sitagliptin
JF-Expert Member
- Mar 10, 2023
- 1,208
- 2,525
kisa makonda na bado ally happy afu makala anapigwa chini
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ally Hapi nasikia anapiga jaramba 😅kisa makonda na bado ally happy afu makala anapigwa chini
Mwenyekiti ni mtu mkubwa sana ndani ya Chama !kisa makonda na bado ally happy afu makala anapigwa chini
Kwa nchi ambazo zinapima hata maelezo ya mtu tu kabla ya kumpa nafasi ya kugombea urais, Kikwete hakutakiwa kuwa rais.
Tatizo Tanzania hatupimi.
Kikwete anaweza kuwa anaelezea kitu, ukaona kafika katikati ya kukielezea, hajamaliza, halafu kumbe mwenzako ndiyo kashamaliza bila conclusion hapo.
Hata hiyo story ya Zacharia Hans Poppe sijui ni muandishi kafanya uzembe hakuandika conclusion ilikuwa vipi, au ni Kikwete mwenyewe hakutoa conclusion alilifanyia kazi vipi hilo suala.
Ila siwezi kushangaa ikiwa Kikwete katoa story nusu bila conclusion halafu kawaacha watu homework, fill in the blanks.
Ana tabia hiyo sana, halafu ni kama yeye mwenyewe haelewi kwamba amesema mambo in unfinished sentences.
Kikwete ana tabia ya kuongea kama vike watu wote wanaweza kuona anafikiria nini kichwani mwake, hivyo hata asipomalizia sentensi, wataelewa tu kwa kuona mawazo yake.
Unashangaa, huyu kapewaje urais?
Sema waliojengewa na Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na Mzee Karume wale ndio waliasisi misingi ya taifa hili. Wengine tunatambua jitihada zao.Huku anaongea kijana Mzalendo Makonda, Polepole, Heche, Lisu Halafu kule anatokea MTU aliyegawa Vitalu vyote Vya gesi Kwa Wageni Tena Kwa kupitia mtutu Wa Bunduki.
Leo hakuna faida yoyote kwenye gesi.
Huyu MTU anatumia nguvu ya pesa aliyojilimbikizia kuhujumu nchi Kwa muda Mrefu.
Anakera WATANZANIA wengi waliojengewa uzalendo na JPM.
Word...Ndio maana kuna umuhimu sana wa utawala wa kimajimbo, kutawanya risks na kupunguza ukali wa maumivu ya makosa ya watawala yanapofanyika.
Wivu na chuki zitakuua wewe hater.ukitaka kupima uwezo wa raisi yoyote mstaafu Duniani angalia post presidency yake anafanya nini? Hata tu foundation ya kusaidia jamii hakuna, haandiki vitabu, hakuna chochote intelectually, I mean nothing, hilo peke yake linakwambia mengi sana, kila kukicha majungu tu …
Ukiwa CCM huwezi kuwa na uwezo Huo kwani wasio na uwezo ndiwo wanaotakiwaHata kama Rais hajui kila kitu, lazima awe na uwezo wa kuchanganua mambo ili asidanganywe, tatizo linakuja kama hata huo uwezo wa kuchanganua mambo haupo, hapo inakuwa bora hata huo ushauri wenyewe asipewe.
Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Wivu na chuki zitakuua wewe hater.
Kikwete ndiye owner wa Tanzania
Hawezi kukaa kimya nchi ikiyumba
URAIS uliishia kwa KIKWETE! Hawa wengine wanajaribu jaribu tu 🙏🏽 😂Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete amesema Serikali ikikosa ushauri mzuri ama ikipuuza nchi itakwenda pasipostahili.
Kikwete ametoa kauli hiyo leo Jumatano, Novemba 22, 2023 alipokuwa akielezea umuhimu wa makongamano na mikutano katika kuishauri Serikali na Rais, kwenye mkutano wa nne wa Maendeleo ya Biashara na Uchumi ulioandaliwa na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) ambapo alikuwa mgeni rasmi.
“Ukikosa ushauri mzuri ama ukipata ushauri mzuri ukaupuuza hii nchi itakwenda kusikotakiwa kwenda. Ndio maana makongamano haya ni muhimu sana unachota mawazo,” amesema Kikwete aliyekuwa Rais wa nne wa Tanzania (2005-2015).
