Kilimo cha Kisasa cha Mahindi: Mbegu bora, Mbolea bora na magonjwa

MwanawaMUNGU41

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2015
Posts
1,036
Reaction score
737
Habari wadau,

Baada ya kuwa kwenye ajira kwa miaka 10 na kuona msoto uko pale pale,nimeamua kuingia kwenye kilimo kama njia ya kuongeza kipato cha ziada.

Nimeanza kwa kukodi shamba Ruvu kwani mimi niko Dar na niko kamili kwa kuanza na heka 2.
GHARAMA

Nimekodi shamba laki 3(@150,000),nikafyeka 120,000/=(@60,000 hii ni kutoka na kwamba kule maji yalikiwa yamejaa so hakuna magugu majani yaliyobaki siyo marefu sana),mbegu PANNAR kg 10 kwani ndo mbegu wanayolima wenyeji kule elf 60(@6000)kupanda ni elfu 70(35000).

Nimeanza kupanda leo na nimeanzia hapo najua nitadaiwa mbolea,palizi na dawa kwani nitabase na mahindi ya kuchoma.

Nipe gharama na namna bora ya kilimo cha mahindi.

Pia soma => Nimeamua Kulima kwa mara ya Pili kilimo cha mahindi

------- Michango------



Mkulima wa Mahindi: Msimu wa kilimo umefika, zingatia sana yafuatayo

Kwa mikoa ya Iringa, Mbeya,Ruvuma, Njombe, Singida, Rukwa, Katavi, Kigoma, Tabora na Shinyanga ni mwanzo msimu wa kilimo.

Ni vema mkulima wa mahindi akazingatia yafuatayo ili kupata ufanisi:

1.Muda huu ni vema uwe tayari umeandaa au unaandaa shamba.

2. Andaa samadi ya ng'ombe iliyoiva vizuri na isambaze shambani kabla ya kulima hasa maeneo ambao msimu uliopita mazao hayakustawi vizuri. Samadi/ mboji ndio siri kubwa ya ustawi mzuri wa mazao hasa mahindi. Mbolea za viwandani pekee si suluhisho la mavuno mazuri.

Maeneo mengi nchini yana upunguvu mkubwa wa virutubisho vya Nitrogen hivyo ni lazima mkulima arutubishe shamba lake ili kupata tija. Ukiweka samadi mfululizo kwa misimu 3 unaweza usiweke tena mbolea kwa miaka 5 hadi 7 ijayo.

3.Andaa mbegu bora mapema. Kwa mbegu chotara au Hybrids tumia mbegu km DK8053,DK90789,DK777,H614, H625Seedco nk. Waone wataalamu wa kilimo au maduka ya kilimo wakupe ushauri upande mbegu ipi kwa eneo lako, japo Dk. 9089,H625 zinastawi maeneo mengi.

4.Panda mbegu kwa nafasi mfano Sm75xSm30 ambapo ekari moja utapata miche 44,000.

5. Andaa pesa au nguvu kazi ya kutosha kupalilia shamba. Wakulima wengi hukosea hapa. Wengi huchelewa kupalilia shamba. Shamba la mahindi lipaliliwe wiki 3 hadi ya 4 toka kupanda. Ukichelewa mahindi hushindwa kukua vizuri na huenda yakadumaa.

6. Andaa mbolea ya kukuzia hasa kama Urea na CAN ili muda wiki 6 na isizidi wiki 8 uwekee mbolea. Wakulima wengi huchelewa kuweka mbolea kwa sababu huwa hajajiandaa.

7. Shamba lisiwe mbali sana na makazi yako utashindwa kulisimamia. Kwa kifupi haya ndio mambo ya msingi ya kuzingatia katika kilimo cha mahindi.

Mhitimu Chuo cha kilimo Uyole 2010, SUA 2017.

Mungu abariki kazi ya mikono yenu.
 
Kg 10 ni eka huku ni laki 6 kwa eka. Kama wewe sio mkulima
 
Hicho ni kilimo cha umwagiliaji?

Na hiyo kilo kumi kama utapanda vizuri sidhani kama inatosha kwa wastani eka ni kg 7 hadi 8 na kwa eka mbili unatakiwa uwe na kg si chini ya 14
 
Hicho ni kilimo cha umwagiliaji?
Na hiyo kilo kumi kama utapanda vizuri sidhani kama inatosha kwa wastani eka ni kg 7 hadi 8 na kwa eka mbili unatakiwa uwe na kg si chini ya 14
Ni umwagiliaji make niko karibu na mto, na bado upungufu wa mbegu si tatizo kwani naweza kuongeza lakini mpaka sasa nishapanda heka moja imetumika kilo sita tu, so naongeza kilo 2
 
Nimeamini kilimo kinahitaji mtaji yale yanayosemwa kwenye majarida au magazeti yasitupotoshe jitose uone, mahindi tu mpk sasa nishatumia laki 8 na bdo ndo kwanza yameota bado palizi, madawa, mbolea na mengineyo!
 
Narudi ngoja nikusanye hints zote nije tujadili mambo ya msingi.
Utakaporudi naomba unijulishe ni kweli maeneo mengine waweza lima mahindi na ukapata bila ya kutumia mbolea mm ni mzaliwa wa mkoa wa Ruvuma hivyo najua bila mbolea uko kwetu upati kitu ss nasikia Morogoro wanalima bila mbolea na baadhi ya maeneo uko Tanga.
 
Arusha, Manyara, Moro, Njombe
Hawatumii mbolea
 
Cjui ni uoga au uzembe, au nini cjui

Hivi kweli umekaa katika kazi miaka 10 ukaona msoto afu unataka ujikomboe kwa heka 3.

Inakuja akilini kweli? Sio ndio unajiongezea matatizo?

Ukiamua kutupa jiwe... litupe mbaali hata likirudi chini lisikupige.... next time tupa karibu uone km halikugongi kichwani
 
Nenda Morogoro au Babati.utakodi shamba kwa Tsh: 50000 or 70000/= kwa heka moja.uwe na mtaji iwapo unataka kulima kibiashara.kodi heka kuanzia 30 na ulime kwa trekta.

Kukodi trekta kulima kwa heka moja ni Tsh: 40000 or 50000/=.kumbuka kama mahindi umepanda kisasa na kumwaga mbolea na kupalilia vizuri bila kuacha majani yakazorotesha mazao utavuna gunia 10 mpaka 13 kwa heka.

Hesabu zingine piga mwenyewe.nimekusaidia kidogo.kulima heka mbili za mahindi ni kulima chakula cha familia yako tu.

Na si kilimo cha kupata mtaji kwa mtu aliechoka kuajiliwa na kuamua kua mkulima.huwezi toka kuajiliwa kama nilivyo mimi hapa then nikaenda kulima heka 2 au 3 ni kupoteza muda. Lima shamba heka kuanzia 30 mpaka 50.na kwa uchache kilimo hicho ili kikutoe andaa mtaji japo milion 8 mpaka 10m

JAH RASTAFARI MORNING AFRICA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…