Kigezo cha Rais bora hakipimwi na wanyonge, Wanyonge hawaelewi chochote kuhusu siasa wala uchumi

Kigezo cha Rais bora hakipimwi na wanyonge, Wanyonge hawaelewi chochote kuhusu siasa wala uchumi

Nafikiri hujaielewa .

Point sio kuwa wanyonge wakandamizwe, lakini ubora wa Rais haupimwi kwa kuwafurahisha wanyonge

Mfano akitokea Rais akasema wananchi wanaruhusiwa kuvamia hifadhi na misitu, wanyonge watafurahi sana, je huyo atakuwa rais bora?
Mfano population imeongezeka hawana Ardhi wala lkipato chochote utawaacha wafe na njaa wakati eneo la kulima lipo hiyo mbuga Utaona wanyama muhimu kuliko uhai wao?
 
Wanyonge ukiwauliza "katiba na umeme kipi bora?" Utasikia umemeéeee!! Hahahaha
Wako sahihi.wanachohitaji ni kutimiziwa mahitaji yao sio porojo za katiba au tume huru
 
Hivi mkuu hao watawala wa zamani walikuwa wakichaguliwa na wanyonge?
Zilikuwa ni tawala za kiukoo na mabwanyenye na zilikubakika kwa Mungu

Point hapa sio kukandamiza wanyonge, ila kuna mambo mengine sio popular ila yana faida kwa muda mrefu na hapo huihitaji maoni ya wanyonge kuyatekeleza
Kuwajali wanyonge ni sifa ya kipekee haswa unapokuwa unapanda kimaisha na kupata utajiri. Ni sifa ya ubinadamu.
 
Naona watu fulani wanapiga sana ngonjera kuhsu rais huyu kupendwa na wanyonge na mwingine kutopendwa na wanyonge, siju kama ni kweli

Lakini hebu tuwaangalie hawa wanyonge ni watu gani.. Wanyonge wanasemwa kuwa ni watu wa kipato kidogo wasio na ajira rasmi wala elimu kubwa, hata hapa JF wanasema mitandao kama ya Facebook ina wanyonge wengi ambao wanamkubali kiongozi fulani na kumkataa mwingine

Sasa ukipima uelewa wa hawa wanyonge kuhusu maswala ya siasa, utawala na uchumi ndio utajua kuwa hawa watu maoni yao hayana maana yoyote kuhusu rais bora ama asiye bora ni yupi

Ukiwauliza kuhusu ripoti ya CAG hawajui lolote, ukiwauliza majukumu ya bunge hawajui, ukiwauliza kuhusu uchumi wa kati ni nini hawajui lolote, yaani hawaelewi chochote kuhusu mihimili na mifumo ya serikakali


Na kutokana na uelewa finyu wanyonge hawa ni rahisi sana kulaghaiwa na wanasiasa, mfano kipindi cha mwaka 2010 hadi 2015 Chadema walijipatia sifa na umaarufu sana kutoka kwa wanyonge kwa kuwaambia kuhusu ufisadi wa Lowassa, lakini Chadema walipobadilisha gia angani na kumsimamisha Lowassa kwenye urais, Wanyonge waliwakubali tena Chadema na kufikia kudeki barabara na kumpa Lowassa kura nyingi sana

Miaka ya hivi karibuni kulitokea kiongozi mmoja akafanikiwa sana kuwalaghai wanyonge, na ndio mtaji mkubwa unaotumika na wanaomtetea huyo kiongozi

Wanyonge wanapenda kuambiwa tu nitawapa vitu vya bure, nitawafilisi matajiri, nitrawaruhusu kufanya biashara popote, nitawaruhusu kuchunga mifugo popote n.k bila kuelewa hasara za hivyo vitu kwa mapana

hivi sasa crisis ya dunia na vitu kupanda bei imewapa nafasi nzuri wanasiasa laghai kuwatapeli wanyonge, utasikia mtandoni wakisema ingekuwa flani angekuwepo vitu visingepanda na wanyonge kutokana na kutoelewa wanawaamini

Sisemi wanyonge wakandamizwe ila sio kipimo cha ubora wa Rais
Wanyonge wanahitaji kukombolewa na Sio kusifiwa unyonge
 
Hoja yangu Ni kwamba unachotaka kukipata Ni kitu kisichokiwepo, utahangaika mpaka kufa.

