Kimei alaani mauaji ya kijana Octavian, ataka haki itendeke na kuwatuliza wananchi

Kimei alaani mauaji ya kijana Octavian, ataka haki itendeke na kuwatuliza wananchi

Ifikie mahali familia ziamue kuwasusia polisi miili wakae nayo huku taratibu nyingine zikiendelea

Kisheria Halmashauri wana mamlaka ya kuuzika mwili ambao umekaa zaidi ya siku tano bila ndugu kuufata na au kuutambua.

Watanzania wote wapo chini ya Himaya ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Sitetei hili lakini alikuwa anakata ndani ya hifadhi kitu ambacho walishapigwa marufuku kisheria, according tu habari ni katika purukushani za ukamataji sidhan kama askari alidhamiria
Hoja yako haina mashiko,huko walikosomea kozi zao za askari hawajafundishwa jinsi ya kumkamata mvunja sheria na kumpeleka sehemu stahiki?Yaani maaskari wote watatu washindwe kumkamata mtu mmoja tu ambaye hana silaha yoyote hadi option iwe ni kumuua tu?Tusitetee uovu hapo mfumo ni mbovu na vitengo vimeshikiliwa na watu wenye uono mdogo haiwezekani wanyama wathaminiwe kuliko uhai wa binadamu.
 
Hoja yako haina mashiko,huko walikosomea kozi zao za askari hawajafundishwa jinsi ya kumkamata mvunja sheria na kumpeleka sehemu stahiki?Yaani maaskari wote watatu washindwe kumkamata mtu mmoja tu ambaye hana silaha yoyote hadi option iwe ni kumuua tu?Tusitetee uovu hapo mfumo ni mbovu na vitengo vimeshikiliwa na watu wenye uono mdogo haiwezekani wanyama wathaminiwe kuliko uhai wa binadamu.
Sorry kukwambia maybe siijui kozi yao kiundani but niliyopita mimi tulifundishwa, na uzuri mmoja kozi za askari almost wote tz zimefanana mitaala kwa 60%, 40% ni mafunzo separate inategemea na jeshi au taasisi.

Kuna taarifa nyingi sana zinatoka eneo husika, wapo wanaosema ni accidental firearm discharge (huwa inatokea, kwa wale waliopitia) wakat wa mikurupushano, wengine mshukiwa alitaka kumdhuru askari kwa panga, wengine wanasema askari wametumia nguvu kupitiliza.

Until then mm nasema tungoje uchunguzi zaidi ili kupata picha halisi nini kilitokea
 
Watanzania tumezidi upole hadi tumekuwa wajinga,ccm na serikali yake wanatutesa na kutuua kadri wapendavyo lakini tunawachekea tu,
Leo anaweza kutokea muuaji mmoja akajifanya yeye ni muungwana na mtetezi wa watu(wenyewe wanatuita wanyonge)tunampigia makofi na kumpa sifa za kila aina kumbe ni usanii tu kwa sababu nyuma ya pazia kuna maelfu ya Watanzania wanadhulumiwa haki zao na hao hao wanaojifanya watetezi wa hao wanaowaita "wanyonge".
Inatia uchungu sana.
 
Watanzania tumezidi upole hadi tumekuwa wajinga,ccm na serikali yake wanatutesa na kutuua kadri wapendavyo lakini tunawachekea tu,
Leo anaweza kutokea muuaji mmoja akajifanya yeye ni muungwana na mtetezi wa watu(wenyewe wanatuita wanyongr)tunampigia makofi na kumpa sifa za kila aina kumbe ni usanii tu kwa sababu nyuma ya pazia kuna maelfu ya Watanzania wanadhulumiwa haki zao na hao hao wanaojifanya watetezi wa hao wanaowaita "wanyonge".
Inatia uchungu sana.
Umenena,kwa nchi zingine itokee tukio kama hilo panakuwa hapatoshi aisee,uhai wa mtu sio jambo la masihara
 
TAARIFA YA KIFO CHA NDG OCTAVIAN HUBERT TEMBA

Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mhe Dkt Charles Stephen Kimei amelaani vikali mauaji ya Ndg Octavian Hubert Temba miaka 25-30 toka kijiji cha Komela, kitongoji cha Komela Kaskazini kata ya Marangu Magharibi ambaye anashukiwa kuuwawa na askari wa hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro (KINAPA).

Dkt Kimei amesema kwa muda mrefu sasa mahusiano baina ya wananchi wanaoishi jirani na hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro sio mazuri kutokana na namna watumishi wa hifadhi hiyo hususani askari wa uhifadhi wanavyowatendea wananchi kwa madai ya kwamba wanasimamia uhifadhi endelevu jambo ambalo sio sawa.

