Kilimo cha vitunguu (saumu na maji): Ushauri na Masoko

Kilimo cha vitunguu (saumu na maji): Ushauri na Masoko

Mkuu baraka607, wazo na
ushauri wako ni mzuri sana kwa wanajamii wanaotaka kujishughulisha na
Zao tajwa. hesabu ulizoweka juu ni za kuvutia hasa kwa anayehitaji
changamoto kutoka kwa mtu aliyejaribu biashara hio.
USHAURI WANGU KWAKO

Nadhani ungewavuta wengi sana na kununua mbegu kwa wingi iwapo
ungewaekea takriban za gharama. kwa mfano, kama inaitajika mbolea ni ipi
na kiasi gani, upandaji wake ni vipi, utaalamu wa kutoa vitunguu vingi
na kadhalika nyingine nyingi tu. mimi sio fundi wa haya mambo ila
nadhani umenipata. na kwenye gharama ukitaka mteja wa mbegu arudi
ungepiga kama ulivyosema hapojuu wewe umeuza at minimum price of 85K.
85k *100 gunia = 8500,000/=
Ans - 600,000 za mbegu kutoka kwako=7900,000 Then Gharama za uzalishaji
kwa takriban. kwa hilo mtu anaweza kujikuta faida ni ndogo kuliko
ulivyotaja na hapo akaamua kununua mbegu za eka mbili ama zaidi ili
kufikia malengo. kwa mtindo huu wewe utauza mbegu na mteja lazima
atasambaza sifa za mbegu yako.

Wazo zuri sana mkuu, na ili kutanua soko lake ni vyema kufanya utafiti wa udongo na hali ya hewa ili kujua mbegu hizo zinastawi zaidi sehemu gani.
 
Hata mimi napenda kufanya iyo kt but maelezo yako mkuu hayajitoshelezi.
 
Wazo ni zuri sana. Mimi nalima vitunguu Singida Wilaya mpya ya Mkarama Kata ya Mwanga.

Baraka alichosema kimsingi anapenda watu waweze kupanua mawazo kuelekea kwenye kilimo kitu ambacho nakiunga mkono sana. Tatizo ambalo hajaweza kulijua na huende anasikia siyo MKULIMA ekari moja inapandwa kilo tatu za mbegu. Bei za mbegu ni tofauti sana kulingana na maeneo kwa mfano Red Bombay ambazo tunazalisha sisi wenyewe huku mashambani debe moja halizidi laki moja.

Mbegu aina ya Neptune inapatikana Barton Tanzania Ltd inauzwa 120,000/- kwa nusu kilo, Red Caraoke ya South Afrika inauzwa 80,000/- kilo moja.
Kuhusu bei ya soko huyu ndugu anazungumzia Hapa Dar, hajasema huyo mkulima kutoka Mang'ora, au Singida Vijijini kwa bei anayosema dalali wa sokoni hamzungumzii najua huwezi kuleta bidhaa sokoni ukauza mpaka uwaone madalali.

Nina uzoefu mkubwa mwaka jana nilileta gunia 130 kwa mtu aliyesema angenunua akaja akaona mzigo akaufungua na kushona upya akatoa gunia 124 kwa bei ya 73,000/- wakati nimevitoa shambani singida akalipa advance millioni sita na laki tano pesa nyingine mpaka leo hajalipa simu hapokei.

Mwezi wa tano vitunguu shambani wanunuzi walileta bei ya shilingi 40,000/- hadi 50,000/- kwa gunia la wavu wanapakia viroba vitatu wanasema ni gunia moja, nikaona ni bora nilete vitunguu soko la misuna singida mjini, bei yao ilikuwa shilingi 53,000/- kwa gunia moja. Ushuru ni shs 1000/- kwa gunia, dalali 2,000/- kwa gunia, wanaochmbua shs 1,000/- kwa gunia, mshonaji 1,000/- kwa gunia nilikuwa na gunia 67.

Rafiki bei ya vitunguu haijawa na msimamo inategemea baraka za madalali na wingi wa mzigo uliopo sokoni.

Nitakupigia Baraka simu ila ukweli ndio huo.
 
