Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

- Kama CC ya CCM itashindwa kumzuia Lowassa asigombee kama ilivyofanya mara mbili kwa Mzee wetu JSM ambaye hatujawahi kuelezwa kosa lake ni nini hasa;
- Kama UwT nao watashindwa kuwashawishi CCM kuliondoa mapema jina la mlafi huyu kama walivyomwacha JMK akampa UwaziriMkuu wa NCHI yetu;
- Kama vyombo vya habari navyo vitajiingiza kwenye kampeni chafu dhidi ya wagombea wengine SAFI ili kumsaidia Lowasa kama walivyofanya akina Salva mwaka 2005;
- Kama KATIBA MPYA haitakuwa na MIIKO na SIFA nzito za KIONGOZI MKUU wa TAIFA hili;

TANZANIA kama TAIFA baada ya 2015 iko mashakani.
 
August, nakuomba uamini sio kweli watetezi wote wa Lowassa humu wamelipwa!. Just amini hivyo!.
Mimi Pasco (wa jf) ni mmoja wa watetezi wa Lowassa ateuliwe kuwa mgombea wa CCM nikiwa sina chama wala sijapewa senti tano ya mtu awaye yote!.

Nature ya mwanadamu inadictate kuwa lazima kuna motive inakudrive kufanya uamini kitu/mtu bila malipo yeyote. Only logical proposition labda kama alivyosema mtoahabari unaweza kuwa ni big fan wa Mh. WILLIAM HAGUE. Wewe uliyepo nje hujui huku bongo tumechoka kiasi gani na huyu mtu.
 
Nature ya mwanadamu inadictate kuwa lazima kuna motive inakudrive kufanya uamini kitu/mtu bila malipo yeyote. Only logical proposition labda kama alivyosema mtoahabari unaweza kuwa ni big fan wa Mh. WILLIAM HAGUE. Wewe uliyepo nje hujui huku bongo tumechoka kiasi gani na huyu mtu.

Wrong thinking. We have to remain positive on others unless propelled by positive and constructive evidence to think otherwise.

Hii dhana ya kila anayefikiria tofauti KAHONGWA au kuna kitu ndo inafanya Tanzania haiendelei. Tumejifungia kwenye BOX. Vipi ukiambiwa kuna kitu najua ambacho sitaki kusema kwa hao mnaoona wanafaa ambacho ni kibaya kuliko mabaya mnayozungumzia ya EL?.

Anyway, acha sisi tuendelee kufunga mikanda kwenye ELairline.
 
The boss, unazungumzia laana mara ngapi?. Hii iliyopo haitoshi?!. Ndio maana tunataka ukombozi na ukombozi huo ni kwa kupitia kwake!.

Najaribu sana kukuelewa Pasco kupitia post zako mbalimbali. Mwshowe, nafikiri unamaanisha kuwa kupitia kwake, itakuwa rahisi kwa upinzani kuchukua uongozi i.e. kama akichaguliwa kuwa mgombea urais wa CCM. Kwa maneno mengine, si yeye atakayeleta ukombozi huo moja kwa moja, ila unaombea na unashabikia ili CCM wafanye kosa la kumruhusu yeye kuwa mgombea.
 
Najaribu sana kukuelewa Pasco kupitia post zako mbalimbali. Nafikiri unamaanisha kuwa kupitia kwake, itakuwa rahisi kwa upinzani kuchukua uongozi i.e. kama akichaguliwa kuwa mgombea urais wa CCM. Kwa maneno mengine, si yeye atakayeleta ukombozi huo moja kwa moja, ila unaombea na unashabikia ili CCM wafanye kosa la kumruhusu yeye kuwa mgombea.

LOL ahahaha Umenichekesha.
 
Wrong thinking. We have to remain positive on others unless propelled by positive and constructive evidence to think otherwise.

Hii dhana ya kila anayefikiria tofauti KAHONGWA au kuna kitu ndo inafanya Tanzania haiendelei. Tumejifungia kwenye BOX. Vipi ukiambiwa kuna kitu najua ambacho sitaki kusema kwa hao mnaoona wanafaa ambacho ni kibaya kuliko mabaya mnayozungumzia ya EL?.

