Kero ya Walimu msingi kudai michango mingi; ni makubaliano ya kikao feki cha wazazi feki

Kero ya Walimu msingi kudai michango mingi; ni makubaliano ya kikao feki cha wazazi feki

Shule nyingi za msingi za serikali siku hizi zimejaa michango mingi sana ambayo inaleta matabaka kwa watoto!

Walimu wanachangisha hela ya mitihani kila siku 1000.
Ndoo mpya kila term,
Fagio jipya kila mwezi,

Hela ya safari (tour) kwa mgongo wa hiari huku nyuma wanawapiga mkwara watoto kwenda!

Vitabu vidogodogo wanalazimishwa kununua n.k

Hii tabia ukihoji wanasema ni makubaliano ya kikao cha wazazi lakini ajabu kila mzazi analalamika! Sasa hiko kikao huwa wanakalia wapi?

Mambo haya yameshamili sana na maafisa elimu wapo, wakurugenzi wapo, DC na RC wapo, mawaziri wapo, tamisemi wapo, Yaani ni kero mtupu lakini kiiimyaaa!

Walimu wanachukua mikopo halafu wanarudi kulalamika mshahara hautoshi wanasahau mikopo ya anasa ndo tatizo!

Ugumu wa maisha wao kutwa kuchangisha michango isiyo na kichwa wala miguu kila siku!
Kwanza tuition za kulipia za nini kwenye shule za serikali?
Badala ya kuja JF nenda office ya afisa elimu wa shule za msingi upeleke malalamiko yako
 
Badala ya kuja JF nenda office ya afisa elimu wa shule za msingi upeleke malalamiko yako
Asante kwa ushauri lakini nimewakilisha wazazi nchi nzima!
Yamkini naweza kuwa sina mtoto au wanangu wako inje au private!
Kwahiyo usimaindi chukua ujumbe tafakali!
Lisipokuhusu wewe linamhusu mwenzio, na humu kuna viongozi na wazazi
 
Asante kwa ushauri lakini nimewakilisha wazazi nchi nzima!
Yamkini naweza kuwa sina mtoto au wanangu wako inje au private!
Kwahiyo usimaindi chukua ujumbe tafakali!
Lisipokuhusu wewe linamhusu mwenzio, na humu kuna viongozi na wazazi
Shida ni kuwa hoja yako haiwezi kutatuliwa kwa malalamiko ya Jf.

Kwa nia njema kabisa mshauri mzazi /wazazi anayedaiwa michango aende ofisini, atasaidiwa tu. Maana michango imekatazwa isipokuwa kwa makubaliano ya wazazi na Kibali maalum.
Wasibaki wanalalamikiana wenyewe kwa wenyewe,

Maana hapo atakuwa specific, ni shule gani na wamedaiwa michango ya nini na nini.
 
Shida ni kuwa hoja yako haiwezi kutatuliwa kwa malalamiko ya Jf.

Kwa nia njema kabisa mshauri mzazi /wazazi anayedaiwa michango aende ofisini, atasaidiwa tu. Maana michango imekatazwa isipokuwa kwa makubaliano ya wazazi na Kibali maalum.
Wasibaki wanalalamikiana wenyewe kwa wenyewe,

Maana hapo atakuwa specific, ni shule gani na wamedaiwa michango ya nini na nini.
Wewee ni mgeni BONGO! Michango ni hiari huyo mzazi wa kushitaki anakuwa anamuwekea mazingira magumu mtoto!
na mtoto asipotoa hapewi kipaumbele, hata madawati yakipelea atakalishwa chini
 
Wewee ni mgeni BONGO! Michango ni hiari huyo mzazi wa kushitaki anakuwa anamuwekea mazingira magumu mtoto!
na mtoto asipotoa hapewi kipaumbele, hata madawati yakipelea atakalishwa chini
Hakuna kitu km hicho. Hivi wakienda wazazi km kumi kupeleka malalamiko kwa afisa elimi watoto wao wote watapata adhabu? Sio kweli
Na hakuna kiongozi atakayekwenda shule na kusema mzazi fulani kaleta malalamiko,

Wazazi wanalea uovu kwa kutofikisha hoja mahala husika. Serikali imeshatoa tamko na kurudia mara nyingi kukataza michango.
Mfano hao wahusika wa Elimu wakiona hii mada watachukua hatua gani na kwa nani? Watasoma watapita hivi.

Washauri wapeleke malalamiko ofisi husika.
 
Nimeitwa shuleni juzi, dogo anawasalimia waalimu za saaizi? , kijana yupo darasa la kwanza, ikabidi aitwe, nikamuuliza mbele ya Mwalimu wake wa darasa kwanini unawasalimia waalimu za saa izi? Anasema akiwasalimia Asallam Aleykum hawaitikii ndio akaamua awe anawasalimia za saaizi!. Dogo miyeyusho sana. Shule yenyewe ya Masister yeye anapeleka uarabu..
 
Well said mkuu,,
Hayo mambo yapo Sana kwenye hizi shule zetu za serikali.

Halafu ukiuliza wanasema wazazi walikaa na kupanga yote hayo.

