====================
Jaji ameingia..
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire na Wenzie imetajwa
Jaji: Wakili wa Mshtakiwa wa kwanza
Mtobesya: Shahidi Unakumbuka Ushawahi Kuandika Maelezo Polisi
Shahidi: Nakumbuka
Mtobesya: Unakumbuka Uliyasoma Maelezo Yako na Ukahakikisha Kwamba ni sahihi
Mtobesya: Unakumbuka Uliandika Siku gani ya Tarehe Ngapi Mwezi na Mwaka
Shahidi: 20 Mwezi 03 Mwaka 2021
Mtobesya: Kuanzia wakati huo Mpaka Sasa ni Muda gani umepita?
Shahidi: Miezi Saba
Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema wakati Unaandika Memory Yako ilikuwa sahihi wakati unaandika Maelezo yako ulikuwa Umesha andika Barua Iliyopokelewa Kama Kielelezo Namba 10?
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Uliongelea pia Kuhusu hiyo Barua
Shahidi: Rudia Swali tafadhali
Mtobesya: Kwenye Maelezo Yako Unakumbuka Uliongelea Barua Uliyoitoa, Lakini hukukumbuka Wakati Ule kama Ulikosea Jalada Namba Umekuja Kukumbuka Leo?
Shahidi: Kwenye Maelezo Yangu nilikuwa nimesimamia kazi ya kile nilichokifanya Kuhusu Uchunguzi Enheeeeeeee..
Mtobesya: Malizie hiyo Enheeeeeee
Shahidi: Sikuiangalia
Mtobesya: Barua yenye Matatizo ya Kiuandishi ndiyo hiyo hiyo ulikuwa unaielezea
Shahidi: Tatizo la Kiuandishi lilikuwa Kwenye Jalada
Mtobesya: Ndiyo nakuuliza sasa Barua yenye Matatizo ya Kiuandishi Ndiyo hiyo uliyoifanyia Uchunguzi
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Ulitaja Mapungufu ya Barua yako
Shahidi: Sikumbuki Kama nilitaja
Mtobesya: Mheshimiwa Naomba Original Statement ya Shahidi aweze Ku' refresh Memory
Mawakili wa Serikali Wanaitafuta Bado
Mtobesya: anampatia Shahidi
Mtobesya: angalia Kama haya Ndiyo Maelezo ya Kwako Uliyoyaandika Polisi Kama ni ya Kwako kwa Mujibu wa Kesi hii
Shahidi: Ndiyo yenyewe
Mtobesya: Soma yote kwa Sauti ilituone Kama Kuna sehemu Uliomba Kurekebisha
Jaji: Sorry Kwani alisema yeye aliandika?
Mtobesya: alisema Hakumbuki
Nimemwambia asome tusikie Kama alisema. Unless kama Mahakama ina maoni tofauti aseme Hakuna tuishie hapo
Jaji: anaposema hakumbuki, naona ungem' lead labda, Kusema asome statement Yote naona Mhhhh Sijui lakini
Shahidi: Kwenye Maelezo CD IR 2097 2020
Mtobesya: Unasoma Wapi
Shahidi: Juu kabisa
Mtobesya: Tupo Chini hapo Ndiyo kwenye Content yako
Shahidi: Hakuna Sehemu niliyoandika
Mtobesya: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kwamba Katika Maelezo Yako hiyo Kumbukumbu namba
Shahidi: Nakumbuka ilikuwa 15 March 2021 Baadae nikaja Kuandika Maelezo, kwa hiyo Makosa ya Kibinadamu tu
Mtobesya: Kwa hiyo Kipengele hicho kwenye Maelezo yako kipo au Hakipo
Shahidi: Hakipo
Mtobesya: Umesema Ulifanya kazi Kwa Kutumia Mfumo, Je uliweza Ku' Demonstrate namna huo Mfumo unafanya Kazi
Shahidi: Issue ya Kuwaita watu ili waweze Kushuhudia ninachokifanya ni suala lingine
Mtobesya: Je Uliwahi Kufanya?
