Pre GE2025 Kinana: Rais Samia wanayemsema ndio ameleta uhuru uliopo nchini sasa hivi, akisema kuanzia leo hakuna maandamano itakuwa nini?

Pre GE2025 Kinana: Rais Samia wanayemsema ndio ameleta uhuru uliopo nchini sasa hivi, akisema kuanzia leo hakuna maandamano itakuwa nini?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kinana anasema wabunge hawaendi bungeni kwa idadi ya watu Bali hoja! Kwa hiyo anamaanisha Wazanzibar na uchache wao wanahoja zaidi kuliko sisi wabara! Hapo ndio nimejua hoja ya Lisu itawamaliza ccm.
Huyu mzee anapotosha sana hili suala tena kwa kurudia rudia! Hakuna shida wazanzibari kuwa na Idadi yoyote wa wabunge wanaotaka kama wangekuwa wanaishia Zanzibar, tatizo linakuja wanapovuka na kuingia upande wa pili ambapo kodi za wote zinatumika kuhudumia hao wabunge.
 
Makamu Mwenyekiti wa CCM Abdulrahman Kinana amezungumza na waandishi wa habari na wanaCCM katika Dodoma akiangazia masuala mbalimbali ikiwemo hoja mbalimbali zilizoshika kasi hivi karibuni kutoka upande CHADEMA na hasa Lissu. Nilichokiona ni kwamba Kinana kajichanganya na kukoroga zaidi badala ya kupangua hoja, tujadili aliyosema Kinana kwa kurejea kauli zake

1. Katiba na Sheria
Kinana anaposema mambo ya katiba mpya yanahitaji muda na tafakuri, Je ni Muda gani? Miaka mingapi?
Kinana anapaswa kufahamu raia wengi hawataki "blank cheque", wanataka kujua ni wakati gani hasa umepangwa kuipata hiyo katiba mpya. Hapa hatajazungumzia rasimu ya katiba ya Warioba.

Kinana Anasema Katiba yetu imepokea mabadiliko mara 14, na ukitazama madailiko hayo mara nyingi yalilenga siasa, madaraka na uchaguzi, hata msukumo wa sasa wa CHADEMA lengo lake ni uchaguzi.!
Kwa nini Kinana anafikiri haya ni mambo madogo na sio ya muhimu au kipaumbele?
Kinana anayesifiwa ni mmojwapo wa magwiji wa siasa nchini hafahamu siasa, madaraka na uchaguzi amabavyo kwa pamoja vinaunda muundombinu wa utawala wa nchi ndio injini yenyewe ya nchi ?! Hajui mambo hayo ndivyo dhima kuu ya katiba zote duniani?! Au anataka tuweke barabara, madaraja,umeme, maji n.k katika katiba?



Tume ya Uchaguzi na Mamlaka ya Rais
Kinana anasema hajaona nchi ambayo Rais hahusishwi kwenye maamuzi ya Uchaguzi na kwamba hakuna tume ya Uchaguzi Duniani ambayo Rais hana Mamlaka. Kinana afahamishwe zipo nchi za aina hiyo na US ni mojawapo. Hata hivyo hoja ya msingi ni tume huru, Kenya wana tume inayoundwa na Rais laikini ni huru na Wakenya karibia wote hawana malalamiko kwamba tume yao ya uchaguzi sio huru.

Kinana anasema Katiba na Sheria ya Uchaguzi siyo njia pekee ya kushinda uchaguzi, Sera nzuri, Kukubalika kwa chama chako, Kukubalika wagombea wako na kujipanga ipasavyo kwenye uchaguzi kuna mchango mkubwa sana kwenye ushindi! Kinana hafahamu kwamba wapinzani wakati mwingine huwa hawapati hata hiyo fursa au nafasi ya kuingia katika sanduku la kura?!


2. Muungano
Kinana anasema CHADEMA wamekuja na hoja kwamba Zanzibar ni ndogo wakati ina wabunge wengi, Kinana anapotosha kwa makusudi au haelewi hii hoja?
Hoja sio wingi au uchache, hoja ni uwiano sahihi na hili Lisu amesemea hata kwa kulinganisha mkoa wa Lindi na Dar es Salaam katika kukosekana uwaino sahihi.