Anyway, acha sisi tuendelee kufunga mikanda kwenye ELairline.


haki ya nani mkuu una ujasiri balaa.......nakushauri walau uwe na parachuti pembeni maana.....!!!!
 
haki ya nani mkuu una ujasiri balaa.......nakushauri walau uwe na parachuti pembeni maana.....!!!!

Edson,
Haki ya nani nimecheka balaa mpaka naulizwa na my waifu nacheka nini! ahahahaha yaani una mambo?

Vipi lakini usharudi Bongo?. Sio ujasiri ndugu yangu, Ninaaamini hivyo. Lowassa ndie anafaa.

Karibu basi hata economy class ya ELairline!
 
Mkuu wangu FP,

Leo naomba niwe na Fikira Duni [zama zile za enzi na enzi]. Sidhani kama Tanzania ya leo inahitaji kiongozi aina ya Lowassa. Tanzania ya leo inahitaji kiongozi mwadilifu, asiye na makundi, asiye na mtandao na awe mchapa kazi. Katika hayo yote Lowassa ana sifa moja tu ya uchapa kazi, ambayo kila mtu anaweza kuwa nayo.

Hoja ya UTHUBUTU: Tanzania ina viongozi wengi sana ambao wana UTHUBUTU, lakini je huo uthubutu wanautumia kwa malengo yepi?

Tukumbushane kidogo: Mkapa alishawahi kuonyesha uthubutu pale alipowasemea mbovu wafadhili [specifically UK] pale Mama Clare Short alipojiuzulu kwa kitendo cha BAE kutuuzia radar. Mkapa alionyesha mamlaka na uthubutu wa kufanya maamuzi, kwamba serikali imeridhia kununua radar, lakini ukweli ni kwamba it was a "deal". Wapo waliosema Mkapa ni mwanaume anawakoromea mpaka wafadhili. Leo hii kiko wapi? Radar aliyoitetea imekuja kugundulika ni dili na tena waliogundua ni hao hao aliowatukana. Serikali iko kimya, imepewa details zote za mgao wa fedha, je imefanya nini?

Mkapa alikuwa ni champion wa globalization, watu wakasema Tanzania inaelekea kwenye neema na kwamba ni moja ya top destinations za FDI kwa Sub-Saharan Africa. Kiko wapi? Kumbe hao wawekezaji wote walikuwa ni wapiga dili tu kwenye migodi. Unakumbuka Mkapa alivyokuwa anatetea wawekezaji wa kwenye sekta ya madini? Unakumbuka alivyotumia FFU kuwaingiza NetGroup Solution? Viongozi wetu wengi wana uthubutu na pia huwa wanaonyesha mamlaka, lakini uthubutu wao mara nyingi uthubutu wao na mamlaka waliyonayo huwa wanayatumia kwa faida yao wenyewe, familia zao na marafiki zao. Huo ni uthubutu wa kifisadi wa kuwaambia wananchi wale nyasi na huku yeye anapokea 10%! Huo ni uthubutu wa kifisadi.

Richmond ambayo ndio imekuwa kitanzi cha Lowassa, wengi wamemtetea kwamba hilo halikuwa zigo lake bali la JK. Yeye akiwa Waziri Mkuu ilikuwaje akakubali kutumiwa na huku akiona kabisa kwamba mwelekeo haukuwa mzuri? Kiongozi mwenye uthubutu wa uadilifu angejiweka pembeni. Kama yale maneno ambayo yaliandikwa kwenye magazeti kwamba Lowassa alimpigia simu JK akiwa ughaibuni kwamba wavunje mkataba na Richmond na Rais akasema amepewa ushauri mpya na Kamati ya Makatibu Wakuu, kwanini baada ya hapo Lowassa hakujiweka kando? Huo ndio uthubutu wa uadilifu kwamba umetoa ushauri mzuri na ukaona hausikilizwi, kaa pembeni badala ya kupendekeza kuingizwa mikenge mingine.