Wazo ni zuri sana. Mimi
nalima vitunguu Singida Wilaya mpya ya Mkarama Kata ya Mwanga.
Baraka alichosema kimsingi anapenda watu waweze kupanua mawazo kuelekea
kwenye kilimo kitu ambacho nakiunga mkono sana. Tatizo ambalo hajaweza
kulijua na huende anasikia siyo MKULIMA ekari moja inapandwa kilo tatu
za mbegu. Bei za mbegu ni tofauti sana kulingana na maeneo kwa mfano Red
Bombay ambazo tunazalisha sisi wenyewe huku mashambani debe moja
halizidi laki moja.
Mbegu aina ya Neptune inapatikana Barton Tanzania Ltd inauzwa 120,000/-
kwa nusu kilo, Red Caraoke ya South Afrika inauzwa 80,000/- kilo moja.
Kuhusu bei ya soko huyu ndugu anazungumzia Hapa Dar, hajasema huyo
mkulima kutoka Mang'ora, au Singida Vijijini kwa bei anayosema dalali wa
sokoni hamzungumzii najua huwezi kuleta bidhaa sokoni ukauza mpaka
uwaone madalali.
Nina uzoefu mkubwa mwaka jana nilileta gunia 130 kwa mtu aliyesema
angenunua akaja akaona mzigo akaufungua na kushona upya akatoa gunia 124
kwa bei ya 73,000/- wakati nimevitoa shambani singida akalipa advance
millioni sita na laki tano pesa nyingine mpaka leo hajalipa simu
hapokei.
Mwezi wa tano vitunguu shambani wanunuzi walileta bei ya shilingi
40,000/- hadi 50,000/- kwa gunia la wavu wanapakia viroba vitatu
wanasema ni gunia moja, nikaona ni bora nilete vitunguu soko la misuna
singida mjini, bei yao ilikuwa shilingi 53,000/- kwa gunia moja. Ushuru
ni shs 1000/- kwa gunia, dalali 2,000/- kwa gunia, wanaochmbua shs
1,000/- kwa gunia, mshonaji 1,000/- kwa gunia nilikuwa na gunia 67.
Rafiki bei ya vitunguu haijawa na msimamo inategemea baraka za madalali
na wingi wa mzigo uliopo sokoni.
Nitakupigia Baraka simu ila ukweli ndio huo.

Sasa hizi ndio facts halisi za Site (soma saiti)
Yeyote anayetaka kujiingiza kwenye kilimo hiki ni vyema sana akazingatia haya. Shukrani sana Mkuu Kitange
 
Kwanza kabisa napenda kuchukua nafasi hii kuomba radhi kutokana na mtu niliyemuachia maagizo ya kuweka bandiko hili hakutoa ufafanuzi mzuri.

Ufafanuzi huu ntautoa kwa kifupi hapa na ntaambatanisha na excel ambayo ina mchanganuo mzuri zaidi.
Mbegu hii imeandaliwa kisasa na inazalishwa nchini kenya, nimeitumia huu ni mwaka wa nne na sijawahi kukatishwa tamaa na mbegu hii.

Kwa kawaida hutumia lita 10 hadi 15 kwa eneo la ekari moja.

Suala la bei sokoni kwanza kabisa inatokana na ubora wa kitunguu na pia timing ya mavuno yako. Kwa mfano, mimi nalima Kidete na Bagamoyo. Kidete huwa napanda mwezi wa tatu katikati na nakuja kuvuna mwezi wa saba kwenye tarehe 10 na huwa nakutana na bei ya 110,000 hadi 95,000 na kwa bagamoyo nimepanda mwezi huu mwanzo na nategemea kuvuna mwezi wa tatu ambapo bei ya vitunguu huwa juu sana kwasababu shamban tu gunia hufikia hadi 120,000/=

Naomba nieleweke kwamba haya yote nnayoongea sio kwamba navutia biashara ya mbegu ila ni kitu halisi na mtu yoyote anaweza kufika ofisini na nikamuonyesha risiti za mauzo ya sokoni. Kwa fukara kama mimi anayetafuta kujiajiri hii ni nafasi nzuri na tutasaidiana kwa utaalamu bila malipo yoyote.

NB: Naomba muangalie excel niyoiambatanisha hapo chini nimejaribu kutoa mchanganuo wa gharama kamili ya kilimo kwa shamba la ekari moja na mchanganuo kama ukiamua wewe mwenyewe kuleta mzigo mjini na faida ya biashara nzima ndani ya miezi mitatu.

Kama kuna sehemu ntakua nimesahau kutoa maelezo basi tusameheane na ntashukuru ukinitafuta tukaongea zaidi kulikoni kutoa maneno machafu na ya kejeli mtandaoni.