Kumbe wazazi fake na vikao fake ..
Uwe unahudhuria vikao ili ujue kuwa ni mzazi feki au ni mzazi wa mtoto katika Shule hiyo. Ukihudhuria unaweza kuoneshwa mtoto wa mzazi husika, hapa jamii forums Kuna propaganda nyingi sana.
Kama mtoa hoja alikuwepo kwenye kikao, inawezekanaje kura zikawa asilimia 100%?, Na wakati yeye alipiga kura tofauti?
Kwa kulikomesha hilo wazazi halisi muhudhurie na kuwe na sehemu ya majina ya watoto wenu na madarasa yao wakati wa kusaini.
 
Hilo nilisikia juzi Waziri mkuu akilikemea shule za sekondari za umma kuchapa joining instruction zenye vifaa vingi sana zaidi ya 200k!

Mkuu nimefurahishwa na kichwa cha habari, lakini kwenye 'content' "umemumunya" maneno.

Kifupi michango ni ya gharama kubwa kuliko ada.

Halafu "vikao vya wazazi" nilishavihudhuria vina mamluki vipandikizi waliojipanga huwashindi hoja.

Hakuna cha wazazi hapo ni wazazi feki kama ulivyoandika kichwa chako cha habari.

Utashangaa hoja za rejareja za kijinga jinga zinazotolewa pale zinaungwa mkono 100%, wanakuwa wanejipanga haswa kwa manufaa binafsi.

Hakuna anayehoji matumizi ya hela ya shule inayoletwa mgao na serikali kwa elimu bila malipo na mchanganuo wake kuonesha zinafanya kazi gani.

Rim za karatasi pamoja na vikorombweso kibao ukiunga gharama zake vinazidi ada.

Marufuku ya michango iliyotolewa na serikali ya awamu ya 5 ingeliendelezwa kukomesha umumiani huu ulioibuka tena kama kweli serikali imeamua kulivalia njuga suala la kubeba gharama za kusomesha watoto.

"Mwenye kuguswa ama mkereketwa" apeleke mchango wake kwa Mkurugenzi kama ilivyokwisha kuagizwa, wanashindwa nini?

Hatukatai harambee za ujenzi wa madarasa kutokana na ongezeko la watoto lisilokuwa na kikomo, lakini double standard ya gharama zinazobebwa na serikali halafu wazazi wanageukiwa kuhamasishwa kuchangia gharama hizo hizo, tunasema hapana.
Kama mwanafunzi anaanza form one gharama huwa zinakuwa kubwa zaidi ya hiyo 200k, ila baada ya kujiunga gharama zinakuwa ndogo, nadhani hata vyuo ipo hivyo. Mwanzo huwa unakuwa mgumu.
 
Hakuna kitu km hicho. Hivi wakienda wazazi km kumi kupeleka malalamiko kwa afisa elimi watoto wao wote watapata adhabu? Sio kweli
Na hakuna kiongozi atakayekwenda shule na kusema mzazi fulani kaleta malalamiko,

Wazazi wanalea uovu kwa kutofikisha hoja mahala husika. Serikali imeshatoa tamko na kurudia mara nyingi kukataza michango.
Mfano hao wahusika wa Elimu wakiona hii mada watachukua hatua gani na kwa nani? Watasoma watapita hivi.

Washauri wapeleke malalamiko ofisi husika.
Wazazi kumi kupeleka malalamiko ni maandamano! Ni kinyume na sheria za nchi kuandamana!
Sheria haitaki watu zaidi ya watano kutembea pamoja au kukusanyika bila taarifa
 
Uwe unahudhuria vikao ili ujue kuwa ni mzazi feki au ni mzazi wa mtoto katika Shule hiyo. Ukihudhuria unaweza kuoneshwa mtoto wa mzazi husika, hapa jamii forums Kuna propaganda nyingi sana.
Kama mtoa hoja alikuwepo kwenye kikao, inawezekanaje kura zikawa asilimia 100%?, Na wakati yeye alipiga kura tofauti?
Kwa kulikomesha hilo wazazi halisi muhudhurie na kuwe na sehemu ya majina ya watoto wenu na madarasa yao wakati wa kusaini.
Hivyo vikao tangazo linabandikwa au kutolewa muda mchache kabla ya kikao! NAHISI HUIJUI BONGO VIZURI
 
Kama mwanafunzi anaanza form one gharama huwa zinakuwa kubwa zaidi ya hiyo 200k, ila baada ya kujiunga gharama zinakuwa ndogo, nadhani hata vyuo ipo hivyo. Mwanzo huwa unakuwa mgumu.
Hizo ni za shuleni tu?
Maana mzazi kumvisha mtoto mmoja kuanzia kiatu, mabegi madaftari ya couter books na mazagazaga kibao inazidi 200k.
 
Nimeitwa shuleni juzi, dogo anawasalimia waalimu za saaizi? , kijana yupo darasa la kwanza, ikabidi aitwe, nikamuuliza mbele ya Mwalimu wake wa darasa kwanini unawasalimia waalimu za saa izi? Anasema akiwasalimia Asallam Aleykum hawaitikii ndio akaamua awe anawasalimia za saaizi!. Dogo miyeyusho sana. Shule yenyewe ya Masister yeye anapeleka uarabu..
Mwanao ana vinasaba vya Alishabaab! Kuwa nae makini usicheke
 
Takukuru iingie sasa mpaka mashuleni ili kudhibiti hili mashuleni,waingizwe kama walimu tokea mkoa mwingine!
Walimu wanamchonganisha MH. Rais na wapiga kura.
 
Back
Top Bottom