Kila ninapoweka juhudi za kupungua uzito, ndio naongezeka!

Kila ninapoweka juhudi za kupungua uzito, ndio naongezeka!

Sasa leo nimetimiza wiki bila kugusa chakula cha wanga nyingi kama wali, maharage ugali nyama au samaki, asubuhi na kunywa chai ya tangauzi na juice ya limao yenye maji maji ya vugu vugu, mshana na shindia vipande vya matunda kama tikiti, chungwa, na embe, usiku saa mbili na nusu kula gimbi kipande na spinach strictly hiyo ndo routine ya kula, ntaendelea hivi kwa zaidi ya siku 23 nifikishe mwezi ndo nipime nione hali itakua je.
Safi , ila kma ungeacha kula embe na chungwa ukala Avocado na Apple na uongeze brocoli zaidiili upate Viamin C kwa wingi kama uliihitaji Vitami C toka kwa chungwa .Kingine ongez mazoezi ya kutembea tuu na wala si kukimbia, tembea kadakika 45 hata maratatu kwa week .
Natumai mpaka dakika hii ume sha ona mabadiliko fulani, lazima ume pungua, sababu kiu ha kza kitakacho pungua ni maji , hivyo lazima kuna dalili ya kupungua kama uta jiangaai vizuri .
 
Kwa studies zilizopo kwa sasa zina sema breakfast sio mlo muhimu , hivyo una weza mua kuanza kula saa sita au saa tano, baada ya hapo kule tena baada ya masaa nane, kama utataka fanya intermittent fasting , kula mara mbili ni bora zaidi.
Suala nile nini? Wakati wakufungua kunywa hiyo asubuhi?
 
Suala nile nini? Wakati wakufungua kunywa hiyo asubuhi?
Anza kula lunch , achana na breakfast, kama nilivyosea milo miwili kwa siku ni bora kabisa .Ila kam ahuwezi kula miwili , basi fanya kunya a Bulltet proof cofee au Black cofee na mayai na kipande cha Avocado.
 
Safi , ila kma ungeacha kula embe na chungwa ukala Avocado na Apple na uongeze brocoli zaidiili upate Viamin C kwa wingi kama uliihitaji Vitami C toka kwa chungwa .Kingine ongez mazoezi ya kutembea tuu na wala si kukimbia, tembea kadakika 45 hata maratatu kwa week .
Natumai mpaka dakika hii ume sha ona mabadiliko fulani, lazima ume pungua, sababu kiu ha kza kitakacho pungua ni maji , hivyo lazima kuna dalili ya kupungua kama uta jiangaai vizuri .
Ahsante mkuu kwa ushauri ila hiyo balacori kwa kiswahili ni tunda gani hilo?
 
Sidhani kama lina kiswahili, ila jaribu google utaliona , ni mboga nzuri saa
Sawa nimeliona kumbe ndo hilo hapa kwetu zinatumika sana na wahindi, inapikwa kama mboga mboga au sio?
 
muhimu mkuu naamini ni hapo kwenye sukari, achana na chai nyakati za usiku mkuu
 
muhimu mkuu naamini ni hapo kwenye sukari, achana na chai nyakati za usiku mkuu
Chai nao kunywa siwekei sukali ni viungo tu tangawizi na mdarasini
 
kuruka (skipping meals) siyo suluhu ya kupunguza uzito. Inatakiwa ubadili aina ya vitu unavyokula na mtindo wa maisha kwa ujumla. Kama unachoma kalories kwa kazi ngumu kama kutembea au kazi za mikono basi lazima iendane na kula vitu ambavyo havitafanya replacement ya unavyopoteza.
Fikiria kama bomba la maji linatoa maji lita 5000 kwa 1 hour lakini hapo hapo zinaingia lita 5500 je bomba hilo litaishiwa maji? tumia hiyo formula kuuelewa mwili wako.
Ningekuwa daktari wako ningekuita kwa consultation alafu nikufanyie vipimo nikuambie una ukimwi. unapigwa na stress kwa wiki moja tuu lazima ukonde
 
Sasa leo nimetimiza wiki bila kugusa chakula cha wanga nyingi kama wali, maharage ugali nyama au samaki, asubuhi na kunywa chai ya tangauzi na juice ya limao yenye maji maji ya vugu vugu, mshana na shindia vipande vya matunda kama tikiti, chungwa, na embe, usiku saa mbili na nusu kula gimbi kipande na spinach strictly hiyo ndo routine ya kula, ntaendelea hivi kwa zaidi ya siku 23 nifikishe mwezi ndo nipime nione hali itakua je.

Not sustainable. Tafuta njia sustainable ya kupungua taratibu utayoweza kuidumu for a long time. Naona unataka quick fix.
 
Not sustainable. Tafuta njia sustainable ya kupungua taratibu utayoweza kuidumu for a long time. Naona unataka quick fix.
Siku ya leo nimetimiza mwezi bila kutumia vya kula vya wanga kama ugali wali maharage sukali nk nimepima naona ni mepunguza 8kg tu.....sio haba lengo ni kupunguza mpaka 20kg ili niwe 85kg ila kazi ipo.
 