Bado watetezi wanasema kwamba baada ya JK kuona Richmond imekwama, JK aliomba ushauri kwa Lowassa. Lowassa akasema kuna mtu mmoja [Rostam Aziz] anaweza kutusaidia, na ndio tukaingizwa mkenge mwingine wa Dowans ambayo bado inawatesa mpaka leo. Kiongozi mwenye uthubutu hawezi kutafuta short cuts kwa kuwatumia marafiki zake ili kutatua matatizo makubwa kama hayo. Kiongozi mwenye uthubutu angependekeza kusitisha mkataba wa Richmond na kushauri mchakato uanze upya badala ya kupendekeza kuuingia mkenge mwingine.

Msimamo wangu siku zote ni huu, ndani ya CCM hakuna ambaye ana afadhali au ambaye anafaa kuwa Rais kwa sasa. Wengi wao wana uthubutu, wanajua mamlaka waliyo nayo lakini huwa wanaishia kutumia uthubutu huo na mamlaka kwa faida yao wenyewe na kulindana within CCM circles.

Sababu zinazonifanya niwaogope viongozi kutoka CCM ni hizi:

Hakuna mwana CCM atakayechaguliwa kuwa Rais ambaye atakuwa tayari kushughulikia maswala yote ya ufisadi kwa kuwa ndani ya CCM wapo ambao ni "untouchables" na ndio wamefanya ufisadi mkubwa sana ndani ya nchi hii. Mkapa alipoingia madarakani mwaka 1995, alisema tuhuma za ufisadi/rushwa zinatosha sana kumsimamisha kazi kiongozi wa umma. Kipande cha maneno hayo kilikuwa kikirushwa sana na Redio Tumaini, Redio ya Ujirani. Kauli hiyo ilikuwa ni mwiba mchungu wenye ukweli, kwamba mtu aliahidi kupambana na rushwa na ufisadi lakini alipoingia madarakani akawa fisadi namba moja na mla rushwa mkubwa. That was our dearest Mr. Clean!

JK alipoiingia madarakani watu walikuwa na matumaini makubwa sana kwamba ufisadi uliofanyika chini ya Mkapa ungeshughulikiwa na kama unakumbuka watu walikuwa wakisubiri kwa shauku sana outcome ya ziara ya JK pale BoT wakijua kwamba kitendawili cha Twin Towers kingeteguliwa, maana ndio kilichokuwa kikijulikana wakati huo. Dili za EPA zilikuwa bado hazijawa wazi. Siku JK alipoingia BOT waandishi walizuwiliwa na hakuna anayejua kilichoongelewa huko ndani na hakuna kilichotokea baada ya hapo. Serikali imesubiri mpaka Ballali kafa ndo wanakuja kupeleka kesi ya Twin Towers mahakamani wakati shahidi mkuu ameishapotea. JK alisema nyumba za serikali zingerudi, zilirudi? Alisema mikataba ya madini itapitiwa upya na kusitisha kusaini mikataba mipya, je imeishapitiwa? Sana sana tulishuhudia sakata la Mkataba wa Buzwagi ukisainiwa. Hayo yote yanakuonyesha kwamba JK alikuwa na nia au alionyesha uthubutu hata wa kutamka tu kwamba atayashughulikia, leo hii muulize kulikoni hayajashughulikiwa? Hakuna jibu la kueleweka sana sana anajuta kwanini aliahidi hayo na ndio maana 2010 akaja ahadi mpya zaidi ya 80 na kwa kuwa Tanzagiza ni taifa la wadanganyika, tayari walishasahau na kuamini ahadi mpya za kwenye kampeni.

Mfumo wa CCM uliopo ni wa kulindana. Sophia Simba alishasema kwamba ndani ya CCM hakuna msafi, once wakianza kunyoosheana vidole hakuna atakayesalimika. SO, kabla mtu hajawa rais lazima kwanza mafisadi wakuu wajiridhishe kwamba atacheza kwa tune wanayoitaka wao na kwamba hawezi kufunua mfuniko uliofunika uozo wa ufisadi uliofanywa na CCM na serikali yake. Ndo maana unawasikia akina Pinda wanamtetea Mkapa kwamba tumwache apumzike halafu wanasema Kiwira itarudi serikalini, tena bila aibu kabisa. Pinda huyo huyo anaonyesha jazba kwa Jairo na wakurugenzi wengine wa vimiji huko swekeni, lakini ukimtajia jina la Mkapa ananywea na kuanza kujiuma uma, ukitaja Meremeta anasema yuko tayari kusulubiwa lakini hawezi kuongelea hilo swala! Ukisema EPA anasema mafisadi wana nguvu sana, hivi kuna mtu ana nguvu kuliko serikali iliyo madarakani iliyo na vyombo vya dola kila kona?