Amesema unapokuwa Rais hujui kila kitu lakini unatakiwa kushughulika na kila jambo na kwa sababu huwezi kujua kila kitu inakubidi kutegemea ushauri.
“Wenzako wanakuchagua kwamba unafaa kuwa Rais, lakini utakuwa hujui kila kitu, taaluma yako ni uchumi…lakini ukiwa Serikali na Rais hujui kila kitu. Kwa sababu huwezi kujua kila jambo, lazima utegemee sana ushauri,” amesema.
Amesema ndio maana Rais ana mawaziri, naibu mawaziri, makatibu wakuu, naibu makatibu wakuu, makamishna, wakurugenzi na ofisi binafsi ambayo inawashauri.
Amewataka wasomi hao kutoa ushauri kwa Serikali juu ya mambo mazuri ya kufanya na kile ambacho si kizuri kiachwe na kirekebishwe.
Kikwete amesema uchumi hauwezi kukua bila uwekezaji, na unakuwa mahali ambapo mazingira ya biashara ni rafiki ikiwa vinginevyo wawekezaji wataondoka.
Ametoa mfano wa mfanyabiashara maarufu, marehemu Zacharia Hans Poppe ambaye wakati wa uhai wake alikutana naye nchini Afrika Kusini.
Amesema mfanyabiashara huyo alimweleza amehamishia biashara zake na magari yake yote nchini humo kutokana na mazingira ya biashara kutokaa vizuri nchini.
Amepongeza chuo hicho kwa kuandaa kongamano hilo, lakini akashauri kuangalia uwezekano wakuandaa lingine ambalo litashirikisha taasisi nyingine za elimu za juu.
Kikwete amesema kufanya utafiti ni njia ya kuboresha upeo na maarifa ya kila mtu na itasaidia katika maendeleo ya Taifa.
Bei za mafuta kupanda
Kikwete amesema iwapo bei ya mafuta imepanda katika nchi zinazozalisha ni wazi haiwezi kupungua nchini.
“Namshukuru Rais (Samia Suluhu Hassan) kwa utashi wa kisiasa ameweka ruzuku ya Sh100 bilioni lakini hii inapunguza kwa senti chache. Wakishaweka ruzuku ya Sh100 bilioni bei ya mafuta inapanda tena.
“Kwa hiyo ndio mazingira tuliyonayo hadi wakimaliza vita (Ukraine na Israel) na kuruhusu mafuta yao kuingia katika soko tutakuwa na nafuu,”amesema.
Kikwete amesema hali hiyo ipo pia kwa mbolea, mafuta ya kula na ngano ambazo wazalishaji wakubwa ndio nchi hizo zinazopigana vita.
Amesema nchi moja tu ni vigumu kutatua, hivyo kunatakiwa kuwe na ushirikiano wa nchi zaidi ya moja.
Amesema hakuna nchi iliyopiga hatua za maendeleo kwa kujifungia yenyewe bila kushirikiana na nchi nyingine.
Aidha, amesema maendeleo ya nchi yoyote ya uchumi huchochewa na matumizi sahihi ya tafiti na ushauri wa kitaalamu, kinyume cha hapo maendeleo ni madogo.
Akizungumza awali, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Ashatu Kijaji amesema sasa ni wakati wa kuwa na kozi fupi za wajasiriamali walioko nchini.
“Tumejiwekea malengo ya kuainisha wajasiriamali wale wanaoanza ndani ya mwaka mmoja tuweze kuwakuza baada ya miaka mitatu waweze kuwa wajasiriamali wa kati na hatimaye tutengeneze wafanyabiashara wakubwa na mabilionea,” amesema.
Amesema wao ndio wanaowafundisha wafanyabiashara wanapaswa kuwaonyesha namna ya kutoka walipo, mahali pa kupata mitaji ili waanzishe biashara.
Dk Kijaji amesema yapo machapisho duniani yanayoonyesha kuwa biashara baada ya miaka mitatu hufa, hivyo kuna kazi ambayo wao kama chuo hawajaifanya kikamilifu.
