Kikokotoo(Mafao): Rais Samia anastahili pongezi kwa hili

Kikokotoo(Mafao): Rais Samia anastahili pongezi kwa hili

Hii ni moja kati ya sheria mbovu na mbaya kuwahi kuwepo katika nchi zote duniani! Utekelezaji wa sheria hii ni kinyume na haki za binadamu.
Kwanini iwe hivyo ilihali ni haki ya mstaafu? Wenye kuitunga hii sheria waliwahi kufanya utafiti wowote na kutaja nchi yoyote duniani inayotumia sheria hii? Kama Kuna nchi hiyo wanaweza kututajia faida na hasara zake Kwa mhusika?
Binafsi siuoni Kama hilo jambo litakuwa na afya Kwa serikali na hata mstaafu badala yake wangewapa wastaafu elimu hata ya kununua hisa kwenye mabenki na hata Amana za serikali Kama wanaona atakitumia kiinua mgongo chake vibaya na siyo kumlipa Kama matone ya drip!
Waziri mweñye dhamana irudishe sheria hii bungeni ikafutwe haraka Sana kwani kuiacha inakwenda kusababisha vifo na hata umaskini Kwa wafanyakazi waliojitoa maisha Yao kuijenga nchi hii Kwa uvumilivu mkubwa wa kulipwa mishahara isiyokidhi mahitaji ya mwezi!
Nimwombe mh. Rais aifute hii sheria ikimpendeza na aache kumsikiliza huyo Jenister Mhagama ambaye Hana Nia njema na wastaafu pamoja na wafanyakazi wa taifa hili kwani ndiye aliyeipeleka sheria hii bungeni kutafuta kick Kwa Magufuli! Namlaani Kwa Imani yangu akaaibike na kupata Kila lililo baya Kwa kuwadhulumu wazee wetu Hawa ambao anawalipa mateso Kwa uzalendo wao wa nchi Yao!
Hii sheria ni ya kipuuzi. Ulaya baadhi ya nchi ninazozifahamu wanautaratibu mzuri Sana.

Kila mwananchi akifikisha miaka 60 anakula pension yake. Wameweka kiwango kidogo Cha kuchangia anzia ukiwa kijana kuanzia miaka22.

Yaani hakuna Cha mfanyakazi waserikali au dalali au bodaboda. Wote wanachangia huu mfuko na wanapata pension yao na kila mwezi wanakula posho Safi.

Ndiyo maana wazee ndiyo wanatunza familia za vijana wao. Na wanapesa.

Na ushauri.
 
Hii sheria ni ya kipuuzi. Ulaya baadhi ya nchi ninazozifahamu wanautaratibu mzuri Sana.

Kila mwananchi akifikisha miaka 60 anakula pension yake. Wameweka kiwango kidogo Cha kuchangia anzia ukiwa kijana kuanzia miaka22.

Yaani hakuna Cha mfanyakazi waserikali au dalali au bodaboda. Wote wanachangia huu mfuko na wanapata pension yao na kila mwezi wanakula posho Safi.

Ndiyo maana wazee ndiyo wanatunza familia za vijana wao. Na wanapesa.

Na ushauri.
Ya Ulaya huku kwa wacheza singeli hayatekelezeki!
 
Naomba kujuzwa:-
Mfanyakazi wa mkataba private sector anachangia kule NSSF.
Ikitokea 1) asipewe mkataba mpya au 2) kufukuzwa kazi kabla ya kufika miaka 60 say ajira imekoma either kwa kufukuzwa au kutoongezewa muda wa mkataba akiwa bado janki about 32 years, je anaruhusiwa ku claim pesa yake apo nssf immediately au itabidi asubiri hadi afikishe miaka60?!
 
Ukweli ni kwamba mifuko ime kopwa na serikali na serikali haiwezi kulipa Hilo Deni la trilion 14. Hivyo wanatumia huu ujanja kwa kuwaumiza watu.
Lini vyama vya wafanyakazi walikaa na ATE na serikali wakakubaliana huu ujinga?
Lkn pia mifuko imejiingiza kwenye biashara ya REAL ESTATE ambayo pay back period yake ni miaka mingi isitoshe magorofa mengi ya NSSF, PSPF SIJUI PSSSF hayana wapangaji na yamejengwa kwa mapesa mengi Sana. Lkn pia ubadhirifu. Imagine Kuna mkurugenzi mmoja kila jumamosi liwake au inyeshe alikua anakwenda uingereza kuangalia mechi za premier league.
Yaani yeye mechi za NEW CASTLE , ARSENAL NA MABINGWA LIVERPOOL anazionaga LIVE.
 