Ahsanteni sana
namba yangu no 0655003510
 

Attachments

Nna ushahidi wa risiti tokea nimeanza biashara hii miaka minne iliyopita, kama nna gunia nimewahi kuuza chini ya elfu 85 nafuta tangazo hili. Cha zaidi mtu halazimishwi kuchukua opportunity, ni maamuzi binafsi kaka. Next time "Think before you act" Mr

Alichokisema jamaa kinaweza kuwa sawa kabisa,labda kama wewe unalima kwa misimu yako na kuuza vilevile kwa msimu huohuo,na pia bei inaweza ikategemeana na sehemu ulipo
 
Mkuu baraka 607 .......nimefuatiria na nimeelewa nashukuru sana'09
 
mtoa mada ameisifia sana bei ya mbegu ya red bombay lakini kuna kitu muhimu ameacha mara nyingi wakulima wakivuna vitunguu hawauzi muda huo huo wanasubiri mpaka pale bei ya soko itakapokuwa nzuri tatizo la vitunguu vya red bombay haviwezi kuhifadhiwa muda mrefu baada ya kuvuna ndio maana wengi wanapendelea vitunguu aina ya Red Caraoke kwani ukishavuna unaweza kuhifadhi hadi miezi 3 kabla ya kuuza
 
Heshima kwenu wakuu! Nataka kujua mambo flan khs KILIMO cha kiTUNGUU kwa yeyote anaefaham,Kuna mbegu aina ngapi? ipi BORA na kwanini ni BORA kuliko nyingine?

Inachukua muda gani tangu MBEGU kuwekwa kiTALUNI hd Kuota! kwanini icpandwe 1kwa1 shambani? badala yakuoteshwa kwanza? ni Mbolea gani nzuri yakupandia na kukuzia madawa?

Niko na eka 2 nimepanda NYANYA CHUNGU nikishazitoa nataka kupanda VITUNGUU ntanguliza Shukrani wakuu!
 
Sasa labda sie wakulima itabidi tuwe na mtandao ili Ndugu yetu Baraka atatusaidia kwenye suala la soko.

Naamini bei inaweza kuwa kubwa kutokana na umoja wa wakulima lakini kila mtu akiuza kivyake matokeo ni bei tofauti.

Mimi naendelea kupanda maana nalima jumla ya eka 23 kila msimu pia nalima eka nne kwa kumwagilia ambazo huwa navuna mwezi wa Novemba.

Madalali yeye hajagusia amewezaje kuwakwepa anapopeleka vitunguu vyake sokoni na wanunuzi amwasiliana nao vipi mpaka wakaweza kufika shambani kwake.

Twaweza kupata namba za wanunuzi nasi tukajaribu bahati zetu?
 
Sasa labda sie wakulima itabidi tuwe na mtandao ili Ndugu yetu Baraka atatusaidia kwenye suala la soko.
Naamini bei inaweza kuwa kubwa kutokana na umoja wa wakulima lakini kila mtu akiuza kivyake matokeo ni bei tofauti.
Mimi naendelea kupanda maana nalima jumla ya eka 23 kila msimu pia nalima eka nne kwa kumwagilia ambazo huwa navuna mwezi wa Novemba.
Madalali yeye hajagusia amewezaje kuwakwepa anapopeleka vitunguu vyake sokoni na wanunuzi amwasiliana nao vipi mpaka wakaweza kufika shambani kwake.
Twaweza kupata namba za wanunuzi nasi tukajaribu bahati zetu?

Ndugu Kitange,
Wanunuzi kupatikana ni rahisi sana. Nenda masokoni wiki chache kabla ya kuvuna, ongea na wauzaji wa jumla moja kwa moja, na si madalali, fanya nao mawasiliano na waeleze una mali iko shambani, wengi hupenda kuja kukagua kama shamba lipo karibu au unaweza kwenda na sample kama kilo 10 ulizovuna kabla ya muda kidogo.

Madalali ni janga kubwa sana katika sekta hii ya Kilimo na ufugaji. Siku hizi wakulima wa matunda wengi wameshastuka na kuamua kupanga mazao yao maeneo yenye watu wengi kwa kufata utaratibu maalumu uliowekwa na manispaa husika.

Mfano wakulima wengi wa mananasi, maembe machungwa nk, hukodi Canter na kulipaki sehemu yenye watu wengi kama mwenge, ferry nk.. halafu wanawauzia wateja moja kwa moja bila kupitia dalali... kwa kufanya hivyo wanaokoa usumbufu, utapeli na bei nzuri kwa kila zao... mf nanasi moja shambani utaliuza sh 700 ukilileta kwenye canter utaliuza 1500 na kuendelea.

