Kila nikiwaza haya majanga nakosa hamu ya kupata mtoto

Kila nikiwaza haya majanga nakosa hamu ya kupata mtoto

Natamani sana kuwa na watoto, ila nina mambo yanayonikosesa furaha kila nikiwaza juu ya kuwa na watoto,.
Miongoni mwa mambo hayo nina makubwa mawili nayo ni;-

1. Umasikini, Umasikini ni janga kubwa kwa upande wangu, huwa nakosa amani pale ninapoiona kesho ya watoto wangu kwenye swala umaskini, sina njia mbadala ya kuwa kwamua watoto wangu kwenye hili janga.

2. MARADHI, Hili ni kubwa pia japo halilingani na la kwanza, mfano kwenye hili gonjwa la UKIMWI kila nikiiwaza kesho ya wanangu katika hili janga linanikatisha tamaa na kujiona mwenye hatia endapo ntawaacha watoto waje duniani na niwaingize kwenye hili janga.

3. Upofu, Maradhi ya akili kama uchizi, utahaira nk. Pia kuna maradhi ya moyo. Na hata kifafa. Huwa nakosa furaha kila nikiifikilia kesho ya kizazi changu na naona ni bora niishi mwenyewe na hata nikifa basi nife bila ya kuacha KIZAZI kisicho na furaha.

Nimeikopy facebook

Wee jamaa,hivi Wazazi wako km wangewaza hivyo wewe ungepatikana??.
 
You worry too much.

Have some little babies of your own.

They will be just fine.
 
Mkuu hayo uliotaja ni changamoto za maisha ambazo karibu ya asilimia.kubwa ya wabongo wamezaliwa nazo ila wamepambana na kuweza kupunguza au kumaliza kabisa. Kuhusu ugonjwa kuna watu nawajua wameoa/kuolewa wamezaa na maisha yanaendelea LA msingi amini yupo Mungu aliye hai ndiye ana hatima ya maisha yako fuata ushauri wa wataalamu kuhusu afya mbona utafika mbali na sahau kuhusu matatizo jipe furaha buana.
 
Mkuu hayo uliotaja ni changamoto za maisha ambazo karibu ya asilimia.kubwa ya wabongo wamezaliwa nazo ila wamepambana na kuweza kupunguza au kumaliza kabisa. Kuhusu ugonjwa kuna watu nawajua wameoa/kuolewa wamezaa na maisha yanaendelea LA msingi amini yupo Mungu aliye hai ndiye ana hatima ya maisha yako fuata ushauri wa wataalamu kuhusu afya mbona utafika mbali na sahau kuhusu matatizo jipe furaha buana.
Huyo mungu hausiki kabisa na majanga ya hii dunia, kama mnakumbuka mungu alimkabidhi shetani aijaribu hii dunia ili kuwapata watenda dhambi na wema, hivyo mapambano yaliyopo hapa kwasasa ni ya shetani na binadamu mungu hayupo elewa hivyo,. na kuhusu ugonjwa sijimaanishii mimi, mimi nimeweza je na kizazi changu vipi kuhusu vilio vyao hauoni kuwa mimi ni sehemu ya sababu yao,.
 
Wee jamaa,hivi Wazazi wako km wangewaza hivyo wewe ungepatikana??.
Hatupaswi kuishi kwa kurudi nyuma, tunapaswa kuishi kwa kwenda mbele,. yaani tuitazame leo na kesho yetu. Wazazi kunileta kwa bahati mbaya ndio na mimi na wewe tulete watoto kwa bahati mbaya? kweli tutakuwa timamu?
 
Unahitaji msaada wa kisaikolojia, seems like akili yako imeathirika na mengi.
Ni mengi kweli, yaani ni njaa, magonjwa, madawa ya kulevya, umasikini nk,. na kibaya zaidi sina plan B ya kukifanya kizazi changu kuepukana na haya matatizo. kama una njia ya kukifanya kizazi chako kuepuka niambie tafadhali ili nijifunze kupitia wewe,.
 