Ya Ulaya huku kwa wacheza singeli hayatekelezeki!
Tatizo ni panya. Inawezekana kabisa tukipata katiba mpya. Hela Kama hii haihitaji msukosuko Mara kukopa Mara kuiba Mara matumizi ya office na vikao. Hili linatakiwa liingie kwenye katiba.

Itafutwe chombo Kama bunge lisimamie hao wafanyakazi. Mfanyakazi akivurunda haiwezi kuwa Siri lazima litabumburuka tu hata Kama ni Rais kakopa lazima wabunge watahoji. Na wao si watakuwemo.
 
Itafutwe chombo Kama bunge lisimamie hao wafanyakazi. Mfanyakazi akivurunda haiwezi kuwa Siri lazima litabumburuka tu hata Kama ni Rais kakopa lazima wabunge watahoji. Na wao si watakuwemo
Bunge gani?
Hili hili la Tulia?!!!
 
Mimi naona wangetoa uhuru kwa wastaafu kuchagua aina ya kikokotoo wakipendacho baada ya kustaafu. Mfano mstaafu anayetaka kupewa hela zake zote, apewe! Na yule anayetaka kupewa hiyo 33% kwanza, apewe! Mtu asipangiwe matumizi ya hela yake.

Hii mambo ya kulazimisha kulipana hela pungufu, ni upuuzi. Mbona hao Wabunge hicho kikokotoo hakiwahusu? Au wao wanajiona wana uwezo mkubwa wa kutunza pesa kuliko wastaafu wengine?

Serikali iache mambo ya wizi kwa wastaafu.
Issue kubwa nadhani serikali itakua haipeleki michango huko kwenye mifuko ndo maana wanawekea watu vikwazo kwamba upewe 33% kwanza kubadilisha tu kile kikokotoo cha zamani na kuleta hiki kipwa kuna hela nyingi sana mtumishi anapunjwa...
 
Huyu akimaliza miaka mitano anakusanya jasho lake lote na nyongeza juuu...
images (13).jpeg





Huyu baada ya miaka 60 akistaafu anapewa 33/% na zingine atapewa kidogo kidogo....
images (14).jpeg
 
Bunge gani?
Hili hili la Tulia?!!!
Hapana. Kama katiba mpya ikipatikana. Lazima wabunge wa upinzani watakuwepo. Hili tumwachie Tulia na Msukuma.

Yaani wazee wanatesa ndiyo wenye pesa huko acha kabisa. Ukipokea pension na mkeo na kila mwezi account Zinacheka miaka 💯 lazima uione mjomba.
 
Lakini wabunge wakimaliza miaka mitano wanapewa 200m yote...ila uliesota miaka 60 kuitumikia serikali unakula 33% kwa style hii hakuwezi kua na uwajibikaji serikalini hata siku moja
piga chinu ccm
 
Mimi naona wangetoa uhuru kwa wastaafu kuchagua aina ya kikokotoo wakipendacho baada ya kustaafu. Mfano mstaafu anayetaka kupewa hela zake zote, apewe! Na yule anayetaka kupewa hiyo 33% kwanza, apewe! Mtu asipangiwe matumizi ya hela yake.

Hii mambo ya kulazimisha kulipana hela pungufu, ni upuuzi. Mbona hao Wabunge hicho kikokotoo hakiwahusu? Au wao wanajiona wana uwezo mkubwa wa kutunza pesa kuliko wastaafu wengine?

Serikali iache mambo ya wizi kwa wastaafu.
Mwizi ndiye anayepanga. Ni mwendo wa maumivu
 
Huu ndio upuuzi ambao wanasiasa wanasababisha kwenye hii nchi. Kuweka matabaka kwenye jamii.

Wao ( Mbunge, Mkuu wa mkoa na bosi ) wao haiwahusu ila wafanyakazi ambao ni tabaka linalotawaliwa.

