Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

mzee, hii kampeni yao haijaanza jana wala leo, na wataiendeleza milele, mbaya ni kwamba watu washastuka and its never too late wimbi kugeuka na kuwaandama wao !

tuwafuatilie mpaka hii forum iwe upande wa watanzania ambao walimchagua Kikwete. Kada na wanaccm wengine hapa tuungane hapa ili tuondoe huu uchuro wa kuisakama ccm hapa.
 
tuwafuatilie mpaka hii forum iwe upande wa watanzania ambao walimchagua Kikwete. Kada na wanaccm wengine hapa tuungane hapa ili tuondoe huu uchuro wa kuisakama ccm hapa.

...country comes first sio chama chenu cha majambazi,na signature yako is just disgraceful...utaifa sio chama na JK sio Raisi wa CCM!
 
...country comes first sio chama chenu cha majambazi,na signature yako is just disgraceful...utaifa sio chama na JK sio Raisi wa CCM!

naona bado kuna wachache wenye moyo wa kupigana hapa. Its payback time, ccm wanajibu mapigo hapa na chadema mkome tena.
 
naona bado kuna wachache wenye moyo wa kupigana hapa. Its payback time, ccm wanajibu mapigo hapa na chadema mkome tena.

Masaka! Naomba uelewe kitu kimoja, unaweza ukadhani mtu ambaye hamsifi au akimkosoa Kikwete na chama chako basi ni upinzani, lakini naomba nikupe elimu kidogo kuhusu siasa. Huwa kuna kundi la watu wanaoitwa independents.

Hawa ni watu wasiofungamana upande wowote na si mashabiki, wanaangalia hali ya siasa na kufanya maamuzi yanayoendana na utashi wao yaani they vote according to their conscious.

Sasa ikija kwa siasa za Bongo, mimi ni independent, lakini anachokifanya Muungwana na jopo lake la washikaji hakikubaliki, si tu na mimi bali watanzania wenzangu wengi ninaoongea nao kila siku. hivyo acha ushabiki na leta hapa hoja za maana si kutaka kuleta ubabe. Ubabe wa CCM tumeuchoka, na mark my words in 2010 this will be the end of CCM. Kwa sababu watanzania tumechoka.

We unataka eti kuisafisha chama chako na rais wenu, basi anza na kujikosoa siyo kuficha maovu na kusema 'we are the best'! Acknowledge your mistakes then take steps to rectify the problems, instead of sticking your head in the sand. Na huyo Jk mwelezeni ukweli siyo kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa!
 
Masaka! Naomba uelewe kitu kimoja, unaweza ukadhani mtu ambaye hamsifi au akimkosoa Kikwete na chama chako basi ni upinzani, lakini naomba nikupe elimu kidogo kuhusu siasa. Huwa kuna kundi la watu wanaoitwa independents. Hawa ni watu wasiofungamana upande wowote na si mashabiki, wanaangalia hali ya siasa na kufanya maamuzi yanayoendana na utashi wao yaani they vote according to their conscious. Sasa ikija kwa siasa za Bongo, mimi ni independent, lakini anachokifanya Muungwana na jopo lake la washikaji hakikubaliki, si tu na mimi bali watanzania wenzangu wengi ninaoongea nao kila siku. hivyo acha ushabiki na leta hapa hoja za maana si kutaka kuleta ubabe. Ubabe wa CCM tumeuchoka, na mark my words in 2010 this will be the end of CCM. Kwa sababu watanzania tumechoka.
We unataka eti kuisafisha chama chako na rais wenu, basi anza na kujikosoa siyo kuficha maovu na kusema 'we are the best'! Acknowledge your mistakes then take steps to rectify the problems, instead of sticking your head in the sand. Na huyo Jk mwelezeni ukweli siyo kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa!

wewe kidoogo naona umeeleweka ! na hapo tupo pamoja ! sitokupinga !
 
Freeman Mbowe una undugu na Nyerere jamani, mbona wanaranda wajihi wao, najua watu wengi wanarandana hapa duniani, just curious to know about Freeman and JK nyerere

mhm ! mie sikujua hili !
 