Kwa hiyo hata kama mwana CCM angekuwa mwadilifu kiasi gani, akishapewa Urais kupitia CCM lazima alinde maslahi ya chama chake na serikali zilizotangulia. Ndio maana Lowassa alisema alikubali kujizulu ili kulinda heshima ya chama chake na serikali. Kama angegoma kujiuzulu basi maana yake ni kwamba serikali yote [hapa ninamaanisha kuanzia JK] ingedondoka! Sidhani kama huo ndio Uthubutu unaousema wewe. Kama kweli Lowassa ana uthubutu, basi angeanzia hapo kwa kusema kila kitu kwa uwazi na baada ya hapo anaweka wazi kwamba alikuwa anatumwa na JK kutekeleza maagizo. Huo ndio uthubutu wa kuwa mkweli kwa wananchi unaowaongoza na pia uthubutu wa kufanya maamuzi ambayo hayawaumizi wananchi au kuwaongezea mzigo. Je, kama Lowassa alijiuzulu ili kumlinda rafiki yake [JK] na chama chao, siku yeye [Lowassa] akipewa urais na akaja kuona kuna watu wa JK au vigogo wa CCM wanahusika na ufisadi, tuna hakika gani kwamba ataonyesha utthubutu kwa kuwashughulikia kwenye vyombo vya sheria?

Uthubutu ndani ya CCM haupo, kwa sababu ya mfumo wa kulindana. Kwa hiyo labda tutafute hoja nyingine na sio uthubutu ambao una dalili zote za kifisadi au kulinda ufisadi. Unakumbuka Sitta alipopelekewa nondo za ufisadi na Dr. Slaa? Alisema Slaa ni mzushi mara sijui anatumia info za kwenye mitandao ambazo hazina ushahidi. Sitta huyo huyo leo kuna watu wanasema ana uthubutu wa kutumia mamlaka ya Spika kumsulubu Zitto na kudanganya umma kwamba Dr. Slaa alighushi documents za ufisadi! Siku Zitto anasulubiwa baadaye Lowassa alitoa hotuba ya kufunga kuahirisha Bunge na kuishia kutishia wabunge kwamba wasicheze na serikali na kwamba kilichotokea kwa Zitto ilikuwa ni mvua za rasha rasha tu. Hiyo pekee inaonyesha wazi kwamba uthubutu wa Lowassa una walakini mkubwa sana. Mtu mwenye uthubutu wenye dhamira nzuri hawezi kutishia wananchi/wabunge kwamba watashughulikiwa. Kama serikali ni safi, kwanini iogope hoja za wabunge?

CCM haiwezi kutoa kiongozi [Rais] ambaye atakuja kubadilisha direction ya airline [kwa kutumia maneno yako] ili Tanzania isiende chini. Tayari tuko chini, na tukipata kiongozi mwingine kutoka CCM atakuwa anachimba ardhi ambayo ndio itakuwa kaburi yetu kama nchi.

Hii post namba 763 inamaliza propaganda zote za kina Fair Play, Pasco na wenzao. Mbona hawaijibu, na wanajifanya hawajaiona? Lowasa ana uthubutu , ( au Kama Mwakyembe alivyosema, "UJASIRI WA KIFISADI") wa Kifisadi.....sasa kama huo ndo akina Pasco mnautetea basi mko sahihi. Basi na mpigieni debe huyo "Jasiri" wenu ili nchi hii igeuke Mexico nyingine. Maana hapa Lowasa akipita, ni kwamba nchii hii haitatawalika , kwa vile makundi yaliyopo yote yatajianzishia "empire" zao ndani ya nchi hii, na mwisho tutawaliwe kwa "Cartels" za walevi hawa wa madaraka, kama zilivyo DRUG Cartels za Mexico. God Forbid!
 