Hapo Kenya wana Tume huru ya uchaguzi na Katiba Mpya lakini mpaka Leo bado wanalilia Mabadiliko.

Sasa hivi, wanasiasa wanachofanya Ni kutengeneza magenge ya msimu wanayo yaita vyama kutafutia madaraka lakini watu Ni wale wale.

Kwa taarifa yako hao Wakenya wako vizuri kuliko sisi, na wana uhuru wa kutosha kwenye kujieleza kuliko sisi tuliofubazwa kwa shuruti na ccm. Mabadiliko wanayoyataka ni kuboresha zaidi hatua waliyopo, ambayo ni maili nyingi kulinganisha na sisi. Kwakuwa ww ni mzee sitegemei utake mabadiliko kwani umri na mtazamo wako tayari umeshagota.
 
Kwa taarifa yako hao Wakenya wako vizuri kuliko sisi, na wana uhuru wa kutosha kwenye kujieleza kuliko sisi tuliofubazwa kwa shuruti na ccm. Mabadiliko wanayoyataka ni kuboresha zaidi hatua waliyopo, ambayo ni maili nyingi kulinganisha na sisi. Kwakuwa ww ni mzee sitegemei utake mabadiliko kwani umri na mtazamo wako tayari umeshagota.
Huijui Kenya.
 
Kuwajali wanyonge ni sifa ya kipekee haswa unapokuwa unapanda kimaisha na kupata utajiri. Ni sifa ya ubinadamu.

Kuna kujali wanyonge, na kuwatumia wanyonge kuficha ajenda zako. Unapowajali wanyonge unawapa ajira. Sio kunyanyasa matajiri ili maskini wa kushangilie.
 
Wadharauni sana wanyonge lakini ipo siku mtajua umhimu wao.
Naona watu fulani wanapiga sana ngonjera kuhsu rais huyu kupendwa na wanyonge na mwingine kutopendwa na wanyonge, siju kama ni kweli

Lakini hebu tuwaangalie hawa wanyonge ni watu gani.. Wanyonge wanasemwa kuwa ni watu wa kipato kidogo wasio na ajira rasmi wala elimu kubwa, hata hapa JF wanasema mitandao kama ya Facebook ina wanyonge wengi ambao wanamkubali kiongozi fulani na kumkataa mwingine

Sasa ukipima uelewa wa hawa wanyonge kuhusu maswala ya siasa, utawala na uchumi ndio utajua kuwa hawa watu maoni yao hayana maana yoyote kuhusu rais bora ama asiye bora ni yupi

Ukiwauliza kuhusu ripoti ya CAG hawajui lolote, ukiwauliza majukumu ya bunge hawajui, ukiwauliza kuhusu uchumi wa kati ni nini hawajui lolote, yaani hawaelewi chochote kuhusu mihimili na mifumo ya serikakali


Na kutokana na uelewa finyu wanyonge hawa ni rahisi sana kulaghaiwa na wanasiasa, mfano kipindi cha mwaka 2010 hadi 2015 Chadema walijipatia sifa na umaarufu sana kutoka kwa wanyonge kwa kuwaambia kuhusu ufisadi wa Lowassa, lakini Chadema walipobadilisha gia angani na kumsimamisha Lowassa kwenye urais, Wanyonge waliwakubali tena Chadema na kufikia kudeki barabara na kumpa Lowassa kura nyingi sana

Miaka ya hivi karibuni kulitokea kiongozi mmoja akafanikiwa sana kuwalaghai wanyonge, na ndio mtaji mkubwa unaotumika na wanaomtetea huyo kiongozi

Wanyonge wanapenda kuambiwa tu nitawapa vitu vya bure, nitawafilisi matajiri, nitrawaruhusu kufanya biashara popote, nitawaruhusu kuchunga mifugo popote n.k bila kuelewa hasara za hivyo vitu kwa mapana

hivi sasa crisis ya dunia na vitu kupanda bei imewapa nafasi nzuri wanasiasa laghai kuwatapeli wanyonge, utasikia mtandoni wakisema ingekuwa flani angekuwepo vitu visingepanda na wanyonge kutokana na kutoelewa wanawaamini

Sisemi wanyonge wakandamizwe ila sio kipimo cha ubora wa Rais
 
Huijui Kenya.

