Kinachotokea Afrika Kusini na Kenya inaweza kuwa sawa na Arab Spring kwa nyingine za Afrika

Kinachotokea Afrika Kusini na Kenya inaweza kuwa sawa na Arab Spring kwa nyingine za Afrika

Desprospero

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2023
Posts
1,015
Reaction score
2,493
Mlipuko wa Arab Spring ilianza kama masikhara nchini Tunisia baada kijana mmoja mhitimu wa Chuo Kikuu aliyekosa kazi na kuamua kuuza matunda kwa kutumia toroli mitaani. Lakini alipokatiza mbele ya ofisi za Serikali kuuza matunda alizuiwa na kuadhibiwa kuwa anachafua mwonekano wa mtaa huo. Hasira ya kijana huyu alienda Petrol Station na kununua mafuta akarudi mbele ya ofisi ile ile na kujichoma hadharani.

Wanafunzi wa vyuo vikuu nchi nzima wakapandwa hasira na maandamano nchi nzima kumtaka Rais aondoke ofisini. Upepo huu ukaenea nchi nyingi za Kiarabu na mapinduzi mengi yakafanyika na mauaji pia. Wengi walipoteza maisha kudai mabadiliko.

Leo kuna maandamano makubwa nchini Afrika Kusini na Kenya. Afrika Kusini yanaongozwa na Julius Malems (Juma) wa EFF na Kenya ni Raila Odinga wa Azimio la Umoja. Hofu yangu ni kwamba madai ya waandamanaji SA na Kenya yanafanana. Kupanda kwa gharama za maisha na utawala mbaya wa kifisadi.

Swali ni je, ni nchi ipi za Kusini mwa Jangwa la Sahara ikiwemo Tanzania ni salama katika madai haya? Jakaya Kikwete ametoa clip kumtetea Rais Samia, "mafuta yamepanda hata Uingereza hata wanamlilia gharama kupanda wangefanya nini kama sio unafiki?" Kwangu mimi huu ni utetezi wa kijinga sana maana ni yeye huyo huyo Kikwete aliwahi kuulizwa Kwa nini Watanzania ni masikini? Alisema, "hata mimi sijui". Leo atajuaje Kwa ni gharama za maisha yamepanda? Ushauri wake Kwa Samia ni kuwalambisha asali wapinzani Ili biashara zao zisiathirike Kwa maandamano.

Ninaamini upepo huu ulipoanza kuvuma kutoka J'berg hadi Nairobi utafika Dar es salaam, Kampala, Maputo nakadhalika na watawala wataadhibiwa. Asali isiwapofushe. Teteeni haki na Hali ya wanyonge wasio na sauti. Naomba upepo huo uvume tu kuja Tanzania kuondosha pengo kubwa kati ya walalanjaa na washibenjaa. Nani asimame na umma? Let's count the days ahead!
 
Ni Kenya na South Africa ndiyo wanaweza fanya hivyo. Nchi zingine vijana wengi hawana maarifa, ushinda kwenye vijiwe vya kahawa na kusoma magazeti ya udaku na conspiracy.
Ni vipi, utamshawishi kijana anae amini maandamano ni kazi ya CIA?.
Maadamno yakifanyika ujeruman, Uingereza ama marekani ni sawa. Ila yakifanyika Ribya, Misri inakuwa wamedanganywa wamedanganywa na Marekani.

Uwa ninafurahi sana kusikia watanzania wananyimwa visa ya kwenda nje especially kutafuta maisha ama elimu.
Imejin unapiga kura ccm, Kisha hutaki kuiwajibisha serikali yako pindi inapovuruga na haileti maendeleo then baada ya uchaguzi unatufa visa kwenda ulaya ama marekani ambako wanajenga nchi zao kwa damu, maandamano, kuiwajibisha serikali zao etc.
Wapo tayari kufia barabarani then we ndiyo unataka ukale matunda ya damu yao kiulani.
Kuna majitu yanadhani chumi za Ulaya, Asia na Amerika zilishuka toka mbinguni kama Mana wakati wa Mussa.
 
ngoja tuone Kenya wataandamana Hadi ikulu!?Jana nimeona CDF wa Kenya akisema hawayatambui hayo maandamano na hawataruhusu Hilo Jambo kutokea.
 
Mlipuko wa Arab Spring ilianza kama masikhara nchini Tunisia baada kijana mmoja mhitimu wa Chuo Kikuu aliyekosa kazi na kuamua kuuza matunda kwa kutumia toroli mitaani. Lakini alipokatiza mbele ya ofisi za Serikali kuuza matunda alizuiwa na kuadhibiwa kuwa anachafua mwonekano wa mtaa huo. Hasira ya kijana huyu alienda Petrol Station na kununua mafuta akarudi mbele ya ofisi ile ile na kujichoma hadharani.

Wanafunzi wa vyuo vikuu nchi nzima wakapandwa hasira na maandamano nchi nzima kumtaka Rais aondoke ofisini. Upepo huu ukaenea nchi nyingi za Kiarabu na mapinduzi mengi yakafanyika na mauaji pia. Wengi walipoteza maisha kudai mabadiliko.

Leo kuna maandamano makubwa nchini Afrika Kusini na Kenya. Afrika Kusini yanaongozwa na Julius Malems (Juma) wa EFF na Kenya ni Raila Odinga wa Azimio la Umoja. Hofu yangu ni kwamba madai ya waandamanaji SA na Kenya yanafanana. Kupanda kwa gharama za maisha na utawala mbaya wa kifisadi.

Swali ni je, ni nchi ipi za Kusini mwa Jangwa la Sahara ikiwemo Tanzania ni salama katika madai haya? Jakaya Kikwete ametoa clip kumtetea Rais Samia, "mafuta yamepanda hata Uingereza hata wanamlilia gharama kupanda wangefanya nini kama sio unafiki?" Kwangu mimi huu ni utetezi wa kijinga sana maana ni yeye huyo huyo Kikwete aliwahi kuulizwa Kwa nini Watanzania ni masikini? Alisema, "hata mimi sijui". Leo atajuaje Kwa ni gharama za maisha yamepanda? Ushauri wake Kwa Samia ni kuwalambisha asali wapinzani Ili biashara zao zisiathirike Kwa maandamano.

Ninaamini upepo huu ulipoanza kuvuma kutoka J'berg hadi Nairobi utafika Dar es salaam, Kampala, Maputo nakadhalika na watawala wataadhibiwa. Asali isiwapofushe. Teteeni haki na Hali ya wanyonge wasio na sauti. Naomba upepo huo uvume tu kuja Tanzania kuondosha pengo kubwa kati ya walalanjaa na washibenjaa. Nani asimame na umma? Let's count the days ahead!
Watanzania tuunganishe hapo hapo tudai katiba mpya, tume huru ya uchaguzi na kuondolewa mlolongo wa tozo na maisha magumu. Wiki hii hii sio wiki ijayo.
 
Ingekuwa nimewaona Raila, Karua, na Wajakoya barabarani ningeamoni lakini ni waoga kinyama wamejifungia vyumbani wamewaacha wakala hoi akina Nuru OKANGA wakila gesi ya machozi na virungu vya polisi waliovalia kama wanajeshi
 
Ni Kenya na South Africa ndiyo wanaweza fanya hivyo. Nchi zingine vijana wengi hawana maarifa, ushinda kwenye vijiwe vya kahawa na kusoma magazeti ya udaku na conspiracy.
Ni vipi, utamshawishi kijana anae amini maandamano ni kazi ya CIA?.
Maadamno yakifanyika ujeruman, Uingereza ama marekani ni sawa. Ila yakifanyika Ribya, Misri inakuwa wamedanganywa wamedanganywa na Marekani.

Uwa ninafurahi sana kusikia watanzania wananyimwa visa ya kwenda nje especially kutafuta maisha ama elimu.
Imejin unapiga kura ccm, Kisha hutaki kuiwajibisha serikali yako pindi inapovuruga na haileti maendeleo then baada ya uchaguzi unatufa visa kwenda ulaya ama marekani ambako wanajenga nchi zao kwa damu, maandamano, kuiwajibisha serikali zao etc.
Wapo tayari kufia barabarani then we ndiyo unataka ukale matunda ya damu yao kiulani.
Kuna majitu yanadhani chumi za Ulaya, Asia na Amerika zilishuka toka mbinguni kama Mana wakati wa Mussa.
Umeongea vizuri sana na mfano wa karibu ni Rwanda ambako hakuna chochote Kwa maana ya rasilimali lkn PK anajenga nchi yake Kwa damu za Wakongo.
 
Ingekuwa nimewaona Raila, Karua, na Wajakoya barabarani ningeamoni lakini ni waoga kinyama wamejifungia vyumbani wamewaacha wakala hoi akina Nuru OKANGA wakila gesi ya machozi na virungu vya polisi waliovalia kama wanajeshi
Lazima ujue nini maana ya maandamano. Ukishamuua kinara nani tena atahamasisha maandamano? Au hujui ukimpiga mchungaji nao kondoo hutawanyika?
 
Mtz hata umtie dole la kundu atakaa kimya

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Nimewahi kwenda Ivory Coast ya miaka hiyo wakati ikiitwa "Kisiwa Cha Amani Afrika". Wale watu walikuwa ni wapole kwa dola Yao. Yani upole wa kiwango Cha kuudhi maana ulipokodi teksi ikikufikisha hotelini, dereva anaongozana na wewe Hadi chumbani ahakikishe imefika na utalala salama ndipo unamlipa hela yake. Lakini siku walipochenjiana wenyewe kwa wenyewe kutaka kuondokana na ukondoo ndani ya siku moja mifereji ya Abdijan ilijaa damu kiasi kwamba wanaweza kusimulia tukio hilo ni wanajeshi kutoka Ufaransa waliokuja kutuliza Hali. Walikuwa ni kondoo kuliko Watanzania.
 
Nimewahi kwenda Ivory Coast ya miaka hiyo wakati ikiitwa "Kisiwa Cha Amani Afrika". Wale watu walikuwa ni wapole kwa dola Yao. Yani upole wa kiwango Cha kuudhi maana ulipokodi teksi ikikufikisha hotelini, dereva anaongozana na wewe Hadi chumbani ahakikishe imefika na utalala salama ndipo unamlipa hela yake. Lakini siku walipochenjiana wenyewe kwa wenyewe kutaka kuondokana na ukondoo ndani ya siku moja mifereji ya Abdijan ilijaa damu kiasi kwamba wanaweza kusimulia tukio hilo ni wanajeshi kutoka Ufaransa waliokuja kutuliza Hali. Walikuwa ni kondoo kuliko Watanzania.
Naisikia waliuana kinyama
 
Ingekuwa nimewaona Raila, Karua, na Wajakoya barabarani ningeamoni lakini ni waoga kinyama wamejifungia vyumbani wamewaacha wakala hoi akina Nuru OKANGA wakila gesi ya machozi na virungu vya polisi waliovalia kama wanajeshi

Ona sasa 😁 wenyewe wamejifungia wanakula bata
 
Nchi zote za Afrika wataandamana isipokuwa Tanzania. Awamu ya 6 inafanya mambo makubwa Sana. Hayo ya mfumuko wa bei ni dunia nzima na Sisi Tanzania siyo kisiwa. Mikopo ni sehemu ya maendeleo Kwa nchi au MTU ambaye mtaji hautoshi. Hivi miradi yote inayojengwa Kodi za ndani zitatosha? Acha wakope waweke miundo mbinu Sawa na itachangia uzalishaji na madeni yatalipwa hata miaka 100 ijayo. Tatizo Mh. Rais Hana mtaalam mzuri wa kuelezea majukumu ya mikopo kwa undani. Pia awatumbue wapigaji wanaomwangusha bila kuwaonea huruma. KAZI Iendelee.
 
Mlipuko wa Arab Spring ilianza kama masikhara nchini Tunisia baada kijana mmoja mhitimu wa Chuo Kikuu aliyekosa kazi na kuamua kuuza matunda kwa kutumia toroli mitaani. Lakini alipokatiza mbele ya ofisi za Serikali kuuza matunda alizuiwa na kuadhibiwa kuwa anachafua mwonekano wa mtaa huo. Hasira ya kijana huyu alienda Petrol Station na kununua mafuta akarudi mbele ya ofisi ile ile na kujichoma hadharani.

Wanafunzi wa vyuo vikuu nchi nzima wakapandwa hasira na maandamano nchi nzima kumtaka Rais aondoke ofisini. Upepo huu ukaenea nchi nyingi za Kiarabu na mapinduzi mengi yakafanyika na mauaji pia. Wengi walipoteza maisha kudai mabadiliko.

Leo kuna maandamano makubwa nchini Afrika Kusini na Kenya. Afrika Kusini yanaongozwa na Julius Malems (Juma) wa EFF na Kenya ni Raila Odinga wa Azimio la Umoja. Hofu yangu ni kwamba madai ya waandamanaji SA na Kenya yanafanana. Kupanda kwa gharama za maisha na utawala mbaya wa kifisadi.

Swali ni je, ni nchi ipi za Kusini mwa Jangwa la Sahara ikiwemo Tanzania ni salama katika madai haya? Jakaya Kikwete ametoa clip kumtetea Rais Samia, "mafuta yamepanda hata Uingereza hata wanamlilia gharama kupanda wangefanya nini kama sio unafiki?" Kwangu mimi huu ni utetezi wa kijinga sana maana ni yeye huyo huyo Kikwete aliwahi kuulizwa Kwa nini Watanzania ni masikini? Alisema, "hata mimi sijui". Leo atajuaje Kwa ni gharama za maisha yamepanda? Ushauri wake Kwa Samia ni kuwalambisha asali wapinzani Ili biashara zao zisiathirike Kwa maandamano.

Ninaamini upepo huu ulipoanza kuvuma kutoka J'berg hadi Nairobi utafika Dar es salaam, Kampala, Maputo nakadhalika na watawala wataadhibiwa. Asali isiwapofushe. Teteeni haki na Hali ya wanyonge wasio na sauti. Naomba upepo huo uvume tu kuja Tanzania kuondosha pengo kubwa kati ya walalanjaa na washibenjaa. Nani asimame na umma? Let's count the days ahead!

Watanzania bado unasafari ndefu kuwafahamu.
Mtanzania hawezi kuandamana Kwa ajili ya Haki yake.
 
Back
Top Bottom