Kijana mwenye wazo la Biashara la mtaji wa Mil 5-10

Kijana mwenye wazo la Biashara la mtaji wa Mil 5-10

Habari, kuna aina nyingi sana za biashara kwa mtaji wako, japo ingefika milion 15 ingependeza zaid, unaweza fungua duka la kuuza malidhafili za kutengenezea chakula cha kuku, kama mashudu ya alizet, mashudu ya pamba , damu,chokaaa, pumba nk, hii biashara inalipa na hizi bidhaa kuna baadhi unafuata mkoani nyingine zipo hapa dar,

Biashara ya pili ni kununua nafaka mikoani na kuja kuuza dar, hasa mahindi hii pia iko vuzuli japo kwa kipindi hiki maindi yapo juu sana lkn unaweza kuvuta subila ikifika mwezi wa 5 unaanza na mahindi ya mtukula kwa milioni kumi inatosha kuna kipindi maindi yanauzwa sh 600 kwa hiyo ukiwa na milioni 10 unakwenda kuchukua tani 15 - 18 na ukija kuuza unapata faida nzuli tu,

Kuna biashara ya kufungua mashine, kiukweli hii ndio biashara ya ndoto yangu , biashara hii imegawanyika makundi 3.

Unafungua mashine kwa ajili ya kusaga vipeto vya watu tu, hii kwa cku hukosi kuanzia 20-50 kutokana na eneo ulilopo lkn unawez kuwa na mashine ndogo kama SB 30 kwa ajili ya kukoboa mpunga kwa watumiaji wa chini biashara hii ni nzuli sana kwa nje ya dar.

Biashara nyingine ni kufungua mashine ya kusaga sembe hii unaweza kufanya hapa dar tena ukiwa na mtaji mzuuuli unachofanya unafungua mashine yako unaleta mahindi kutoka shamba unakoboa kwa mashine yako, , kuna wale wasiokuwa na mashine watakuja kukoboa kwako lkn pia kama unamtaji wa kutosha unawakopesha mahindi wajasiliamali wadogo pale pale mashineni wanasaga wanauza sembe wanakulipa pesa yako.

Baishara ya tatu ni kufungua mashine ya kukoboa mpunga ,hii inakuwa ya kukoboa mpunga tu, unanuna SB 50 unafunga mahali pazuuli kisha unakuwa na stoo kuuubwa ya kuhifadhia mpunga ,wakulima wanaleta mpunga kwako wahifadhi kisha ukifika msimu wanakoboa, lkn pia wafanya biashara wanakuja hako kukoboa na kununua mchele hii ni nzuli sana, karibu mp boss,
Safi
 
Tupe sababu.

Na je ukweli ni upi?

Wana JF wanahitaji kujifunza toka kwako, Ukipewa mtaji wa 2.5M utaanzisha biashara gani itakayokupatia angalau TZS 100,000 kama faida.

Karibu, Nami pia Niko tayari kujifunza toka kwako.

Hakuna biashara ya mtaji 2.5M itaingiza faida ya laki moja kila siku. Kwa hapa TZ huo ni uongo.
 
Asiye na wazo achukue hapa. Tampa muongozo na mchanganuo. Yaani business plan yake.
IDEAS ZA KUTOKA KIMAISHA KWA MTAJI MDOGO


