safi, kumbe unakubali kwamba mfumo ulionao ni wa hivyo ee.
Ashughulikiwe???HuyiJaji huyu Jaji, naona mashaka na Giza mbele,naona mashaka na Giza mbele...BIASED KABISA, KWANINI? TIME WILL TELL
Jitu jinga kabisaKwani lazima upaste hii comment kwenye kila uzi? Acha undezi dogo
Sure!!Ashughulikiwe ???
Huyu Jaji hana tofauti na wakurugenzi wakati wa uchaguzi!Kwa kunyimwa nyaraka ili wasiuliuze maswali. ?!
MaCCM wote akili zenu hazina akili.
Ukweli ni kwamba tumefika hapa kuwa CCM ni Chama maiti.
Chama hai hufanya siasa za ushindani na hakiogopi mwenyekiti wa upinzani wake, na kumpa makesi ya uongo yasio na kichwa wala miguu . MaCCM mmekwama sana.
Mbonà hili liko waziHuyu jaji mwenyewe inaonekana anapendelea upande wa jamhuri sana au ni kwamba mawakili wa Mbowe hawajui sheria vizuri?
Najaribu ku track mwenendo wa huyu Jaji sijapenda. Anaanza kunipaashaka Sana. Huyu si mwema hata kidogo. Ana lake Jambo nalionaTuko pamoja
Kamchungulie maaa yako anaogaWamfunge tu mbona ushahidi wa jamhuru umeenyooka hivyo. Kuliko hata ule wa Sabaya wa kuunga unga naa gundi. Kama hii kesi ni ya uwongo niamini kesi ya namna gani. Technologia aidanganyi bhana.
Mnasumbua tu mahakana.
Hajarudi to,[emoji1745]Baada ya jana kuahirishwa, Kesi ya mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe inaendelea kuunguruma leo mahakamani. Jana kesi iliahirishwa kutokana shahidi kupata dharura ya kiafya na upande wa utetezi haukutoa kikwazo chochote kwenye sababu hiyo. Jaji aliahirisha mpaka leo. Kuwa nami.
==============
Jaji ameingia.
Kesi inatajwa
Robert Kidando anatambulisha Jopo lake
Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza kitali
Nassoro Katuga
Esther Martin
Ignasi Mwinuka
Tulimanywa Majige
Peter Kibatala anatambulisha Jopo la mawakili wa utetezi
Peter Kibatala
John Malya
Fredrick Kiwhero
Dickson Matata
Idd Msawanga
Nashon Nkungu
Maria Mushi
Khadija Aron
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shauri lina kuja kwa ajili ya Kusikilizwa na Leo tuna shahidi Mmoja Tupo tayari kuendelea
Wakili wa Serikal: Mmoja anatoka kwenda Kumfuata
Jaji: upande wa Utetezi
Wakili Peter Kibatala: Na sisi pia tupo tayari Kuendelea
Jaji: Shahidi Wenu?
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ameenda Kufuatwa Anaingia Shahidi Mfupi Kavaa Kaunda
Jaji: Majina yako
Shahidi: SSP Sebastien Madembwe
Jaji: umri
Shahidi: 46
Jaji: Kabila
Shahidi: Mhehe
Jaji: Shughuli zako
Shahidi: Afisa wa Polisi
Jaji: Dini yako
Shahidi: Mkrito
Shahidi: Mimi SSP sebastian Madenge Naapa Kwamba Ushahidi nitakaotoa ni Kweli tupu Eeeh Mwezi Mungu nisaidie
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi Ataongozwa na Wakili wa Serikali Pius Hilla
Wakili wa Serikali: Shahidi umesema Majina yako kwa ukamilifu ni nani
Shahidi: SSP sebastian Madenge
Wakili wa Serikali: Unaishi Wapi
Shahidi: Iyumbu Kule Dodoma
Wakili wa Serikali: Mkazi wa Dodoma tangu lini
Shahidi: Mwezi wa Nane 2020
Wakili wa Serikali: Kabla ya hapo ulikuwa unaishi Wapi
Shahidi: Nilikuwa naishi Muongo la Ndege Ukonga, Nikiwa Ofisa wa Polisi Makao Makuu, iliyokuwa Makao Makuu Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Uliajiliwa lini kama Polisi
Shahidi: 02 Mwezi 09 Mwaka 1999
Wakili wa Serikali: Katika Jeshi la Polisi Upo kamisheni gani
Shahidi: Nipo kamisheni ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai
Wakili wa Serikali: Kitengo Gani
Shahidi: Udhibiti na Usajili wa Silaha
Wakili wa Serikali: Kwa Kizungu Mnaitaje
Shahidi: Arms Management and Registration Unit
Wakili wa Serikali: Kitengo hilo kina husika na Nini
Shahidi: Usajili wa Silaha za Raia Utoaji wa Leseni za Kumiliki silaha Kibali Vya Kuingiza Silaha Nchini Vibali Vya Usafirishaji wa Silaha na Risasi Hapa Nchini
Shahidi: Vibali Vya Upotoshaji wa Silaha zinazoenda Nchi mbalimbali kupitia Kwetu Tunatoa Vibali Vya Uuzaji wa Silaha na Risasi Yote yanahusiana na Usajili wa Silaha Tunahusika pia na Nchi Mbalimbali katika Udhibiti wa Silaha katika Kutekeleza Mikataba ya kikanda na Kimataifa
Wakili wa Serikali: Umesema Usajili wa Kiraia Je Unamaanisha Nini Shahidi: Ni zile Silaha zilizoruhusiwa Kwa Mujibu wa Sheria namba 02 ya Mwaka 1995 Sheria imetaja Silaha zinazoruhusiwa ni Pistol, Riffles, Short gun na Silaha yoyote ambayo Bodi ya Udhibiti wa Silaha itapendekeza iingie Miongoni Mwa silaha za Kiraia
Shahidi: Samahani Mheshimiwa Jaji, Silaha Nyingine ni Gobole
Wakili wa Serikali: Silaha Ndogo na nyepesi Fafanua hapo
Shahidi: Udhibiti Wa Silaha hizi tunazomiliki za Kiraia, Silaha Ndogo Ndogo ni zile ambazo Mtumiaji ni Mtu Mmoja. Kwa Mfano AK47 ni Silaha Ndogo Lakini Silaha Nyepesi yani Light Weapon ni Ile ambayo inatumika kwa Urahisi
Wakili wa Serikali: Kwenye Kitengo wewe ni nani
Shahidi: Ni Mrajisi Wa Leseni za Bunduki
Wakili wa Serikali: Kwa Kizungu
Shahidi: ni CEO arms Register
Wakili wa Serikali: Majukumu yako wewe ni Yapi
Shahidi: Ni Kuhakikisha kwamba napokea Maombi yote ya Waombaji wanataka Kumiliki silaha, Yaliyopitishwa na Kamati za Ulinzi na Usalama Kuanzia ngazi ya mtaa ambalo Mwombaji anaishi, Kata, Wilaya na Kamati ya Ulinzi na Usalama Ya Mkoa
Wakili wa Serikali: Jukumu la Pili..?
Shahidi: Kuyakagua Maombi hayo niliyoyapokea ilikuina kama Yana Vigezo kwa Mujibu wa Sheria, Licha ya Kwamba Maombi hayo yatakuwa yamepitishwa kwenye Kamati nilizozitaja Na Kwamba Maombi Yaliyokodhi Vigezo huendelea Kuya Shughulikia Ngazi inayofuata
Maombi Yaliyokidhi Vigezo nayarudisha yalikotoka Kutoa Vibali Vya Uuzaji wa Silaha hapa Nchini, Kibali cha Usafirishaji WA Silaha hapa Nchini na Upitishaji Vibali kwenda Nchi Jirani hasa wanatumia Bandari yetu Tunatoa Vibali Vya Kutunza Silaha (Warehouse License)
Shahidi: Tunatoa silaha Gunsmith Lisence (Kibali Cha Kufanyia Matengenezo silaha kwa Raia endapo itapata hitilafu Na Pia kutoa Leseni kwa wale waonataka Kumiliki Silaha Kutunza Kumbukumbu ya Silaha na Wamiliki wote ambao wamesajiliwa
La Mwisho ni Kupokea Maombi ya Kiuchunguzi pale silaha Inapo okotwa Ili tuweze Kuangalia Kwenye Data Base Kama Silaha hiyo imesajiliwa Au lah
Wakili wa Serikali: Mbali na Maombi hayo, Maombi Mengine huja kwa Namna gani
Shahidi: Ninapozumgumzia Uchunguzi no Uchunguzi wa Taarifa
Yoyote inayohitajika kwa ajili ya Shughuli ya Kiupelelezi, Ni Kitengo Kinacho Support Upelelezi katika Maswala ya Silaha
Wakili wa Serikali: Moja ya Jukumu umesema kutoa Vibali au Leseni za Umiliki wa Silaha Je Mchakato Ukoje Utaratibu wa Mpaka Mtu apewe Leseni
Shahidi: Wa Kwanza ni Kupokea Maombi ambayo yamepitishwa katika Kamati za Ulinzi na Usalama
Wakili wa Serikali: Kabla ya Hilo anaanza na Jambo gani Shahidi Ni Kununua Silaha, anaweza Kununua Katika Vyanzo Vitatu 1. Kwenye Duka ambalo wamepewa Leseni ya Kuuza Silaha (Lisenced Dealer)
2. Kwa Kununua kwa Mtu aliyekuwa anamiliki hiyo silaha Kihalali kwa kuandikishiana Mkataba wa Kisheria Na Kama Silaha ya Mirathi basi Kikao cha Ndugu wa Marehemu Kitakaa chini ya Mwenyekiti ambaye atakuwa amepitishwa na Mahakama Kwamba ni Msimamizi wa Mirathi kwamba ni nani wa Kuirithi Silaha hiyo Endapo wataamua Basi Mrithi anaweza Kumiliki Mwenyewe Kwa Utaratibu wa Kisheria au Kuuza Lakini Mrithi atahakikishq Kwamba Mteja anaye Muuzoa anamkabidhi Nyaraka zote za Mirathi pamoja na Mkataba walioandikishana Kisheria
3. Muombaji anaeleza Kununua Nje ya Nchi kwa Kuomba Kibali cha Kuingiza Hiyo silaha Nchini (Import Lisence) iwe Bandarini au Uwanja wa Ndege TASAKI ndiye atahusika Ku Clear hiyo silaha na Kuhifadhi wakati Muhusika ataendelea na Taratibu za Kuomba Kumiliki Silaha Hiyo
Shahidi: Kwa hiyo katika Vyanzo Vyote VitatuSilaha utatakiwa kuwa Kwenye Ghala, yeye atakuwa na Nyaraka za Mauziano ili ziweze Kumsaidia kama attachments katika Maombi yake Zipo fomu za Umiliki wa Silaha Kwa Mujibu wa Sheria na Kanuni zinaitwa Fomu A
Mwombaji hupaswa kuzijaza na Kuambatisha Nyaraka zote zinazoomyesha Chanzo cha Silaha hiyo Ata attach Fomu za Silaha hiyo, Kama Mfanya Biashara basi Leseni ya Biashara, Kitambulisho Cha Taifa na Nyaraka yoyote ile itakayodhibitisha Anamatishio Kutokana na Kazi anayofanya
Wakili wa Serikali: Inaambatana na nini hiyo fomu Ni lazima Kuwa muhtasari Kuanzia Ngazi ya Mtaa, Kata, Wilaya na Mkoa Wakili wa Serikali: Kingine?
