu zao za kuahirisha game
Safari hii hakuna cha busara, busara hizi za huko nyuma ndizo zilizotugikisha ktk tukio hili, ikumbukwe kuwa 2021 Yanga hao walisababisha derby kuahirishwa kwa maksudi tu, hakufanywa kitu, bado ameendelea kuchezea kanuni maksudi kwa kupitia milango isiyotakiwa kwa imani za kishirikina akijua kuwa faini kiduchu atalipa, na hii ilikuwa mwendelezo.

Hivyo basi sasa tff itumie kanuni na siyo busara, itamke wazi aliyesababisha kosa hili ni nani na apewe adhabu ndipo simba tuendelee na ligi. Simba wanayo haki ya kugomea kama kuna sababu ya kikanuni inayokubalika kwa tff, caf na fifa.
 
Bodi ya Ligi ya Tanzania haina weledi huwa hawaendi eneo la tukio wanategeme meneja wa uwanja na kamishina wa mchezo yaani wako kama sanamu - figure heads

Kwakutegemea meneja wa uwanja na kamishina wa mchezo Ndiyo maana hawana uwezo wa kufanya maamuzi ndani ya saa moja

Bodi ya aina gani huwa haiendi eneo la tukio, (uwanjani)

TFF pia viongozi wake hawana elimu ya ujasiriamali wanaendesha shirikisho kama familia ama ndondo cup

Mashabiki pamoja na scouting wamepoteza pesa nyingi kwa huo mchezo

Wenye akili wataipeleka TFF mahakamani kwa hasara walizopata pamoja na matangazo
 
Usilete matusi Yako hapa,
Nimeamka nimepitia Mitandao yangu pendwa miwili X formerly known as Twitter na JF.

Nilichokiona hata waliokua wanatetea swala la Simba mapema Ile wamegeuka nao saiv wanailaumu Bodi.
Simba wana akili kuliko wote kwenye mpira huu, ila kwakuwa huko wenye akili wawili mnaona kila wakifanyacho simba wanakrupuka.

NARUDIA TENA

"" TAASISI YA SIMBA IMEKAMILIKA KILA IDARA, NA NI DUDE KUBWA MNOOOOO""


Subirini tuwapangie tarehe mje tuwakande fullstops
 
Safari hii hakuna cha busara, busara hizi za huko nyuma ndizo zilizotugikisha ktk tukio hili, ikumbukwe kuwa 2021 Yanga hao walisababisha derby kuahirishwa kwa maksudi tu, hakufanywa kitu, bado ameendelea kuchezea kanuni maksudi kwa kupitia milango isiyotakiwa kwa imani za kishirikina akijua kuwa faini kiduchu atalipa, na hii ilikuwa mwendelezo.

Hivyo basi sasa tff itumie kanuni na siyo busara, itamke wazi aliyesababisha kosa hili ni nani na apewe adhabu ndipo simba tuendelee na ligi. Simba wanayo haki ya kugomea kama kuna sababu ya kikanuni inayokubalika kwa tff, caf na fifa.
2021 sababu ilikua wazi mkuu, wala Yanga hawakua na kosa, fatilia vizuri.
 
Wewe
Maamuzi ya kuahirisha mpira wa jana ni kati ya maamuzi mabovu kuwahi kufanyika
Ni kwa kua sababu zilizokuwepo hazikuwa na uzito wa kutosha kuahirisha mpira

1. Kitendo cha Simba kupeleka team uwanjani bila taarifa jioni/usiku, kilitosha kabisa kuwazuia kwa sababu; uongozi wa Uwanja unatakiwa kuwa na taarifa ili kuweka mazingira sawa ikiwepo kuwa na walinzi, wafanyakazi nk kwa ajili ya kusimamia taratibu za uwanja.

2. Tusiaminishwe kuwa mashabiki wachache tu ndio wenye nguvu ya kufanya kazi ya ulinzi wa uwanja kuliko wafanyakazi/walinzi wa uwanja walio ajiriwa.....tukiamini hivyo kuna siku team zitazuiwa kwenda uwanjani ili team nyingine ipate point tatu....