Sio kosa ila ni hasara kubwa hapa duniani
Wee unavyofikiri kuzaa watoto mateja na kutoka kuzaa kabisa kipi hasara? sikia nikwambie, wote wengekuwa na misimamo kama yangu tanzania ingewa na watu wachache tena wenye faida na wenye maana,.
yaani mijitu mnafyatua vizazi alafu vinawashinda kuvimudu kimatibabu na hata kielimu wee unategemea nini?
 
Hatupaswi kuishi kwa kurudi nyuma, tunapaswa kuishi kwa kwenda mbele,. yaani tuitazame leo na kesho yetu. Wazazi kunileta kwa bahati mbaya ndio na mimi na wewe tulete watoto kwa bahati mbaya? kweli tutakuwa timamu?
Mzee, Imeandikwa "Zaeni mkaongezeke mkaijaze nchi".Hivi ukisafiri barabara ya Iringa -Morogoro kuna mapori kibao,sasa yatajazwa lini?.Acha kuibania nchi.
 
Mzee, Imeandikwa "Zaeni mkaongezeke mkaijaze nchi".Hivi ukisafiri barabara ya Iringa -Morogoro kuna mapori kibao,sasa yatajazwa lini?.Acha kuibania nchi.
Siwezi kushiriki kuleta watu wa motoni, natambua kama ntaleta kizazi cha asilimia 90 motoni. Yaani kwenye watoto 10 wenda mmoja tu ataiona pepo,.
 
From Facebook naona Kama anaingilia kazi ya Mungu
 
Ndugu wee umeongea cha maana kidogo, kwamba Kuna familia ni vizazi mpaka vizazi kwao ni umasikini tu au ni maradhi tuu, hii maana yake ni hivi alivyoishi Babu ndio kaishi baba na ndio ninavyoishi mimi na hata na kizazi changu pia,. Sasa kwa kuliona hili ndio maana nawazaga bora mimi niwe wa mwisho kwenye hiki kizazi, yaani kisiendelee tena ndio njia nzuri,. Au unasemaje mkuu
Naunga mkono hoja

Sent from my TECNO LC6a using JamiiForums mobile app
 
Siwezi kushiriki kuleta watu wa motoni, natambua kama ntaleta kizazi cha asilimia 90 motoni. Yaani kwenye watoto 10 wenda mmoja tu ataiona pepo,.
Hiyo sio kazi yako, Wewe piga pumbu.Mimi nataka fikishe angalau watoto nane,na nimeshakubaliana na mke wangu.
 
Natamani sana kuwa na watoto, ila nina mambo yanayonikosesa furaha kila nikiwaza juu ya kuwa na watoto,.
Miongoni mwa mambo hayo nina makubwa mawili nayo ni;-

1. Umasikini, Umasikini ni janga kubwa kwa upande wangu, huwa nakosa amani pale ninapoiona kesho ya watoto wangu kwenye swala umaskini, sina njia mbadala ya kuwa kwamua watoto wangu kwenye hili janga.

2. MARADHI, Hili ni kubwa pia japo halilingani na la kwanza, mfano kwenye hili gonjwa la UKIMWI kila nikiiwaza kesho ya wanangu katika hili janga linanikatisha tamaa na kujiona mwenye hatia endapo ntawaacha watoto waje duniani na niwaingize kwenye hili janga.

3. Upofu, Maradhi ya akili kama uchizi, utahaira nk. Pia kuna maradhi ya moyo. Na hata kifafa. Huwa nakosa furaha kila nikiifikilia kesho ya kizazi changu na naona ni bora niishi mwenyewe na hata nikifa basi nife bila ya kuacha KIZAZI kisicho na furaha.

Nimeikopy facebook

Ana busara!
 
Back
Top Bottom