Kijana aliyetelekezwa na mke siku ya harusi atunukiwa tuzo ya mwanaume bora wa mwaka na Waziri Gwajima

Mama unaakili sana..
Mungu akubariki na kila kheri kwenye majukumu yako.

Sisi wanajme tunapitia mengi sana.
Poleni sana, hii wizara pia inahudumia wanaume, ila bado wengi hawaamini, tuendelee kuelimisha, wasijione wapweke, waje kwenye wizara yao, na haki itatendeka pasi na ubaguzi wa kijinsia. Mungu akubariki 🀝
 
wakati mwingine lengo yawezekana ilikuwa ni kutoa aibu akazidisha au sio mzoefu kwenye tasnia ya ulevi na unywaji.

Kumhukumu moja kwa moja sio vizzuri
 
Mambo ya kijinga ndio Yana tuzo,by the way huo ni muendelezo wa dharau tuu.
Hujambo?

Tunafanya mambo mengi mbalimbali, sijawahi kukusikia ukitoa maoni au kushirikiana nasi, labda huwa hufuatilii tunapoyafanya. Karibu wizara yako ufuatilie tafadhali, hii ni Wizara ya Jinsi zote yaani wanawake na wanaume pia. Wanaume wengi wamepata na wanaendelea kupata huduma. Haya asubuhi njema na baraka kwako.
 
Umeamkaje mamaπŸ₯°
 
wakati mwingine lengo yawezekana ilikuwa ni kutoa aibu akazidisha au sio mzoefu kwenye tasnia ya ulevi na unywaji.

Kumhukumu moja kwa moja sio vizzuri
Bora wewe useme. Sisi 'angle' yetu ni moja tu hatutaki mambo mengi kuwa, katika mazingira hayo, kwa walio wengi, wao na ndugu zake na wapambe wengi, wangeanzisha zogo na mwisho wake ingeanza vurugu hapo na majeruhi wa ukatili kupatikana. Kitendo cha kuwa watulivu, ni hekima hiyo.

Tumeona watu wakitoana uhai au kuumizana kwa Sababu ndogo kabisa kwa kutokubali tu kupokea maumivu na kuyaacha yapoe. Itakuwa ajabu sana kutotambua hata hatua ya huyu ndugu.

Jamii yetu wengi wameanzisha utaratibu wa kuhukumiana hata kama mtu kasikia kwa mtu wa tatu, tayari anapitisha hukumu. Ukweli haina tija.
 
Mzazi gani atakabidhi binti yake kwa mlevi? Jamaa hana nidhamu!
 
Jamaa ni shujaa.
Lakini asilogwe amrudie kumba la mwitu aliyemkataa
 
Weww mama ninakukubali sana.
Endelea kujitoa na kuisaidia jamii yetu
Ubarikiwe, wachache walio na Imani nami, tutasonga mbele pamoja, huku tukipokea maoni ya wakosoaji wetu na kuyachuja na kuchukua yenye mashiko, na Yale mengine ambayo hayana mashiko, tukiyaacha mikononi mwa Mungu. Nakutakia asubuhi njema na heri. πŸ™πŸ½
 
Amina mama.
Nashukuru ulifanyia kazi kero niliyoileta kwako.
Barikiwa mnoo
 
Mh waziri shkamoo,bila kukuchosha naomba nijaalie chochote kwenye lipa namba ya tigo 7410514,sijatia kitu kinywani kwa saa 36 zilizopita,nawaza kujitoa roho tu,hata kazi ya kubeba tofali nanyimwa,natanguliza shukurani
 
πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ‡ΉπŸ‡Ώ Sijambo mwanangu, naendelea na safari yetu kwa maendeleo na ustawi wa jamii, twende pamoja nami tafadhali πŸ™πŸ½
Kwakweli mama hongera sana mimi siko kwenye hii mada ya leo ila nakupongeza kwa ujasiri wa kuwa mitandaoni kwa uwazi bila kujificha huku ukipokea maoni yote hata yale mabaya. Tunao mawaziri wengi humu ila wengi akiandika uzi ndio harudi tena kujibu.Hongera sana
 
Kwani kabla ya sendoff hamkujua ni mlevi au ni unafki tu, kwa kauli za ajabu ati ametuaibisha.

Huyo mke alotaka kumuoa hajui mumewe anakula vyombo, mbona kamkubali, mbona mahari ya mlevi wameila!! ??

Acha chapombe apewe tuzo, na bila shaka tuzo inakua na kipozeo kidogo, hicho akitumie kugida lager nyingine akili ikae sawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…