Kikatiba Rais Samia yuko sahihi kumteua Naibu Waziri Mkuu

Jamani jamani mbona watu ni waongo hivi? Unabuni kutoka kichwani na kuandika kama ni tukio la ukweli? Salim alishika lini huu wadhifa? Ni Mrema pekee aliyewahi kushika.
Mpaka leo hii, hiki cheo kiliwahi kushikiliwa na watu 2 tuu tena kwa sababu maalumu sana na nyeti, na zenye maslahi mapana kwa taifa.

1. Dr. Salim Ahmed Salim.

Salim alipewa cheo hiki 1986 mpaka 1990, kwasababu aliwahi kuwa Waziri Mkuu kwa mwaka mmoja enzi za Mwalimu Nyerere (Baada ya Kifo cha Sokoine), hivyo baada ya Rais Mwinyi kuingia akaona ni Busara Waziri Mkuu wake aliyemteua Joseph Sinde Warioba awe na Naibu ambaye ni Salim.

2. Augustino Lyatonga Mrema

Akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Augustino Mrema alitumia ujuzi wake kama KACHERO WA USALAMA WA TAIFA, kudadisi na kukamata wezi na wala rushwa katika kila wizara ya Serikali aliyogundua mambo si shwari.

Hali hiyo ikawaudhi baadhi ya mawaziri wenzake serikalini. Wakamwambia "MREMA USIVUKE MIPAKA YAKO, Wewe ni waziri kama sisi na huwezi kuingilia mambo ya ndani kwenye wizara zetu bila kujadiliana nasi kwanza." Mrema anasema alikomaa nao, na ndipo Rais Mwinyi akagundua dhamira yake njema.

Rais Mwinyi mnamo mwaka 1992 akamuongezea cheo kipya Mrema. Akamteua kuwa NAIBU WAZIRI MKUU.

1993, Mrema alipopewa Unaibu Waziri Mkuu anasema "wenzangu walianza kuniogopa na kuniheshimu. Hata kama wanaenda sehemu walikuwa wanalazimika kusimama kwanza ili kupisha msafara wenye ving'ora wa Naibu Waziri Mkuu."

Akiwa Waziri wa Mambo ya ndani na Naibu Waziri Mkuu alishughulika na kila aina ya ubadhirifu, wizi na magendo kwa kadri alivyopata taarifa. Akawa waziri maarufu sana kwa wananchi mijini na Vijijini.

"Rais Mwinyi kila akirudi kutoka mikoani alikua akiniita na kuniambia Mrema nimetoka kwenye ziara, wananchi wanakusalimia sana. Unafanya kazi nzuri," alinisimulia Mzee Mrema katika mahojiano hayo ya MSUMARI WA MOTO.

Miongoni mwa mambo yaliyompa umaarufu Mrema zama hizo za uwaziri wake wa mambo ya ndani na Naibu Waziri mkuu ilikua ni kuhamasisha ujenzi wa vituo vya polisi kwa nguvu za wananchi ili kuimarisha ulinzi lakini pia "Tajirika na Mrema" - UTOAJI WA ZAWADI KWA WATU WANAOFICHUA WAHALIFU.
 
Hiki cheo ni Mrema pekee aliwahi kupewa na Mwinyi na kulikuwa na kelele sana kuwa amevunja katiba.

..wa kwanza alikuwa Dr.Salim Ahmed Salim.

..Salim alikuwa waziri mkuu wakati Mwalimu Nyerere anaondoka madarakani.

..alipoingia Mzee Mwinyi akamteua Joseph Warioba kuwa Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Raisi.

..Mzee Mwinyi pia akamteua Dr.Salim kuwa Waziri wa Ulinzi na Naibu Waziri Mkuu.

..Dr.Salim alipoondoka nchini kwenda kuwa Katibu Mkuu wa OAU[ kabla haijawa AU] kukawa hakuna Naibu Waziri Mkuu tena.

