Tetesi: Kinana agoma kufika mbele ya Kamati ya Maadili ya CCM

Tetesi: Kinana agoma kufika mbele ya Kamati ya Maadili ya CCM

Status
Not open for further replies.
Mkuu vita ya Musiba unaiweza?
Kwanza mpaka sasa bado hakuna uthibitisho kuwa hili ni kweli, lakini ikitokea likawa kweli, Kinana na Makamba wakajitoa CCM kwasababu ya kile kinyangarika, then huu utakuwa ni uthibitisho kuwa wamegundua kile kinyangarika kinatumwa tuu, hivyo ili kulinda heshima zao, wakaamua kujiepusha na CCM.

Kitendo cha watu waliokipigania chama kwa machozi, jasho na damu katika maisha yao yote, halafu, wakaja kuchafuliwa na kudhalilishwa na kinyangarika fulani ambacho kinatumwa, karma ya Kinana na Makamba ni kubwa, hivyo kama hii ni kweli, then just sit and watch jinsi karma itakavyo kishughulikia hicho kinyangarika na anayekituma!.
P

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Busara hakuna, chama gani wazee kama hao Kinana na Makamba wahofie kutoa maoni yao? Kama watu wa hadhi ya kinana na makamba wawe na hofu ya kutoa maoni kuboresha utendaji wa serikali na chama, wananchi wa kawaida itakuwaje? Kuna watu wana USHAMBA sana wa madaraka! Hawathamini kabisa michango ya watu wengine!
Walimkashifu kitu gani? Maana sijaona kashifa
 
Ni vema wameamua kuondoka mapema kwani CCM inahitaji mabadiliko Makubwa Sana.
Uzee na Uzoefu usioenda na Uadilifu Ni hewa tu na hauna maslahi kwa Taifa letu.

Kama Wana Tuhuma zozote za Kijinai Basi nashauri Mamlaka Husika ziingie kazini.
Wewe hauijui CCM, kwanza chama huwa akina mbadhirifu kama mfikirivyo, haina auditing ya mnayo fikiria, mambo yake upangwa na kamati za siasa na ukaguzi ujifanyia zenyewa taarifa upeleka tu kwenye vikao vya halmashauri kuu, na wajumbe wake ni pamoja na wa kamati ya siasa, hivyo vyote waamuavyo ni halali. Na hawana bajeti kukiwa na jambo. Kumbuka lengo kuu la cha cha siasa ni kushika Dola, mengine baadae, hivyo wewe kama unaona mali na pesa vina dhamani si kwa siasa.
 
Ungeeleza kinachoitofautisha CCM ya Magufuli na hiyo ya akina Makamba na Kinana ingesaidia sana kukuelewa.

Tofauti inayoonekana sasa hivi ni kuwa CCM ya Magufuli ni yake. Anaimiliki. Kama unapenda anayofanya mwenye mali yake, bila shaka hata mali utaipenda.

Lakini inashangaza pia kwamba ile CCM ya akina Makamba na Kinana, pamoja na ubovu wake, ndiyo iliyomweka Magufuli alipo na kumkabidhi hiyo mali anayoihodhi.

Hao wawili, Makamba na Kinana kazi kubwa waliyofanya na CCM yao mbovu kumnadi Magufuli sio kazi inayoweza kubezwa kirahisi hapa leo.
Kila zana na kitabu chake baba.

CCM ya Nyerere haikuwa sawa na CCM ya Mwinyi, na haikuwa sawa na CCM ya Mkapa, na vile vile haikuwa sawa na CCM ya Kikwete na haitakuwa sawa na CCM ya Magufuli, na haitakuwa sawa na CCM ya atakayemfuata Magufuli.

It is a simple fact! Tuliambiwa kuwa ya Kaizari mpe Kaizari; usitafute mwingine wa kumpa.

Wazee hawa sijawasikia wakilalamika kuwa serikali haitekelezi Ilani ya CCM, wanacholalamikia kuwa wamesahahuliwa na serikali !!. Hata wakiondoka CCM sidhani kama wana political impact yoyote tena. Ni afadhali wangenyamaza tu; kuna methali inasema ukila na kipofu usimguse mkono, wao walianza kuvuta kabisa mkono wa kipofu huyo wakaiona
 
MAKATIBU wakuu wastaafu wawili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana na Yusuf Makamba, wamejivua uanachama wa chama hicho.

Habari zilizoifikia SAUTI KUBWA zinasema Kinana na Makamba walijiondoa rasmi CCM kwa maandishi. Barua zao, kila mmoja na ya kwake, zilifikishwa ofisini kwa Katibu Mkuu wa CCM tarehe 7 Februari 2020.