Shahidi: Hati ya Tabia Njema inayotolewa na Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha
Kibatala: SAMAHANI Mheshimiwa Jaji Naomba Kwanza Kumuombea Wakili Jeremiah Mtobesya Aweze Kuingia Kwenye Orodha yetu Ambaye kachelewa Kwa sababu nilizotoa Mwanzoni Baada ya hayo nitaomba Sasa Wakili Mtobesya aweze kusema alichotaka
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Shahidi hana Maelezo katika Kifurushi cha Comito Kwa hiyo Ushahidi wake Hauwezi Kuingia Kwa Mujibu wa Kifungu cha 246 cha CPA Hakuna Maelezo yake, na Nimeulizana na Wenzangu Kama Upande wa Mashtaka Uliomba Mwanzoni Ombi lolote nimeambiwa Hapana
Mahakama Kimyaaaaaaa!
Upande wa mashtaka ni kama wamebutwa fulani hivi.
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Tutaomba Pia Maelekezo endapo Wenzetu watafanya Kwa Usahihi, Vipi kuhusu Ushahidi ambao Shahidi ameshaanza kuutoa hapa Mahakamani?
Mtobesya: Na ninataatifiwa hapa na kaka yangu, shahidi anatakiwa aondoke na ushahidi wake tuendelee na ushahidi Mwingine kwa Sababu hawawezi kupata faida baada ya sisi kusema kama wao hawakuomba mwanzoni Mawakili wa Serikali: Wananong'onezana Jaji anainama na kuandika
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ombi hilo halina mashiko yoyote ya kisheria
Jaji: maombi au pingamizi
Wakili wa Serikali: Ahaaa pingamizi, halina mashiko yoyote ya kisheria Sababu limeletwa katikati ya ushahidi Wa PW6 kinyume na sheria
Na Kama wangekuwa na hoja hiyo walitakiwa kufuatilia mapema, Lakini kwa wakili ambaye hakufuatilia tangu mapema proceedings hizi, Hoja yetu ya Pili ni kwamba Shahidi huyu aliorodheshwa tangu Kipindi Cha Committal Proceedings na anasomeka Kama Shahidi namba 23 tangu Mahakama Ya Hakimu Mkazi Kisutu Na hata katika Barua yetu ya 11 August 2021
Wakili wa Serikali: Ukurasa wa 32 na Jina lake linaonekana Katika 23 Labda lile neno S liondoke isomeke Sebastian
Wakili wa Serikali: Lakini Substance ilikuwa Committed na Ilisomwa Katika Mwenendo wa Shauri hilo katika Proceedings za Tarehe 23/8 Siku ambazo COMMITTAL Proceedings zilifanyika Na Jina lake limeandikwa sebastian Madembwe SSP
Lakini pia Katika Ile list ya Exhibit katika Ukurasa wa 33 Nyaraka Anayokuja Kuzungumzia imekuwa Litsted pale Namba 18 Ambayo pia imesainiwa na Sebastian Madembwe SSP nilikuwa Committed na Substance yake ilisomwa
Kwa hiyo kwa namna yoyote ile Hatukutakiwa Kuleta Ombi kupitia Kifungu cha 289 cha CPA ili Shahidi huyu aweze Kutoa Ushahidi Wake.. Na tunasema Pia Matakwa ya Rule 8 Sub 2 ya The Economic and Organized Crime Control (Corruption and Procedure Rules ya 2016),
Takwa hili la Kisheria lilitekelezwa na Mahakama. Iwe Jina ama Substance ya Ushahidi Anaotoa Leo hii hakuna Kitu Kipya kama Ambavyo wakili anajaribu Kuonyesha Mahakama yako Tukufu Na Kama hali Iko hivyo hakuna Haja Wa Kutoa Amri yoyote ile Kutokana na Ushahidi ambao Umeolewa na Shahidi Kwa sababu Shahidi Yupo Sahihi Kwa Mujibu wa sheria Hivyo Mheshimiwa Jaji tunaomba hilo Pingamizi ulitupilie Mbali ili Shahidi wetu aweze Kuendelea na Ushahidi Wake
Jaji anaandika Kidogo
Mtobesya: Kwanza Kabisa Wenzangu wameni attack, Personally Sikuwepo Kwenye Proceedings tangu Mwanzo, Mimi Kuchelewa Kufika sidhani kunaweza Kuathiri. Sisi tunachofanya hapa ni Kuisaidia Mahakama Kufanya Shughuli Zake Kwa Mujibu wa Sheria
Mtobesya: Nimesema Kwenye Committal Documents hakuna Ushahidi wa shahidi i huo. Substance inaongelea mambo matatu. 1. MAJINA Ingawa yamekosa hatuna Shida na hilo, 2 Cheti atakachotoa na 3. Hakuna Kile ambacho "Ataongea nini Mbele ya Mahakama"
Mtobesya: Tumeongea mara Nyingi kuhusu hili Kuwa kuna Sababu Ipo ya Kumpatia Mtu Nyaraka za Ushahidi kupitia Committal, Na Wasipokuwa wamefanya Upo Mlango Mwingine wa wao Kuomba kupitia Kifungu cha 289 Criminal Procedure Act
Wakili wa Serikali: Kama namwelewa Mtobesya anazumgumzia % Documents kutosomwa
Jaji: kama nimekuelewa umesema haipo kwenye Committal Bandle!
Mtobesya: Nimesema haipo kwenye Committal bundle kwa maana hiyo haijakidhi matakwa hayo ya kwenye 246 CPA
Jaji: Umeridhika na line yake ya argument sasa
Wakili wa Serikali: Hapana Sikubaliani na Mtobesya. Yeye ana argue kwamba haijasomwa, Maana akianza kujielekeza kwenye mengine na mengine inakuwa siyo sawa
Jaji: Hoja yao ni Kwamba argue kwa namna ambayo umeletea pingamizi
Mtobesya: Kwasababu Haipo ina maana haijasomwa, na kwa sababu haijasomwa inakiuka sheria aliyosoma Kaka yangu Kidando ya uhujumu uchumi na makosa ya uchumi ya mwaka 2016 Kingine Kaka Yangu anasema P. O imeletwa Kinyume na Sheria Kwa sababu Ilishapitwa
Hiyo siyo Sawa, Jambo lolote linaweza Kuibuliwa pale tu tunapoona tunaenda Kinyume na Sheria, tunalo hilo Jukumu Kama Wawakilishi wa wateja wetu na Pia kama Maafisa wa Mahakama Kwa hiyo kama ilivyoombwa Mwanzoni Mahakama Itoe Maelekezo na Kukidhi Matakwa YA Sheria. Ni hayo tu
Jaji anainama na kuandika kidogo
Jaji: Mmesikia hoja zote, Naomba nipate muda na mimi Tutarudi tena hapa saa tano na robo. Anasimama na kutoka nje ya chumba cha mahakama
Jaji alitoka Mahakamani 10:50 saa za Afrika Mashariki, akasema atarudi saa 11:15 ili akapitie sheria ambazo zimetajwa. Sasa ni saa 11:52 na bado hajarejea katika chumba cha mahakama. Tunaendelea kusubiri.
