Kinachopelekea wanaookoka au kusilimu na kuwa swala tano kufeli kimaisha

Maandiko Matakatifu yanasema, ombeni mtapewa, tafuteni mtapata, bisheni hodi mtafunguliwa…
 

"Amefungia akili kwenye kabati." Buhahahahahaja
 
Hapa kariakoo misikiti inajaa, Njoo usiku hao wenye maghorofa/Apartment ambao bilioni kadhaa haziwqsumbui utawakuta kibao misikitini, hakuna mahusiano yoyote baina ya Ibada na umasikini/Utajiri.
 
Unaonekana hujui hata fundamentals za elimu ya hii dunia, ngoja nikufundishe na huyo mjinga mwenzio.

Siku zote, ukiwa popote kwa wanaojielewa, ukizungumzia fani yoyote, lazima uje na mifano husika toka kwenye vitabu vya hiyo fani, sio unakurupuka tu kama unavyofanya na mwenzio.

For instance, hapa unazungumzia dini ya kikristu, ambayo muongozo wake ni kitabu cha biblia, ajabu badala ulete vifungu husika toka kwenye biblia kusapoti unachoandika, unakuja na porojo zako na kulazimisha watu wakuamini.

Wewe ni mjinga unaenipotezea muda, unaziamini pumba zako kichwani ambazo haziko kwenye maandiko ya biblia, simply, wewe ni mpagani unaejaribu kubadili maandiko.
 
Not quite true! Kuna point flani hapa ila at the expense of the truth. Mungu yupo na sisi tunamhitaji na yeye anatuhitaji pia katika mission yake. Kati ya hekima kubwa sana kati ya wanadamu ni kutambua kuwa ushirikiano kati ya Mungu na mwanadamu ndio mafanikio na lengo kuu la maisha.
 
Upo sahihi mtoa mada, pia binafsi naona kitu pekee cha kumuomba Mungu ni hekima na busara ya kufanya uamuzi/chaguo sahihi wakati sahihi hapa chini ya jua.

Kupitia hekima, binadamu ataweza kutumia uwezo wake aliopewa kwa 100%. Atakwepa vikwazo/majanga lukuki ya ulimwenguni.

Mfano ni Suleiman.
 
Salute mkuu, Kiwango cha upeo wako wa akili na fikra kinashangaza.

Ujumbe mzuri umenyooka na ndio uhalisia, ingawai unaweza usikubalike katika jamii kulingana na mazoea.

👍
Pamoja sana mkuu. denooJ
 
Nakazia

Cc denooJ
 


Mkuu, u love my message but you hate why love it. You are just in denial.
 
Naam, umeelezea vyema.

Kwa lugha rahisi ni kwamba watu wenye Imani Kali ni kwamba hawajiamini.

Mungu anataka tujiamini, Sababu yeye mwenyewe aliyetuumba anajiamini na anajua ukubwa wake.

Tunaposema binadamu ni dhaifu machoni pa Mungu tunakosea. Mungu hawezi kuimba kitu dhaifu. Kwasababu udhaifu wowote wa kitu alichokiumba unatoa tafsiri ya kwamba yeye Muumbaji ni dhaifu pia.

Watu wenye Imani Kali za kidini, hushindwa kutumia uwezo wao mzuri wa kiakili na kimaarifa kupembua vitu kwa usahihi. Wao muda wote hudhani kwa kumtukuza Mungu na kumsifia muda wote basi Mungu atawapa ridhiki kimiujiza. Kitu ambacho si sahihi.

Mungu anafahamu uwezo wake, haitaji tumsifie au tumwambie mara kwa mara juu ya nguvu zake kwetu Sisi wanadamu.

Mungu anataka tumaini ndani yetu, tutende ndani yetu katika namna inayofata. Na ndo mana watu ambao sio wafia dini huwa na mafanikio sababu hufanya vitu kwa kutumia uwezo wao wa ndani waliopewa na Mungu.
 
@Likud unajichanganya.

Umeshasema kule juu Mungu anatutaka tutumie nguvu zetu za asili, sasa iweje tena utake tumuombe Mungu atupe maarifa?!

Hayo maarifa sio nguvu za asili?!

Thread yako imekosa support ya maandiko ndio maana inapoteza muelekeo.
 
Yesu mwenyewe anasema imetupasa kuomba bila kuchoka, Mungu kupitia nabii isaya anasema tumkumbushe, tujadiliane atupe haki yetu.


Wewe unasema tunakosea? Hii imekaaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…