Sisi wengine ndio tumesimamia ukucha kuzitafuta Hilo kill 80- 90 ila mpaka leo hii bado kimbau mbau tu mambo hayajatiki.
 
Sisi wengine ndio tumesimamia ukucha kuzitafuta Hilo kill 80- 90 ila mpaka leo hii bado kimbau mbau tu mambo hayajatiki.
Yatatiki tu kupata uzito ni rahisi sana kuliko kuutoa, utakapo ridhika na maisha kwa kiasi filani mwili utaachia.
 
Mwezi wa pili uzito umegoma kupungua, baada kupungua kilo nane mwezi wakwanza wakati dieti ni ile ile tatizo ni nini?
 
Polee sana kiongozi :
Kuna huu ukweli ambao wengi huona kama uongo na kukomalia yanayoandikwa na influencers. Ukweli ni hivi, mazoezi yanamchango kidogo mnoo kwenye kupungua uzito. Tafiti nyingi zimeonyesha mtu ambaye huwa na Nidhamu kwenye chakula hupungua uzito kwa kilo nyingi sana ikilinganishwa na anayefanya mazoezi.
Mazoezi yanasaidia sana katika kuuweka mwili imara na kuzuia kuwepo kwa magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama presha ya kupanda.
Ukitaka kupungua uzito kuwa na nidhamu n chakula. Kama unataka kujua namna gani.. Quote hii reply na uulize How.
How
 
Iko hivi ndugu mleta maada. Wazungu wanasema Unlearn to Learn. Kuna njia nyingi sana ambazo watu huzishauri zitumike katika kupunguza uzito na njia hizi zinapishana katika ufanisi wa kuleta matokeo tarajiwa. Ili uweze kupungua uzito ni lazima matumizi ya Calories katika mwili wako yawe makubwa zaidi ya kiasi unachoingiza mwilini mwako (Energy consumed
1. Kufunga kula: Njia hii ya kufunga kula kwa masaa 12 hadi 24 imekuwa na uwezo mkubwa sana (40%) wa kuleta matokeo. Katika njia hii Matumizi ya Nishati mwilini huwa ni makubwa zaidi ya kiasi cha Nishati iliyoingizwa mwili hivyo kupelekea mwili kupungua uzito kupitia kuunguza mafuta ya ziada yanayotunzwa katika sehemu mbali mbali za mwili kama vile Chini ya Ngozi na ndani ya viungo. Ukianza kufunga hakikisha pia chakula unachotumia kuvunja funga yako (breakfast) kiwe kisiwebkila chakula chenye Nishati nyingi sana (High caloric value) kama vile ugali mkubwa, sahani iliyojaa wali na mihogo n.k. Kumbuka mtu akiwa katika haki ya kushiba chakula kinchotumika sana ni kile alichotoka kula kilichotunzwa hakivunjwi vunjwi hata kidogo na kama mtu amefunga chakula huvunjwa katika mtiririko huu

Wanga > Mafuta > Protini. Kwahiyo kama haujala mwili hauna wanga, mafuta hutumika kuzalisha nishati na kama mafuta yameisha Protini hutumika (Autolysis). Swali linaweza kuwa ni kufunga kwa namna ganj kwafaa kati ya ile kufunga mfululizo(continuous fasting) au kufunga kwa kurusha siku (intermittent fasting), mimj nakuambia Tumia intermittent fasting. Has been proven effective enough to make your body loose weight.

2. Kupunguza kula wanga(Cutting off carbs) : Wanga umeonekana kuwa ndio chanzo kikubwa cha mafuta mwilini. Hivyo sasa, ili kuzuia mafuta yaliyotunzwa mwilini kuongezeka tunapunguza ulaji wa wanga na kuhamia kula vyakula kama Nyama (Protein) na Mboga za majani. Kufanya hivi hupelekea mwili kuanza kutumia mafuta ya yaliyotunzwa kabla kuzigeukia protini. Hivyo hii nayo inasaidia kupungua uzito. Na kiasi cha wanga unapaswa kula kama unataka kupungua uzito kiwango cha ngumi yako.

3. Kufunga kula huku ukinywa maji tu. Hii njia inaweza kukupa matokeo within 7days unaisha kabisa bila hata kuhangaika sana. Swali je, utaweza kujizuia kula kwa hizo siku zote huku ukiwa unakunywa maji tu? Inawezekana sana ila fanya kwa kuruka siku moja moja (intermittent fasting).

4. Achana na hizi tabia : Acha kunywa pombe usiku na uende kulala, acha kula sana usiku na uende kulala muda huo huo, punguza matumizi ya sukari au vyakula au vinywaji vyenye sukari nyingi, Acha tabia kula usiku muda umeenda sana jizoeze kula chakula chako cha usiku saa moja jioni kama ilivyokuwa boarding schools.

Kama umeisoma hii na unataka niendelee, Quote tena na andika More
More more
 
Back
Top Bottom