Ni wazi sasa hakuna wa kuwasemea wasio na sauti. Shame on you politicians!
Shame on us wananchi. We failed big kuendelea kutawaliwa na CCM mpaka sasa.
 
Ufafanuzi kwa wanaujua madhara au faida zake tafadhali. Kwa maelezo hayo tuu haitoshi kujua mataafu anafaidika au anapunjwa kwa kiasi gani. Weka nyama nyama na supu tuweze kuelewa, kwa mwenye uelewa wa kutosha. Hesabu ya ulinganifu inahusika hapo
Faida ni chache hasa ni ongezeko la posho ya kila mwezi. hasara ni nyingi mfano mtmishi akifa mapema kila kitu kinaishia hapo. Mtumishi aliyejiandaa akiwa kazini na anataka kukuza mtaji wake na hela ya mkupuo atapungukiwa mtaji. Mfano mtumishi alitamani kukuza mradi wake wa kilimo kwa kununua mashine kama trekta na mashine za uchakataji ataweza kushindwa kufanya hivyo.
Kwa walevi na wazembe inaweza kuwa na manufaa
 
Tatizo ni panya. Inawezekana kabisa tukipata katiba mpya. Hela Kama hii haihitaji msukosuko Mara kukopa Mara kuiba Mara matumizi ya office na vikao. Hili linatakiwa liingie kwenye katiba.

Itafutwe chombo Kama bunge lisimamie hao wafanyakazi. Mfanyakazi akivurunda haiwezi kuwa Siri lazima litabumburuka tu hata Kama ni Rais kakopa lazima wabunge watahoji. Na wao si watakuwemo.
Tanzania fedha inayokopesheka haraka haraka ni ya mifuko ya hifadhi ya jamii. Serikali inaitumia ovyo ovyo zaidi ya inavyotumia fedha za wahisani.
 
Jana, statement toka Ikulu ilieleza kuwa Rais Samia amepokea mapendekezo ya kanuni mpya ya mafao ya Pensheni, kama ilivyoombwa na chama cha wafanyakazi Tanzania (TUCTA) siku ya sherehe za wafanyakazi (Mei Mosi, 2022), ambapo sasa amekubali ombi la kupandisha malipo ya mafao, kutoka 25% iliyokataliwa na wadau hadi 33.3%.

Ametaka TUCTA, wizara ya fedha na Chama cha Waajiri (ATE), kuendelea kushirikiana ili kukamilisha taratibu za malipo ya mkupuo huo wa asilimia 33.3% badala ya 25% iliyokataliwa mwaka 2018.

Kanuni za Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ya Mwaka 2018, ziliweka kikokotoo kimoja cha asilimia 25 ambacho kiliweka usawa kwa wastaafu wote kupata mafao yenye fomula moja, tofauti na awali kulipokuwa na fomula mbili.

Kikokotoo kipya kwenye kanuni kilikuwa ni asilimia 25 kwa mafao ya mkupuo na asilimia 75 inayobaki kulipwa kama pensheni ya mwezi kwa kila mwezi hadi mwanachama atakapofariki dunia.

Hata hivyo, katika kikokotoo hicho, umri wa kuishi ulikadiriwa kuwa ni miaka 12.5, ikiwa ni umri uliokadiriwa kuwa mwanachama ataishi baada ya kustaafu.

Kwa mujibu wa kikokotoo cha NSSF ambacho kimekuwapo kwenye kanuni za shirika hilo tangu mwaka 2014, mwanachama anapostaafu analipwa asilimia 25 ya mafao ya mkupuo na kilichobaki kinalipwa kama mshahara wa kila mwezi.

Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ya Mwaka 2018, imetaja jumla ya mafao saba ambayo ni manne ya muda mfupi (fao la upotevu wa ajira, fao la ugonjwa, fao la uzazi na mkopo wa nyumba) na matatu ya muda mrefu ambayo ni pensheni ya uzeeni, fao la ulemavu na fao la warithi.

Kwa hili, niseme Rais Samia na serikali yake wanastahili pongezi.
Pensheni ya Kila Mwezi nayo kaongeza kwa Asilimia 17 Hongera sana Mama

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom