Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
KENYA ABDALLAH HASSAN KATIBU MKUU WA KWANZA MUISLAM WIZARA YA ELIMU AMEFARIKI
Kenya Abdallah Hassan nimemfahamu toka utoto wangu Moshi katika miaka ya 1960.
Siku hizo mimi nikiwa shule ya msingi madarasa ya chini sana yeye alikuwa Mawenzi Secondary School.
Kenya alikwenda Makerere, Uganda nilikuja kujua baadae.
Kenya angefariki na mimi wala nisingenyanyua kalamu yangu kuandika chochote kuhusu yeye kama isingetokea mwaka wa 1987 jambo lililogusa Waislam wengi Tanzania.
Mwaka huo Prof. Kighoma Malima alichaguliwa na Rais Ali Hassan Mwinyi kuwa Waziri wa Elimu.
Hili lilikuwa halijapata kutokea.
Ilikuwa kama vile Rais Mwinyi amevunja mwiko alioweka Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere toka uhuru mwaka wa 1961kuwa nafasi hiyo haishikwi na Muislam.
Baada ya kuwa Waziri wa Elimu Prof. Malima Rais Mwinyi akamchagua Kenya Abdallah Hassan kuwa Katibu Mkuu katika Wizara hiyo.
Rais alikuwa kapiga msumari wa moto juu ya kidonda.
Wizara ilichafuka na wahariri wa magazeti wakawa wanachonga penseli zao ziandike vizuri.
Kuna watendaji ndani ya wizara waliona kama vile sasa bwawa limeingia luba itakuwa tabu kuogelea kwa raha na salama.
Yaliyotokea sasa ni historia.
Prof. Malima aliondolewa kwenye Wizara ya Elimu baada ya kujadiliwa Dodoma.
Hayo ndiyo yaliyofanya mimi hii leo nimkumbuke kaka yangu Kenya Hassan.
Mola amghufirie dhambi zake na amlipe Pepo ya Firdaus.
Amin.
Kenya Abdallah Hassan nimemfahamu toka utoto wangu Moshi katika miaka ya 1960.
Siku hizo mimi nikiwa shule ya msingi madarasa ya chini sana yeye alikuwa Mawenzi Secondary School.
Kenya alikwenda Makerere, Uganda nilikuja kujua baadae.
Kenya angefariki na mimi wala nisingenyanyua kalamu yangu kuandika chochote kuhusu yeye kama isingetokea mwaka wa 1987 jambo lililogusa Waislam wengi Tanzania.
Mwaka huo Prof. Kighoma Malima alichaguliwa na Rais Ali Hassan Mwinyi kuwa Waziri wa Elimu.
Hili lilikuwa halijapata kutokea.
Ilikuwa kama vile Rais Mwinyi amevunja mwiko alioweka Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere toka uhuru mwaka wa 1961kuwa nafasi hiyo haishikwi na Muislam.
Baada ya kuwa Waziri wa Elimu Prof. Malima Rais Mwinyi akamchagua Kenya Abdallah Hassan kuwa Katibu Mkuu katika Wizara hiyo.
Rais alikuwa kapiga msumari wa moto juu ya kidonda.
Wizara ilichafuka na wahariri wa magazeti wakawa wanachonga penseli zao ziandike vizuri.
Kuna watendaji ndani ya wizara waliona kama vile sasa bwawa limeingia luba itakuwa tabu kuogelea kwa raha na salama.
Yaliyotokea sasa ni historia.
Prof. Malima aliondolewa kwenye Wizara ya Elimu baada ya kujadiliwa Dodoma.
Hayo ndiyo yaliyofanya mimi hii leo nimkumbuke kaka yangu Kenya Hassan.
Mola amghufirie dhambi zake na amlipe Pepo ya Firdaus.
Amin.