Kinana anasema wabunge hawaendi bungeni sababu ya idadi ya watu, wanaenda kwa uzito wa hoja!
Kinana katika hili amepotoka vibaya sana, usahihi na inavyopaswa kuwa ni wabunge wanaenda bungeni kwa sababu ya idadi ya watu. Rai wanaweza kumchagua hata mjinga kabisa akawawakilishe bungeni na katika demokrasia maamuzi hayo yanaheshimiwa pia.

Kinana anasema CHADEMA Wanasahau muungano wetu ni wa nchi huru, tumeunganisha nchi mbili, na huu Tunakubali na kukiri hizi ni nchi mbili tofauti zilizoamua kuungana kwa hiyari, zikiwa na ukubwa ardhi tofauti, ukubwa wa uchumi tofauti na ukubwa wa watu tofauti, tukiungana lazima tukubali kuwe na uwakilishi wa kutoka pande zote mbili. Usipime watu kwa udogo wao na ukubwa wao, wapime kwa walivyo, walikuwa huru tukaungana nao anasema Nchi ya Seychelles wako 100,007 wana wabunge 35, Lesotho ina watu 2,300,000 wana wabunge 130, Switzerland ina watu 1,700,000 wabunge wa 246 sawa na Tanzania ambapo sisi ni milini 60 na wabunge 300 , Sweden 10,500,000 wana wabunge 349 kwanini hatuwaulizi? Anasema hoja hii ya CHADEMA haina maana, ni hoja ya kuzua, kukorooga vichwa vya watu, kuchanganya watu, kuleta, uhasama, uchochezi. Aansema Haya yote wanayoongea hayaondoi umasikini wala kuleta maendeleo, basi tu tuvurugane!
Kinana afahamishwe hoja kuu ni UWIANO wa uwakilishi, ikiwa tumeamua kuwa na wabunge 50, 100, 400, 1,000 au hata 3,000 n.k, hoja kuu ni UWIANO wa hao wabunge. Sio sahihi mbunge mmoja anawakilisha raia 5000 halafu mbunge mwingine anawakilisha raia 500,000 katika bunge hilo hilo moja.
Swala la kwmba Zanzibara ina sheria zake hata haikufaa alizungumzie kwa sababu litazua mjadala zaidi hasa katika jambo hili ambalo lina athari na maslahi makubwa kwa upande wa pili pia.


3. Kuligawa taifa katika majimbo
Kinana anasema Duniani nchi nyingi hazina majimbo zina mfumo wa umoja, inaitwa unitary system of government, mfumo wa serikari ya umoja.
Suala sio nchi nyingi, suala ni je mfumo tulio nao unatufaa na kukidhi haja yetu. Hata hivyo nchi nyingi kubwa kama Marekani, India, Russia, Brazil n.k zina mfumo wa majimbo au ni unitary system lakini raia ndio wanachagua viongozi wa mikoa na wilaya zao na sio Rais anachagua kila mtu katika kila nafasi.


Rais Samia ameleta uhuru nchini
Kinana anasema Rais huyu wanayemsema, Rais Samia na mtakubaliana na mimi ndiye aliyeleta uhuru ulioko sasa hivi nchini, uhuru wa kusema, kushutumu, kuandamana, uhuru wa mikutano ya hadhara, nina hakika watajibu watasema lakini ipo kwenye katiba, kwani huko nyuma waliponyimwa katiba haikuwepo? Walikwenda barabarani? Katiba ilikuwepo, uhuru huo ulikuwepo lakini ulipigwa marufuku na hawakwenda barabarani. Sasa amekuja kiongozi muungwana amesema katiba inaruhusu na mimi naondoa kifungo kile mlichokuwa mmefungwa kuzuiwa kutumia uhuru wenu halafu wanasema hapana, unajua hii ipo kwenye katiba siyo kwamba ameturuhusu. Leo hii akisema kuanzia leo hakuna maandamano itakuwa nini?
Kinana hafahamu haya anayojivunia ndio chanzo hasa cha watu kutaka katiba mpya?! Rais kuweza kuzuia haki zilizoko ndani ya katiba ndio udhaifu hasa wa katiba yenyewe, sababu zake zinaweza kuwa nyingi ikiwemo na Rais kuteua wakuu wa polisi bila check yeyote, mahakama kutoweza kumshughulikia Rais n.k
Kinana afahamu kwamba tungekuwa na katiba imara ingempa hata yeye fursa ya kushitaki makampuni ya simu yaliyowafanyia udukuzi katika maongezi yao binafsi yeye, Yusuph Makamba na Nape wakipiga soga tu.

Nadhani Kinana akili amechoka kama ulivyoka mwili wake. Hakuna cha maana alichokijibu.

Hawa ni watu wanaofikiria, hata vitu vinavyohitaji vitendo, vinaweza kujibiwa kwa hadithi. Mchakato wa katiba ulifikia hatua ya kupiga kura karibia miaka 10 iliyopita. Katiba pendekezwa ya Warioba ilihusisha maoni ya watu wengi wa kila makundi. Halafu Kinana kwenye porojo zake inasema inahitaji muda, haitakiwi kuwa ya vyama vya siasa tu! Huyu labda akili imekwishaanza kupoteza kumbukumbu. Hivi maoni kuhusiana na katiba mpya, ya jaji Warioba, walikuwa wanawahoji CHADEMA pekee yake? Kweli Kinana amechoka, aachwe apumzike.

Masuala ya Muungano, amepigapiga tu porojo, hakuna cha maana alichojibu. Anasema Muungano ni wa nchi 2, kuna mtu amekataa kuwa siyo wa nchi mbili? Kama anajua ni Muungano wa nchi 2, moja ina serikali yake, nyingine haina. Imeenda wapi?

Wasio na hoja tuwapuuze, madai ya msingi yamebakia pale pale:

1) Wananchi wanataka katiba mpya. Kazi aliimaliza Jaji Warioba na timu yake.

2) Tunataka Tume huru ya uchaguzi, siyo ya kimagumashi, iliyowekwa na mtu mmoja.

3) Tunataka Muungano wenye muundo mzuri wenye kulinda maslahi ya wabia wote wa Muungano.

Kama mtu hana majibu, kama alivyokosa majibu Mzee Kinana, asipoteze muda wa wananchi kwa kuleta hadithi, awaache wananchi waendelee na kuipigania nchi yao ya Tanganyika iliyopotezwa. Au la na Zanzibar ipotee, ibakie nchi moja tu.
 
Kwanini hawataki yaani ikizungumzwa katiba ccm wanakua mbogo hivi hawaoni hata wao itawasaidia pia hivi haya maisha wao wanaona ni sawa? Kawann wamekua wajinga kiasi hiki? Yaan 90 % tunaitaka katiba wao hata asilimia moja ya watanzania hawazidi mbona ni wajinga hivi?
 
Mwalimu Nyerere alituasa kuwa makini sana na wanasiasa wanaoutumia dini , kabila na rangi katika kutafuta uongozi. Wanasiasa waliokosa hoja hukimbilia mambo hayo ili kuwahadaa wananchi.
Tundu lissu wa chadema ni mfano Hai wa ambacho alikielezea Mwalimu Nyerere. Watanzania mpuuzeni maana hajui analoongea lina athari gani kwa jamii yetu.
Yule UVCCM wa Bukoba anayepanga kuwapoteza wapinzani unamuweka kundi lipi? Sabaya na Makonda ambao nao walisema watamaliza wapinzani nao unawaweka kundi gani ati! Mtu wa Tanganyika hawezi kumiliki ardhi visiwani Zanzibar, ila mtu wa Zanzibar anawexa kumiliki ardhi hapa Tanganyika. Huu sio ubaguzi?
 
Kenya walishatoka katika huo ujinga wa tume kubeba wagombea wa uchaguzi.
Hakuna mbunge, seneta, gavana au MCA waliolamika katika huo uchaguzi kuhujumiwa na tume, Odinga peke yake hatoshi kuwa rejea kuhusu tume yao.
Na pia Odinga sio mtu wa kuhujumiwa na tume na kukubali yaishe mepema tu.
Kenya wana matatizo yao mengine katika demokrasia ila tume kuibia watu kura, kuengua au kutangaza wagombea walioshindwa sio mojawapo.
Ukiongea huo ujinga mbele ya wakenya unaweza chapwa makofi mengi Sana
 
Makamu Mwenyekiti wa CCM Abdulrahman Kinana amezungumza na waandishi wa habari na wanaCCM katika Dodoma akiangazia masuala mbalimbali ikiwemo hoja mbalimbali zilizoshika kasi hivi karibuni kutoka upande CHADEMA na hasa Lissu. Nilichokiona ni kwamba Kinana kajichanganya na kukoroga zaidi badala ya kupangua hoja, tujadili aliyosema Kinana kwa kurejea kauli zake

1. Katiba na Sheria
Kinana anaposema mambo ya katiba mpya yanahitaji muda na tafakuri, Je ni Muda gani? Miaka mingapi?
Kinana anapaswa kufahamu raia wengi hawataki "blank cheque", wanataka kujua ni wakati gani hasa umepangwa kuipata hiyo katiba mpya. Hapa hatajazungumzia rasimu ya katiba ya Warioba.