Kama Mbowe alisema haijamchukulia hatua?

Membe kasema eti serikali haihusiki je?hilo linatosha kuwa jibu juu ya kifo cha Balali?

Serikali hii ina wakati mgumu sana hadi sasa na tunasubiria Bunge la bajeti ......kuhakikisha kuwa hakuna jiwe litakalosalia juu ya jiwe, na ripoti ya EPA itawekwa hadharani waziwazi..

wewe inaelekea hujui kwa nini membe ahivyo ! hilo jibu alilotoa siyo kama "press" yake mwenyewe, bali hilo jibu linatokana na yeye kuulizwa na mwandishi wa habari kama serikali inahusika, and he was clear on that, kwamba serikali haikuhusika ! got it ?
 
Mchungaji naye nilidhani atathibitisha japo kwa kusema aliuona mwili wa Ballali? Naona na yeye anaimba statements zile zile za mama Muganda.

Aliumwa kwa muda mrefu, wakati wengine hapa wanasema alikufa ghafla. Alikufa tarehe 16, wakati wengine wanasema alikufa Jumapili tarehe 18.

Changa la macho tu.

Mchungaji aliyemzika Ballali anena

*Athibitisha aliumwa kwa muda mrefu
*Aeleza alivyoongoza ibada, maziko

Na Hassan Abbas

WAKATI Watanzania wakiwa bado katika hali ya sintofahamu kuhusu ukweli juu ya kifo cha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Daudi Ballali, Mchungaji aliyeendesha misa na hatimaye maziko yake nchini Marekani amekizungumzia kifo hicho na namna maziko yalivyokuwa.

Akizungumza katika mahojiano na gazeti hili kwa njia ya mtandao, Mchungaji Klaus Sirianni wa Kanisa Katoliki la St. Stephen Martirs' lililoko District of Columbia, Washington DC, amelithibitishia gazeti hili kuwa Dkt. Ballali alikufa na yeye ndiye aliyeongoza misa na baadaye ibada ya maziko.

"Ni kweli Dkt. Daud T.S Ballali alifariki Mei 16, 2008 akiwa na baadhi ya wana ndugu zake hapa nchini Marekani," alisema Mchungaji Sirianni.

Kumekuwa na uvumi unaozidi kuenea nchini ambapo wengi wanahoji ukweli wa kifo cha Dkt. Ballali huku baadhi wakitaka kujua kama kweli kulifanyika ibada ya maziko mjini Washington kama ilivyokuwa imetangazwa.

Akithibitisha kufanyika kwa misa na ibada ya maziko ya Ballali, Mchungaji huyo ameliambia Majira Jumapili kuwa: "Misa iliyofanyika katika tamaduni za kikristo ya Dkt. Ballali ilifanyika kwenye Kanisa la St. Stephen Martyr, Washington, District of Columbia, kuanzia saa nne asubuhi, Mei 23, 2008."

Akaongeza kuwa yeye ndiye aliyesimamia misa na baadaye maziko hayo. "Aliyeongoza misa na ibada ya maziko ni mimi Mchungaji Klaus Sirianni," alisema mchungaji huyo ambaye pia ni mmoja wa viongozi wa parokia ya kanisa hilo.

Katika maziko hayo Mchungaji Sirianni amethibitisha kuwa wahudhuriaji walikuwa ndugu, jamaa wa karibu na watu waliowahi kufanyakazi na marehemu huku akimtaka mwandishi kwa maelezo zaidi kuhusu sababu za kifo hicho awasiliane na wanafamilia.

"Maziko yalifanyika kwenye makaburi ya kikatoliki ya Gate of Heaven yaliyoko eneo la Silver Spring, Maryland na kwa mara nyingine mimi ndiye niliyesimamia ibada hiyo tena."
 
::Habari za Tanzania Jumatatu Juni 09, 2008

Imetolewa mara ya mwisho: 08.06.2008 1519 EAT
•
Mchungaji aliyemzika Ballali anena


*Athibitisha aliumwa kwa muda mrefu
*Aeleza alivyoongoza ibada, maziko

Na Hassan Abbas

WAKATI Watanzania wakiwa bado katika hali ya sintofahamu kuhusu ukweli juu ya kifo cha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Daudi Ballali, Mchungaji aliyeendesha misa na hatimaye maziko yake nchini Marekani amekizungumzia kifo hicho na namna maziko yalivyokuwa.