Naye Mkuu wa Chuo cha CBE, Profesa Edda Luoga amesema tafiti zitakazokuwa bora zaidi katika kongamano hilo wanatarajia zitachapishwa kwenye majarida, kmtandao wa chuo hicho.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi wa Chuo hicho, Profesa Wineaster Anderson amesema wana mpango wa kupanua huduma zake ili kuwafikia walengwa wengi nchini na mipango hiyo inatazama zaidi visiwa vya Zanzibar, mikoa ya Lindi na Iringa.
Classic Kikwete 1.ukitaka kupima uwezo wa raisi yoyote mstaafu Duniani angalia post presidency yake anafanya nini? Hata tu foundation ya kusaidia jamii hakuna, haandiki vitabu, hakuna chochote intelectually, I mean nothing, hilo peke yake linakwambia mengi sana, kila kukicha majungu tu …
Huyu mzee Rajabu ndie kamshauri amteue Makonda?Ukisikia system, wenye chama au wenye nchi ni watu kama ‘Rajabu Lhuwavi’.
Kipindi cha JK alikuwa mshauri wake wa siasa, sasa hivi mshauri wa ‘bi tozo’ wa siasa, kwa akili ya kawaida nani kamrudisha Ikulu kama sio JK.
Nina uhakika alichosema JK kimechukuliwa out of context; vinginevyo JK akitaka ku influence siasa za Samia anawatu wake ndio wanaomshauri raisi serikalini na kwenye chama.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Classic Kikwete 1.
Kikwete akiwa rais wa Tanzania alikaa kwenye panel katika mkutano wa kimataifa, alikuwa kakaa karibu na Bob Geldof. Bob Geldof ni mwanamuziki wa ki Irish aliyekuja kuwa mwanaharakati na kusaidia sana kuandaa kurekodi na kufanya concert ya "We Are The World" kuokoa watu kutoka njaa Ethiopia. So alikuwa anti povery activist.
Bob Geldof alimuuliza Kikwete swali moja dogo sana.
Aliuliza, kwa nini Tanzania ni masikini?
Kikwete akasema hajui kwa nini Tanzania ni masikini!
Nilisikitika sana. Huyu ni mtu aliyegombea urais wa hii nchi bila hata kuwa na jibu la swali hili.
Yani si kwamba hana utatuzi wa matatizo ya umasikini Tanzania, hajui hata sababu ya umasikini, na bila kujua sababu za tatizo, atatatua vipi tatizo?
Classic Kikwete 2.
Kikwete aliylizwa na muandishi wa Tanzania. Hii ni baada ya kustaafu. Kumbukumbu yake nzuuri kabisa kutoka urais wake ni ipi?
Akasema walikuwa wameenda kwenye mkutano Spain, akaona concert ya Michael Jackson, ile concert ndiyo ilikuqa kumbukumbu kubwa kabisa ya urais wake wote!
Nikasema sawasawa.
Kwa viongozi kama hawa, naweza kuelewa kwa nini Tanzania ipo katika lindi la umasikini.
Makonda kafanya nini?Duniani kote makampuni makubwa yanawalipa mabilioni wale wenye mchango Mkubwa kwenye kampuni.
Paulo Makonda anafanya KAZI kubwa sana .
Makonda anastahili kulipwa Hata pesa yote ya chama . Na pia pesa ya Mwenge yote alitakiwa apewe Makonda. Makonda ni Mzalendo halisi. Natamani 2025 ningekua Rais nimteue Makonda kuwa Waziri Mkuu.
CCM inamuhitaji makonda kuliko makonda anavyoihitaji CCM Kwa WAKATI Huu ambao vijana wengi zaidí ni maskini na wanaamini kuwa Dr. Samia yupo Kwa ajili ya kutetea maslahi ya matajiri Wa Chache na familia Zao. Vijana wengi sana Wana Imani na Makonda kuliko MTU yeyote Kwa Sasa ndani ya CCM .
Kwani hukumbuki waliambiwa wanawashwawashwa?Nawaza kama angeyasema hayo wakati wa JPM sijui angejibiwaje?
Wewe kujiaminisha huko CCM au serikalini, sijui Kinana na Chongolo wamekwazika kwa sababu ya uteuzi wa Makonda aina maana huo ndio uhalisia.Huyu mzee Rajabu ndie kamshauri amteue Makonda?