Ifahamike kwamba panapotokea moto mlima Kilimanjaro wananchi wa vijiji vinavyopakana na KINAPA ndio wanaobebwa kwenda kushiriki kuzima moto pamoja na madhila wanayokutana nayo.

Mara zote nilizofanya mikutano katika maeneo hayo wananchi wamekuwa wakieleza kuteswa, wanawake kubakwa, kupigwa na hata kunyang'anywa mali zao kwa kudaiwa wameingia kwenye hifadhi au wamevuna miti ndani ya hifadhi madai ambayo hayatoi uhalali wa matendo ya kinyama na kikatili wanayowatendea wananchi wenzetu.

Familia ya marehemu Octavian ilipofuatilia polisi Himo na Kituo kikuu Moshi Mjini walijulishwa kuna mwili wa mtu anayedaiwa kujinyonga ndani ya hifadhi ya KINAPA ambao polisi wameuchukua na kuupeleka hospital ya KCMC.

Familia ikamjulisha diwani wa kata hiyo Mhe Filbert Shayo ambaye alitushirikisha ofisi ya Mbunge na taarifa zikamfikia Mhe Dkt Charles Stephen Kimei ambaye alishauri Familia ikautambue Mwili kama ni wa kijana wao pamoja na kuukagua kuona kama una majeraha ya kuashiria kushambuliwa (physical torturing). Familia iliridhia na OCD alitoa ushirikiano kwa Familia na ikafanikiwa kufika mochwari KCMC na kuutambua mwili ni wa kijana wao, katika kuukagua wanadai ulikuwa na jeraha linalodhaniwa alipigwa risasi kichwani na wala shingoni hakukua na alama ya kujinyonga kama walivyoelezwa awali.

Familia ilitoa mrejesho kwa haraka sana mamlaka za kiserikali kwa maana ya mkuu wa wilaya alijulishwa pamoja na Mbunge ambaye alimjulisha Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe Anjela Kariuki ambaye alimhakikishia hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wote watakaobainika kusababisha mauaji hayo ambayo yanachafua taswira ya uhifadhi pamoja na utalii wa Nchi yetu.

Mpaka sasa zipo hatua kadhaa zimechukuliwa ikiwemo askari wa uhifadhi waliokuwa doria usiku huo kuwekwa chini ya ulinzi huku jeshi la polisi likiendelea na taratibu zake za kiuchunguzi.

Dkt Kimei amesisitiza uhifadhi endelevu hauwezi kujitenga na mahusiano mazuri na jamii. Matukio ya kikatili kama haya ya mauaji, ubakaji na hata kutesa wananchi kwa dhana ya kukabiliana na uvamizi ndani ya maeneo ya hifadhi au kukabiliana na ujangili haukubaliki kwani ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

Wanyamapori na misitu tuliyojaliwa nchini kwetu ni zawadi toka kwa Mungu tuvitumie kwa maendeleo yetu na vikawe neema kwetu badala ya vilio, hofu na mateso kwani hiyo ni laana.

Dkt Kimei ameendelea kuwasihi wananchi wawe watulivu wakati huu ambao serikali inaendelea na taratibu za kisheria pamoja na kuitaka serikali kuhakikisha haki inatendeka, utaratibu wa uhifadhi endelevu uzingatie mahusiano mazuri na jamii zinazopakana na maeneo yanayohifadhiwa.

Serikali imelipokea jambo hili kwa uzito mkubwa na haki itaonekana kutendeka.

View attachment 2987947
Polisi wa nchi hii ni mashetani kabisa. Yaani Mtu wa kawaida anakwenda kuona maiti anasema huyu kapigwa risasi ya kichwa lakini wao waliona kajinyonga? Na bado OCD Yuko ofisini na dhamira yake ya kuficha uhalifu?
 
TAARIFA YA KIFO CHA NDG OCTAVIAN HUBERT TEMBA

Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mhe Dkt Charles Stephen Kimei amelaani vikali mauaji ya Ndg Octavian Hubert Temba miaka 25-30 toka kijiji cha Komela, kitongoji cha Komela Kaskazini kata ya Marangu Magharibi ambaye anashukiwa kuuwawa na askari wa hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro (KINAPA).

Dkt Kimei amesema kwa muda mrefu sasa mahusiano baina ya wananchi wanaoishi jirani na hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro sio mazuri kutokana na namna watumishi wa hifadhi hiyo hususani askari wa uhifadhi wanavyowatendea wananchi kwa madai ya kwamba wanasimamia uhifadhi endelevu jambo ambalo sio sawa.

