Kero ya wananchi mbele ya Mkuu wa Mkoa Arusha ndugu Makonda

Kero ya wananchi mbele ya Mkuu wa Mkoa Arusha ndugu Makonda

Nimekuwa nikifuatilia wananchi wa Mkoa wa Arusha wakitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Makonda. Kwa asilimia kubwa lazima sheria zifuatwe na Mkuu wa Mkoa hayuko juu ya sheria. Inawezekana kero nyingi zilizotolewa tayari aidha ziko Mahakamani au uamuzi wa kisheria ulikwishapitiwa.

Mimi naona wananchi wengi wanapoteza muda wao na hawatasaidiwa chochote na Mkuu wa Mkoa ni vema wakafuata taratibu za kisheria. Hata yule Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha alioagiza ahamishwe, mimi naona siyo utawala bora kusema mbele ya watu kuwa ahamishwe.

Usitafute popularity ambayo haisaidii. Najua wananchi wana kero nyingi na wanaonewa lakini ni budi sheria zifuatwe kutatua kero hizo.
Huwezi kutatua shida kwa njia ya maonyesho kama wanavyofanya!
Kuna taasisi ilibidi ziwe zinashughulikia haya Mambo, Polisi, takukuru, mahakama,
Kama kila mkuu wa mkoa akiitisha mkutano kusikiliza kero za watu, tuna wakuu wa mikoa 26! Wananchi wapo milioni 60! Utaweza vipi kusikiliza kero zao? Ofisi zenu zina kazi gani?
 
Arusha Kuna kero nyingi kwasababu wakuu wa mikoa waliopita walikua vyama vya upinzani au walikua hawatoshi.
Mrisho anasemaje kuhusu hizo kero?
 
Nimekuwa nikifuatilia wananchi wa Mkoa wa Arusha wakitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Makonda. Kwa asilimia kubwa lazima sheria zifuatwe na Mkuu wa Mkoa hayuko juu ya sheria. Inawezekana kero nyingi zilizotolewa tayari aidha ziko Mahakamani au uamuzi wa kisheria ulikwishapitiwa.

Mimi naona wananchi wengi wanapoteza muda wao na hawatasaidiwa chochote na Mkuu wa Mkoa ni vema wakafuata taratibu za kisheria. Hata yule Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha alioagiza ahamishwe, mimi naona siyo utawala bora kusema mbele ya watu kuwa ahamishwe.

Usitafute popularity ambayo haisaidii. Najua wananchi wana kero nyingi na wanaonewa lakini ni budi sheria zifuatwe kutatua kero hizo.

Subiri mumeo apate shida ndo utaona msaada unavyokuwa. Sisi wanaume tunapambana na vita haichagui macho.
 
Inawezekanaje wamiliki 72 wa Law firms za Arusha wakiongozwa na wanasheria wa Tanganyika Law Society washiriki kwenye "jambo" mnalodai ni kuvunja sheria?

Inachekesha kwamba watu wanashindwa kutofautisha kwamba wale ambao kesi zao zipo mahakamani wanapewa msaada na ushauri wa kisheria. Wale ambao kero zao hazipo mahakamani wanasaidiwa kwa kuwawajibisha wanaokwamisha hizo haki kwa ukiritimba, rushwa, upendeleo na kutokujua wajibu wao.

Hao wanaopinga walete hata kero hata moja tu sheria za Nchi zimekiukwa au uhuru wa mahakama umeingiliwa.

Kama hawawezi just shut up na waachieni wenye kero wasaidiwe.
Wewe kama huna kero kaa kwa shemeji kwa raha mustarehe waache wenye kero wasaidiwe.

Wisdom is chasing you guys but you are always faster.
 
aisee nashangaa arusha ghafla nao wamegeuka wamekuwa kama watu wa kule katavi na tandahimba kulialia wakati wanaelewa sheria na utaratibu wa kupata haki,wanahangaika na mtu wakuwapotosha tu na kisha kuwaacha kwenye mataa ya mianzini
Hao Arusha sasa wote wamekuwa wadudu!
 
Nikichogundua kwa haraka haraka wewe unamchukia makonda, tena unamchukia bila sababu, nahii chuki umepandikizwa au umefata mkumbo.

Siku ukiwa na uwezo wa kumanage kile unacholishwa na mitandao na wanasiasa hutarudia kuandika ulichoandika hapa.
 