Kinana Anasema Katiba yetu imepokea mabadiliko mara 14, na ukitazama madailiko hayo mara nyingi yalilenga siasa, madaraka na uchaguzi, hata msukumo wa sasa wa CHADEMA lengo lake ni uchaguzi.!
Kwa nini Kinana anafikiri haya ni mambo madogo na sio ya muhimu au kipaumbele?
Kinana anayesifiwa ni mmojwapo wa magwiji wa siasa nchini hafahamu siasa, madaraka na uchaguzi amabavyo kwa pamoja vinaunda muundombinu wa utawala wa nchi ndio injini yenyewe ya nchi ?! Hajui mambo hayo ndivyo dhima kuu ya katiba zote duniani?! Au anataka tuweke barabara, madaraja,umeme, maji n.k katika katiba?



Tume ya Uchaguzi na Mamlaka ya Rais
Kinana anasema hajaona nchi ambayo Rais hahusishwi kwenye maamuzi ya Uchaguzi na kwamba hakuna tume ya Uchaguzi Duniani ambayo Rais hana Mamlaka. Kinana afahamishwe zipo nchi za aina hiyo na US ni mojawapo. Hata hivyo hoja ya msingi ni tume huru, Kenya wana tume inayoundwa na Rais laikini ni huru na Wakenya karibia wote hawana malalamiko kwamba tume yao ya uchaguzi sio huru.

Kinana anasema Katiba na Sheria ya Uchaguzi siyo njia pekee ya kushinda uchaguzi, Sera nzuri, Kukubalika kwa chama chako, Kukubalika wagombea wako na kujipanga ipasavyo kwenye uchaguzi kuna mchango mkubwa sana kwenye ushindi! Kinana hafahamu kwamba wapinzani wakati mwingine huwa hawapati hata hiyo fursa au nafasi ya kuingia katika sanduku la kura?!


2. Muungano
Kinana anasema CHADEMA wamekuja na hoja kwamba Zanzibar ni ndogo wakati ina wabunge wengi, Kinana anapotosha kwa makusudi au haelewi hii hoja?
Hoja sio wingi au uchache, hoja ni uwiano sahihi na hili Lisu amesemea hata kwa kulinganisha mkoa wa Lindi na Dar es Salaam katika kukosekana uwaino sahihi.

Kinana anasema wabunge hawaendi bungeni sababu ya idadi ya watu, wanaenda kwa uzito wa hoja!
Kinana katika hili amepotoka vibaya sana, usahihi na inavyopaswa kuwa ni wabunge wanaenda bungeni kwa sababu ya idadi ya watu. Rai wanaweza kumchagua hata mjinga kabisa akawawakilishe bungeni na katika demokrasia maamuzi hayo yanaheshimiwa pia.

Kinana anasema CHADEMA Wanasahau muungano wetu ni wa nchi huru, tumeunganisha nchi mbili, na huu Tunakubali na kukiri hizi ni nchi mbili tofauti zilizoamua kuungana kwa hiyari, zikiwa na ukubwa ardhi tofauti, ukubwa wa uchumi tofauti na ukubwa wa watu tofauti, tukiungana lazima tukubali kuwe na uwakilishi wa kutoka pande zote mbili. Usipime watu kwa udogo wao na ukubwa wao, wapime kwa walivyo, walikuwa huru tukaungana nao anasema Nchi ya Seychelles wako 100,007 wana wabunge 35, Lesotho ina watu 2,300,000 wana wabunge 130, Switzerland ina watu 1,700,000 wabunge wa 246 sawa na Tanzania ambapo sisi ni milini 60 na wabunge 300 , Sweden 10,500,000 wana wabunge 349 kwanini hatuwaulizi? Anasema hoja hii ya CHADEMA haina maana, ni hoja ya kuzua, kukorooga vichwa vya watu, kuchanganya watu, kuleta, uhasama, uchochezi. Aansema Haya yote wanayoongea hayaondoi umasikini wala kuleta maendeleo, basi tu tuvurugane!
Kinana afahamishwe hoja kuu ni UWIANO wa uwakilishi, ikiwa tumeamua kuwa na wabunge 50, 100, 400, 1,000 au hata 3,000 n.k, hoja kuu ni UWIANO wa hao wabunge. Sio sahihi mbunge mmoja anawakilisha raia 5000 halafu mbunge mwingine anawakilisha raia 500,000 katika bunge hilo hilo moja.
Swala la kwmba Zanzibara ina sheria zake hata haikufaa alizungumzie kwa sababu litazua mjadala zaidi hasa katika jambo hili ambalo lina athari na maslahi makubwa kwa upande wa pili pia.