Shahidi: Ndiyo Mara yangu ya kwanza
Jaji: Kuna sehemu hamuelewani naona
Mtobesya: labda Nirudie Swali
Ulionyesha Wakati Unaelekezwa na Wakili wa Serikali namna Mfumo unavyofanya kazi
Shahidi: Sikuonyesha
Ni mallya anasimama
Mtobesya amemaliza, anaketi, anasimama John Mallya
Mallya: Dhumuni la Usajili wa Silaha ni Kudhibiti Silaha isifanye Uhalifu
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kwa hiyo wewe Ulipewa silaha Kuchunguza ni Rahisi Kujua Kama ilifanya Uhalifu
Shahidi: Mie naletewa Kuchunguza Silaha ni ya nani
Mallya: Sasa ulisema Hapa Mahakamani Leo kuwa Results ni No Records?
Shahidi anatoa Macho tu hajibu swali, anashangaa
Mallya: Mheshimiwa Jaji nasubiri Jibu
Shahidi: nilicho present Leo ndiyo kilichokuwepo
Mallya: Kwa hiyo umeleta au hujakileta
Shahidi: Hakipo
Mallya: Umeingia Polisi Ukiwa na Miaka 24
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kwa hiyo unauzoefu Wa Miaka zaidi ya 20
Shahidi: Ndiyo
Mallya: hiko Kitengo Unamuda nacho gani
Shahidi: Miaka 20
Mallya: Ulipata Kujua hiyo silaha imepatikana wapi
Shahidi: hiyo siyo Kazi yangu
Mallya: Kwa hiyo wewe unatolea Majibu ya Uchunguzi Silaha iliyosajiwa tu?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Ulizungumzia Ufanisi wa huo Mfumo wakati unaongozwa
Shahidi: Data base Ipo Vizuri na ina Speed
Mallya: Ulizungumzia hilo suala
Shahidi: Sikuzungumzia
Mallya: Nilikusikia Kwamba Ukibonyeza Save, huwezi Kufuta bila Ruhusa ya Admin
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Je Kama hukueleza Admin Ndiyo Mwenye Mandate Vipi Kama Admin Alibadilisha umiliki wa Silaha Ya Kingai aweze Kumbambikia Mtu
Shahidi: Adimn hana Mandate ya Moja Kwa Moja
Mallya: Sasa Unabadili Ushahidi Wako?
Shahidi: Hapana Kuna mambo Sikuulizwa
Mallya: Je ulielezea namna Admin anavyotoa ruhusa
Shahidi: Sikueleza
Mallya: Ulisema Pia Kuna Taarifa Unazitumia katikati, Je ulipata Mazingira ya Serial Namba Kufuta na wahalifu
Shahidi: Ni sahihi
Mallya: Mwambie Mheshimiwa Jaji Sasa Namna kama hiyo inaweza kujitokeza
Shahidi: Endapo Parameters Zimefutwa tunashirikiana na watu wa Ballistic
Mallya: Kwa hiyo tunakubaliana Parameters Zako siyo Kitu Pekee cha kutambua Silaha
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kwa hiyo Ulielezea wakati Unaulizwa
Shahidi: Hapana Sikueleza
Mallya: umewahi Kupata Mazingira ambapo namba imefojiwa kutoka namba 04 kwenda namba 07
Shahidi: Unajua kwa Mazingira yangu
Mallya: Jibu swali Shahidi
Shahidi: Issue za Ku temper hatujazishuhudia
Mallya: Ulieleza Kwamba Uliletewa Barua tu siyo Bastola
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kwa hiyo Ujajisumbua Kama namba ulizo letewa zilikuwa tempered
Shahidi: Siyo Jukumu langu
Mallya: Unafanya Kazi Siku Ngapi katika wiki
Shahidi: Maasa 24 kwa Siku Saba
Fedrick Kihwelo sasa
Fredrick Kihwelo: Ni kweli tarehe 25 ulipokea Barua Kutoka kwa ASP Msangi
Shahidi: Ndiyo nilipokea
Fredrick: Mpo wangapi Kwenye hicho Kitengo
Shahidi: Tupo 20
Fredrick: Barua ya ASP Msangi Ilikuwa inakutaka Ufanye nini
Shahidi: Kutoa Majibu ya Umiliki
Fredrick: Wewe Ulitoa Taarifa ya Umiliki au Uchunguzi
Shahidi: Nilifanya Uchunguzi nikatoa Taarifa ya Umiliki
Fredrick: Barua Yako ya majibu ni ya Uchunguzi au Umiliki
Shahidi: Umiliki
Fredrick: Ni sahihi Mnafanyia Uchunguzi Siku hiyo hiyo Mnapopokea Barua
Shahidi: Ndiyo
Fredrick: Wewe Ulipokea Barua Siku gani 25 /11/2020, ukatoa majibu lini?