Jaji Ameingia 12:00 Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe imetajwa tena
Wakili wa Serikali: Upande wa Jamhuri tupo tayari na Hakuna Mabadiriko ya column
Kibatala: Na sisi Pia Mheshimiwa Jaji tupo vizuri
Jaji: Tuli' break Kwa muda Kwa nia ya kuandika maamuzi madogo, maamuzi yanalenga kutatua mgogoro wakati shahidi namba 06 anatoa ushahidi Mtobesya alieleza mahakama shahidi huyo anakiuka kutoa ushahidi wakati ushahidi wake haukuwa umesomwa kwenye committal mahakama ya Kisutu
Na akaeleza Kuwa hivyo Inakiuka Kifungu 246 cha Sheria 8 Sub ya CPA Sura ya 20 Na Pia GN 267/2017 na Kifungu cha 63 cha CPA na Sheria Ya Uhujumu Uchumi
Jaji: Hivyo Inakiuka Haki ya Washitakiwa na wao Kama wawakilishi Wa Washtakiwa Kutokuona Nyaraka hiyo na Pia Kwamba Haikusomwa Anaomba Mahakama imkatae SHAHIDI na Ushahidi Wake utupwe Upande wa Serikali Walikuwa na Hoja Mbili
1. HAINA Mashiko Kwa sababu Pingamizi limekuja Kwa Kuchelewa 2. Ushahidi wa Ushahidi Huo (Substance) ni sehemu ya Ushahidi tu, Mahakama Ijeielekeze Ukurasa wa 33 ambapo Inaonyesha Ushahidi Wake Ulisomwa Mahakamani
Akaongeza Kuwa Ushahidi Ambao unakuja Kutolewa Mahakamani Unakuwa Umesomwa basi Shahidi anatakiwa kuendelea Kutoa Ushahidi Wake Na Kwamba Kanuni zilifuatwa kama ambavyo imefanyika Kwenye Mahakama ya HAKIMU Mkazi Kisutu
Jaji: Mtobesya kwenye Kuhitimisha Hoja ya Serikali ya Kuchelewa haina Mashiko Yoyote, Pingamizi Linaweza Kuletwa Wakati wote wote Ni Jukumu la Upande wa Mashtaka Kutoa Nyaraka Mapema na Orodha Ya Watu wanaopangwa Kufanya Ushahidi Mahakamani
Jaji: Anaomba Mahakama Itamke Shahidi amefika Kinyume na Sheria na Ushahidi alitoa Upo Kinyume na Sheria Na Kwamba Disclosure ni kwamba Mahakama itumie Hivyo kama Msimamo wake
Jaji: Sasa Katika Hukumu nitatumia Sheria zilizotaja hapo Juu Pande Mbili wanakubaliana kuwa Malengo Mahususi Ni kwamba Ushahidi Unaokuja kutolewaa Mapema Unajulikana Mapema Ushahidi Wote Unaotakiwa Kuja Mahakama Kuu Unatakiwa Kujulikana
Moja kwa Kusomwa Kwa Kuandaliwa Kwa Mfumo wa kitabu na Kukabidhiwa Majukumu haya yanafanywa na Upande wa Mashtaka Kusambaza Ni kazi ya Mahakama Pingamizi lolote linaweza Kuja wakati wowote Pale anapogundua Kuwa kuna Mapungufu anaweza Kuleta Mahakamani
Jaji: Ni Msimamo wa sheria Kuwa pale ambapo Ushahidi unakuwa haujasomwa basi hauwezi kupokelewa mahakamani labda kama wataomba kama ilivyoelezwa na Wakili Mtobesya kwenye Kifungu cha 289 CPA Jambo linalobishaniwa ni kwamba ushahidi haukusomwa hapa mahakamani
Jaji: Mahakama inayo Jukumu la kukagua Kama Ushahidi Kama Ulisomwa au Haukusomwa Mbele Ya Hakimu Mkazi wa Kisutu wakati Wa Committal Inasomwa Mahakama Wakati Ina Examine Record Imeona Kwenye Ukurasa wa 21 Maneno Yafuatayo Kwamba Ushahidi Na Mashahidi Yamesomwa kwa Washtakiwa
Akasema Hakimu Simba Tarehe 23 08 2021 Akaorodhesha Mashahidi 21 na Jina la Shahidi Namba 06 linaonekana Katika Ukurasa wa 31 Na Kwamba Mashahidi hao waliorodheshwa na Maelezo yao yalisomwa Mbele ya mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Huo ndiyo Msimamo na Kumbukumbu za Mahakama
Kwamba Maelezo yote yalisomwa na Kwamba Ushahidi huo Ukisomwa Na Mahakama haikuishia hapo Kama Nilivyosema Katika ku' Examine Mahakama Ikaona Kuna Maelezo Ya Shahidi namba 06 Kumbe yalisomwa na Kwamba Tatizo Maelezo hayo hayakuunganishwa Katika Kifurushi cha Comito Proceedings
Jaji: Kutokwemo Katika kifurushi haimaanishi Ushahidi Wa shahidi Namba 06 haukusomwa Mahakama Inaona Pingamizi Halina Mashiko Lengo la Pingamizi Ilikuwa Ku Impeach Record za Mahakama Maelezo Yalipo Mahakamani Yana onyesha Ushahidi Ulisomwa hivyo naelekeza Sasa Shahidi Aendelee
Mawakili Wote wanamyanyuka Ishara ya Kukubaliana na Jaji
Jaji: Mara Ya Mwisho alisema huyo Mwombaji lazima awe na Cheti cha Tabia Njema kutoka Jeshi la Polisi
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Iwapo zipo Nyaraka zingine zinaambatanishwa na Maombi
Shahidi: Zile zinazo onyesha Mwombaji kuwa Upo Umuhimu wa Yeye Kumiliki Silaha Vielelezo anavyoweza Kuambatanisha ni Ile kazi anayofanya WS: Maombi ya kisha wakilishwa
Shahidi: Yakishawakilishwa kwangu nayakagua ili Kujiridhisha Kama Yanakidhi Vigezo Vilivyowekwa Kwa Mujibu wa Sheria
Wakili wa Serikali: Ka Maombi hayajakidhi Vigezo nini hufanyika
Shahidi: Mambo Mawili hufanyika 1.Yanaweza Kurudihswa Kwenye Mkoa Husika Ilikukamilisha Vigezo Vinavyokksekana 2. Endapo itaonekana Mwombaji hana Sifa zilizo ainiahwa Kisheria na Kwamba hata akirekebisba
Vigezo vianvyopungua basi Maombi hayo ubaki Makao Makuu na Mkoa unaohusika Ujulishwa kuwa Mwombaji hana Sifa
Wakili wa Serikali: Maombi Yanayokidhi Vigezo? Nimi hufanyika
Shahidi: NiKumjulisha Mwombaji Kwamba amekubaliwa
Wakili wa Serikali: Kwenye Barua hii husika Muhisika atakiwa nini
Shahidi: Mwombaji anajulishwa Kuwa Maombi yake yamekubaliwa anatakiwa kwenda Kwa Mkuu Wa Wilaya Kwenda Kukamilisha Malipo Na Baada ya Kukamilisha Malipo arudi Katika Ofisi ya Mrajisi Akiwa na Barua aliyopewa ya akumjulisha kuwa ameruhusiwa Kumiliki Silaha Kutoka Ofisi ya Mrajisi ikiwa imeambatanishwa na Risiti ya malipo Ambapo Malipo hayo hufanyika kwa mkuu wa polisi Wilaya
Wakili wa Serikali: Nini tena hufanyika Shahidi: Kama amekamilisha malipo, kinachofuata ni Hatua ya Usajili
Wakili wa Serikali: Unakamilishwaje
Shahidi: Kwa Mambo Mawili Kwanza Kwa kuipa Silaha Husika Registration Number, Central Arm Register Numbe Kwa kifupi tunaita CAA number Ambapo kitabu hicho Chenye CAA namba kitaandikwa Mambo yafuatayo Maelezo ya Silaha ambayo Muhusika ameomba
Wakili wa Serikali: yanapatikana wapi Shahidi: Kwenye Ukurasa wa Kwanza kwenye hicho Kitabu
Wakili wa Serikali: unayapata wapi Mambo ya Kujaza
Shahidi: Ile Barua ya Kumjulisha Mwombaji inakuwa na Maelezo yote Pamoja na Maelezo ya Muhusika yanaingizwa Kwemye Kitabu
Shahidi: Na Kisha Kuandika Picha Kwenye Kitabu hicho Chenye CAA Namba Nitaffungua faili na Kuingiza Document kwenye Faili Na Juu ya faili Nita andika Registration namba yani CAA namba Kwa ajili ya Kumbukumbu
Nilisha Kamilisha Sasa Kusajili Katika Mfumo wa Makaratasi namuingiza sasa Katika Electronic Data Base
Wakili wa Serikali: kwenye Mfumo ni taarifa zipi unazoingiza
Shahidi: Mfumo utanitaka Kuingiza Kwanza CAR namba
Shahidi: Mfumo utanitaka niingize aina ya silaha
Mtengemezaji kwa Maana ya Kampuni iliyotengemeza na Serial Namba Ambayo Mtengemezaji ameigonga Kwenye silaha Husika
Shahidi: Kuna parameters za Nyongeza Kama Nchi ambayo Silaha hiyo Imetengenezwa, Model Namba pamoja na Callibre Size
Hizi parameters nilizo it aja Mwishoni siyo za a Umuhimu sana Bali za Nyongeza Katika Kusaidia Utambuzi
Wakili wa Serikali: Ulizungumzia particular za Mhusika, Ni kitu gani
Shahidi: kwa Ruhusa ya Mheshimiwa Jaji, tunaingiza IDADI ya Risasi ambazo Mmiliki anaruhusiwa Kuzimiliki kwa Wakati Mmoja
Shahidi: Majina, Uraia wake, Jinsi a Yake, Kazi yake, Namba ya Kitambulisho Cha Taifa au Mpiga Kura kwa wale ambao hawana Cha Taifa, Makazi yake Tukiingiza kuanzia Mtaa, Kata anayotaka Mwombaji, Tarafa, Wilaya na Mkoa
Wakili wa Serikali: Kama Kuna Taarifa zingine mnazo ingiza kwa simu
Shahidi: namba ya Simu, anuani ya Barua pepe, Chanzo cha silaha Kama ameinunua
Wakili wa Serikali: Ukiisha Kamilisha Kuingiza Taarifa zote kwenye Mfumo Kinachofuata ni nini Shahidi Kinachofuata ni Kusave, na baada ya kubonyeza Button ya Kusave hakuna Chochote Kitakachokuwa ammended
Shahidi: Kuweka Kumbukumbu, Kurejea Kumbukumbu endapo Silaha itakuwa inatafutwa Pangine imepatikana katika Tukio la Uhalifu ili Kujua inaweza Ikawa Miomgoni Mwa silaha zilizo sajiliwa