Najaribu sana kukuelewa Pasco kupitia post zako mbalimbali. Mwshowe, nafikiri unamaanisha kuwa kupitia kwake, itakuwa rahisi kwa upinzani kuchukua uongozi i.e. kama akichaguliwa kuwa mgombea urais wa CCM. Kwa maneno mengine, si yeye atakayeleta ukombozi huo moja kwa moja, ila unaombea na unashabikia ili CCM wafanye kosa la kumruhusu yeye kuwa mgombea.
Wee Chief, usitake kutuharibia kampeni ya mgombea wetu, Lowassa msafi, mtakatifu!

Wewe hushangai Mzee Mwanakijiji hachangii thread hii?. Ameelewa soma na kujikalia kimya, waelewa wameelewa tunasimamia wapi, ndio maana na sisitiza ukombozi wa kweli wa nchi hii utapatikana kupitia kwake!.

CCM siku zote inashinda chaguzi mbalimbali kwa sababu inapendwa sana!, sio kwa kutake advantage ya ignorance yetu sisi Watanzania hivyo CCM hata wakisimamisha jiwe tuu litapita, sembuse Lowassa!.

Sasa baada ya kulielewa somo, tuungane, tumsafishe Lowassa, tumpake mafuta ang'are na kumeremeta, tumpulizie na manukato anukie vizuri, apendeke na kuongeza mvuto, CCM wamsimamishe awe mgombea wao!.
 
Hii post namba 763 inamaliza propaganda zote za kina Fair Play, Pasco na wenzao. Mbona hawaijibu, na wanajifanya hawajaiona? Lowasa ana uthubutu , ( au Kama Mwakyembe alivyosema, "UJASIRI WA KIFISADI") wa Kifisadi.....sasa kama huo ndo akina Pasco mnautetea basi mko sahihi. Basi na mpigieni debe huyo "Jasiri" wenu ili nchi hii igeuke Mexico nyingine. Maana hapa Lowasa akipita, ni kwamba nchii hii haitatawalika , kwa vile makundi yaliyopo yote yatajianzishia "empire" zao ndani ya nchi hii, na mwisho tutawaliwe kwa "Cartels" za walevi hawa wa madaraka, kama zilivyo DRUG Cartels za Mexico. God Forbid!
Mkuu Nyumbu hii tuliiona na tuliijibu, Lowassa ndiye atachaguliwa na ataigeuza nchi hii ya Tanzania kuwa ni nchi ya ahadi, nchi ya maziwa na asali!
 
Wee Chief, usitake kutuharibia kampeni ya mgombea wetu, Lowassa msafi, mtakatifu!

Wewe hushangai Mzee Mwanakijiji hachangii thread hii?. Ameelewa soma na kujikalia kimya, waelewa wameelewa tunasimamia wapi, ndio maana na sisitiza ukombozi wa kweli wa nchi hii utapatikana kupitia kwake!.

CCM siku zote inashinda chaguzi mbalimbali kwa sababu inapendwa sana!, sio kwa kutake advantage ya ignorance yetu sisi Watanzania hivyo CCM hata wakisimamisha jiwe tuu litapita, sembuse Lowassa!.

Sasa baada ya kulielewa somo, tuungane, tumsafishe Lowassa, tumpake mafuta ang'are na kumeremeta, tumpulizie na manukato anukie vizuri, apendeke na kuongeza mvuto, CCM wamsimamishe awe mgombea wao!.

Hewala, nimekuelewa.
 
Hewala, nimekuelewa.

Kumbe mna akili hivyo sasa kwanini toka zamani hamjiungi na ELairline?

Kauli mbiu hapa JF ELairline for 2015! hiyo ndo inatakiwa iwe salamu yetu humu watu wa EL hapa JF.
Pasco ukiiona ipo sawa basi tui endorse ianze kutumika. Kabla ya kuandika chochote tunaanza na hilo.
 
Keil,

Mkuu wangu sijui nianzie wapi. Maana umesema sana na upo sahihi kabisa. Bado namtetea Lowassa, naamini vyama vya upinzani havijakomaa na sio instutionalized kama CCM.
CUF = Maalim
CDM = Mtei, Ndesa, Mbowe, Makani
NCCR = Mbatia

Kwahiyo mgombea urais wa CCM ndio atashinda na CCM ndo chama huru ANGALAU.