Shahidi: 15 March 2021
Fredrick: Ni Muda gani umepita
Shahidi: Miezi 05
Fredrick: Je Katika Majukumu yako ulitaja Jukumu lako la Kutaja Umiliki
Shahidi: Hapana
Fredrick: Ni kweli Kuna Njia 2 za Kumiliki Silaha?
Shahidi: swali sijaelewa
Fredrick: Katika Maelezo Yako ulisema Mtu anaweza Kumiliki Silaha Kwa Njia ya Kuingiza ndani ya Nchi, Kununua Ndani ya Nchi na Kama amerithi, Sasa Nakuuliza Je kuna namna Mbili tu za Kumiliki Silaha
Shahidi: Si kweli
Fredrick Kihwelo anaketi na anasimama Peter Kibatala
Kibatala: Kielelezo Cha Mashtaka namba 10 umetaja Barua ya Tarehe 25 Nov Mwaka 2020 aje ni sahihi Kwamba Barua hii Ndiyo Chanzo Chote cha wewe Kuandika Barua
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba bila Barua hiyo wewe Usingeandika hiyo Barua
Shahidi: Ndiyo sahihi Kabisa
Kibatala: Siyo Kawaida yako kuandika tu barua
Shahidi: itakuwa Kinyume na kazi.
Kibatala: Je hiyo Barua iliyokufanya Uandike Barua Umekuja nayo?
Shahidi: Si kuja nayo Lazima aionyeshe mahakama msingi wa yeye kuandika hiyo barua si vinginevyo maana yake atakuwa ameitunga tu
Kibatala: kwa Ufahamu wako wewe ni Muhimu au Siyo Muhimu
Shahidi: kwa Upande wangu sikuona Umuhimu wa Kuja nayo
Kibatala: na Kwa hiyo Barua ndimo ambapo tungepata Details za Hiyo Bunduki ambayo wewe Ulipswa Uifanyie Uchunguzi
Shahidi: Sahihi Kabisa
Kibatala: na Ndiyo humo tungeona Namba CZ 100,Callibre 9mm hatuwezi Kuona Popote zaidi ya hiyo Barua
Shahidi: Sahihi kabisa
Kibatala: hujazungumza kabisa Kuhusu CZ 100 9MM za Ulikuwa unachunguza kwenye hiyo Barua Uliyoandikiwa
Shahidi: Sahihi Kabisa
Kibatala: sahihi Kabisa hujazungumza Kuhusu CZ 100, Callibre 09mm
Shahidi: Sahihi sikuzungumzia
Kibatala: Kuhusu Electronic Data Base Ulizungumza Kuhusu Mmiliki wa Risasi
Shahidi: Kwenye electronic Data Base inaonyesha kuwa Idadi ya Risasi za kutumia wakati wa Uhai wa Leseni
Kibatala: Je Katika huo Mfumo Usajili wa Bunduki na Risasi ni Kitu kimoja au tofauti
Shahidi: Ni Kitu Kimoja
Kibatala: Kwa hiyo Ni kisha Sajiliwa Bunduki naona na Risasi zilizopo..?
Mfano TRA Umiliki wa Gari Unaonyesha na Kiasi cha Mafuta Kilichomo
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kwa hiyo Mfano niondoe
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Risasi zinasajiliwa..?