Wakili wa Serikali: Nyaraka zipi sasa Muhusika upewa Shahidi Kwa Mujibu wa Sheria kesi ya Udhibiti wa Silaha ya Mwaka 2015 na Kanuni zake za 2016 Mmiliki anacbokabidhiwa ni Kule Kitabu
Wakili wa Serikali: Shahidi Sasa umesema kumbukumbu za Umiliki kwa Maana Hard copy na Sosty Copy, na Madhumuni ni Ka. MAOMBI ya Uchunguzi wa Silaha yatafanyika Je ni watu gani huketa Maombi
Shahidi: Sisi Upokee Kutoka Kwenye Ofisi inayopeleleza Kwenye Shauri husika
Wakili wa Serikali: Pengine ni wapi
Shahidi: Kwenye Taasisi zinazosimamia Utekelezajibwa Sheria mbalimbali Mfano tumepokea Maombi Kutoka PCCB Kutoka Nna Taasisi inayodhibiti Madawa ya Kulevya
Wakili wa Serikali: Maombi ya Uchunguzi wa Silaha Yanatakiwa Kwmuwa na nini
Shahidi: Yawe na Taarifa 03 za Msingi, Taarifa za lazima au zile za ziada Taarifa ya Kwanza iwe ni Aina ya Silaha Kingine ni Jina la Mtengemezaji (Makers name au Manufacturer name) Namba zilizohongwa na Mtengenezaji (Manufactural serial number) Itatuwezsha Kujua hii silaha Imesajiliwa au Haikusajiliwa
Wakili wa Serikali: Unapopokea Maombi kama hayo unafanyia Nini
Shahidi: Kwanza Tunagongq Muhuri kwamba tumepokea Baada ya hapo tunaanza Kufanyia Kazi
Wakili wa Serikali: Kwa namna gani
Shahidi: Kwa Kuingiza Parameters ya Yale a Maombi katika Mfumo Sababu Parameters ni Unique hata Kama Silaha zimetemgezwa NA Mmiliki huyo huyo bado pan kuwa hakuna Coalition
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kinafanyika Kuwa na Unique Serial Number
Shahidi: Hawa watenhenezajonwanakutana Kupeana kuhusu Serial number na Kuhakikisha Namba haziingiliani
Wakili wa Serikali: Mkishaingiza kwenye parameter kwenye mifumo
Shahidi: Na Click Okey Kama Silaha Imesajiliwa itaketa amatokeo Chanya na ninaweza Sasa Kwenda Kwenye Hard Copy
Wakili wa Serikali: Matokea Hasi ni Yapi
Shahidi: Nilipo ingiza Parameters na Mfumo Kutafuta Nakubaini Hakuna Kumbukumbu zozote katika Mfumo huo
Wakili wa Serikali: Mwisho wa Siku unafanya nini Shahidi Kama Matokeo Chanya Nafanya Mambo Mawili kwenye Taasisi iliyooomba Uchunguzi ufanyike
Nita Print Out Mfumo Umetuleeza Hivi na Itakuwa Kiambatisho Katika Barua Yangu Kama Matokeo Yatakuwa Hasi itaandikwa Barua na Haoatakuwa na Printout Yoyote
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama tarehe 25 Nov 2020 ni Kitu gani Kilitokea
Shahidi: Nikiwa Ofisini Kwangu Makao Makuu Dodoma Nilipokea Barua ya Kufanya Uchunguzi Silaha aina ya Bastola
Wakili wa Serikali: Ilitoka Wapi
Shahidi: Makao Makuu Madogo Police Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Idara Gani
Shahidi: Idara ya Upelelezi Makosa ya Jinai Barua ilinitaka Kufanya Uchunguzi wa Aina Ya Silaha Bastola Mtengenezaji ni Luger na Serial Number A5340
Wakili wa Serikali: Maombi hayo Ukitanyia kazi kwa namna gani
Shahidi: kama ifuatavyo, Kwanza nilijiridha Matokea ya silaha ya
naweza Kunifanya niendelee Nikaingiza parameter kwenye Mfumo Na Matokea yakwa silaha hiyo haijawahi Kusajiliwa
Wakili wa Serikali: Baada ya Matokeo hayo
Shahidi: Niliandika Barua ya Matokeo Ya Uchunguzi
Wakili wa Serikali: Uliandika kwenda Kwa nani Shahidi Kwa mwombaji aliyeomba Uchunguzi Kufanyika
Wakili wa Serikali: Ulimueleza Kitu gani
Wakili wa Serikali: Nilieleza Kwamba Kufuatia Uchunguzi uliofanyika, SILAHA HAIJAWAHI KUSAJILIWA
Wakili wa Serikali: Barua Yako uliyoandika Ukiona Utaweza Kuitambua
Shahidi: Nililetewa naweza Kuziona na Kuitambua
Wakili wa Serikali: Utaitambuaje
Shahidi: Nitaitambua Kwa Kuangalia Majina yangu Pamoja na Sahihi yani Siganture
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi anaonyesha Uwezo wa Kuutambua kwa a ridhaa ya mahakama naomba Kumuonyesha
Wakili wa Serikali: Tizama Nyaraka hii ninayokuinyesha
Shahidi: Nimeiona
Wakili wa Serikali: Mueleze Jaji Nyaraka hiyo ni Kitu gani
Shahidi: Barua niliyo andika Kuonyesha, Sahihi yangu Mwenyewe
Wakili wa Serikali: Kingine Kuna a Majina yangu Pamoja na wadhifa nilionao
Wakili wa Serikali: Unaiomba nini Mahakama
Shahidi: Ni aliomba Mahakama Kwamba Barua hii inayo onyesha Taarifa ya Kiuchunguzi Ipokelewe na Mahakama Kama Ushahidi
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi anaomba Nyaraka hii Ipokelewe
Wanapelekewa Mawakili wa Utetezi na wote wanasema hawana pingamizi Sasa anapelekwa Jaji
Jaji: Basi Tunaipokea Barua hii inayoelekezwa kwa ASP Msangi Kama Kielelezo Namba 10 JAJI naomba Shahidi Utusomee
Shahidi: Barua Kutoka Kwa Mkurugenzi wa Makosa Ya Jinai CID HQ CAR C12 VOL VII Kwenda Kwa Msangi Yahusu Kupatiwa Taarifa ya Bastola Luvern A5340 Rejea Barua Kutoka Kwa Mkurugenzi wa Makosa Ya Jinai CID HQ CAR C12 VOL VII Kwenda Kwa Msangi
Ofisi umefanya Uchunguzi Wa Silaha aina Ya Luger A5340 haikusajiliwa na Ofisi hii
Wakili wa Serikali: Barua Yako ni ya Tarehe ngapi 15/03/2021
Wakili wa Serikali: Unahusu nini
Shahidi: Kufanya Uchunguzi Wa Silaha Luger namba A5340
Wakili wa Serikali: Uchunguzi Ulikuwa unataka Kubaini Jambo Gani
Shahidi: Kubaini Taarifa ya silaha niliyoitaja Endapo Inamilikiwa na Mtu yoyote
Wakili wa Serikali: Kwa Mujibu wa Kielelezo Cha Mahakama namba 10 (Barua Yako) Matokeo ya Uchunguzi wako ni nini
Shahidi: Kumbukumbu za Silaha aina ya Bastola yenye Kumbukumbu namba A 5340 haijawahi Kusajiliwa
Wakili wa Serikali: Kwa Mujibu wa Barua Yako Kwenye Yahusu Mojawapo ya Vitu Ulivyo andika Jalada Ndani Ukirejea Kumbukumbu Namba za Barua ya aliyekuleta no ya 15 Nov 2020 Eleza Mahakama Namba sahihi hapo ni Ipo
Shahidi: Barua ambayo tuliletewa Maombi ya Kufanya Uchunguzi Ili onyesha Kumbukumbu ya Jalada husika, Ili Kumsaidia Aliyeomba Taarifa hiyo, Kwamba Inahusiana na Lile alichokiomba Kwenye Barua hii ambayo tuliipokea ni ya Tarehe 15 CID HQ SO. 63 VOL XI / 41/25, Nov 2020
Shahidi: Ukija Kumbukumbu ya Jalada ni CD/IR/2097/2021 Kwa hiyo Mheshimiwa Jaji nilichobaini hapa kwa Haraka Haraka palikuwa na Mistake ya Kiuandishi Naomba Msamaha Mheshimiwa Jaji Kwa Mapungufu ya yalijitokeza
MTOBESYA: OBJECTION. anachokifanya Shahidi hakiruhusiwi, Document inatakiwa kujieleza yenyewe na wenzetu wanajua hicho cha kumuomba msahama Jaji hakiruhusiwi kabisa.
KIBATALA: kwa kuongeza hapo kifungu 63 ya Sheria ya ushahidi na 64 (1) ya sheria ya ushahidi inazuia hapo
Wakili wa Serikali: Pamoja na Vifungu walivyorejea Vya Sheria ya Ushahidi hakuna Mahala popote ambapo Shahidi anazuiwa Kuelezea (fafanua) Ushahidi wake Na Shahidi Yupo Kizimbani na Yupo Chini na Mwongozaji wa Dodoso nafiikiri Wamesoma Vifungu bila Kujipa Muda
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji sidhani kama tunatakiwa Kujiingiza Kwenye Mambo yaliyowazi Basi tupewe Muda tulete Nyaraka, Hayo ni Mambo yapo wazi tangu tupo shule
Jaji: Nafikiri Kifungu kipo wazi Kwamba Documents Hauwezi Kufanyia Marekebisho
Jaji: Lakini anachokifanya yeye anafafanua hafanyi Marekebisho Sasa Kwenye Maamuzi Ya Mahakama itarejea hivyo Vifungu ulivyotaja
Mtobesya: Nina Mtazamo tofauti, proove ya Documents wakati huu ambapo Mahakama imeshapokea, Ndiyo tunasema Sheria inakataza
Jaji: Ndiyo sasa hiyo itafanyika wakati wa maamuzi ya Mahakama, Labda kama Una wasiwasi Mahakama haitotafsiri sheria vizuri
Mtobesya: Hapana Jaji: basi iachie Mahakama
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Shahidi ulikuwa unasema Kumbukumbu ya Jalada
Shahidi: Kumbukumbu Ya Jalada iliyopo kwenye Taarifa CD IR 2097 2021 na Ilipaswa Kusomeka CD IR 2097 2020
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwasilisha
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kabla hujamualika Mshtakiwa Wa Kwanza, kwa kuwa sisi sote wawakilishi wa washtakiwa. VIfurushi Vya Committal, Hatuna Statement ya Shahidi ili tuweze kutumia wakati wa Cross examination Na Tunatumia Maombi haya Kifungu cha 264 cha Sheria ya Ushahidi
Jaji: Serikali Mapingamizi?