3. Kuligawa taifa katika majimbo
Kinana anasema Duniani nchi nyingi hazina majimbo zina mfumo wa umoja, inaitwa unitary system of government, mfumo wa serikari ya umoja.
Suala sio nchi nyingi, suala ni je mfumo tulio nao unatufaa na kukidhi haja yetu. Hata hivyo nchi nyingi kubwa kama Marekani, India, Russia, Brazil n.k zina mfumo wa majimbo au ni unitary system lakini raia ndio wanachagua viongozi wa mikoa na wilaya zao na sio Rais anachagua kila mtu katika kila nafasi.


Rais Samia ameleta uhuru nchini
Kinana anasema Rais huyu wanayemsema, Rais Samia na mtakubaliana na mimi ndiye aliyeleta uhuru ulioko sasa hivi nchini, uhuru wa kusema, kushutumu, kuandamana, uhuru wa mikutano ya hadhara, nina hakika watajibu watasema lakini ipo kwenye katiba, kwani huko nyuma waliponyimwa katiba haikuwepo? Walikwenda barabarani? Katiba ilikuwepo, uhuru huo ulikuwepo lakini ulipigwa marufuku na hawakwenda barabarani. Sasa amekuja kiongozi muungwana amesema katiba inaruhusu na mimi naondoa kifungo kile mlichokuwa mmefungwa kuzuiwa kutumia uhuru wenu halafu wanasema hapana, unajua hii ipo kwenye katiba siyo kwamba ameturuhusu. Leo hii akisema kuanzia leo hakuna maandamano itakuwa nini?
Kinana hafahamu haya anayojivunia ndio chanzo hasa cha watu kutaka katiba mpya?! Rais kuweza kuzuia haki zilizoko ndani ya katiba ndio udhaifu hasa wa katiba yenyewe, sababu zake zinaweza kuwa nyingi ikiwemo na Rais kuteua wakuu wa polisi bila check yeyote, mahakama kutoweza kumshughulikia Rais n.k
Kinana afahamu kwamba tungekuwa na katiba imara ingempa hata yeye fursa ya kushitaki makampuni ya simu yaliyowafanyia udukuzi katika maongezi yao binafsi yeye, Yusuph Makamba na Nape wakipiga soga tu.
Tunataka mgombea binafsi. Wanaogopa nini?
Taifa linaingia gharama kubwa kufanya uchaguzi wa magirini kila baada ya miaka mitano. Ni heri usiwepo uchaguzi kuliko kutumia mabilioni ya shilingi kuhadaa ulimwengu kuwa tunafanya uchaguzi;

Kinana asikie tunataka mgombea binafsi.
 
Makamu Mwenyekiti wa CCM Abdulrahman Kinana anazungumza na waandishi wa habari na wanaCCM katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Dodoma. Kinana anategemewa kuzungumzia masuala mbalimbali ikiwemo kujibu shutuma mbalimbali zilizoibuliwa na upinzania ambazo CCM wameziita ni za kibaguzi dhidi ya Muungano.



CHADEMA wametutuhumu CCM, Serikari na Rais kwa mambo ya uongo. Hatukatai kukosolewa na kusahihishwa, lakini hatukubali kuzuliwa wala kushtumiwa kwa mambo ambayo hayapo au ni ya kutunga. Kubwa walilofanya kwenye mizunguko yao ni kujenga chuki na mfarakano miongoni mwa Watanzania.

Hoja zao na ufafanuzi wa Chama cha Mapinduzi

1. Katiba na Sheria
Wanasema wanataka Katiba Mpya na kutushawishi katiba mpya ni muhimu - Mwaka jana 2023 tumekubali hoja ya katiba mpya, na wanatanzania wanaitaka katiba mpya, tunachobishania ni lini, wao wanataka ipatikane leo. Rais Samia wakati anandoa zuio la mikutano ya hadhara alikubali pia kuhusu suala la katiba. Haya mambo yanahitaji muda na tafakuri, lakini wenzetu wanasema hapana, katiba inahitajika sana.