Akizungumza katika mahojiano na gazeti hili kwa njia ya mtandao, Mchungaji Klaus Sirianni wa Kanisa Katoliki la St. Stephen Martirs' lililoko District of Columbia, Washington DC, amelithibitishia gazeti hili kuwa Dkt. Ballali alikufa na yeye ndiye aliyeongoza misa na baadaye ibada ya maziko.

"Ni kweli Dkt. Daud T.S Ballali alifariki Mei 16, 2008 akiwa na baadhi ya wana ndugu zake hapa nchini Marekani," alisema Mchungaji Sirianni.

Kumekuwa na uvumi unaozidi kuenea nchini ambapo wengi wanahoji ukweli wa kifo cha Dkt. Ballali huku baadhi wakitaka kujua kama kweli kulifanyika ibada ya maziko mjini Washington kama ilivyokuwa imetangazwa.

Akithibitisha kufanyika kwa misa na ibada ya maziko ya Ballali, Mchungaji huyo ameliambia Majira Jumapili kuwa: "Misa iliyofanyika katika tamaduni za kikristo ya Dkt. Ballali ilifanyika kwenye Kanisa la St. Stephen Martyr, Washington, District of Columbia, kuanzia saa nne asubuhi, Mei 23, 2008."

Akaongeza kuwa yeye ndiye aliyesimamia misa na baadaye maziko hayo. "Aliyeongoza misa na ibada ya maziko ni mimi Mchungaji Klaus Sirianni," alisema mchungaji huyo ambaye pia ni mmoja wa viongozi wa parokia ya kanisa hilo.

Katika maziko hayo Mchungaji Sirianni amethibitisha kuwa wahudhuriaji walikuwa ndugu, jamaa wa karibu na watu waliowahi kufanyakazi na marehemu huku akimtaka mwandishi kwa maelezo zaidi kuhusu sababu za kifo hicho awasiliane na wanafamilia.

"Maziko yalifanyika kwenye makaburi ya kikatoliki ya Gate of Heaven yaliyoko eneo la Silver Spring, Maryland na kwa mara nyingine mimi ndiye niliyesimamia ibada hiyo tena."


Kinepi
Baada ya kusoma habari hii, nilinyanyua simu nikampigia Padri Klaus Sirianni wa kanisa katoliki mtakatifu Stephen Martyr, Washington, District of Columbia,

Maswali na majibu yalikuwa kwa lugha ya kiingireza ila nitachapa kiswahili.

swali. padri habari za leo
jibu: Nzuri

maelezo: mimi ni kinepi Mtanzania,Nimepata taarifa kuwa wewe ndiye ulieendesha misa ya marehemu Dr. Daudi Balali

jibu: Ndio

swali: utajali kama nikikuuliza maswali kuhusu misa ile na huduma yote kwa ujumla
jibu: hapana
Ndio, Balali alifariki na mimi ndie niliyeendeshasha ibada ile mpaka makaburini akazikwa.

Swali: Padri je katika huduma yako hiyo ulipata kuuona mwili wa DR. balali ???

Jibu: Hapana.sikuuona.
Swali: Je ulipata wasaa wa kufunguliwa jeneza hata mara moja?"
Jibu: Hapana jeneza halikufunguliwa, niliamini maneno ya ndungu za marehemu kwamba aliyeko humo kwenye Jeneza ni Balali.

Swali: Je si lazima kujua nini kipo ndani ya jeneza kabla ya kukiombea?
jibu: ni vyema ukauliza ndugu za marehemu kwa maelezo zaidi.

kinepi: asante padri kwa muda wako, kwaheri.