Wakili wa Serikali: Hapana
Jaji: tukubaliane tuna' break kwa muda gani Mawakili wote wanateta
Kibatala: Tumekubaliana Kwa dadika 45, Turudi hapa saa 8:15
Jaji: tunahairisha mpaka saa 8:15 mchana, naelekeza Maofisa wangu wawapatie hizo nyaraka
Jaji: anatoka
Ashughulikiwe kwa kufanyiwa physical attackNajaribu ku track mwenendo wa huyu Jaji sijapenda. Anaanza kunipaashaka Sana. Huyu si mwema hata kidogo. Ana lake Jambo naliona
StupidWamfunge tu mbona ushahidi wa jamhuru umeenyooka hivyo. Kuliko hata ule wa Sabaya wa kuunga unga naa gundi. Kama hii kesi ni ya uwongo niamini kesi ya namna gani. Technologia aidanganyi bhana.
Mnasumbua tu mahakana.
hahahaahah we jamaa una majibu, jamaa atakimbia sasaKamchungulie maaa yako anaoga
Updates mkuuBaada ya jana kuahirishwa, Kesi ya mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe inaendelea kuunguruma leo mahakamani. Jana kesi iliahirishwa kutokana shahidi kupata dharura ya kiafya na upande wa utetezi haukutoa kikwazo chochote kwenye sababu hiyo. Jaji aliahirisha mpaka leo. Kuwa nami.
==============
Jaji ameingia.
Kesi inatajwa
Robert Kidando anatambulisha Jopo lake
Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza kitali
Nassoro Katuga
Esther Martin
Ignasi Mwinuka
Tulimanywa Majige
Peter Kibatala anatambulisha Jopo la mawakili wa utetezi
Peter Kibatala
John Malya
Fredrick Kiwhero
Dickson Matata
Idd Msawanga
Nashon Nkungu
Maria Mushi
Khadija Aron
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shauri lina kuja kwa ajili ya Kusikilizwa na Leo tuna shahidi Mmoja Tupo tayari kuendelea
Wakili wa Serikal: Mmoja anatoka kwenda Kumfuata
Jaji: upande wa Utetezi
Wakili Peter Kibatala: Na sisi pia tupo tayari Kuendelea
Jaji: Shahidi Wenu?
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ameenda Kufuatwa Anaingia Shahidi Mfupi Kavaa Kaunda
Jaji: Majina yako
Shahidi: SSP Sebastien Madembwe
Jaji: umri
Shahidi: 46
Jaji: Kabila
Shahidi: Mhehe
Jaji: Shughuli zako
Shahidi: Afisa wa Polisi
Jaji: Dini yako
Shahidi: Mkrito
Shahidi: Mimi SSP sebastian Madenge Naapa Kwamba Ushahidi nitakaotoa ni Kweli tupu Eeeh Mwezi Mungu nisaidie
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi Ataongozwa na Wakili wa Serikali Pius Hilla
Wakili wa Serikali: Shahidi umesema Majina yako kwa ukamilifu ni nani
Shahidi: SSP sebastian Madenge
Wakili wa Serikali: Unaishi Wapi
Shahidi: Iyumbu Kule Dodoma
Wakili wa Serikali: Mkazi wa Dodoma tangu lini
Shahidi: Mwezi wa Nane 2020
Wakili wa Serikali: Kabla ya hapo ulikuwa unaishi Wapi
Shahidi: Nilikuwa naishi Muongo la Ndege Ukonga, Nikiwa Ofisa wa Polisi Makao Makuu, iliyokuwa Makao Makuu Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Uliajiliwa lini kama Polisi
Shahidi: 02 Mwezi 09 Mwaka 1999
Wakili wa Serikali: Katika Jeshi la Polisi Upo kamisheni gani
Shahidi: Nipo kamisheni ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai
Wakili wa Serikali: Kitengo Gani
Shahidi: Udhibiti na Usajili wa Silaha
Wakili wa Serikali: Kwa Kizungu Mnaitaje
Shahidi: Arms Management and Registration Unit
Wakili wa Serikali: Kitengo hilo kina husika na Nini
Shahidi: Usajili wa Silaha za Raia Utoaji wa Leseni za Kumiliki silaha Kibali Vya Kuingiza Silaha Nchini Vibali Vya Usafirishaji wa Silaha na Risasi Hapa Nchini
Shahidi: Vibali Vya Upotoshaji wa Silaha zinazoenda Nchi mbalimbali kupitia Kwetu Tunatoa Vibali Vya Uuzaji wa Silaha na Risasi Yote yanahusiana na Usajili wa Silaha Tunahusika pia na Nchi Mbalimbali katika Udhibiti wa Silaha katika Kutekeleza Mikataba ya kikanda na Kimataifa
Wakili wa Serikali: Umesema Usajili wa Kiraia Je Unamaanisha Nini Shahidi: Ni zile Silaha zilizoruhusiwa Kwa Mujibu wa Sheria namba 02 ya Mwaka 1995 Sheria imetaja Silaha zinazoruhusiwa ni Pistol, Riffles, Short gun na Silaha yoyote ambayo Bodi ya Udhibiti wa Silaha itapendekeza iingie Miongoni Mwa silaha za Kiraia
Shahidi: Samahani Mheshimiwa Jaji, Silaha Nyingine ni Gobole
Wakili wa Serikali: Silaha Ndogo na nyepesi Fafanua hapo
Shahidi: Udhibiti Wa Silaha hizi tunazomiliki za Kiraia, Silaha Ndogo Ndogo ni zile ambazo Mtumiaji ni Mtu Mmoja. Kwa Mfano AK47 ni Silaha Ndogo Lakini Silaha Nyepesi yani Light Weapon ni Ile ambayo inatumika kwa Urahisi
Wakili wa Serikali: Kwenye Kitengo wewe ni nani
Shahidi: Ni Mrajisi Wa Leseni za Bunduki
Wakili wa Serikali: Kwa Kizungu
Shahidi: ni CEO arms Register
Wakili wa Serikali: Majukumu yako wewe ni Yapi
Shahidi: Ni Kuhakikisha kwamba napokea Maombi yote ya Waombaji wanataka Kumiliki silaha, Yaliyopitishwa na Kamati za Ulinzi na Usalama Kuanzia ngazi ya mtaa ambalo Mwombaji anaishi, Kata, Wilaya na Kamati ya Ulinzi na Usalama Ya Mkoa
Wakili wa Serikali: Jukumu la Pili..?
Shahidi: Kuyakagua Maombi hayo niliyoyapokea ilikuina kama Yana Vigezo kwa Mujibu wa Sheria, Licha ya Kwamba Maombi hayo yatakuwa yamepitishwa kwenye Kamati nilizozitaja Na Kwamba Maombi Yaliyokodhi Vigezo huendelea Kuya Shughulikia Ngazi inayofuata
Maombi Yaliyokidhi Vigezo nayarudisha yalikotoka Kutoa Vibali Vya Uuzaji wa Silaha hapa Nchini, Kibali cha Usafirishaji WA Silaha hapa Nchini na Upitishaji Vibali kwenda Nchi Jirani hasa wanatumia Bandari yetu Tunatoa Vibali Vya Kutunza Silaha (Warehouse License)
Shahidi: Tunatoa silaha Gunsmith Lisence (Kibali Cha Kufanyia Matengenezo silaha kwa Raia endapo itapata hitilafu Na Pia kutoa Leseni kwa wale waonataka Kumiliki Silaha Kutunza Kumbukumbu ya Silaha na Wamiliki wote ambao wamesajiliwa
La Mwisho ni Kupokea Maombi ya Kiuchunguzi pale silaha Inapo okotwa Ili tuweze Kuangalia Kwenye Data Base Kama Silaha hiyo imesajiliwa Au lah
Wakili wa Serikali: Mbali na Maombi hayo, Maombi Mengine huja kwa Namna gani
Shahidi: Ninapozumgumzia Uchunguzi no Uchunguzi wa Taarifa
Yoyote inayohitajika kwa ajili ya Shughuli ya Kiupelelezi, Ni Kitengo Kinacho Support Upelelezi katika Maswala ya Silaha
Wakili wa Serikali: Moja ya Jukumu umesema kutoa Vibali au Leseni za Umiliki wa Silaha Je Mchakato Ukoje Utaratibu wa Mpaka Mtu apewe Leseni
Shahidi: Wa Kwanza ni Kupokea Maombi ambayo yamepitishwa katika Kamati za Ulinzi na Usalama
Wakili wa Serikali: Kabla ya Hilo anaanza na Jambo gani Shahidi Ni Kununua Silaha, anaweza Kununua Katika Vyanzo Vitatu 1. Kwenye Duka ambalo wamepewa Leseni ya Kuuza Silaha (Lisenced Dealer)
2. Kwa Kununua kwa Mtu aliyekuwa anamiliki hiyo silaha Kihalali kwa kuandikishiana Mkataba wa Kisheria Na Kama Silaha ya Mirathi basi Kikao cha Ndugu wa Marehemu Kitakaa chini ya Mwenyekiti ambaye atakuwa amepitishwa na Mahakama Kwamba ni Msimamizi wa Mirathi kwamba ni nani wa Kuirithi Silaha hiyo Endapo wataamua Basi Mrithi anaweza Kumiliki Mwenyewe Kwa Utaratibu wa Kisheria au Kuuza Lakini Mrithi atahakikishq Kwamba Mteja anaye Muuzoa anamkabidhi Nyaraka zote za Mirathi pamoja na Mkataba walioandikishana Kisheria
3. Muombaji anaeleza Kununua Nje ya Nchi kwa Kuomba Kibali cha Kuingiza Hiyo silaha Nchini (Import Lisence) iwe Bandarini au Uwanja wa Ndege TASAKI ndiye atahusika Ku Clear hiyo silaha na Kuhifadhi wakati Muhusika ataendelea na Taratibu za Kuomba Kumiliki Silaha Hiyo
Shahidi: Kwa hiyo katika Vyanzo Vyote VitatuSilaha utatakiwa kuwa Kwenye Ghala, yeye atakuwa na Nyaraka za Mauziano ili ziweze Kumsaidia kama attachments katika Maombi yake Zipo fomu za Umiliki wa Silaha Kwa Mujibu wa Sheria na Kanuni zinaitwa Fomu A
Mwombaji hupaswa kuzijaza na Kuambatisha Nyaraka zote zinazoomyesha Chanzo cha Silaha hiyo Ata attach Fomu za Silaha hiyo, Kama Mfanya Biashara basi Leseni ya Biashara, Kitambulisho Cha Taifa na Nyaraka yoyote ile itakayodhibitisha Anamatishio Kutokana na Kazi anayofanya
Wakili wa Serikali: Inaambatana na nini hiyo fomu Ni lazima Kuwa muhtasari Kuanzia Ngazi ya Mtaa, Kata, Wilaya na Mkoa Wakili wa Serikali: Kingine?