Chanzo kinachoaminika kutoka CCM Makao Makuu kimeiambia SAUTI KUBWA: “Barua zao zimefika kwa nyakati tofauti, zimepokelewa. Lakini inaonekana kama walikuwa wameziandika muda mrefu baada ya kushauriana, maana zinafanana na zimewasilishwa siku moja. Taarifa hizi zilipofikishwa kwa Mzee (Rais John Magufuli) zilimvuruga kwa kweli.”

Kwa mujibu wa chanzo hicho, ambacho hakitatajwa hapa, Rais Magufuli, baada ya kupokea ujumbe wa Kinana na Makamba kujivua uanachama, aliwaomba wazee wawili waandamizi – Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na Spika Mstaafu Pius Msekwa – wamsaidie kuzungumza na akina Kinana ili kuwashawishi wabadili msimamo wao.

Hata hivyo, Kinana na Makamba wamegoma kusikiliza ushawishi wa mtu yeyote. Katika barua zao za kujiondoa CCM, kwa mujibu wa chanzo chetu, Kinana na Makamba waliambatanisha pia kadi zao za uanachama.

“Tayari wameturudishia kadi zetu, maana yake wao si wanachama wetu tena,” kimesema chanzo hicho.

Kinana na Makamba ni miongoni mwa makatibu wakuu wanaoheshimika katika CCM, wenye ushawishi, na ambao wametumikia nchi katika nyadhifa mbalimbali kuanzia jeshini hadi serikalini na kwenye chama.

Siku ambayo walikabidhi barua na kadi zao na kutangaza rasmi kujiondoa CCM, ndiyo siku walipotarajiwa kuhojiwa na Kamati ya Maadili ya CCM iliyoagizwa na Rais Magufuli katika kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), ili wajieleze kuhusu waraka walioanidika kwa Baraza la Wazee la chama hicho wakilalamikia kubezwa na kudhalilishwa na mhuni mmoja anayetumia jina la rais kudhihaki na kushambulia wakosoaji wa rais na serikali.

Mbali na Kinana na Makamba, mwingine aliyeitwa kuhojiwa na kamati hiyo ni Bernard Membe, waziri wa zamani wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ambaye aliunga mkono waraka wa wazee hao, na pia alidukuliwa akizungumza katika simu mambo ambayo hayakumfurahisha Rais Magufuli.

Yeye alikutana na kamati hiyo Mjini Dodoma Ijumaa tarehe 7, Februari 2020; na baada ya mahojiano alionekana mwenye kujiamini na mwenye furaha. Mmoja wa wajumbe walioshiriki mahojiano hayo amezungumza na SAUTI KUBWA kwa sharti la kutotajwa, akisema: “Tulijuta kumuita Membe. Kuna maswali amehoji na masuala amezungumza nasi hadi tukahisi yeye ndiye anayetuhoji. Ukweli ni kwamba chama chetu kinahitaji mabadiliko makubwa ya kimsingi, maana kuna shida mahali. Bwana mkubwa anatupelekesha, na watu jasiri wa kumwambia ukweli hawapo, tunaishia kuagizwa tu, hata kutenda mambo yaliyo kinyume cha misingi ya CCM. Membe ametukumbusha yote haya. Kwa kweli, sijui kinachoofuata.”

Hata hivyo, SAUTI KUBWA iliambiwa wiki iliyopita kuwa agizo la kamati kuwahoji wakongwe hao lilikuwa kama igizo tu, kwani Rais Magufuli na watu wake walishaamua kuwa Membe na Kinana wavuliwe uanachama, na Mzee Makamba apewe onyo kali.

Kwa Kinana na Makamba kujivua uanachama na kugoma kuhojiwa, wamewaza hatua mbili mbele ya Magufuli. Chama hakiwezi kuwahoji kwa kuwa wao hawafungwi tena na nidhamu wala maadili ya CCM kwa kuwa si wanachama CCM.

Ingawa barua zao zilipelekewa kimya kimya, na uongozi wa juu wa CCM umekuwa unahangaika kuzuia taarifa hizi kuvuja, zilivuja mapema mno; na kitendo chao cha kutofika mbele ya kamati kuhojiwa kimezua maswali na mjadala mpana ndani nanje ya CCM.

Baadhi ya wadau wa siasa za Tanzania wanasema inawezekana kitendo hiki kikawaingiza wote wawili, au mmoja wao, kwenye matata makubwa, kwani uongozi wa CCM ni wa visasi, unaweza kutaka kuwakomoa na kuwadhalilisha.

Profesa mmoja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam amesema: “Tusishangae sasa kusikia siku moja Kinana au Makamba wametiwa mbaroni na wanashitakiwa kwa utakatishaji fedha, maana hii ndiyo fimbo mpya ambayo inatumika kuumiza wanaotofautiana na watawala. Lakini iwapo watashitakiwa umma utajua kuwa sababu hasa si uhalifu wao bali ni hii barua yao na uamuzi wao.”