..Muda ulipita kabla Mzee Mwinyi hajamteua Augustino Mrema kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Naibu Waziri Mkuu.
 
Rais Samia amefanya mabailiko na Teuzi mpya kwenye Baraza lake la Mawaziri. Wadau na wananchi wamepokea kwa mtizamo tofauti juu ya Cheo Kipya Cha Naibu Waziri mkuu ,kwa maana ya kwamba Cheo hicho hakipo kikatiba.

MAJIBU HAYA HAPA.

Udaifu wa hii Katiba yetu ya 1977 ,kwenye hiyo Ibara ya 36(1)&(2) Hamna specific Limitation ya Rais kwenye kufanya Teuzi za kiongozi anaetaka, kuunda na Kufuta Wizara yoyote pindi akiwa madarakani, Ndomana Serikali imeitumia itakavyo, na wadau pia wanaitafsiri watakavyo.

Solution wa hayo yote ni

P#Katiba Mpya , itakayopunguza Madaraka ya Rais, Tume huru ya Uchaguzi, Utawala wa Sheria na Mgawanyo wa mamlaka kwa mihimili yote mitatu
 
Nawasalimu Waungwana wa JF,

Mwanzo mwanzoni nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa uhai na afya anazotujalia hata kuendelea kupashana habari za hapa na pale kupitia mtandao wetu huu pendwa wa JamiiForums...
KAMA NDIO HIVYO KWANINI MREMA ALIKATALIWA KULIPWA MAFAO YA CHEO CHA UNAIBU WAZIRI MKUU?
 
Nawasalimu Waungwana wa JF,

Mwanzo mwanzoni nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa uhai na afya anazotujalia hata kuendelea kupashana habari za hapa na pale kupitia mtandao wetu huu pendwa wa JamiiForums...
Sawa KABISA
 
Kwa maelezo yako! Swali je!? Rais anaweza kufuta nafasi ya urais katika JMT...!?? Kama anaweza kwanini na kama awezi kwanini...!??
 
Kuna mambo inabidi tupeane taarifa na kuelimishana. Sote tunajua muundo wa vyeo vya baraza la mawaziri ni suala la kikatiba na sio utashi wa Rais aliyepo madarakani.

Alianza, Rais Mstaafu Ally Hassan Mwinyi miaka ya mwanzoni mwa 1990s alipomteua Augustino Lyatonga Mrema kuwa naibu waziri mkuu, cheo ambacho kilikuwa hakipo kikatiba.

Leo, Rais wetu Mama Samia amemteua Dotto Biteko kuwa naibu waziri mkuu. Hili linatokea miaka 30 tangu kuwepo kitu kama hicho katika nchi yetu. Tangu alipoondoa Rais Mwinyi madarakani, marais wengine watatu wamepita bila kuwa na uteuzi wa cheo cha naibu ya waziri mkuu.

Sasa ni vyema tukapeana taarifa na kuelimishana hapa. Na haya ni maswali fikirishi.

1. Je, Katiba yetu inatambua cheo cha naibu waziri mkuu?

2. Je, rais ana mamlaka ya kuunda cheo kwa utashi wake pasipo kutumia katiba?

3. Cheo kinachoundwa nje ya katiba, wajibu wa hicho cheo unatokea wapi?

4. Ikiwa waziri mkuu mara baada ya kuteuliwa ni lazima uteuzi wake uthibitishwe na bunge, Je, naibu waziri mkuu atapaswa kuthibitishwa na bunge?
 
Sawa, lakini kama waziri mkuu mwenyewe ni picha tu,naibu waziri mkuu anakwenda kufanya Nini zaidi msafara na ving'ora. Gharama za kuendesha serikali zinakuwa kubwa mno kuliko uwezo wa nchi yenyewe.
 
Kwa maneno mengine unatuambia kuwa anaweza hata kufuta nafasi za Waziri Mkuu, CAG, Gavana n.k.?

Amandla...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…