Shahidi: Hati ya Tabia Njema inayotolewa na Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha
Kibatala: SAMAHANI Mheshimiwa Jaji Naomba Kwanza Kumuombea Wakili Jeremiah Mtobesya Aweze Kuingia Kwenye Orodha yetu Ambaye kachelewa Kwa sababu nilizotoa Mwanzoni Baada ya hayo nitaomba Sasa Wakili Mtobesya aweze kusema alichotaka
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Shahidi hana Maelezo katika Kifurushi cha Comito Kwa hiyo Ushahidi wake Hauwezi Kuingia Kwa Mujibu wa Kifungu cha 246 cha CPA Hakuna Maelezo yake, na Nimeulizana na Wenzangu Kama Upande wa Mashtaka Uliomba Mwanzoni Ombi lolote nimeambiwa Hapana
Mahakama Kimyaaaaaaa!
Upande wa mashtaka ni kama wamebutwa fulani hivi.
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Tutaomba Pia Maelekezo endapo Wenzetu watafanya Kwa Usahihi, Vipi kuhusu Ushahidi ambao Shahidi ameshaanza kuutoa hapa Mahakamani?
Mtobesya: Na ninataatifiwa hapa na kaka yangu, shahidi anatakiwa aondoke na ushahidi wake tuendelee na ushahidi Mwingine kwa Sababu hawawezi kupata faida baada ya sisi kusema kama wao hawakuomba mwanzoni Mawakili wa Serikali: Wananong'onezana Jaji anainama na kuandika
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ombi hilo halina mashiko yoyote ya kisheria
Jaji: maombi au pingamizi
Wakili wa Serikali: Ahaaa pingamizi, halina mashiko yoyote ya kisheria Sababu limeletwa katikati ya ushahidi Wa PW6 kinyume na sheria
Na Kama wangekuwa na hoja hiyo walitakiwa kufuatilia mapema, Lakini kwa wakili ambaye hakufuatilia tangu mapema proceedings hizi, Hoja yetu ya Pili ni kwamba Shahidi huyu aliorodheshwa tangu Kipindi Cha Committal Proceedings na anasomeka Kama Shahidi namba 23 tangu Mahakama Ya Hakimu Mkazi Kisutu Na hata katika Barua yetu ya 11 August 2021
Wakili wa Serikali: Ukurasa wa 32 na Jina lake linaonekana Katika 23 Labda lile neno S liondoke isomeke Sebastian
Wakili wa Serikali: Lakini Substance ilikuwa Committed na Ilisomwa Katika Mwenendo wa Shauri hilo katika Proceedings za Tarehe 23/8 Siku ambazo COMMITTAL Proceedings zilifanyika Na Jina lake limeandikwa sebastian Madembwe SSP
Lakini pia Katika Ile list ya Exhibit katika Ukurasa wa 33 Nyaraka Anayokuja Kuzungumzia imekuwa Litsted pale Namba 18 Ambayo pia imesainiwa na Sebastian Madembwe SSP nilikuwa Committed na Substance yake ilisomwa
Kwa hiyo kwa namna yoyote ile Hatukutakiwa Kuleta Ombi kupitia Kifungu cha 289 cha CPA ili Shahidi huyu aweze Kutoa Ushahidi Wake.. Na tunasema Pia Matakwa ya Rule 8 Sub 2 ya The Economic and Organized Crime Control (Corruption and Procedure Rules ya 2016),
Takwa hili la Kisheria lilitekelezwa na Mahakama. Iwe Jina ama Substance ya Ushahidi Anaotoa Leo hii hakuna Kitu Kipya kama Ambavyo wakili anajaribu Kuonyesha Mahakama yako Tukufu Na Kama hali Iko hivyo hakuna Haja Wa Kutoa Amri yoyote ile Kutokana na Ushahidi ambao Umeolewa na Shahidi Kwa sababu Shahidi Yupo Sahihi Kwa Mujibu wa sheria Hivyo Mheshimiwa Jaji tunaomba hilo Pingamizi ulitupilie Mbali ili Shahidi wetu aweze Kuendelea na Ushahidi Wake
Jaji anaandika Kidogo
Mtobesya: Kwanza Kabisa Wenzangu wameni attack, Personally Sikuwepo Kwenye Proceedings tangu Mwanzo, Mimi Kuchelewa Kufika sidhani kunaweza Kuathiri. Sisi tunachofanya hapa ni Kuisaidia Mahakama Kufanya Shughuli Zake Kwa Mujibu wa Sheria
Mtobesya: Nimesema Kwenye Committal Documents hakuna Ushahidi wa shahidi i huo. Substance inaongelea mambo matatu. 1. MAJINA Ingawa yamekosa hatuna Shida na hilo, 2 Cheti atakachotoa na 3. Hakuna Kile ambacho "Ataongea nini Mbele ya Mahakama"
Mtobesya: Tumeongea mara Nyingi kuhusu hili Kuwa kuna Sababu Ipo ya Kumpatia Mtu Nyaraka za Ushahidi kupitia Committal, Na Wasipokuwa wamefanya Upo Mlango Mwingine wa wao Kuomba kupitia Kifungu cha 289 Criminal Procedure Act
Wakili wa Serikali: Kama namwelewa Mtobesya anazumgumzia % Documents kutosomwa
Jaji: kama nimekuelewa umesema haipo kwenye Committal Bandle!
Mtobesya: Nimesema haipo kwenye Committal bundle kwa maana hiyo haijakidhi matakwa hayo ya kwenye 246 CPA
Jaji: Umeridhika na line yake ya argument sasa
Wakili wa Serikali: Hapana Sikubaliani na Mtobesya. Yeye ana argue kwamba haijasomwa, Maana akianza kujielekeza kwenye mengine na mengine inakuwa siyo sawa
Jaji: Hoja yao ni Kwamba argue kwa namna ambayo umeletea pingamizi
Mtobesya: Kwasababu Haipo ina maana haijasomwa, na kwa sababu haijasomwa inakiuka sheria aliyosoma Kaka yangu Kidando ya uhujumu uchumi na makosa ya uchumi ya mwaka 2016 Kingine Kaka Yangu anasema P. O imeletwa Kinyume na Sheria Kwa sababu Ilishapitwa
Hiyo siyo Sawa, Jambo lolote linaweza Kuibuliwa pale tu tunapoona tunaenda Kinyume na Sheria, tunalo hilo Jukumu Kama Wawakilishi wa wateja wetu na Pia kama Maafisa wa Mahakama Kwa hiyo kama ilivyoombwa Mwanzoni Mahakama Itoe Maelekezo na Kukidhi Matakwa YA Sheria. Ni hayo tu
Jaji anainama na kuandika kidogo
Jaji: Mmesikia hoja zote, Naomba nipate muda na mimi Tutarudi tena hapa saa tano na robo. Anasimama na kutoka nje ya chumba cha mahakama
Jaji alitoka Mahakamani 10:50 saa za Afrika Mashariki, akasema atarudi saa 11:15 ili akapitie sheria ambazo zimetajwa. Sasa ni saa 11:52 na bado hajarejea katika chumba cha mahakama. Tunaendelea kusubiri.