Nimeishi Kenya, sasa sijui kama siijui kijiografia ama kisiasa? Na nina uwezo wa kupambanua mazingira yao na yetu na kujua ukweli. Ukiitazama Kenya kwa mtazamo wa kiccm utawaona wanakosea. Lakini wako vizuri kuanzia kiuchumi, kijamii, kielimu, kiafya na hata kisiasa kulinganisha na sisi wenye amani ya kwenye vitabu.
 
Naona watu fulani wanapiga sana ngonjera kuhsu rais huyu kupendwa na wanyonge na mwingine kutopendwa na wanyonge, siju kama ni kweli

Lakini hebu tuwaangalie hawa wanyonge ni watu gani.. Wanyonge wanasemwa kuwa ni watu wa kipato kidogo wasio na ajira rasmi wala elimu kubwa, hata hapa JF wanasema mitandao kama ya Facebook ina wanyonge wengi ambao wanamkubali kiongozi fulani na kumkataa mwingine

Sasa ukipima uelewa wa hawa wanyonge kuhusu maswala ya siasa, utawala na uchumi ndio utajua kuwa hawa watu maoni yao hayana maana yoyote kuhusu rais bora ama asiye bora ni yupi

Ukiwauliza kuhusu ripoti ya CAG hawajui lolote, ukiwauliza majukumu ya bunge hawajui, ukiwauliza kuhusu uchumi wa kati ni nini hawajui lolote, yaani hawaelewi chochote kuhusu mihimili na mifumo ya serikakali


Na kutokana na uelewa finyu wanyonge hawa ni rahisi sana kulaghaiwa na wanasiasa, mfano kipindi cha mwaka 2010 hadi 2015 Chadema walijipatia sifa na umaarufu sana kutoka kwa wanyonge kwa kuwaambia kuhusu ufisadi wa Lowassa, lakini Chadema walipobadilisha gia angani na kumsimamisha Lowassa kwenye urais, Wanyonge waliwakubali tena Chadema na kufikia kudeki barabara na kumpa Lowassa kura nyingi sana

Miaka ya hivi karibuni kulitokea kiongozi mmoja akafanikiwa sana kuwalaghai wanyonge, na ndio mtaji mkubwa unaotumika na wanaomtetea huyo kiongozi

Wanyonge wanapenda kuambiwa tu nitawapa vitu vya bure, nitawafilisi matajiri, nitrawaruhusu kufanya biashara popote, nitawaruhusu kuchunga mifugo popote n.k bila kuelewa hasara za hivyo vitu kwa mapana

hivi sasa crisis ya dunia na vitu kupanda bei imewapa nafasi nzuri wanasiasa laghai kuwatapeli wanyonge, utasikia mtandoni wakisema ingekuwa flani angekuwepo vitu visingepanda na wanyonge kutokana na kutoelewa wanawaamini

Sisemi wanyonge wakandamizwe ila sio kipimo cha ubora wa Rais
kweli
 
Hakuna kitu kinaitwa Chatto (International Airport) ila Geita Airport na IATA Code yake ni GIT. Unajikuta mjuaji kumbe haujui chochote. 🚮

Mimi sio rubani boss utegemee nitafuata code za kirubani, najua kuna Geita na Chato. Isitoshe sioni sifa yoyote ya kujua huo uwanja kwa hizo code unazotaka nizijue.
 