Ifahamike kwamba panapotokea moto mlima Kilimanjaro wananchi wa vijiji vinavyopakana na KINAPA ndio wanaobebwa kwenda kushiriki kuzima moto pamoja na madhila wanayokutana nayo.

Mara zote nilizofanya mikutano katika maeneo hayo wananchi wamekuwa wakieleza kuteswa, wanawake kubakwa, kupigwa na hata kunyang'anywa mali zao kwa kudaiwa wameingia kwenye hifadhi au wamevuna miti ndani ya hifadhi madai ambayo hayatoi uhalali wa matendo ya kinyama na kikatili wanayowatendea wananchi wenzetu.

Familia ya marehemu Octavian ilipofuatilia polisi Himo na Kituo kikuu Moshi Mjini walijulishwa kuna mwili wa mtu anayedaiwa kujinyonga ndani ya hifadhi ya KINAPA ambao polisi wameuchukua na kuupeleka hospital ya KCMC.

Familia ikamjulisha diwani wa kata hiyo Mhe Filbert Shayo ambaye alitushirikisha ofisi ya Mbunge na taarifa zikamfikia Mhe Dkt Charles Stephen Kimei ambaye alishauri Familia ikautambue Mwili kama ni wa kijana wao pamoja na kuukagua kuona kama una majeraha ya kuashiria kushambuliwa (physical torturing). Familia iliridhia na OCD alitoa ushirikiano kwa Familia na ikafanikiwa kufika mochwari KCMC na kuutambua mwili ni wa kijana wao, katika kuukagua wanadai ulikuwa na jeraha linalodhaniwa alipigwa risasi kichwani na wala shingoni hakukua na alama ya kujinyonga kama walivyoelezwa awali.

Familia ilitoa mrejesho kwa haraka sana mamlaka za kiserikali kwa maana ya mkuu wa wilaya alijulishwa pamoja na Mbunge ambaye alimjulisha Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe Anjela Kariuki ambaye alimhakikishia hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wote watakaobainika kusababisha mauaji hayo ambayo yanachafua taswira ya uhifadhi pamoja na utalii wa Nchi yetu.

Mpaka sasa zipo hatua kadhaa zimechukuliwa ikiwemo askari wa uhifadhi waliokuwa doria usiku huo kuwekwa chini ya ulinzi huku jeshi la polisi likiendelea na taratibu zake za kiuchunguzi.

Dkt Kimei amesisitiza uhifadhi endelevu hauwezi kujitenga na mahusiano mazuri na jamii. Matukio ya kikatili kama haya ya mauaji, ubakaji na hata kutesa wananchi kwa dhana ya kukabiliana na uvamizi ndani ya maeneo ya hifadhi au kukabiliana na ujangili haukubaliki kwani ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

Wanyamapori na misitu tuliyojaliwa nchini kwetu ni zawadi toka kwa Mungu tuvitumie kwa maendeleo yetu na vikawe neema kwetu badala ya vilio, hofu na mateso kwani hiyo ni laana.

Dkt Kimei ameendelea kuwasihi wananchi wawe watulivu wakati huu ambao serikali inaendelea na taratibu za kisheria pamoja na kuitaka serikali kuhakikisha haki inatendeka, utaratibu wa uhifadhi endelevu uzingatie mahusiano mazuri na jamii zinazopakana na maeneo yanayohifadhiwa.

Serikali imelipokea jambo hili kwa uzito mkubwa na haki itaonekana kutendeka.

View attachment 2987947
Dola inayolinda watawala waovu, nayo ina kinga ya kutochukuliwa hatua dhidi ya maovu wanayoifanyia nchi hususani wananchi.

Haki ni adimu Tanzania
 
Sitetei hili lakini alikuwa anakata ndani ya hifadhi kitu ambacho walishapigwa marufuku kisheria, according tu habari ni katika purukushani za ukamataji sidhan kama askari alidhamiria
Ni sawa ila majani tu yamtoe mtu uhai, kila siku yanaota? Wanajeshi tu ndio rafiki wa wananchi
 
Majani yemyewe mwisho wa siku lazima yaote tena na kua kichaka!!
Kabisaa, mtu ametolewa uhai kisa majani, ninachojua damu ya mtu huwa inalia maana imwagika isivyo halali, kumtoa mtu uhai ni kujitafutia laana pamoja na kizazi chako
 
Back
Top Bottom