Kutoka ubalozini wanarushiana mpira kuwa ni nani aliuona mwili.
Mpaka sasa Kifo cha Balali ni kitendawili.
Ninafanya jitihada kujua ni hospitali gani alilazwa. Nikipajua tu au mtu yeyote kama ana info tafadhali anipatie lazima ni jue Balali yuko wapi.
Majibu ya wizi wa fedha zetu ni muhimu sana.
 
heading;

Re;Balali hata Padri hakuona mwili

...wallaaaaaahi billaaaaah,....nimeisoma hiyo article mara tatu sijaona wapi padri kasema hakuuona mwili wa balali!
 
Baada ya kusoma habari hii, nilinyanyua simu nikampigia Padri Klaus Sirianni wa kanisa katoliki mtakatifu Stephen Martyr, Washington, District of Columbia,

Maswali na majibu yalikuwa kwa lugha ya kiingireza ila nitachapa kiswahili.

swali. padri habari za leo
jibu: Nzuri

maelezo: mimi ni kinepi Mtanzania,Nimepata taarifa kuwa wewe ndiye ulieendesha misa ya marehemu Dr. Daudi Balali

jibu: Ndio

swali: utajali kama nikikuuliza maswali kuhusu misa ile na huduma yote kwa ujumla
jibu: hapana
Ndio, Balali alifariki na mimi ndie niliyeendeshasha ibada ile mpaka makaburini akazikwa.

Swali: Padri je katika huduma yako hiyo ulipata kuuona mwili wa DR. balali ???

Jibu: Hapana.sikuuona.
Swali: Je ulipata wasaa wa kufunguliwa jeneza hata mara moja?"
Jibu: Hapana jeneza halikufunguliwa, niliamini maneno ya ndungu za marehemu kwamba aliyeko humo kwenye Jeneza ni Balali.

Swali: Je si lazima kujua nini kipo ndani ya jeneza kabla ya kukiombea?
jibu: ni vyema ukauliza ndugu za marehemu kwa maelezo zaidi.

kinepi: asante padri kwa muda wako, kwaheri.

Kutoka ubalozini wanarushiana mpira kuwa ni nani aliuona mwili.
Mpaka sasa Kifo cha Balali ni kitendawili.
Ninafanya jitihada kujua ni hospitali gani alilazwa. Nikipajua tu au mtu yeyote kama ana info tafadhali anipatie lazima ni jue Balali yuko wapi.
Majibu ya wizi wa fedha zetu ni muhimu sana.
 
samahani maelezo ya mahojiano na Padri yamechelewa kidogo.
Bali Padri kwa kinywa chake amekiri hakuona mwili wa Balali.
Simu ya kanisa ni : 202 785 0982.
 
Naona polepole watu wanapobanwa wanakiri hawakuona maiti... we are getting there slowly...
 
Kama kuna mtu anaweza kuaccess birth and death registration office ya mji aliozikiwa balali anaweza kupata data za kutuwezesha kufikia kitanda alicholazwa alipofika kule.... na kwa kuwa data za kila mmgonjwa zinahifadhiwa nadhani akienda wizara ya afya ya USA anaweza kupata some dataz hata kama alikuwa anahama-hama vitanda vya hospito....
 
Mkuu FMES,

Basi tueleze huyo balozi Sefue aliona maiti wapi?

Mimi nilikuwa najua kwa asilimia 100 kwamba kwenye misa hakukuwa na kuona maiti. Sijui ndugu yangu FMES alipata wapi hiyo ya kusema balozi aliona maiti?

Pia FMES data zako zinasema Ballali alikufa jumapili tarehe 18, padre anasema 16.

Data za Jasusi zinasema alikufa ghafla, padre anasema aliumwa kwa muda mrefu.

Hapo tukubali tu tumefungwa goli la kisigino na kwasababu serikali nayo haimtafuti basi huko aliko ataendelea kufaidi pesa za wizi.

Ila wengine tutaendelea kuirudisha hii habari mpaka kieleweke.
 
heading;
...wallaaaaaahi billaaaaah,....nimeisoma hiyo article mara tatu sijaona wapi padri kasema hakuuona mwili wa balali!
Wait !!! Inamaana kila uliposoma wewe ni kuwa Padire ameuona mwili wa Balali ?
 
Back
Top Bottom