Ofcourse njia hii sio muafaka kwa wanaolima hekari nyingi kama wewe, huwezi kuuza magunia 200 ya vitunguu kwa mtindo huu.. Lakini ukifanya mawasiliano na wauzaji wa jumla moja kwa moja bila kupitia madalali inawezekana.

option nyingine ni Kupunguza ukubwa wa eneo unalolima... kwa kujaribu unaweza kulima eneo unaloweza kumudu kuuza mazao yako kwa bei nzuri tu...(kulima kidogo na ukauza kwa uhakika ni bora kuliko kulima kingi ukaishia kutapeliwa)

Option nyingine ni kufanya utafiti wa magenge na meza za masokoni wananunuaje bidhaa zao.. unaweza kufanya nao mawasiliano na kuwauzia mzigo moja kwa moja.. mf ukipata magenge 100 yatakayonunua gunia moja kila genge maana yake utakuwa umeuza gunia 100 bila matata.. ( Hii inahitaji uwe na makazi Dar, Sehemu ya kuhifadhi mzigo na Gari ya kusambazia mzigo)

Ni hayo tu.
Mi nilishawahi kuuza mkaa magunia mengi sana kwa style hii ya kusambaza gunia moja moja kwa store... mpaka mkaa wangu wote ukaisha na nilipata faida ya elf zaidi ya 5 kwa kila gunia kuliko bei niliyopewa na dalali...
 
Asante mkuu Kubota,mimi ni graduate nina mpango wa kujikita kwa mara ya kwanza ktk kilimo cha vitunguu maji huko ruaha mbuyuni, nimeona changamoto nying hususan ktk masoko na hili la mbegu bora kiukwel umetoa darasa zuri, nitakapoanza nitaomba msaada wako zaid.shukran mkuu.
 
Huo ni ushauri mzuri MamaNa!
Unafaa kwa wakulima, Ahsante Ubarikiwe!!
 
Nimevutiwa sana na hii ya kulima vitunguu. Vp hapa dar vinaweza kustawi? Namaanisha maeneo kama chanika. Naomba msaada wadau.
 
Nimevutiwa sana na hii ya kulima vitunguu. Vp hapa dar vinaweza kustawi? Namaanisha maeneo kama chanika. Naomba msaada wadau.

Nimewahi kupanda vitunguu maeneo ya Mbezi makabe aina ya red bombay vilisitawi sana na nilipata mavuno mengi japo nilitumia kumwagilia maji ya bomba wakati panakituo cha CHILD IN THE SUN
 
Kwanza kabisa napenda kuchukua nafasi hii kuomba radhi kutokana na mtu niliyemuachia maagizo ya kuweka bandiko hili hakutoa ufafanuzi mzuri.

Ufafanuzi huu ntautoa kwa kifupi hapa na ntaambatanisha na excel ambayo ina mchanganuo mzuri zaidi.
Mbegu hii imeandaliwa kisasa na inazalishwa nchini kenya, nimeitumia huu ni mwaka wa nne na sijawahi kukatishwa tamaa na mbegu hii.

Kwa kawaida hutumia lita 10 hadi 15 kwa eneo la ekari moja.

Suala la bei sokoni kwanza kabisa inatokana na ubora wa kitunguu na pia timing ya mavuno yako. Kwa mfano, mimi nalima Kidete na Bagamoyo. Kidete huwa napanda mwezi wa tatu katikati na nakuja kuvuna mwezi wa saba kwenye tarehe 10 na huwa nakutana na bei ya 110,000 hadi 95,000 na kwa bagamoyo nimepanda mwezi huu mwanzo na nategemea kuvuna mwezi wa tatu ambapo bei ya vitunguu huwa juu sana kwasababu shamban tu gunia hufikia hadi 120,000/=

Naomba nieleweke kwamba haya yote nnayoongea sio kwamba navutia biashara ya mbegu ila ni kitu halisi na mtu yoyote anaweza kufika ofisini na nikamuonyesha risiti za mauzo ya sokoni. Kwa fukara kama mimi anayetafuta kujiajiri hii ni nafasi nzuri na tutasaidiana kwa utaalamu bila malipo yoyote.

NB: Naomba muangalie excel niyoiambatanisha hapo chini nimejaribu kutoa mchanganuo wa gharama kamili ya kilimo kwa shamba la ekari moja na mchanganuo kama ukiamua wewe mwenyewe kuleta mzigo mjini na faida ya biashara nzima ndani ya miezi mitatu.

Kama kuna sehemu ntakua nimesahau kutoa maelezo basi tusameheane na ntashukuru ukinitafuta tukaongea zaidi kulikoni kutoa maneno machafu na ya kejeli mtandaoni.

Ahsanteni sana
namba yangu no 0655003510

Mkuu naona unasema unalima vitunguu bagamoyo naomba kuuliza vitunguu vinakubali katika mazingira ya pwani na kwenye udongo wa Kichanga? Sehemu kama Mkuranga unaweza lima vitunguu?
 
Nimewahi kupanda vitunguu maeneo ya Mbezi makabe aina ya red bombay vilisitawi sana na nilipata mavuno mengi japo nilitumia kumwagilia maji ya bomba wakati panakituo cha CHILD IN THE SUN

Mbezi makabe udongo wake ni ule mwekundu au Kichanga?
 
Back
Top Bottom