1.Nunua pikipiki ya Dhamana ukaanza biashara ya Boda boda.
2.Fungua saluni
3.Mradi wa tofali za kuchoma
3.Fuga kuku
4.Somea ujuzi wowote
5.Mradi wa kushona nguo
6.kijiwe cha kuchomelea
7.kijiwe cha milango na madirisha ya aluminum
8.Mgahawa Mdogo
9.Kijjwe cha kahawa
10.Mashine ya kupukuchua mazao mfano mahindi, mpunga, mtama, karanga, nk
11.Mashine ya kukata nyasi, kupalilia
12.Kuuza mbuzi, kuku,
13.Biashara ya mazao.
14.kukodi bus, daladala na kuzisimamia upate cha juu
15.Kutengeneza sabuni, sanitizer, handwash,
16.Kutengeneza unga wa lishe
17.Kilimo cha umwagailiaji water pump, mbegu, madawa
18.Jiko la supu
19.kutengeneza mkaa mbadala
20.Kuuza chips
21.Kukaanga kuku
22.Kutengeneza vitafunio
23.Kuzalisha ethanol
24.kufuga poko mbuzi katoliki
25.Kufungua kilabu cha pombe za kienyeji
26.Kufungua vijiwe vya Kukusanya ubuyu maporini yakitimia magunia unaleta mjini
27.Kuuza juice
28.Kuuza juice ya miwa
29.Kijiwe cha kukaanga samaki jioni
30.Shughuli za upambaji kumbi
31.Kusambaza bidhaa majumbani
32.Kusambaza bidhaa basic needs kwenye maduka ya vijijini yaani unanua mjini unasambaza kwa oda viduka vya vijijini.
33.Kuzunguka minadani kuuza nguo za mitumba, vyombo, nk
34.Kufungua tuition center
35.Kufungua grocery
36.Kuwa wakala wa bidhaa za viwandani
37.kijiwe cha kukusanya taka za plastic, chuma,oil chafu na tairi chakavu.
38.Kufungua genge la kuuza basic home need
39.Kufungua ofisi ya kupiga nguo pasi.
40.Ofisi ya kutengeneza viatu na mabegi
41.Kutengeneza vyombo vya kupikia mfano, majiko, ndoo, sufuria, mifuniko, vikaangio, nk
42.Saluni ya kutengeneza kucha za wanawake
43......Jengea vyumba vitatu wazazi wako nyumba ya Bati upate baraka
44..Nunua shamba
45.Nunua ng'ombe wadogo watano kwa laki na nusu anza ufugaji.
Au nunua mbuzi anza kufuga
46.Fungua kijiwe cha kuonyesha mpira
47.duka la nguo za kupoint classic za mitumba piga pasi tundika kwenye enga
48..Ofisi za baiskeli za kukodi hapo unapata baiskeli nane
49..Duka la spea za pikipiki na baiskeli
50.Duka la dawa na vipodozi
51..ofisi ya kuchaji simu kwa sola vijijini
52..ofisi ya uwakala wa kutuma na kutoa pesa
53.. Bustani za kuzalisha miche ya miti na matunda
54... Ufugaji nyuki na kuuza asali
55.. Kuzalisha unga wa muhogo
56..Direct sale yaani door to door delivery hapa unakuwa na torori na speaker unapita KILA nyumba unauza bidhaa na kuchukua oda ya nini wanataka Ili kesho uwaletee.
57.Utengenezaji pellets chakula cha mifugo,samaki.
58..unga wa lishe
59..mikeka
60.bidhaa za mianzi.
61.utengenezaji wine,
62.usafi wa majumbani
63.kuuza uji wa ulezi,mchele
64.utengenezaji mbolea za mboji na za maji.
65.utengenezaji wa vigae vya cement na vya udongo.
66.kupanda miti kwa ajili ya nguzo na mirunda
67.utengenezaji wa ndala
68.utengenezaji viatu
69.Upondaji kokoto
70.ufundi simu na radio
71.Utengenezaji mifagio
72.utengenezaji crips za Mihogo,ndizi,viazi,nk
73.Utengenezaji tambi,ubuyu
74.panda mlonge,au nyonyo,au mibono au muarobaini Ili uje uuze mafuta,au utengeneze sabuni.
75.Kutengeneza siagi ya karanga
76.Home delivery hapa ni kupita KILA nyumba na kuchukua oda za mahitaji yao then unaenda kununua unawaletea
77.Utengezaji wa vifungashio vya karatasi
78.utengenezaji mitungi,vyungu,majiko ya udongo
79.Kuwatengeneza kucha wadada
 
Hakuna biashara ya mtaji 2.5M itaingiza faida ya laki moja kila siku. Huo ni uongo.
Sasa jifunze hili.
- 2.5M itakuwa converted na kuwa US $5,000 , Hii Dola $5,000 ambayo ni 5% Daily Drawdown ya $100,000 account utakayopewa ku_trade na prop firm utakayochagua.

Ukibadili $5,000 kuwa TZS utapata TZS 11,500,000, Yes 11.5M hiki ndicho kiasi unachopewa ku_trade kwa siku, maana hiyo ndio DD ya 5% ya $100,000 kwa account utakayopewa.