Jaji Ameingia 12:00 Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe imetajwa tena
Wakili wa Serikali: Upande wa Jamhuri tupo tayari na Hakuna Mabadiriko ya column
Kibatala: Na sisi Pia Mheshimiwa Jaji tupo vizuri
Jaji: Tuli' break Kwa muda Kwa nia ya kuandika maamuzi madogo, maamuzi yanalenga kutatua mgogoro wakati shahidi namba 06 anatoa ushahidi Mtobesya alieleza mahakama shahidi huyo anakiuka kutoa ushahidi wakati ushahidi wake haukuwa umesomwa kwenye committal mahakama ya Kisutu
Na akaeleza Kuwa hivyo Inakiuka Kifungu 246 cha Sheria 8 Sub ya CPA Sura ya 20 Na Pia GN 267/2017 na Kifungu cha 63 cha CPA na Sheria Ya Uhujumu Uchumi
Jaji: Hivyo Inakiuka Haki ya Washitakiwa na wao Kama wawakilishi Wa Washtakiwa Kutokuona Nyaraka hiyo na Pia Kwamba Haikusomwa Anaomba Mahakama imkatae SHAHIDI na Ushahidi Wake utupwe Upande wa Serikali Walikuwa na Hoja Mbili
1. HAINA Mashiko Kwa sababu Pingamizi limekuja Kwa Kuchelewa 2. Ushahidi wa Ushahidi Huo (Substance) ni sehemu ya Ushahidi tu, Mahakama Ijeielekeze Ukurasa wa 33 ambapo Inaonyesha Ushahidi Wake Ulisomwa Mahakamani
Akaongeza Kuwa Ushahidi Ambao unakuja Kutolewa Mahakamani Unakuwa Umesomwa basi Shahidi anatakiwa kuendelea Kutoa Ushahidi Wake Na Kwamba Kanuni zilifuatwa kama ambavyo imefanyika Kwenye Mahakama ya HAKIMU Mkazi Kisutu
Jaji: Mtobesya kwenye Kuhitimisha Hoja ya Serikali ya Kuchelewa haina Mashiko Yoyote, Pingamizi Linaweza Kuletwa Wakati wote wote Ni Jukumu la Upande wa Mashtaka Kutoa Nyaraka Mapema na Orodha Ya Watu wanaopangwa Kufanya Ushahidi Mahakamani
Jaji: Anaomba Mahakama Itamke Shahidi amefika Kinyume na Sheria na Ushahidi alitoa Upo Kinyume na Sheria Na Kwamba Disclosure ni kwamba Mahakama itumie Hivyo kama Msimamo wake
Jaji: Sasa Katika Hukumu nitatumia Sheria zilizotaja hapo Juu Pande Mbili wanakubaliana kuwa Malengo Mahususi Ni kwamba Ushahidi Unaokuja kutolewaa Mapema Unajulikana Mapema Ushahidi Wote Unaotakiwa Kuja Mahakama Kuu Unatakiwa Kujulikana
Moja kwa Kusomwa Kwa Kuandaliwa Kwa Mfumo wa kitabu na Kukabidhiwa Majukumu haya yanafanywa na Upande wa Mashtaka Kusambaza Ni kazi ya Mahakama Pingamizi lolote linaweza Kuja wakati wowote Pale anapogundua Kuwa kuna Mapungufu anaweza Kuleta Mahakamani
Jaji: Ni Msimamo wa sheria Kuwa pale ambapo Ushahidi unakuwa haujasomwa basi hauwezi kupokelewa mahakamani labda kama wataomba kama ilivyoelezwa na Wakili Mtobesya kwenye Kifungu cha 289 CPA Jambo linalobishaniwa ni kwamba ushahidi haukusomwa hapa mahakamani
Jaji: Mahakama inayo Jukumu la kukagua Kama Ushahidi Kama Ulisomwa au Haukusomwa Mbele Ya Hakimu Mkazi wa Kisutu wakati Wa Committal Inasomwa Mahakama Wakati Ina Examine Record Imeona Kwenye Ukurasa wa 21 Maneno Yafuatayo Kwamba Ushahidi Na Mashahidi Yamesomwa kwa Washtakiwa
Akasema Hakimu Simba Tarehe 23 08 2021 Akaorodhesha Mashahidi 21 na Jina la Shahidi Namba 06 linaonekana Katika Ukurasa wa 31 Na Kwamba Mashahidi hao waliorodheshwa na Maelezo yao yalisomwa Mbele ya mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Huo ndiyo Msimamo na Kumbukumbu za Mahakama
Kwamba Maelezo yote yalisomwa na Kwamba Ushahidi huo Ukisomwa Na Mahakama haikuishia hapo Kama Nilivyosema Katika ku' Examine Mahakama Ikaona Kuna Maelezo Ya Shahidi namba 06 Kumbe yalisomwa na Kwamba Tatizo Maelezo hayo hayakuunganishwa Katika Kifurushi cha Comito Proceedings
Jaji: Kutokwemo Katika kifurushi haimaanishi Ushahidi Wa shahidi Namba 06 haukusomwa Mahakama Inaona Pingamizi Halina Mashiko Lengo la Pingamizi Ilikuwa Ku Impeach Record za Mahakama Maelezo Yalipo Mahakamani Yana onyesha Ushahidi Ulisomwa hivyo naelekeza Sasa Shahidi Aendelee
Mawakili Wote wanamyanyuka Ishara ya Kukubaliana na Jaji
Jaji: Mara Ya Mwisho alisema huyo Mwombaji lazima awe na Cheti cha Tabia Njema kutoka Jeshi la Polisi
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Iwapo zipo Nyaraka zingine zinaambatanishwa na Maombi
Shahidi: Zile zinazo onyesha Mwombaji kuwa Upo Umuhimu wa Yeye Kumiliki Silaha Vielelezo anavyoweza Kuambatanisha ni Ile kazi anayofanya WS: Maombi ya kisha wakilishwa
Shahidi: Yakishawakilishwa kwangu nayakagua ili Kujiridhisha Kama Yanakidhi Vigezo Vilivyowekwa Kwa Mujibu wa Sheria
Wakili wa Serikali: Ka Maombi hayajakidhi Vigezo nini hufanyika
Shahidi: Mambo Mawili hufanyika 1.Yanaweza Kurudihswa Kwenye Mkoa Husika Ilikukamilisha Vigezo Vinavyokksekana 2. Endapo itaonekana Mwombaji hana Sifa zilizo ainiahwa Kisheria na Kwamba hata akirekebisba
Vigezo vianvyopungua basi Maombi hayo ubaki Makao Makuu na Mkoa unaohusika Ujulishwa kuwa Mwombaji hana Sifa
Wakili wa Serikali: Maombi Yanayokidhi Vigezo? Nimi hufanyika
Shahidi: NiKumjulisha Mwombaji Kwamba amekubaliwa
Wakili wa Serikali: Kwenye Barua hii husika Muhisika atakiwa nini
Shahidi: Mwombaji anajulishwa Kuwa Maombi yake yamekubaliwa anatakiwa kwenda Kwa Mkuu Wa Wilaya Kwenda Kukamilisha Malipo Na Baada ya Kukamilisha Malipo arudi Katika Ofisi ya Mrajisi Akiwa na Barua aliyopewa ya akumjulisha kuwa ameruhusiwa Kumiliki Silaha Kutoka Ofisi ya Mrajisi ikiwa imeambatanishwa na Risiti ya malipo Ambapo Malipo hayo hufanyika kwa mkuu wa polisi Wilaya
Wakili wa Serikali: Nini tena hufanyika Shahidi: Kama amekamilisha malipo, kinachofuata ni Hatua ya Usajili
Wakili wa Serikali: Unakamilishwaje
Shahidi: Kwa Mambo Mawili Kwanza Kwa kuipa Silaha Husika Registration Number, Central Arm Register Numbe Kwa kifupi tunaita CAA number Ambapo kitabu hicho Chenye CAA namba kitaandikwa Mambo yafuatayo Maelezo ya Silaha ambayo Muhusika ameomba
Wakili wa Serikali: yanapatikana wapi Shahidi: Kwenye Ukurasa wa Kwanza kwenye hicho Kitabu
Wakili wa Serikali: unayapata wapi Mambo ya Kujaza
Shahidi: Ile Barua ya Kumjulisha Mwombaji inakuwa na Maelezo yote Pamoja na Maelezo ya Muhusika yanaingizwa Kwemye Kitabu
Shahidi: Na Kisha Kuandika Picha Kwenye Kitabu hicho Chenye CAA Namba Nitaffungua faili na Kuingiza Document kwenye Faili Na Juu ya faili Nita andika Registration namba yani CAA namba Kwa ajili ya Kumbukumbu
Nilisha Kamilisha Sasa Kusajili Katika Mfumo wa Makaratasi namuingiza sasa Katika Electronic Data Base
Wakili wa Serikali: kwenye Mfumo ni taarifa zipi unazoingiza
Shahidi: Mfumo utanitaka Kuingiza Kwanza CAR namba
Shahidi: Mfumo utanitaka niingize aina ya silaha
Mtengemezaji kwa Maana ya Kampuni iliyotengemeza na Serial Namba Ambayo Mtengemezaji ameigonga Kwenye silaha Husika
Shahidi: Kuna parameters za Nyongeza Kama Nchi ambayo Silaha hiyo Imetengenezwa, Model Namba pamoja na Callibre Size
Hizi parameters nilizo it aja Mwishoni siyo za a Umuhimu sana Bali za Nyongeza Katika Kusaidia Utambuzi
Wakili wa Serikali: Ulizungumzia particular za Mhusika, Ni kitu gani
Shahidi: kwa Ruhusa ya Mheshimiwa Jaji, tunaingiza IDADI ya Risasi ambazo Mmiliki anaruhusiwa Kuzimiliki kwa Wakati Mmoja
Shahidi: Majina, Uraia wake, Jinsi a Yake, Kazi yake, Namba ya Kitambulisho Cha Taifa au Mpiga Kura kwa wale ambao hawana Cha Taifa, Makazi yake Tukiingiza kuanzia Mtaa, Kata anayotaka Mwombaji, Tarafa, Wilaya na Mkoa
Wakili wa Serikali: Kama Kuna Taarifa zingine mnazo ingiza kwa simu
Shahidi: namba ya Simu, anuani ya Barua pepe, Chanzo cha silaha Kama ameinunua
Wakili wa Serikali: Ukiisha Kamilisha Kuingiza Taarifa zote kwenye Mfumo Kinachofuata ni nini Shahidi Kinachofuata ni Kusave, na baada ya kubonyeza Button ya Kusave hakuna Chochote Kitakachokuwa ammended
Shahidi: Kuweka Kumbukumbu, Kurejea Kumbukumbu endapo Silaha itakuwa inatafutwa Pangine imepatikana katika Tukio la Uhalifu ili Kujua inaweza Ikawa Miomgoni Mwa silaha zilizo sajiliwa
Wakili wa Serikali: Nyaraka zipi sasa Muhusika upewa Shahidi Kwa Mujibu wa Sheria kesi ya Udhibiti wa Silaha ya Mwaka 2015 na Kanuni zake za 2016 Mmiliki anacbokabidhiwa ni Kule Kitabu
Wakili wa Serikali: Shahidi Sasa umesema kumbukumbu za Umiliki kwa Maana Hard copy na Sosty Copy, na Madhumuni ni Ka. MAOMBI ya Uchunguzi wa Silaha yatafanyika Je ni watu gani huketa Maombi
