Hapana, si kweli nilikuwepo.
Nyerere aliiacha Tanzania ikiwa ni nchi ya mwisho kwa umasikini duniani. Aliiwacha hata chakula inabidi tukae foleni, wakati yeye aliipokea kwa Mkoloni ikiwa ni nchi ya kwanza katika Afrika inayosfirisha mazao ya kilimo.
Unajuwa kuwa Tanzania Nyerere alituwacha chakula hatuna, mafuta hatuna, akiba benki hatuna.
Umri wa kutenegemea kuishi mtanzania(life expectancy) wakati wa nyerere ulikuwa haufiki miaka 45.
Yule mzee usisikie anavyopambwa, alituwachia na mabalaa ya kila kitu Kawacha nchi foleni kila kitu foleni.
Kwa mtazamo wangu, Nyerere hakuwa na baraka za Mwenyezi Mungu kabisa katika kipindi chake. Majanga mwanzo mwisho.
Naamini huwezi kudhulumu watu Mwenyezi Mungu akakubariki.
Mwalimu Nyerere aliwahi kutawala nchi hii kwenye kipindi kigumu zaidi kuliko maRais wote waliowahi na watakaowahi kuitawala Tanzania; usisahau hilo. Alichukua nchi kutoka kwenye mikono ya wakoloni, na ambao walikuwa hawataki atawale yeye, bali walikuwa wanataka mtawala kutoka kwenye Kabila kubwa ambalo ni wasukuma
Sasa kuanzia pale walipomwachia nchi wakawa wako standby wakiwa wanataka kuwatumia wanachi wenzake kumwondoa, na hiki ndicho kilichopelekea Army Mutiny ya mwaka 1964
Mbali na haya yote, wakati sisi tunapata Uhuru baadhi ya nchi za Afrika zilikuwa bado hazipata Uhuru wakiwemo majirani kabisa Msumbiji na Zimbabwe. Huko Afrika Kusini nako bado kulikuwa na shida ya Aparthedi rule
Nyerere asingeweza kuyavumilia matataizo haya yote yaendelee kuwepo Afrika, ukizingatia kuwa yeye pamoja na Nkrumah, walikuwa na mkakati wa kuja kuinganisha Afrika iwe USA (United Staes of Africa)
Kosa unaloweza kusema kuwa Nyerere alifanya, ni kuingia mno kwenye Siasa za Afrika baada ya Uhuru, wakati nchi yetu ilikuwa bado ni maskini mno. Pengine siasa hizo alienda nazo kwa umbali mrefu zaidi ya alivyostahili kwenda nazo, na hapo ndipo matatizo yalipoanza kujitokeza ndani kwake
Nampenda sana Nyerere kwa sababu hata makosa yake aliyowahi kufanya wakati wa utawala wake, alikuwa anakosea akiwa na nia njema ya kutafuta kitu kikubwa na chenye manufaa zaidi kwa wanachi wake. Na kwa sababu hakuwa Mungu, alikuwa anapanga jambo akiwa ametarajia neema zaidi kutoka kwenye jambo hilo lakini kwa bahati mbaya, mambo mengine yalikuwa yanageuka otherwise.
Hujuma pia zilikuwepo kutoka kwa baadhi ya wenzake waliokuwa wametarajia kutanua baada ya Uhuru, huku Nyerere yeye lengo lake likiwa kwa wananchi wake maskini
Nia njema iliyokuwa ndani ya Mwalimu, ilikuja kujidhihirsha tena hata kwa Marais wengine waliomfuatia, wakiwemo Mwinyi na Kikwete, na inaendelea kujidhihirsha hadi leo. Alipnada mbegu njema, anaendelea kuvuna kile alichowahi kupanda
Hapa sisemi kwamba watu hawa walifanya maajabu mno, hapana, ila najaribu tu kuilezea ile nia yao njema kwa nchi wakati wanaomba ridhaa ya kuongoza nchi kutoka kwa wanchi, na baada ya kuwa wamepata ridhaa hiyo. Kama kuna mahali walionekana kupwaya aua kukwama, basi pengine tatizo halikuwa wao, bali sisi wanachi.Wanachi wana nguvu kubwa mno kwa sababu wao ndiyo wanaoamua Rais kuwa madarakani
Unaweza ukaiona nguvu ya wanachi kwenye hili swala la uwekezaji Bandarini; dhahabu inayotaka kutpwa kwenye jalala kisa tu wanachi wanapotoshwa
Haipo nchi duniani ambayo Bunge lake na Serikali yake vyote vinaweza kushrikiana kuuza nchi au kuingia kwenye mkataba wa kuiumiza Nchi; nchi ya namna hiyo kwenye dunia hii haipo!