Shahidi: Hazisajiliwi
Kibatala: Na hujazungumza kuhusu Risasi
Shahidi: Sijazungumza
Kibatala: na wala Kwenye Barua p10 hujazungumza kuhusu Risasi
Shahidi: Ni sahihi Kabisa
Kibatala: Kuna swali umeulizwa kuhusu Umiliki Possession, Je Mtu aki import Bunduki inakwenda Wapi
Shahidi: Lisenced Warehouse
Kibatala: Wewe Katika System Yako Muda huo Inasomeka nini
Shahidi: Muda huo inakuwa haijaingizwa Kwenye Mfumo
Kibatala: Ulisema Chochote a kuwa Inawe zekana Bastola Ile Inaweza Kuwa Imetoka Lisenced Warehouse
Shahidi: Sikusema Chochote
Kibatala: Ulisema hiyo Possibility kwenye hiyo Barua yako
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Ulitaka Jaji akusamehe Kwa Makosa ya Kumbukumbu namba, Je ni sahihi Kwamba ili tukusamehe ni lazima marekebisho yako tuangalie Kwenye Barua (mama) ambayo yenyewe ndiyo ina mwaka sahihi
Shahidi: Sahihi Kabisa
Kibatala: Barua hujaitoa Mahakamani
Shahidi: sahihi Kabisa
Kibatala: Kwa hiyo sasa Msamaha wako Unaelea kwa sababu hatuna Control
Shahidi: Ni sahihi kabisa
Kibatala: hii Barua Yako inaonekana Ulikuwa unaipeleka ASP H. MSANGI, Je Kuna Mtu anaitwa Inspector Swila, Je Ulimtaja
Shahidi: Sikumtaja
Kibatala: Kwa hiyo akisema Inspector Swila Kuwa yeye Ndiyo aliyeandika hiyo Barua atakuwa anasema ni Uongo
Shahidi: Mimi nilipewa na ASP H. MSANGI
Kibatala: ASP H. MSANGI Hukum' Adress kwa Bahati Mbaya, Ni Kwa sababu Yeye ndiye alikuandikia Barua Mama, akija Inspector Swila kasema Ulimpelekea Majibu ya Uchunguzi atakuwa Muongo
Shahidi: Mimi Najua ASP H. Msangi
Kibatala: Wakati Unaandika Barua Ofisi yako ilikuwa Chini ya Mkurugenzi ya Makosa ya Jinai
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ni sahihi wewe na Msangi Mlikuwa Mpo wote Chini ya Mkurugenzi wa Makosa Ya Jinai
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kama Serial Namba ikichezewa Ikafutwa Je hilo ni Jukumu la nani
Shahidi: Jukumu la Ballistic
Kibatala: Umesema ulipokea Barua Ukagonga Barua na Utaratibu Wa Kupokea Barua lazima Pawe na Kitabu Kama Ili Sajiliwa Kuingia Ofiini kwenu
Shahidi: Ikihitajia nitaileta
Kibatala: Lakini Hapa hujaitoa
Shahidi: Hapa Sijaitoa
Unaileta wapi bwana hatutaki kitu kipya sisi
Kibatala: Ulitoa Maelezo Kwa Jaji kwanini Hiyo Register hukuleta Kama Sababu ni Nzito au Kubwa
Shahidi: Sababu Sikutoa
Kibatala: ulisema kwamba Result ni Negative
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je ulifafanua Kwa Jaji Kwanini Hukuleta hiyo Negative Results
Shahidi: Sikufafanua
Kesi za kijinga kijinga kabisa si wafute tu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Ushahidi Wako Lazima Upitie Sehemu kadhaa, Mahakama lazima Ipime Ushahidi wako
Shahidi: Hiyo nafahamu
Kibatala: Mwambie Sasa Mheshimiwa Jaji Kama Ulifafanua kwanini ulishindwa a kuleta Extract ya Negative Result
Shahidi: Sikufafanua
Kibatala: Nilisikia Kwamba Kuna Typing Error Kwenye P10
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Sasa Mahakama Itajuaje Kama Hakuna tena Makosa ya Kibinadamu humu?
Shahidi: Ni Jukumu la Mahakama Sasa Kupima
Kibatala: Kuna Sheria Yoyote au Kanuni yoyote ambayo inasema usilete Barua Mama, Report iwe Inajitegemea
Shahidi: Hakuna
Kibatala Ni wewe tu Uliamua
Shahidi: Kimyaaaaaaaaa
Kibatala: Swali langu la Mwisho
Kibatala: Unakubaliana na Mimi Kuwa hakuna Kosa Linajitegemea Kumiliki Silaha Bila Kibali
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Sheria Inaitwaje
Shahidi: Inaitwa Sheria ya Umiliki na Udhibiti wa silaha Kifungu cha 20
Kibatala: Mheshimiwa Jaji sina Mengine
WS: Shahidi Umeulizwa Maswali Mengi kuhusiana na Barua Mama, Uliposema Hukuona Umuhimu ulimaanisha nini
Shahidi: Ile ilikuwa Inaonyesha Guidance Ya Uchunguzi Ninaopaswa Kufanya
Baada ya Kukamilisha Kwangu Sikuona kama Kuna Ulazima wa Kuleta Ile Barua
WS: Uliona Umuhimu kitu gani
Shahidi: Taarifa ya Uchunguzi
WS: Ieleze Mahakama Ulifanya Kazi Jambo gani
Shahidi: Particulars nilizozitumia Kutoka Kwenye Barua Mama, Ndiyo Key Issues Katika Uchunguzi wa Umiliki wa Silaha
WS: Elezea Kuhusu Tukio la Uhalifu
Kibatala: OBJECTION hayo ni Mambo Mapya
Shahidi: Tunapopokea Taarifa hizo Majibu Kwamba Ni Chanya, Data Base Inaonyesha Silaha Inamilikiwa na Mtu fulani tuna Command Button, Kisha Report Inatoka
Mallya: OBJECTION hiyo ni fact Mpya tunapinga
WS: Mheshimiwa Jaji sijui lakini ni Maoni yetu Kwamba Cross examination ndiyo imeibua Extract Kuhusu Negative Results
Ameulizwa hiyo, Shahidi aachwe aeleze
Kama Wakili angeona siyo Issues Sana alipaswa asiibue
Ni hayo tu, Tunaomba Shahidi ajibu
Kibatala Wakili hakatai Those are Neww matters anajaribu Ku Exclude New Matters
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Sahamani, halafu Hakuongelea Printabiliy ya Negative Results
Jaji: Hoja Mmelewa ya Upande wa Utetezi?
