Kikwete atoa kauli kuhusu kikombe cha Babu wa Loliondo msibani kwa Malecela. Kauli hiyo inasemekana kumlenga aliyekuwa Waziri katika Serikali yake

Kikwete atoa kauli kuhusu kikombe cha Babu wa Loliondo msibani kwa Malecela. Kauli hiyo inasemekana kumlenga aliyekuwa Waziri katika Serikali yake

Huyu 'cheka cheka' anaonesha alikuwa na bifu kali sana na Magu.
Hata haamini kwamba ameshafunga kauli na hawezi kujitetea tena.
Ukiwa umeacha amali nzuri huku duniani, ukiwa umeacha hadithi nzuri ya maisha yako huku duniani basi utakuwa hadithi nzuri, na amali nzuri zitakusemea pale ambapo hautakuwa na uwezo wa kusema... (Mzee Ruksa, 2021)
 
Jk kwa sasa anaonekana sana kwenye media.

Sijui kuna jambo gani nyuma ya pazia.
FB_IMG_16449986919504410.jpg

uongozi tulionao sasa, kwenye media tunaona anamchoma na kisu kumbe anakimbia asichomwe na kisu.

tunaona tunaongozwa na gauni kumbe ni kanzu.
 
Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DR.Jakaya Mrisho Kikwete ametia ya moyoni akiwa msibani kwa John Malecela kuwa wakati wa kikombe cha babu wa Loliondo wamo Mawaziri katika Serikali yake walienda kunywa kikombe hicho na amesema kuwa wengine walikuwa wakimwambia wanatengeneza barabara.

Na ameenda mbali zaidi kwa kusema kuwa katika jamii ya kitanzania wapo wanaoamini kuwa kama mganga akimwambia anakuloga huamini moja kwa moja na akiambiwa kuwa ameoteshwa na kitu chochote huamini hivyo hivyo.

Aidha hiki ni kipande cha clip alichosema msibani hapo.

Kumsema marehemu ni vibaya sana.
Naomba niishie hapo.
 
Hii katiba ina viraka vingi sana.

Maana ni katiba hii ya mwaka 1977, ilifanyiwa amendment ili kuanzia 1995 Rais agombee na mgombea mwenza (running mate) kama US. Na bila shaka walifanya hivi ilikitokea Rais wa JMT katokea chama A na Zenji CUF ilikuwa na nguvu sana, basi Rais wa Zenji asiwe VP by default na ndio Zenji Rais wao akawa sio makamu wa Pili wa Rais kama Rais katokea Zenji.

Kiukweli hii katiba ya 1977 imeshonwa sana, ni vema ile rasimu ya Warioba ingesongeshwa; ila sasa ndio hivyo. Walioanzisha mchakato hawakuwa na nia ya kweli ya kutupa katiba.
Walitaka katiba iwe kick ya mpito ili muda wao wa kuondoka madarakani uende huko focus ya watu ikiwa katiba mpya.

Tanzania ni zaidi ya tujuavyo.
Hivi Kuna anayejua ni kwa nini JK alianzisha ule mchakato wa katiba mpya? Maana wala haikuwa kwenye ilani wala mipango yao, nini kilimsukuma hasa?
 
Back
Top Bottom