3. Mimi bado naamini team ya SIMBA ILIZUILIWA na walinzi wa uwanja kwa kutokufuata taratibu (kwenda uwanjani jioni/usiku bila taarifa) hayo ya mashabiki wa Yanga yamejazilishiwa tu.....

Kimsingi sababu zilikuwa Nyepesi ukiangalia gharama za maandalizi na washabiki ambao wengi tu walisafiri kutoka mikoani na Nnje ya Nchi. Inamaana mechi za Yanga na simba wanaenda kuzipunguzia ushabiki (fedha) kwani hakuna mtu ataliipa hela yake kwenda dar wakati kwa sababu nyepesi nyepesi mechi inaweza kuaharishwa!
Wewe na mbwa na chagua MBWA
 
Kama Yanga watacheza basi tusitegemee hizi tabia za timu za kariakoo kususia mechi kama zitaisha.
Kila muwamba ngoma anavutia kwake, simba wanasema kosa la Yanga, Yanga kosa la simba, wengine kosa la tff.

Tegemea "busara" kuamua na game itapigwa tena.
 
Simba wameiogopa mechi wakala kona.
Kiwango Cha Sasa cha Yanga kinatisha hakuna namna zaidi ya Simba kutimua mbio, wangekula saba bila.

Msimamo wa ligi Yanga bado iko mbele point moja iwapo Simba itashinda kiporo chake na Jana wangefungwa na kuwepo gepu la points 4 na biashara ingeishia hapo maana Simba isingeikamata tena Yanga.

Kinachotakiwa ni TFF kukubali mziki wa Yanga na kuiacha ijichukulie ubingwa wake wa 4 kwa amani , maana tff wanahangaika sana kulazimisha Simba ibebe kombe na uwezo haina, marefa wanaharibu mechi za Simba na sasa ujinga umehamia kwao kuvunja kanuni ili kuibeba Simba mbovu.
 
Kama Yanga watacheza basi tusitegemee hizi tabia za timu za kariakoo kususia mechi kama zitaisha.
Kucheza watacheza watake wasitake hawana ubavu wa kukataa maana kosa hili limefanyika ktk unasaba wao na pengine waweza kukutwa na hatia kupitia mabaunsa wao waliowatuma fuatilia crips zao.
 
Nyie mnaosema simba hawans makosa,wamefanya maandalizi wiki nzima,meneja wa uwanja kuwakatalia wasiingie ndiyo sababu ya kukataa kucheza? Kwani uwanja hawaujui? Umebadilika? Azim dewji alishaanza kumlalamikia refa aliepangwa kwamba atawaonea,kwa kifupi simba walipanga kutokucheza mechi.
 
Tff kutwa nzims leo wanambembeleza gsm pale salamander ili yanga wacheze,lakini, za ndaaaani kabisa gsm kachomoa kabisa.
 
Kiwango Cha Sasa cha Yanga kinatisha hakuna namna zaidi ya Simba kutimua mbio, wangekula saba bila.

Msimamo wa ligi Yanga bado iko mbele point moja iwapo Simba itashinda kiporo chake na Jana wangefungwa na kuwepo gepu la points 4 na biashara ingeishia hapo maana Simba isingeikamata tena Yanga.

Kinachotakiwa ni TFF kukubali mziki wa Yanga na kuiacha ijichukulie ubingwa wake wa 4 kwa amani , maana tff wanahangaika sana kulazimisha Simba ibebe kombe na uwezo haina, marefa wanaharibu mechi za Simba na sasa ujinga umehamia kwao kuvunja kanuni ili kuibeba Simba mbovu.
Ni wazi kolo kala kona , walianza kugomea marefa, juzi wakafanya ambush uwanjani, wakaenda na waandishi wao kabisa si ajabu hata hao mabounsa ni wao.
 
Back
Top Bottom