Ccm ni kenge kabisa,huwezi kutatua shida kwa njia ya maonyesho kama wanavyofanya!
Kuna taasisi ilibidi ziwe zinashughulikia haya Mambo, Polisi, takukuru, mahakama,
Kama kila mkuu wa, mkoa akiitisha mkutano kusikiliza kero za watu, tuna wakuu wa mikoa 26! Wananchi wapo milioni 60! Utaweza vipi kusikiliza kero zao? Ofc zenu zina kazi gani?
Nani kakuambia watu milioni 60 wote wana kero?
Swali la kijinga kabisa. Hizo ofisi nyingi ndio zimesababisha hizo kero kwa kuwanyima au kuwacheleweshea watu haki zao. Justice delayed is justice denied
Upofu wa kisiasa usikupofue ukapinga hata jambo zuri.
 
Nimekuwa nikifuatilia wananchi wa Mkoa wa Arusha wakitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Makonda. Kwa asilimia kubwa lazima sheria zifuatwe na Mkuu wa Mkoa hayuko juu ya sheria. Inawezekana kero nyingi zilizotolewa tayari aidha ziko Mahakamani au uamuzi wa kisheria ulikwishapitiwa.

Mimi naona wananchi wengi wanapoteza muda wao na hawatasaidiwa chochote na Mkuu wa Mkoa ni vema wakafuata taratibu za kisheria. Hata yule Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha alioagiza ahamishwe, mimi naona siyo utawala bora kusema mbele ya watu kuwa ahamishwe.

Usitafute popularity ambayo haisaidii. Najua wananchi wana kero nyingi na wanaonewa lakini ni budi sheria zifuatwe kutatua kero hizo.

Ulichokiandika ni hoja za kujibia mtihani ILA kiuhalisia mambo hayako hivyo huku nje...
Tunaposoma Vyuoni tunafundishwa taratibu ambazo zinatekelezeka kwa Nchi za ulimwengu wa Kwanza au niseme kwa Nchi ambayo watu wame Elimika kwa asilimia 85% na vyombo vyote vinatekeleza majukumu yake kwa wakati na kwa haki kwa asilia angalau 85%.
Huku kwetu wananchi wameelimika pengine kwa asilia kama 35%; Inamaana ulichokiandika, hakina uhalisia

Ukweli wananchi wanateseka na kama umefuatilia mikutano kwa lengo la kujifunza, utagundua kitu...
1. Yapo mengi tu yaliamuliwa kwa rushwa (fuatilia maamuzi ya mwanasheria waziri wa Ardhi)_
2. Yapo mengi tu yalisha amuliwa lakini hakuna utekelezaji
3. Wapo wengi wamenyimwa nafasi hata ya kukutana na watu wenye nafasi ya kuwasaidia
4. Zipo kesi zimeripotiwa ambapo matukio yalipuuzwa badala ya kufanyiwa upelelezi nk nk
LAKINI pia, tuache kulindana kwa kigezo cha kufuata utaratibu; kwani huyo mzembe alifuata utaratibu wa kuwanyima wananchi haki zao?

Natamani, anachokifanya mkuu wa mkoa wa Arusha Kifanyike Nchi Nzima ndipo Viongozi wa Juu wangejua madudu yaliyoko huku chini
Kinacho onekana kuna gap mahala****kuna watendaji hawatimizi majukumu yao vizuri; Ungeanzia hapo
 
.....wakati wanaelewa sheria na utaratibu wa kupata haki,
Tatizo ni kwamba wanaosimamia taasisi zote za kisheria(mahakimu, mawakili na polisi) wamegubikwa na ulaji wa rushwa uliopindukia.
Kwa mantiki hiyo, kupata haki kupitia hiyo mifumo kama Huna pesa ni nadra sana.

Wananchi wa kada ya chini wanataabika sana na hali hiyo ndio maana wakipata fursa kama hii hujitokeza kwa wingi.
 
Huko kwenye vyombo vya sheria kwenyewe kuna matatizo
Ukiona kama watu wanamkimbiliac Rc hata kama wee unaona maigizo,jua nchi ina shida na siyo ndogo

Ova
 
Siyo kuingilia Mahakama.
Ni kusubiri mchakato wa Sheria uishe halafu kukata rufaa kwa rais.
 
Nimekuwa nikifuatilia wananchi wa Mkoa wa Arusha wakitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Makonda. Kwa asilimia kubwa lazima sheria zifuatwe na Mkuu wa Mkoa hayuko juu ya sheria. Inawezekana kero nyingi zilizotolewa tayari aidha ziko Mahakamani au uamuzi wa kisheria ulikwishapitiwa.

Mimi naona wananchi wengi wanapoteza muda wao na hawatasaidiwa chochote na Mkuu wa Mkoa ni vema wakafuata taratibu za kisheria. Hata yule Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha alioagiza ahamishwe, mimi naona siyo utawala bora kusema mbele ya watu kuwa ahamishwe.

Usitafute popularity ambayo haisaidii. Najua wananchi wana kero nyingi na wanaonewa lakini ni budi sheria zifuatwe kutatua kero hizo.
Sijakuelewa kabisa. Yaani unachozungumza hapa eti sheria wakati wenye haki sheria inapindishwa kabisa na wenye pesa. Makonda japo anaweza kutafuta popularity lakini angalau kuna watu wamepatiwa haki yao. Anyway mzuri hakosi wabaya wake. ninatamani wakuu wote wa mikoa wawe kama yeye angalau watu wapatiwe haki yao. Nikuulize tu nina hati yangu imekaa hapo Arusha ardhi na unazungushwa tu bila saabu ukiuliza pembeni unaambiwa ukito pesa inatoka chapuchapu. Kuzungushwa kote ni pesa inahitajika. nimeamua kuiacha mpaka hapo wataamua wenyewe. Ninakuuliza tu. Mimi nikaishtaki wapi maana hata nikienda kuwashitaki ndiyo watazidi kuniweka mikwara na kunizungusha zaidi. Mwisho tu ni kwamba Nchi yetu ina uozo mkubwa sana kila mahali na mtu kupata haki yake kama huna pesa ni majaliwa.
 
aisee nashangaa arusha ghafla nao wamegeuka wamekuwa kama watu wa kule katavi na tandahimba kulialia wakati wanaelewa sheria na utaratibu wa kupata haki,wanahangaika na mtu wakuwapotosha tu na kisha kuwaacha kwenye mataa ya mianzini
Ww unaona watu wanavyotapeliwa, wanakosa haki zao au naww ni zulma kama hao wengine.
 
Sijakuelewa kabisa. Yaani unachozungumza hapa eti sheria wakati wenye haki sheria inapindishwa kabisa na wenye pesa. Makonda japo anaweza kutafuta popularity lakini angalau kuna watu wamepatiwa haki yao. Anyway mzuri hakosi wabaya wake. ninatamani wakuu wote wa mikoa wawe kama yeye angalau watu wapatiwe haki yao. Nikuulize tu nina hati yangu imekaa hapo Arusha ardhi na unazungushwa tu bila saabu ukiuliza pembeni unaambiwa ukito pesa inatoka chapuchapu. Kuzungushwa kote ni pesa inahitajika. nimeamua kuiacha mpaka hapo wataamua wenyewe. Ninakuuliza tu. Mimi nikaishtaki wapi maana hata nikienda kuwashitaki ndiyo watazidi kuniweka mikwara na kunizungusha zaidi. Mwisho tu ni kwamba Nchi yetu ina uozo mkubwa sana kila mahali na mtu kupata haki yake kama huna pesa ni majaliwa.
Nenda kwenye ofisi ya Ardhi ufuatilie hati yako.Kama unazungushwa nenda kwanza kwa Kamishna.Usiposaidiwa kuna dawati la malalamiko kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa utapata msaada.Haki haipotei na kupewa hati yako ni haki yako
 
Ttzo watu weng huwa atujui ni wap pakuanzai na wap pakuishia na wanasiasa uwa wanatumia nafasi iyo kujijengea majina
 
Namshauri Mkuu wa Mkoa ajikite na maendeleo ya Arusha kwa wananchi kulima, biashara na mwisho wa siku wananchi wa Mkoa wa Arusha wawe matajiri. Yote haya anayofanya yata backfire. Alipokuwa Mwenezi wa CCM Taifa alitembelea karibu mikoa kumi akisikiliza kero niambie mpaka leo hii kero gani imetatuliwa na mwananchi akaona ahueni. Tuna utaratibu uliowekwa na nchi jinsi ya kushughulikia kero za wananchi. Unapata wapi sheria ya kutamka kuwa mtumishi hatoshi kwenye nafasi yake. Kila alipokuwa anataka kuongea yule Mwanasheria wa Halmashauri anamkatisha. Huo ni utawala gani. Yeye ajikite na maendeleo ya wananchi wa Mkoa wa Arusha.
 
Nimekuwa nikifuatilia wananchi wa Mkoa wa Arusha wakitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Makonda. Kwa asilimia kubwa lazima sheria zifuatwe na Mkuu wa Mkoa hayuko juu ya sheria. Inawezekana kero nyingi zilizotolewa tayari aidha ziko Mahakamani au uamuzi wa kisheria ulikwishapitiwa. Mimi naona wananchi wengi wanapoteza muda wao na hawatasaidiwa chochote na Mkuu wa Mkoa ni vema wakafuata taratibu za kisheria. Hata yule Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha alioagiza ahamishwe, mimi naona siyo utawala bora kusema mbele ya watu kuwa ahamishwe. Usitafute popularity ambayo haisaidii. Najua wananchi wana kero nyingi na wanaonewa lakini ni budi sheria zifuatwe kutatua kero hizo.
 
Nafikiri lab
Kweli umemsikiliza vizuri namna anavyosikiliza kero hizo na namna anavyozitanzua, au mmejipanga tu kutafuta huruma ya umma kwa kuleta mada za namna hii humu?

Kwa jinsi kero za watu wengi wanavyozisema wazi mahakama kutumika kudhulumu haki zao, ama haki zinazotolewa mahakamani kutokupatikana kwa kushindikana utekelezaji wake, ninamuunga mkono sana Rc Makonda, angalau kuonesha kupoza machungu ya raia.

Hakuna popote Makonda alipoingilia Mahakama, bali anasikiliza kero zote zikiwemo dhuluma za kisheria na wanasheria na kuelekeza kufuatilia kuziba tobo ulipoanzia uharibifu.

Serikali ina utatu wake: Serikali kuu, Bunge na Mahakama.

Vyombo vyote hivyo vimewekwa kusaidia watu , hakuna kilicho juu ya sheria kutokuchunguzwa kikitenda kinyume na maadili ya umma.

Huyo mwanasheria wako wa Halmashauri ni mtumishi wa umma mzembe na mbinafsi sana, ni mfano wa uozo wa watumishi wa umma iliotamalaki nchini.

Hakutakiwa hata kupewa upendeleo wa uhamisho kwa namna uzembe wa wazi ulivyojidhihirisha katika eneo lake kiuwajibikaji.

Tungelikuwa na maRc wengine kama Makonda huko kwingine, Serikali hii isingelichukiwa na kutukanwa kama ilivyo sasa na sababu kubwa za wazi watu kuichukia Serikali yao ni kuwa Serikali yote imelala usingizi wa pono, hakuna anayeweza kumuamsha mwingine kutoka usingizini.

Makonda kaonesha njia ya namna kiongozi mwajibikaji anatakiwa awe.

Tumpeni moyo na shime kwa kumuunga mkono.
Nafikiri labda ungewashauri nao watumie watu wa macamera kama mwenzao.
Awamu ya tatu ya Mzee Benjamin Mkapa,aliwahi kuunda Tume chini ya Jaji Mzee Warioba ya kujua vyanzo na hali ya rushwa nchini, kama yale yaliyoibuliwa na tume hiyo ungepata nafasi ya japo kidogo tu kuyasoma naamini usingeamini kama yanafanyika Tanzania. Na kama ripoti ya ile tume ingefanyiwa kazi haya unayosikia Arusha kwa kiasi kikubwa yasingekuwepo.
Ukweli ni kwamba ccm haina Nia ya dhati ya kukomesha rushwa,huo ndio ukweli.
Hapa wanacheza na akili za watu basii. Kama unabisha Yuko wapi yule mfanya biashara aliyedhurumiwa na Tra zaidi ya million mia nane kariakoo na suala lake lilitua mpaka kwa JPM kwenye mkutano wa wafanya biashara,na waziri mkuu aliagizwa ahakikishe amelipwa hela yake, mwishowe majuzi tumesikia amejiua!! Tena akiwa amekimbilia Tabora kunusuru maisha yake kama alivyowahi kusema mwenyewe kuwa alikuwa akipokea vitisho.
Sasa kama mpaka Rais anapuuzwa na watu walio chini yake tutegemee nini kwa maRc?
Ripoti ya Warioba ilieleza mengi sana, nini kimewapa kigugumizi kuifanyia kazi?
 
Yeye hajui sheria lakini ana wanasheria wake kila wakati wanaompa ushauri na jinsi ya kuzitatua
Mimi naona kwa hilo anasaidia wengi na kujaribu kuonyesha kuwa wafanyakazi wengi ni majizi na wala rushwa
 
Back
Top Bottom