Tukubaliane kutokubaliana mpaka nitakapomshawishi Mkandara akija bongo naye anisaidie namna ya kuelezea kuhusu Lowassa.

Ila bado naamini ELairline ndo airline pekee inayostahili kuwa NATIONAL carrier wa kuanzia 2015.

Hili bandiko ni matusi kwa baadhi yetu. Nitalitafuta na kulirejesha baada ya uchaguzi mkuu 2015 kama nitakuwa hai.
 
Pasco and company ya watetezi wa Lowassa,hatupingia au kutomtaka kwetu EL kuongooza nchi yetu si kwa sababu ya Richmond scum na hata sasa wanaomshabikia au kumchukia Lowassa sababu ya Richmond labda hawamfahamu vizuri.BTW sisi wengine kwa kuitakia mema nchi hii na kuiepusha janga(Lowassa) lingine kubwa ni ripoti ya mwalimu Nyerere kuhusu Lowassa na ukwasi aliovuna kwa kipindi kifupi akiwa mtumishi wa umma.Haya mengine ya kulawiti wanaume wenzie na wizi na ufisadi mwingine baada ya kuwa waziri mkuu ni muendelezo tu wa nia yake ovu juu ya nchi hii na uthibitisho wa dhahiri kwa walio-doubt ripoti ya Mwalimu au wale wasiomfahamu EL kwa undani.
 
Pasco and company ya watetezi wa Lowassa,hatupingia au kutomtaka kwetu EL kuongooza nchi yetu si kwa sababu ya Richmond scum na hata sasa wanaomshabikia au kumchukia Lowassa sababu ya Richmond labda hawamfahamu vizuri.BTW sisi wengine kwa kuitakia mema nchi hii na kuiepusha janga(Lowassa) lingine kubwa ni ripoti ya mwalimu Nyerere kuhusu Lowassa na ukwasi aliovuna kwa kipindi kifupi akiwa mtumishi wa umma.Haya mengine ya kulawiti wanaume wenzie na wizi na ufisadi mwingine baada ya kuwa waziri mkuu ni muendelezo tu wa nia yake ovu juu ya nchi hii na uthibitisho wa dhahiri kwa walio-doubt ripoti ya Mwalimu au wale wasiomfahamu EL kwa undani.

Kwani wewe huwezi kupima au kuona au kuelewa na kutoa mtazamo wako mpaka umtegemee MWALIMU(rip)?
MIE MAWAZO TEGEMEZI SIYAPENDI KABISA
 
The problem we are having is that; every body thinks that old people a wise and a true leaders. But be assured that is not applicable here in Tanzania and never will.

For CCM none who is mentioned is clean so for the next president i don't see anybody. they are all thieves and liars.

For the seak for of the new nation we are having so many educated young Boy and Girls, and i think we should take this opportunity and become true and patriotic leaders by claiming back our country from this traitors.

Am tied of all these people mention above because i know surely what they deserve is to stay behind bar at Keko period and all their properties taken.
 
....
Ukombozi wa kweli unaendana na uwazi [transparency]. Kwamba kila kitu kifanyike kwa uwazi na ikitokea madudu then watu wahoji na kupewa majibu na siyo kutishana ili watu wawe na hofu ili wasihoji madudu then mafisadi wanaendelea kutafuna mali kama mchwa!...

Mkuu Keil,
Nakubaliana na wewe kwamba uwazi katika siasa na mahali pengine ni kitu muhimu sana. Lowassa na viongozi wenzake wameshindwa kabisa kusema vyanzo vya utajiri wao usio na idadi , ndio sababu mpaka sasa hawajakabidhi tamko la mali zao kwa sekretarieti ya maadili ya umma, kwa kuwa hazitamkiki/hazina maelezo timilifu namna zilivyopatikana.

......Sasa Bwana Rashidi, nakuomba hivi, kamwambie mwenyekiti wa CCM Mhe. Mwinyi aitishe wajumbe wote wa Kamati Kuu, chagueni tarehe na mahali popote Tanzania, mimi nitakuja kumsafisha Bwana Lowasa na nitagharamia mkutano huo kwa hela zangu. Kamwe msitumie hela za chama wala serikali. Monduli sitokwenda,umesikia eh?”.....

