SoC04 Kilimo na ufugaji vinawezekana serikali ikiboresha mazingira

SoC04 Kilimo na ufugaji vinawezekana serikali ikiboresha mazingira

Tanzania Tuitakayo competition threads

hauleibrahim

Senior Member
Joined
May 17, 2024
Posts
183
Reaction score
125
Kumekuwa na dhana potofu hasa katika maswala ya kilimo na ufugaji kwamba vijana hawapendi kilimo na ufugaji vijana ni wavivu.mm niseme hata hao wanao sema vijana hawapendi kilimo na ufugaji nao ni wavivu Sana ajabu wao wenyewe wameajiliwa na mtu hyo wanae msimanga mvivu na hapendi kilimo na ufugaji ikiwa wao hayo mambo hawatekelezi ipasavyo

Tufanyeje vijana wapende vilimo na ufugaji Kwa wingi kwenye mikoa ya vilimo na ufugaji.

Tutafute masoko yenye uhakika Kwa kijana akipata nafasi ya kulima na kufuga awe na uhakika wa soko lenye usawa n juhudi za kike anacho kizalisha kwenye kilimo ama ufugaji

Tuhakikishe mbolea za viwandani zinapatikana Kwa wepes pamoja n chakula Bora Cha mifugo ili kijana anapo hitaji mbolea kama niya kukuuzia isiwe ni swala la kuhangaika akihitaji chakula Cha mifugo Bora asihangaike sana kuvipata Kwa Gharama

Tuhakikishe tunapata wataalamu wa kilimo na ufugaji walio Lima na kufuga wanatoa elimu mara Kwa mara:elimu hii itakayo tolewa iwe ya vitendo zaidi na iendane na wakati husika tuliopo sio maneno mengi yasiyo na vitendo ni vizuri wakawa na mashamba darasa ya kile wanacho fundisha vijana wapate kuona na kutamani.

Ziwepo mbegu Bora za kilimo na mifugo Kwa wakulima na Kwa wafugaji pia itapendeza ikiwa ni rahisi kupatikana sehemu zote ZeNye kuhusika na vilimo na ufugaji:mbegu ndio chanzo Cha matokeo ya mche au mfugo bora niombe watu wa tari na mifugo mifugo Kwa pamoja wahusika wavumbue na kuuza mbegu ZeNye kuendana na hali ya eneo husika Kwa ufugaji na kilimo ili kupunguza gharama za kuhudumia Miche na mifugo inapo shambuliwa na magonjwa mbalimbali.

Wawepo wataalam wa magongwa ya mimea na mifugo wanao patikana mda mwingi:Kuna wakati Miche na mifugo hushambuliwa na magonjwa kama tutapata wataalam ni rahisi Kwa kijana asie na utaalam kumuita mtaalam amuambie ugonjwa na dawa Bora kutumia kuponesha magonjwa ya mifugo yake na Miche yake shambani

Tupunguze makodi y mzigo barabarani isiyo na ulazima.leo Kuna kijana n mkulima na mfugaji mzuri pale njombe wa kiazi na ng'ombe ila anashindwa kusafirisha mzigo wa viazi na ng'ombe vifike dar ili auze haraka apate fedha sababu ya hawa wachukua fedha barabarani matokeo kiazi na mifugo vinafelishwa kufika kufika dar na mtu wa njiani na wakati huo kiazi na mifugo vinahitajika sana wakati huo mijini.

Uwepo utaratibu wa serikali kufanya mikutano: wafanye mikutano ya kuhusu kilimo na ufugaji na wakulima kila mkoa inayo husika na kulima na kufuga ama kimoja wapo tu ya mara kw mara kusikiliza kero za wakulima na wafugaji wengi kwa ujumla.kuna wakulima na wafugaji wana mbinu na mawazo Bora ya kilimo na ufugaji ila hakuna kiongozi Alie tyari kumsikiliza mtu anae Kaa kwenye nyumba ya udongo Kwa sababu haaminiki kama ni mtu mwenye kutoa mawazo Bora.

Kijijini hakuna kijana mvivu ila hakuna kijana asie penda kilimo na ufugaji ila wanao Felisha mambo mengi ni hao watendaji wa serikali.leo kama soko lipo zuri kijana hawezi kuacha kulima na kufuga Kwa pamoja Leo kama mbolea na mbegu Bora za mifugo uhakika kijana hato acha kulima na kufuga mana atakuwa n uhakika wa kupata fedha kama wenzake.

Serikali ikiboresha haya vijana hawato kimbilia mijini miaka yote


Hakuna vijana wavivu ila wenye dhamana waboreshe vitu hivi ili kijana afurahie juhudi zake huko huko kijijini kwao

Yakiboreshwaa hayo pia tutapunguza wimbi na ukosefu wa ajira na wimbi la vijana kukimbilia kimbilia dar hata Kwa miaka kumi
 
Upvote 1
Tutafute masoko yenye uhakika Kwa kijana akipata nafasi ya kulima na kufuga awe na uhakika wa soko lenye usawa n juhudi za kike anacho kizalisha kwenye kilimo ama
La maingi sana hili bwana Haule, la msingi sana. Maana kijana atavutiwa na maslahi yanayojionesha ikiwa kuna soko zuri.

Tupunguze makodi y mzigo barabarani isiyo na ulazima.leo Kuna kijana n mkulima na mfugaji mzuri pale njombe wa kiazi na ng'ombe ila anashindwa kusafirisha mzigo wa viazi na ng'ombe vifike dar ili auze haraka apate fedha sababu ya hawa wachukua fedha barabarani matokeo kiazi na mifugo vinafelishwa kufika kufika dar na mtu wa njiani na wakati huo kiazi na mifugo vinahitajika sana wakati huo mijini
Mfumo mzuri wa ugavi, kila siku nashauri posta ichukue jukumu la kuwa kama damu ya taifa inavyohakikisha rasilimali zinasambaa mwili mzima Tanzania nzima kupitia huduma ya vifurushi. Fikiria kama tukifika hatua kwa ahilingi alfu tano tu unaweza kisafirisha gunia la viazi kwenda popote nchini??? Uchumi wetu utakua kwa kasi gani?

Yakiboreshwaa hayo pia tutapunguza wimbi na ukosefu wa ajira na wimbi la vijana kukimbilia kimbilia dar
Hakika. Ahsante
 
Back
Top Bottom