Katiba yetu imepokea mabadiliko mara 14, na ukitazama madailiko hayo mara nyingi yalilenga siasa, madaraka na uchaguzi, hata msukumo wa sasa wa CHADEMA lengo lake ni uchaguzi.

Tume ya Uchaguzi na Mamlaka ya Rais
Serikali imetunga sheria tatu za uchaguzi ambazo zimepita bungeni na Rais kutia saini, sheria ambazo zilitolewa maoni na wadau mbalimbali ikiwemo mpaka bungeni kwa siku nne, ambapo hoja za msingi zilikubaliwa lakini CHADEMA hawakuridhika, bado wasema Rais asihusishwe kwenye uchaguzi wa viongozi wa Tume, sijaona nchi ambayo Rais hahusishwi kwenye maamuzi mfano China, India, Kenya, Afrika Kusini kote Rais anakuwa na mamlaka fulani juu ya Tume. Hakuna Tume ya Uchaguzi Duniani ambayo Rais hana Mamlaka.


CHADEMA walitaka suala la Katiba liwe la CHADEMA na CCM kama chama kikuu cha upinzani na chama tawala, hili haliwezi kufanyika, sababu katiba sio suala la vyama hivi viwili pekee.


Kwa sheria hii nawahakikishia Tume hii itakuwa Huru na kufanya kazi kwa uadilifu, Mweyekiti, Makamu na watendaji watakula kiapo kufanya hiyo kazi, labda kama tunataka malaika kufanya hizo kazi, lakini kazi hizi lazima zifanywe na binadamu.


Katiba na Sheria ya Uchaguzi siyo njia pekee ya kushinda uchaguzi, Sera nzuri, Kukubalika kwa chama chako, Kukubalika wagombea wako na kujipanga ipasavyo kwenye uchaguzi kuna mchango mkubwa sana kwenye ushindi.


2. Muungano
CHADEMA wamekuja na hoja hizi;
  • Zanzibar ni ndogo wakati ina wabunge wengi
  • Rasi samia ni Mzanzibari hana nia njema na sisi - uongo ukirudiwa rudiwa usiposahihishwa unageuka kuwa ukweli, ndicho wanachotaka kuaminisha Watanzania, Watanznia kataeni sumu hiyo inayojaribu kujengwa miongoni mwenu. Kama zanzibar ingekuwa na wnanchi milioni 40 au 60 sawa na sisi je, swali hilo lingekuja? Jibu ni hapana, swali linakuja sababu wako 1,400,000!

Wabunge hawaendi bungeni sababu ya idadi ya watu, wanaenda kwa uzito wa hoja
Wanasahau muungao huu ni wa nchi huru, tumeunganisha nchi mbili, na huu Tunakubali na kukiri hizi ni nchi mbili tofauti zilizoamua kuungana kwa hiyari, zikiwa na ukubwa ardhi tofauti, ukubwa wa uchumi tofauti na ukubwa wa watu tofauti, tukiungana lazima tukubali kuwe na uwakilishi wa kutoka pande zote mbili. Usipime watu kwa udogo wao na ukubwa wao, wapime kwa walivyo, walikuwa huru tukaungana nao. Nchi ya Seychelles wako 100,007 wana wabunge 35, Lesotho ina watu 2,300,000 wana wabunge 130, lakini ndivyo walivyojipanga, Switzerland ina watu 1,700,000 wabunge wa 246 sawa na Tanzania ambapo sisi ni milini 60 na wabunge 300, ndivyo walivyokubaliana uwakilishi wao, Sweden 10,500,000 wana wabunge 349 kwanini hatuwaulizi? Kwahiyo hoja hii ya CHADEMA haina maana, ni hoja ya kuzua, kukotroga vichwa vya watu, kuchanganya watu, kuleta, uhasama, uchochezi. Haya yote wanayoongea hayaondoi umasikini wala kuleta maendeleo, basi tu tuvurugane, mimi naamini muungano huu utadumu.


Ubunge hauwakilishi idadi ya watu, ubunge unawakilisha hoja, matakwa ya watu, maoni, na mahitaji ya wnanchi. Wabunge hawaendi bungeni sababu ya idadi ya watu, wanaenda kwa uzito wa hoja, kuzungumza matatizo ya wananchi, kuzungumza juu ya shida za nchi yetu sio idadi, idadi sawa itafikiriwa lakini sio msingi pekee. Tukatae kugawanywe, waje na hoja za mashiko kuondoa umasikini

3. Kuligawa taifa katika majimbo
Tukishakubali hilo baadaye watasema kila kabila lipate jimbo liwe mkoa, baadaye watasema waislamu na wakristo wawe na eneo lao, mambo huwa yaanza hivi hivi, kuwagawa watu, moja ya sifa ya nchi yetu ni ummoja wa kitaifa, watanzania endeleeni kuikataa hoja hii.

Duniani nchi nyingi hazina majimbo zina mfumo wa umoja, inaitwa unitary system of government, mfumo wa serikari ya umoja.

CHADEMA wanataka kujenga uhasama miongoni mwetu, Watanzania nawasihi tukatae mgawanyiko.

4. Hoja ya Rais Samia na Uzanzibari
Kila kitu kipo kwenye Katiba, mgombea mwenza lazima atoke Zanzibari, kipi cha ajabu? Rais ipo kwa Msingi wa Katiba, hakwenda mwenyewe. Tusisikilize hoja za reja reja, hoja za msimu zinazotaka kutugawa. Mkiwasikiliza sana hawasemi watafanya nini, wanasema kasoro zetu.


Rais Samia ameleta uhuru nchini
Rais huyu wanayemsema, Rais Samia na mtakubaliana na mimi ndiye aliyeleta uhuru ulioko sasa hivi nchini, uhuru wa kusema, kushutumu, kuandamana, uhuru wa mikutano ya hadhara, nina hakika watajibu watasema lakini ipo kwenye katiba, kwani huko nyuma waliponyimwa katiba haikuwepo? Walikwenda barabarani? Katiba ilikuwepo, uhuru huo ulikuwepo lakini ulipigwa marufuku na hawakwenda barabarani. Sasa amekuja kiongozi muungwana amesema katiba inaruhusu na mimi naondoa kifungo kile mlichokuwa mmefungwa kuzuiwa kutumia uhuru wenu halafu wanasema hapana, unajua hii ipo kwenye katiba siyo kwamba ameturuhusu. Leo hii akisema kuanzia leo hakuna maandamano itakuwa nini?


Rais ametoa uhuru wa habari, kila mtu aandika leo, andika unachotaka, ukweli, uongo watu wanaandika, haki za raia sasa hivi zina nafasi kubwa kuliko wakati wowote, tume ya haki jinai juu ya kuboresha haki za watanzania na kuhakikisha watanzania wanatendewa ipasavyo, haya yote yanaitwa maendeleo ya watu na jambo la msingi ni uhuru. Rais amejenga madarasa 20,000 nchi nzima, bwawa la Mwl. Nyerere limekamilika kwa 96%, SGR treni imefika mpaka Dododma, viwanja vya ndege vikubwa vya kimataifa na hajafanya kitu hata kimoja Zanzibar lakini wanalalamika, hoja nyepesi lakini imejaa fitna.


Hitimisho la Kinana
Lazima tukubali, Rais wetu anajitolea sana, Rais anajituma, tukatae kugawanywa na kufarakanishwa, watu wanatafuta uongozi CCM, CHADEMA ACT, CUF, tutafute uongozi kwa hoja zinazosaidia wananchi, zinazoleta maendeleo, zinazopunguza umasikini, tusitafute hoja rahisi za kuchonganisha watu, kufarakanisha watu, za kuvunja umoja wetu.

Kuna ukweli tunatotakiwa kuufafanua na kama ni kero irekebishwe kama kweli tunafikiri muungano huu ni wa muhimu.

1. Wazanzibar wengi sana wanamiliki ardhi na majengo bara, kama raia. ila Wabara wanachukiwa wakienda kule, wanaitwa chogo, na katiba yao inazuia watu wa bara kumiliki ardhi. Juzi nilikuwa Dodoma, kwenda benjamin Mkapa kwenye kona ya Udom, kuna migorofa fulani hivi imejengwa, wanasema karibu na vile vijengo vya majaji, wengine wanamtaja mzanzibari fulani anamiliki hiyo migorofa. tukisema wazanzibar leo hii muungano umevunjika waondoke, wengi wataanza kuuza nyumba nyingi na ardhi kubwa wanayoimiliki. KWANINI BARA HATURUHUSIWI KUMILIKI KULE? faida yao ni nini?