Hapa anakuja na Ufafanuzi Kwamba Siku weza Ku' command
Ila Print na Mimi nakubaliana nao Kwamba hilo ni Jambo Jipya ambalo hakuzungumza na Sasa anataka Kuzungumza
Wakili wa Serikali: Shahidi Nitakuuliza suala hilo hiyo kama Majibu yakiwa Negative guwezi Kuprint, Kwanini sasa!?
Wakili wa Serikali: Shahidi Nitakuuliza suala hilo hilo kama Majibu yakiwa Negative huwezi Kuprint, Kwanini sasa?
Shahidi: Ukikomand ina Print........
Mallya OBJECTION
Kibatala OBJECTION
Mtobesya OBJECTION
Jaji: nafikiri unaweza Kwenda Kwa njia Nyingine
WS: Nilisikia Umeulizwa kuhusu Inspector Swila kwamba Ile Barua Mama Kaandika Nani
Shahidi: ASP H. MSANGI
WS: Kwamba Ile Barua Mliandikiana Wenyewe, Hebu fafanua
Shahidi Ni sahihi Kabisa Kwamba Vitengo Vyote Vipo kwa DCI, Yeye kazi yake ni Kuhakikisha Je tuna Mfumo, linapokuja suala la Kiuchunguzi yeye hausiki tena
Ofisi yangu ya Mrajisi Kama Mtaalamu wa Kufanya Uchunguzi ni Kufanya Uchunguzi Bila Kuingiliwa na Maamuzi au Msukuko wowote wa Mkurugenzi wa Makosa Ya Jinai
WS: Uliulizwa kuhusu forgery, ELEZEA Mahakama Ulichunguza nini
Shahidi: Mimi Sikuletewa Silaha nilichunguza Barua na Particulars Zilizokwepo kwenye Zile Barua zilikuwa ni Key Parameters zilizoniwezesha Mimi Kufanya Uchunguzi
Sasa kama wewe hukuletewa SILAHA na uliletewa BARUA uichunguze kwanini hiyo BARUA uliyoichunguza hukuionyesha mbele ya mahakama ???
WS: Uliulizwa pia kuhusiana na Silaha inayoingizwa Nchini kutoka nje, wewe Maelezo yako hayajaondoa possibility
Shahidi: Mfumo wetu wa Silaha na Usajili, Mfumo wetu Unamuingiza Mwishoni kabisa baada ya silaha Imeshaingia Nchini au Kukamilisha Utaratibu wa malipo
WS: Mheshimiwa Jaji Mimi naishi hapo Kama Kuna Wenzangu waendeleeeee
WS: Wenzangu na wao hawana kitu
Jaji: Shahidi tunakushukuru, unaweza Kuendelea
WS: Ndiye Shahidi Tuliyekuwa naye Leo, Tunaomba Hairisho Hadi Kesho Tuweze Kuendelea na Shahidi Mwingine
Jaji: Upande wa Utetezi
Kibatala: hatuna Pingamizi
Jaji anaandika, Mahakama ipo kimya
Jaji: Maombi yaliyoletwa na mashtaka mahakama inakubali mpaka kesho Saa 3 asubuhi
Upande wa Mashtaka mnaelekezwa kuleta mashahidi. washtakiwa wataendelea kuwa chini ya magereza mpaka kesho