Kiongozo mmoja mwandamizi wa CCM ameiambia SAUTI KUBWA: “Kiukweli, Mzee Kinana na Mzee Makamba hawana cha kupoteza. Nadhani sisi ndio tuna cha kupoteza, maana ukisoma waraka unaowasababishia haya yote utagundua kuwa wao ni watetezi wa misingi ya chama chetu. Wanachotetea ndicho wanaCCM wote tunapaswa kutetea, lakini sasa tofauti iliyopo kati yetu na wao ni kwamba wao wameonyesha ujasiri ambao sisi hatuna. Wengi wetu tumebaki kutii maagizo ya bwana mkubwa, huku chama kinaporomoka!”

SAUTI KUBWA inatambua kuwa kuna mtifuano mkubwa ndani ya CCM ambao haujawahi kutokea tangu uwepo wa chama hicho, ingawa wanafanikiwa kuufunika kwa kutishana – kwa kutumia vuombo vya dola.
Zitto kabwe umeibuka na vioja vyako!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa Ma- Komredi, lazima waumie. Ilikuwa badala ya kusikilizwa malalamiko yao, wao ndio wakaonekana ndio wakosaji, na kutakiwa kufikishwa KIZIMBANI huko Dodoma.
Ina maana msingi wa mashitaka ni kudukuliwa, kwanza ashitakiwe mdukuwaji!
 
CCM CHAMA LAO....MANYUMBU WAMESAHAU WANACHOPIGANIA SASA WOTE TUMEWAGEUZISHA WAMEHAMIA KWENYE MJADALA WA KINANA NA MAKAMBA MKIJA KUSANUKA UCHAGUZI HUU.....


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kumbe yule bwana ni kinyangarika,
Kwanza mpaka sasa bado hakuna uthibitisho kuwa hili ni kweli, lakini ikitokea likawa kweli, Kinana na Makamba wakajitoa CCM kwasababu ya kile kinyangarika, then huu utakuwa ni uthibitisho kuwa wamegundua kile kinyangarika kinatumwa tuu, hivyo ili kulinda heshima zao, wakaamua kujiepusha na CCM.

Kitendo cha watu waliokipigania chama kwa machozi, jasho na damu katika maisha yao yote, halafu, wakaja kuchafuliwa na kudhalilishwa na kinyangarika fulani ambacho kinatumwa, karma ya Kinana na Makamba ni kubwa, hivyo kama hii ni kweli, then just sit and watch jinsi karma itakavyo kishughulikia hicho kinyangarika na anayekituma!.
P

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata Mimi ningekua makamba au kinana nisingeenda
 
Mara nyingi niwaonapo wazee hawa huwa naikumbuka vita ya Kagera iliyomng'oa dikteta nduli fashisti Iddi Amini Dada pale Uganda.

Wakati huo nilikuwa nafanya kazi pale TRC Mwanza station......hakika niliwashuhudia wapiganaji wetu WAZALENDO wengi wakielekea vitani. Nasi tulitoa kila aina ya msaada uliohitajika ili kuwawezesha wapiganaji hawa.

Ndio maana siku mzee Lowassa alipotangaza kujiuzulu uwaziri mkuu sikushangaa kabisa.

Na hata nikisikia mzee Kinana na mwenzie Makamba wamestaafu siasa na kurudisha kadi za chama cha siasa kwa wamiliki wa kadi sitashangaa.

Kuchukua maamuzi magumu ni sehemu ya maisha ya mjeda popote pale duniani.

Nawatakia Dominika yenye Baraka!
 
Kinana na makamba Wana heshima zao.hawawezi kukubali kuburuzwa vikamati "uchwara" ili tuu kumsujudia magufuli.
Kukataa kuhojiwa wameonesha kuwa hawana hoja za kujibu
Ccm hatujawahi kuyumbishwa na viongozi hata siku moja
Jumbe alivuliwa nyadhifa zake zote,zaidi ya nne,Maalim sefu na genge lake walitimuliwa itakua hao wastaafu
 
Hawana tuhuma zozote magufuli anataka kuiendesha CCM kwa mkono wa chuma.wazee wamegoma
Ni vema wameamua kuondoka mapema kwani CCM inahitaji mabadiliko Makubwa Sana.
Uzee na Uzoefu usioenda na Uadilifu Ni hewa tu na hauna maslahi kwa Taifa letu.

Kama Wana Tuhuma zozote za Kijinai Basi nashauri Mamlaka Husika ziingie kazini.
 
Watu Kama nyie humu nchini tunawaita wasindikizaji.hujui ulikotokaa,ulipo, naunapokwenda.
CCM CHAMA LAO....MANYUMBU WAMESAHAU WANACHOPIGANIA SASA WOTE TUMEWAGEUZISHA WAMEHAMIA KWENYE MJADALA WA KINANA NA MAKAMBA MKIJA KUSANUKA UCHAGUZI HUU.....


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom