Kesi ya Mbowe na Wenzake: Polisi Wazuia watu kuingia kufuatilia, Mawakili wa Utetezi watoka nje. Kesi yarejea na kuahirishwa mpaka 17 Sept
Weka kwanza kifungu kinachokupa uhalali wako wa kuingia na simu ndipo uadhiriwe peupe
Endapo mwalimu shuleni angekuwa akimuuliza swali mwanafunzi na mwanafunzi nae amuulize mwalimu sijui ingekuwaje, wewe umeuliza swli, jibu swali. iko wapi sheria inayokataza kuingia na simu mahakamani ?

Jana tu watu walikuwa wnaingia na simu, baada ya jamuhuri kuumbuliwa na kuzuiwa kumtumia shaidi wa uongo imekasirika na kuelekeza vidampa wao wazuie watu kuingia na simu, kama wanayoyafanya ni ya haki nini kinachowatia hofu?
 
Hamna kazi za kufanya kazi yenu ni kukaa mahakamani siku nzima kufuatilia kesi ya Mbowe????

Anyway, kuna kitu watu wengi hawajui. Gaidi siyo lazima awe anamiliki AK47 au M16 Rifle au mabomu.
Gaidi anaweza akawa na kisu tu na akafanya ugaidi. Gaidi anaweza akawa na "ideology" tu kichwani na akafanya ugaidi.

By the way sisemi Mbowe ni gaidi, hapana. Kwa sasa hivi Mbowe is innocent until proven guilty.

Time will tell.
WE HAPA JF NDO KAZINI KWAKO SIO MFUUU
 
Hii kesi kama ikiachwa iendelee inakwenda kumwaibisha mtu.. hii kesi ni ya kuachana nayo haraka ili tusonge mbele kama taifa. Tunatakiwa kuanza mapema kumalizia mchakato wa katiba mpya kabla ya 2023 iwe tayari ili tuanze kujiandaa kwa 2025.
Mimi siyo hakimu lakini kwa jinsi hii kesi ilivyo namwona Mbowe akila mvua ya kutosha.

Hii kesi imebeba maslahi mapana ya Serikali iliyopo madarakani. Kushinda kwa Mbowe au kufutwa kwa hii kesi is likely impossible.
 
Freeman Mbowe na wenzake wameletwa tayari. Lakini ulinzi mkali umeimarishwa. Askari wengi. Pia kuna zuio la watu kuingia ndani ya mahakama. Wanasema ni mawakili 20 tu, wanahabari 10 (leo wameruhusiwa), ndugu 5, Viongozi 5, lakini simu marufuku.

Askari magereza wanalalamika kwamba jana tumefanya ujinga sana. Ujinga gani, tunawaukliza, wanasema tulikuwa tunatuma habari nje. Wanamueleza Benson Kigaila, NKM CHADEMA. Tumewaeleza kwamba, anayetakiwa kulalamika ni Jaji sio wao. Mahakama siyo gereza. Wajishikilie vizuri.

Mahakama imechelewa kwa dakika 40, yote hii ni kutokana na Jamhuri kutaka kuhodhi mamlaka ya mahakama, bila kujua kwamba wote hapa tuna interest na kesi hii, wao ni walalamikaji, sisi ni watuhumiwa. Kwanini watuzuie kuingia mahakamani na simu?

Watoto wote wa Freeman Mbowe, (Nicole na Dudley) pia wapo nje ya mahakama, pamoja na ndugu zao wengine.

Kama kawaida yao, makarao waliovalia kiraia, wamekaa kwenye siti karibu zote za mahakama, wamechukua nafasi kama kesi ni yao pekee yao.

Mambo ya ajabu yanafanyika

Lakini kitu cha muhimu hadi sasa ndugu zangu ni kwamba, kwa umoja wetu wote tupo nje ya mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi na Rushwa, Ubungo-Mawasiliano, tumeshawaelekeza MAWAKILI wetu wasomi kwamba "No ENTRANCE NO CASE"... And it's done, hii ni open court!

Updates
Jana Jaji Mustapha Siyani alisema watuhumiwa waletwe mapema, saa 3 asubuhi kesi ianze, lakini mpaka saa 5 na Dakika 24 sasa kesi haijaanza kwa sababu ya polisi kuzuia watu. Mawakili wetu walikwenda kumuona Jaji, wanatupa taarifa kwamba Jaji amekana kuzuia Jambo hilo mahakamani.

Updates
Wakili Msomi Kibatala ameandika Jaji ameruhusu watu waachwe huru


C&P Martin
Asante sana tunafatilia kesi hii ya kihistoria chini ya utawala dhalimu uliopo.
 
Baada ya Jana jamii kupata habari ya kila kilichotokea Mahakamani kwa ufasaha bila kupindisha Leo jeshi la Polisi limedhibiti uingiaji Mahakamani pamoja na kuzuia matumizi ya simu. Sababu zakufanya hivyo hazijawekwa wazi. Ikumbukwe ACP Ramadhani Kingai ambaye ni mkuu wa Polisi Kinondoni leo anaendelea kuhojiwa katika kesi ndogo iliyoibuka kutoka kesi ya msingi.

Wakati jana anahojiwa kuhusu uwepo wake Mahakamani hapo Mara kwa mara kesi hii inapokuwa inasikilizwa alikiri kuwa anafika Mahakamani hapo na kwa mazingira haya yeye akiwa ni shahidi pia yeye ndiyo kiongozi wa Askari kwa eneo hili la mahakama na hivyo yawezekana baada ya Jana kuona Hali ya utata na maswali yaliyoibuka Mahakamani Leo hii amejiwekea ulinzi kuepusha taarifa za ushahidi wake kutokufika kwa jamii.

Hali hii imelalamikiwa muda mrefu na tatizo halijawekwa wazi kwamba serikali ndiyo inafanya haya au mahakama yenyewe ndiyo imeamua kutokuonekana matendo yake kwa wananchi. Katika ulimwengu wa Sasa nchi nyingi Duniani zimeruhusu live cavarage Mahakamani tofauti na Tanzania ambapo hata waandishi wa habari wanaoruhusiwa kuingia mahakamani ni wale tu ambao Jamhuri inaamini wataripoti kile ambacho wao wanataka.

Mfano mzuri ni tukio la Jana ambalo hakuna chombo Cha habari kilichokuwa mahakamani kiliweza kuweka updates ya kinachoendelea mahakamani. Vyombo vyote vilikaa kimya isipokuwa JF na Kurasa za tweeter.

Mahakama kwa mwendo huu inaonyesha wazi kwamba siyo chombo huru, vinginevyo itoe tamko kwa dola kuruhusu watu kuingia kulingana na ukubwa wa ukumbi wa mahakama na ikumbukwe hakuna sheria inayokataza kesi kuripotiwa moja kwa moja kwa wananchi.
Watanzania tufike mahali tuamue na kukataa ushenzi huu!
 
Baada ya Jana jamii kupata habari ya kila kilichotokea Mahakamani kwa ufasaha bila kupindisha Leo jeshi la Polisi limedhibiti uingiaji Mahakamani pamoja na kuzuia matumizi ya simu. Sababu zakufanya hivyo hazijawekwa wazi. Ikumbukwe ACP Ramadhani Kingai ambaye ni mkuu wa Polisi Kinondoni leo anaendelea kuhojiwa katika kesi ndogo iliyoibuka kutoka kesi ya msingi.

Wakati jana anahojiwa kuhusu uwepo wake Mahakamani hapo Mara kwa mara kesi hii inapokuwa inasikilizwa alikiri kuwa anafika Mahakamani hapo na kwa mazingira haya yeye akiwa ni shahidi pia yeye ndiyo kiongozi wa Askari kwa eneo hili la mahakama na hivyo yawezekana baada ya Jana kuona Hali ya utata na maswali yaliyoibuka Mahakamani Leo hii amejiwekea ulinzi kuepusha taarifa za ushahidi wake kutokufika kwa jamii.

Hali hii imelalamikiwa muda mrefu na tatizo halijawekwa wazi kwamba serikali ndiyo inafanya haya au mahakama yenyewe ndiyo imeamua kutokuonekana matendo yake kwa wananchi. Katika ulimwengu wa Sasa nchi nyingi Duniani zimeruhusu live cavarage Mahakamani tofauti na Tanzania ambapo hata waandishi wa habari wanaoruhusiwa kuingia mahakamani ni wale tu ambao Jamhuri inaamini wataripoti kile ambacho wao wanataka.

Mfano mzuri ni tukio la Jana ambalo hakuna chombo Cha habari kilichokuwa mahakamani kiliweza kuweka updates ya kinachoendelea mahakamani. Vyombo vyote vilikaa kimya isipokuwa JF na Kurasa za tweeter.

Mahakama kwa mwendo huu inaonyesha wazi kwamba siyo chombo huru, vinginevyo itoe tamko kwa dola kuruhusu watu kuingia kulingana na ukubwa wa ukumbi wa mahakama na ikumbukwe hakuna sheria inayokataza kesi kuripotiwa moja kwa moja kwa wananchi.
Wanazuia wasiwasiliane na UAMSHO......na El Qaeda.....na magaidi wenzao Tarime..
 
Kesi zote za kigaidi huko dunia ya kwanza huwa zinafanyikia mafichoni. Kwahiyo hakuna cha kushangaza.
 
Back
Top Bottom