Shahidi: Sisi Upokee Kutoka Kwenye Ofisi inayopeleleza Kwenye Shauri husika
Wakili wa Serikali: Pengine ni wapi
Shahidi: Kwenye Taasisi zinazosimamia Utekelezajibwa Sheria mbalimbali Mfano tumepokea Maombi Kutoka PCCB Kutoka Nna Taasisi inayodhibiti Madawa ya Kulevya
Wakili wa Serikali: Maombi ya Uchunguzi wa Silaha Yanatakiwa Kwmuwa na nini
Shahidi: Yawe na Taarifa 03 za Msingi, Taarifa za lazima au zile za ziada Taarifa ya Kwanza iwe ni Aina ya Silaha Kingine ni Jina la Mtengemezaji (Makers name au Manufacturer name) Namba zilizohongwa na Mtengenezaji (Manufactural serial number) Itatuwezsha Kujua hii silaha Imesajiliwa au Haikusajiliwa
Wakili wa Serikali: Unapopokea Maombi kama hayo unafanyia Nini
Shahidi: Kwanza Tunagongq Muhuri kwamba tumepokea Baada ya hapo tunaanza Kufanyia Kazi
Wakili wa Serikali: Kwa namna gani
Shahidi: Kwa Kuingiza Parameters ya Yale a Maombi katika Mfumo Sababu Parameters ni Unique hata Kama Silaha zimetemgezwa NA Mmiliki huyo huyo bado pan kuwa hakuna Coalition
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kinafanyika Kuwa na Unique Serial Number
Shahidi: Hawa watenhenezajonwanakutana Kupeana kuhusu Serial number na Kuhakikisha Namba haziingiliani
Wakili wa Serikali: Mkishaingiza kwenye parameter kwenye mifumo
Shahidi: Na Click Okey Kama Silaha Imesajiliwa itaketa amatokeo Chanya na ninaweza Sasa Kwenda Kwenye Hard Copy
Wakili wa Serikali: Matokea Hasi ni Yapi
Shahidi: Nilipo ingiza Parameters na Mfumo Kutafuta Nakubaini Hakuna Kumbukumbu zozote katika Mfumo huo
Wakili wa Serikali: Mwisho wa Siku unafanya nini Shahidi Kama Matokeo Chanya Nafanya Mambo Mawili kwenye Taasisi iliyooomba Uchunguzi ufanyike
Nita Print Out Mfumo Umetuleeza Hivi na Itakuwa Kiambatisho Katika Barua Yangu Kama Matokeo Yatakuwa Hasi itaandikwa Barua na Haoatakuwa na Printout Yoyote
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama tarehe 25 Nov 2020 ni Kitu gani Kilitokea
Shahidi: Nikiwa Ofisini Kwangu Makao Makuu Dodoma Nilipokea Barua ya Kufanya Uchunguzi Silaha aina ya Bastola
Wakili wa Serikali: Ilitoka Wapi
Shahidi: Makao Makuu Madogo Police Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Idara Gani
Shahidi: Idara ya Upelelezi Makosa ya Jinai Barua ilinitaka Kufanya Uchunguzi wa Aina Ya Silaha Bastola Mtengenezaji ni Luger na Serial Number A5340
Wakili wa Serikali: Maombi hayo Ukitanyia kazi kwa namna gani
Shahidi: kama ifuatavyo, Kwanza nilijiridha Matokea ya silaha ya
naweza Kunifanya niendelee Nikaingiza parameter kwenye Mfumo Na Matokea yakwa silaha hiyo haijawahi Kusajiliwa
Wakili wa Serikali: Baada ya Matokeo hayo
Shahidi: Niliandika Barua ya Matokeo Ya Uchunguzi
Wakili wa Serikali: Uliandika kwenda Kwa nani Shahidi Kwa mwombaji aliyeomba Uchunguzi Kufanyika
Wakili wa Serikali: Ulimueleza Kitu gani
Wakili wa Serikali: Nilieleza Kwamba Kufuatia Uchunguzi uliofanyika, SILAHA HAIJAWAHI KUSAJILIWA
Wakili wa Serikali: Barua Yako uliyoandika Ukiona Utaweza Kuitambua
Shahidi: Nililetewa naweza Kuziona na Kuitambua
Wakili wa Serikali: Utaitambuaje
Shahidi: Nitaitambua Kwa Kuangalia Majina yangu Pamoja na Sahihi yani Siganture
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi anaonyesha Uwezo wa Kuutambua kwa a ridhaa ya mahakama naomba Kumuonyesha
Wakili wa Serikali: Tizama Nyaraka hii ninayokuinyesha
Shahidi: Nimeiona
Wakili wa Serikali: Mueleze Jaji Nyaraka hiyo ni Kitu gani
Shahidi: Barua niliyo andika Kuonyesha, Sahihi yangu Mwenyewe
Wakili wa Serikali: Kingine Kuna a Majina yangu Pamoja na wadhifa nilionao
Wakili wa Serikali: Unaiomba nini Mahakama
Shahidi: Ni aliomba Mahakama Kwamba Barua hii inayo onyesha Taarifa ya Kiuchunguzi Ipokelewe na Mahakama Kama Ushahidi
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi anaomba Nyaraka hii Ipokelewe
Wanapelekewa Mawakili wa Utetezi na wote wanasema hawana pingamizi Sasa anapelekwa Jaji
Jaji: Basi Tunaipokea Barua hii inayoelekezwa kwa ASP Msangi Kama Kielelezo Namba 10 JAJI naomba Shahidi Utusomee
Shahidi: Barua Kutoka Kwa Mkurugenzi wa Makosa Ya Jinai CID HQ CAR C12 VOL VII Kwenda Kwa Msangi Yahusu Kupatiwa Taarifa ya Bastola Luvern A5340 Rejea Barua Kutoka Kwa Mkurugenzi wa Makosa Ya Jinai CID HQ CAR C12 VOL VII Kwenda Kwa Msangi
Ofisi umefanya Uchunguzi Wa Silaha aina Ya Luger A5340 haikusajiliwa na Ofisi hii
Wakili wa Serikali: Barua Yako ni ya Tarehe ngapi 15/03/2021
Wakili wa Serikali: Unahusu nini
Shahidi: Kufanya Uchunguzi Wa Silaha Luger namba A5340
Wakili wa Serikali: Uchunguzi Ulikuwa unataka Kubaini Jambo Gani
Shahidi: Kubaini Taarifa ya silaha niliyoitaja Endapo Inamilikiwa na Mtu yoyote
Wakili wa Serikali: Kwa Mujibu wa Kielelezo Cha Mahakama namba 10 (Barua Yako) Matokeo ya Uchunguzi wako ni nini
Shahidi: Kumbukumbu za Silaha aina ya Bastola yenye Kumbukumbu namba A 5340 haijawahi Kusajiliwa
Wakili wa Serikali: Kwa Mujibu wa Barua Yako Kwenye Yahusu Mojawapo ya Vitu Ulivyo andika Jalada Ndani Ukirejea Kumbukumbu Namba za Barua ya aliyekuleta no ya 15 Nov 2020 Eleza Mahakama Namba sahihi hapo ni Ipo
Shahidi: Barua ambayo tuliletewa Maombi ya Kufanya Uchunguzi Ili onyesha Kumbukumbu ya Jalada husika, Ili Kumsaidia Aliyeomba Taarifa hiyo, Kwamba Inahusiana na Lile alichokiomba Kwenye Barua hii ambayo tuliipokea ni ya Tarehe 15 CID HQ SO. 63 VOL XI / 41/25, Nov 2020
Shahidi: Ukija Kumbukumbu ya Jalada ni CD/IR/2097/2021 Kwa hiyo Mheshimiwa Jaji nilichobaini hapa kwa Haraka Haraka palikuwa na Mistake ya Kiuandishi Naomba Msamaha Mheshimiwa Jaji Kwa Mapungufu ya yalijitokeza
MTOBESYA: OBJECTION. anachokifanya Shahidi hakiruhusiwi, Document inatakiwa kujieleza yenyewe na wenzetu wanajua hicho cha kumuomba msahama Jaji hakiruhusiwi kabisa.
KIBATALA: kwa kuongeza hapo kifungu 63 ya Sheria ya ushahidi na 64 (1) ya sheria ya ushahidi inazuia hapo
Wakili wa Serikali: Pamoja na Vifungu walivyorejea Vya Sheria ya Ushahidi hakuna Mahala popote ambapo Shahidi anazuiwa Kuelezea (fafanua) Ushahidi wake Na Shahidi Yupo Kizimbani na Yupo Chini na Mwongozaji wa Dodoso nafiikiri Wamesoma Vifungu bila Kujipa Muda
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji sidhani kama tunatakiwa Kujiingiza Kwenye Mambo yaliyowazi Basi tupewe Muda tulete Nyaraka, Hayo ni Mambo yapo wazi tangu tupo shule
Jaji: Nafikiri Kifungu kipo wazi Kwamba Documents Hauwezi Kufanyia Marekebisho
Jaji: Lakini anachokifanya yeye anafafanua hafanyi Marekebisho Sasa Kwenye Maamuzi Ya Mahakama itarejea hivyo Vifungu ulivyotaja
Mtobesya: Nina Mtazamo tofauti, proove ya Documents wakati huu ambapo Mahakama imeshapokea, Ndiyo tunasema Sheria inakataza
Jaji: Ndiyo sasa hiyo itafanyika wakati wa maamuzi ya Mahakama, Labda kama Una wasiwasi Mahakama haitotafsiri sheria vizuri
Mtobesya: Hapana Jaji: basi iachie Mahakama
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Shahidi ulikuwa unasema Kumbukumbu ya Jalada
Shahidi: Kumbukumbu Ya Jalada iliyopo kwenye Taarifa CD IR 2097 2021 na Ilipaswa Kusomeka CD IR 2097 2020
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwasilisha
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kabla hujamualika Mshtakiwa Wa Kwanza, kwa kuwa sisi sote wawakilishi wa washtakiwa. VIfurushi Vya Committal, Hatuna Statement ya Shahidi ili tuweze kutumia wakati wa Cross examination Na Tunatumia Maombi haya Kifungu cha 264 cha Sheria ya Ushahidi
Jaji: Serikali Mapingamizi?
Wakili wa Serikali: Hapana
Jaji: tukubaliane tuna' break kwa muda gani Mawakili wote wanateta
Kibatala: Tumekubaliana Kwa dadika 45, Turudi hapa saa 8:15
Jaji: tunahairisha mpaka saa 8:15 mchana, naelekeza Maofisa wangu wawapatie hizo nyaraka
Jaji: anatoka
Huyu shahidi leo sijui hata kama atatamani unyumba home kwakeNi break tu au shahidi kakimbia!
WAKILI WA UTETEZI JOHN MALYA ANAMALIZIA SASA.Updates mkuu