Nimeishi Kenya, sasa sijui kama siijui kijiografia ama kisiasa? Na nina uwezo wa kupambanua mazingira yao na yetu na kujua ukweli. Ukiitazama Kenya kwa mtazamo wa kiccm utawaona wanakosea. Lakini wako vizuri kuanzia kiuchumi, kijamii, kielimu, kiafya na hata kisiasa kulinganisha na sisi wenye amani ya kwenye vitabu.
 
Ukisema uongo hakikisha unajua pia na ukweli wake😂😂😂. Natumia sana uwanja wa Chato na nimekuja Dar jumamosi narudi jumanne. Sijaona kufutwa kwa safari za ATCL kwenda Chato

Uko sahihi, kwenda kwenye hiyo route hakumaanishi kuna faida. Wanaweza wasifunge kwa sababu za kisiasa lakini hiyo route ni baadhi ya maeneo yatakayozidi kulipa hilo shirika hasara. Rejea mashirika mengi ya umma yalivyokufa kutokana na hasara kwani yaliendeshwa kisiasa nani si kwa nguvu ya soko.
 
Mnyonge tulia.

Wenzenu kina SABAYA, ALLY HAPI, HERI JAMES, ALEXANDER MNYETI, MAKONDA Ni MATAJIRI wa KUTISHA.

Mnyeti ndio alikuwa anashika FUKO LA PESA ZA KUNUNUA WABUNGE.

Amejenga MAHEKALU,

Amejenga Uwanja Bora kabisa wa Gwambina.

Anaendesha timu ya Gwambina,

Amenunua TCC CHANG'OMBE na sasa inaitwa GWAMBINA TCC CHANG'OMBE Hapo ndio Kuna Gym, na vifaa vyote vya mazoezi vya Gwambina.

Sasa wewe endelea kubweka bweka mitandaoni Ndugu mnyonge
Bonge la ukweli
 
Kuna kujali wanyonge, na kuwatumia wanyonge kuficha ajenda zako. Unapowajali wanyonge unawapa ajira. Sio kunyanyasa matajiri ili maskini wa kushangilie.
Unapowajengea majengo na kuagiza waishi humo miaka mitano ni ishara kubwa sana ya kuwajali.

Unaposoma watoto wao bure kabisa ni ishara nyingine ya kuwajali kwa vitendo.

Binadamu anaharibikiwa kwa ubinafsi wake na sio zaidi ya hapo.
 
Naona umepanic mpaka umeokota tu link na kuitupa hapa.
Mimi nipanic kwasababu ipi?

Kenya ukitoa Genge la Wanasiasa wanaomiliki Kenya tangu UHURU na Makampuni ya kimataifa ambayo yameifanya Kenya Kama Hub ya East Africa.

Mtu wa Kawaida anaishi Kama Yuko JEHANUM ya MOTO na hajui atajiokoa lini.
 
Unapowajengea majengo na kuagiza waishi humo miaka mitano ni ishara kubwa sana ya kuwajali.

Unaposoma watoto wao bure kabisa ni ishara nyingine ya kuwajali kwa vitendo.

Binadamu anaharibikiwa kwa ubinafsi wake na sio zaidi ya hapo.

Wanyonge ni hao tu kwenye hayo magorofa? Elimu bure aliirukia maana waanzilishi walitaka iwe bure mpaka chuo kikuu.
 
Mimi nipanic kwasababu ipi?

Kenya ukitoa Genge la Wanasiasa wanaomiliki Kenya tangu UHURU na Makampuni ya kimataifa ambayo yameifanya Kenya Kama Hub ya East Africa.

Mtu wa Kawaida anaishi Kama Yuko JEHANUM ya MOTO na hajui atajiokoa lini.
Kwani kuna tofauti na hapa kwetu? watu huko vijijini wanatumia maji na mifugo tena maji yenyewe ni tope tupu.
Makampuni ya kimataifa ndio hayo serikali hii ya ccm imekuwa ikizunguka duniani kuyaleta yawezekeze hapa nchini, huenda hujui mambo hayo.
 
Back
Top Bottom