Angalia hapa baadhi ya Prop firm.
Code:
https://docs.google.com/spreadsheets/d/1U0M8mZBnGMa9NQoC6o6qaYphTbM58T28_2LgDbBVfrw/edit#gid=0
1678253764491.png

Ndugu Fernando Wolle , Kwa upande wako, jirekebishe na utumie busara, Ukiona kitu ambacho hakina maana kwako, badala ya kutumia neno "UONGO", omba ufafanuzi au maelekezo zaidi ili uweze kujifunza.

Trading ndio biashara pekee ambayo utatumia mtaji mdogo kuweza kupata faida kubwa, iwapo tu unafahamu nini unachotakiwa kufanya.
==
1678339728062.png
 
Kampuni ya Engineering (ipo active), ina-deals na engineering works. Kwa sasa inafanya kazi na baadhi ya mashirika, ila changamoto ipo kwenye running Capital. Once kazi 2 zikifanyika, Cap inakata hivyo hatuna budi kusubiri mpaka hela itakapolipwa ndio tuweze kufanikisha (kuomba kazi nyingine).

Hivyo nafasi ya Investors ipo wazi.

MY CV's
Proffesion: Mechanical Engineer
Works experience: 6+ yrs
 
Biashara ipo ya kuuza personal care products kwa wholesale tunaingiza mizigo kutoka viwanda vyahapa East Africa tunauza wholesale njoo uongeze mtaji tunakubaliana faida tugawaneje siku ukiona unahitaji pesa yako unachukua unaacha mtaji niliokuwa nao.

Karibu mkuu.

Personal care gani mnaleta?
 
Tembea uone

Nanunua carton 450,000 within a few hours nimemaliza mzigo kwa 700,000 na hapo nauza Bei ya chini Ili mzigo utoke chapchap

Ni mwendo wa kucheza na fast moving products na wholesalers only
Hello Hornet, sijakuona siku nyingi kwenye jukwaa la biashara I hope you are doing fine. Happy women's day
 
Kampuni ya Engineering (ipo active), ina-deals na engineering works. Kwa sasa inafanya kazi na baadhi ya mashirika, ila changamoto ipo kwenye running Capital. Once kazi 2 zikifanyika, Cap inakata hivyo hatuna budi kusubiri mpaka hela itakapolipwa ndio tuweze kufanikisha (kuomba kazi nyingine).

Hivyo nafasi ya Investors ipo wazi.

MY CV's
Proffesional: Mechanical Engineer
Works experience: 6+ yrs
Nipe notes mkuu kama itakupendeza, hiyo kampuni inafanya kazi za aina gani hasa na inajiendeshaje? Sina pesa ya kuweka ila naomba notes coz mi mecha kama wewe ila ni fresh from school.
 
Sasa jifunze hili.
- 2.5M itakuwa converted na kuwa US $5,000 , Hii Dola $5,000 ambayo ni 5% Daily Drawdown ya $100,000 account utakayopewa ku_trade na prop firm utakayochagua.

Ukibadili $5,000 kuwa TZS utapata TZS 11,500,000, Yes 11.5M hiki ndicho kiasi unachopewa ku_trade kwa siku, maana hiyo ndio DD ya 5% ya $100,000 kwa account utakayopewa.

Angalia hapa baadhi ya Prop firm.
Code:
https://docs.google.com/spreadsheets/d/1U0M8mZBnGMa9NQoC6o6qaYphTbM58T28_2LgDbBVfrw/edit#gid=0
View attachment 2541308
Ndugu Fernando Wolle , Kwa upande wako, jirekebishe na utumie busara, Ukiona kitu ambacho hakina maana kwako, badala ya kutumia neno "UONGO", omba ufafanuzi au maelekezo zaidi ili uweze kujifunza.

Trading ndio biashara pekee ambayo utatumia mtaji mdogo kuweza kupata faida kubwa, iwapo tu unafahamu nini unachotakiwa kufanya.

Mwl.RCT achana nae hana hoja yyte.
 
Nipe notes mkuu kama itakupendeza , hizo kampuni inafanya kazi za aina gani hasa na inajiendeshaje? , sina pesa ya kuweka ila naomba notes coz mi mecha kama wewe ila ni fresh from school.
Kama ni fresh from school ushauri ninaoweza kukupa ni tafuta kwanza experience (Experience ndio gold huku nje) kwa kujitolea au kufanya kazi kwenye engineering company (kuna gap kubwa sana kati ya theory za darasani na mambo yalivyo huku nje). Kama unataka kujitolea nichek PM , sina uwezo wa kukuajiri kwa sasa.
 
Back
Top Bottom