Sipati picha hii Kamati Kuu ambayo Mwalimu aliagiza iitwe kwa gharama zake kwa ajili ya "KUMTETEA" (if any, at all) mtu ambaye hana imani naye hata tone, ingetoka na maazimio gani katika kikao hicho. Hatujaambiwa pia ni kwanini huyu 'Rais' mtarajiwa hakuhudhuria kikao hicho cha ana kwa ana na Mwalimu pale Msasani. Pasco tupe jibu, hope unafahamu.

...Kwa utetezi wangu kwa Lowassa bora tugombane tuu kwa sasa akishateuliwa tutapatana tuu!.
Mkuu Pasco,
Katiba inakuruhusu kuwa na msimamo huo, na uko sahihi. Unaweza kutupa mwanga kidogo kuhusu hoja za Kasori juu ya mgombea wetu mtarajiwa? Kwa nini hakwenda Msasani 'Kusafishwa' alipoitwa? Aliomba msaada wa Nyerere kusafishwa, je juhidi hizi zilifia wapi?

...SMU nakuhakikishia asilimia 100% kwa 100% utetezi wangu kwa EL ni kwa maslahi ya taifa!. Sina maslahi binafsi yoyote na sijapokea hata senti tano ya yeyote!
Mh. I smell something here. Hujaahidiwa kuteuliwa kweli?

- Kama CC ya CCM itashindwa kumzuia Lowassa asigombee kama ilivyofanya mara mbili kwa Mzee wetu JSM ambaye hatujawahi kuelezwa kosa lake ni nini hasa;..
WC,
Wewe ni mkongwe sana hapa JF, ina maana mpaka leo hujajua kwa nini JSM alienguliwa katika kugombea urais? Mbona tumeandika sana na hajakanusha? Suala ni kwamba, wakati wa hoja ya kuanzishwa serikali ya Tanganyika iliyopepelekwa na wabunge waliojiita G55 wakiongozwa na mbunge wa Chunya Mhe. Njellu Kassaka, JSM alikuwa waziri mkuu (kiongozi wa shughuli za serikali bungeni). JSM alishindwa kuwakemea wabunge wa chama chake kuacha hoja hiyo, kwa sababu si ilani ya chama chao na wala chama hakikuwatuma kwenda kuianzisha na kuitetea, hivyo walikuwa wanakiuka katiba ya chama. Kukiuka katiba ya chama kilichokuweka madarakanini makosa, hivyo wabunge hawa (G55) walikukua wamekosea sana.
Mantiki ikawa kwamba, kama alipokuwa waziri mkuu, alishindwa kusimamia kufutwa kwa hoja ndogo kama ile kiasi kwamba ikaleta rabsha bungeni na kutaka kugawa nchi, je akiwa raisi si ndo ataua muungano kabisa? Sababu hii ilitosha kabisa kumnyima ugombea. Hakuwa na msimamo. Hakuaminika. Soma kitabu cha 'Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania', kimekuwa-uploaded hapo juu kwenye jukwaa hili.
 
Híi michezo ipo katika kila chama ama nchi yeyote unapofika wakati wa chaguzi, lakini mwisho wa yote watu hurudi kati na kumpa nafasi aliyeshinda kugombea na kuongoza, umesahau ya Obama na H. Clinton? Mbona le wanaendesha Taifa na kila mmoja kwa nafasi yake.

Humtishi kikwete wala humtahadharishi hapa umeleta story2 ya kupokea mwaka 2012 tukiburudika.. ccm imekomaa bwana haya yote yatapita na jembe la 2015 litapatikana kwa njia hz hz lakini patabaki kuwa shwari watu wakila bata. Hata ungekuwa wewe madarakani ni lazima wangekuwepo ambao hawakukuunga mkono wakati wa mchakato, ila baada ya hapo ni kufanya nao kazi.

JK unadhani ananoma na hilo?.. Semeni na mengine yeye anajuwa kilichomgusa mpaka akagombea urais.

Aliguswa na wizi, ukwapuaji, ufisadi, udini, uuaji na ushirikiana tuu! hana lolote!! his days are numbered! hata kama atakwapua kiasi gani zijui atazitafunia wapi!! ha! ha!
 
Back
Top Bottom