2. kwenye ajira, hii ni kero, wazanzibar maelfu na maelfu wameajiriwa bara, hata kwenye mambo yasiyo ya muungano, wameajiriwa bara ambayo kiukweli ipo bara kwasababu zanzibar kuna utawala wao, lakini wabara hawaruhusiwi kabisa kuajiriwa zanzibaar, hii ni kero, inatakiwa iondolewe, ama la kila mtu abaki kwake.

3. wazanzibar wanakuwa wabunge kule kwao, na huku. akiwa mbunge kule kwao, atakula masurufu ya kule na atakuja kula masurufu ya bara kwa kodi za watu wa bara. tuambieni, yale mipesa wanaku wabunge 50 wa zanzibar wanakiula, zanzibar huwa imechangia bei gani? ni pesa za walipa kodi wa bara. na hao hao wakifika huku wakishiba, wanasenma twende kule kwa passport, kwa msiojua, kile ameongea yule mbunge wa zanzibar kwamba wabara twende kwa passport kwao ndicho kilichopo kwenye mioyo ya wazanzibari wote hata wenye mamlaka huku na hata walioajiriwa huku na hata wanaomiliki ardhi huku, amesema kilichopo kwenye mioyo ya wengi. wala hatakiwi kulaumiwa. kwa waliofika zanzibar wanajua kuwa hicho ndio huwa matamanio yao.

4. mzanzibar anaweza kuwa Mkuu wa wilaya, mkoa, na waziri bara, ila sisi kule marufuku. kwanini?

nimeongea hayo kwa uchache tu, lakini ukweli mwingi hata wanaopinga wanaujua, kama tunataka muungano uwepo, ondoeni kero hizi kwa watu wa bara, ama la, kila mtu achukue hamsini zake kwasababu hakuna kitu wabara wanafaidika nacho as of now. na hawajawahi kufaidika. watu wasioelewa watasema huu ni uchochezi, ila jibuni kwa hoja kama mnazo.
 
Huyu mzee anapotosha sana hili suala tena kwa kurudia rudia! Hakuna shida wazanzibari kuwa na Idadi yoyote wa wabunge wanaotaka kama wangekuwa wanaishia Zanzibar, tatizo linakuja wanapovuka na kuingia upande wa pili ambapo kodi za wote zinatumika kuhudumia hao wabunge.

Hapo Kinana amebwabwaja ili kuwachanganya watu. Hata CCM hawakuonekana kuwa impressed.

Lissu hakuzungumzia idadi ya Wabunge au Waakirishi kwenye baraza lao la Wawalkirishi Zanzibar. Ameongelea Bunge la Jamhuri. Sasa Kinana anatuambia kuwa Zanzibar ni nchi ambayo wanajiamulia mambo yao. Sasa kesho wakiamua kutuletea Wabunge 100 sisi tutasema ni sawa tu ..... Vile vile Kinana anaitaja Zanzibar kama nchi lakini nchi ya pili inayounda Muungano kashindwa kuitaja hata mara moja.

Kwa ujumla Kinana kachochea kuni kwenye moto.
 
Kama hayo yaliyoandikwa ni kweli ameyasema Kinana basi amekosea katika baadhi ya majibu yake. Hapa nitazungumzia kuhusu idadi ya wabunge katika jimbo.
Kinana ametoa mfano wa nchi za Seychelles, Lesotho, Switzerland na Sweden kupinga hoja ya Lissu ya kulinganisha idadi ya wapiga kura na wabunge kutoka Zanzibar na hali ilivyo Tanzania ambako alitoa mfano wa Temeke. Kinana alitakiwa kutoa idadi ya wapiga kura na idadi ya wabunge katika majimbo ya uchaguzi ya nchi alizotaja na sio ya nchi nzima. Lissu hakulalamikia idadi ya wawakilishi katika Baraza la Mapinduzi bali idadi ya wapiga kura katika majimbo yanayotoa wabunge katika Bunge la JMT.
Kosa lingine ni kuwa ukiondoa Switzerland nchi nyingine ni Unitary States.

Tuzungumzie Switzerland. Switzerland ina Cantons 26 ambazo zinatofautiana idadi kutoka watu 16,003 hadi 1,487,969. Switzerland ina mabunge 2 ambayo yote yana nguvu sawa. Kuna National Councilambayo ina viti 200. Viti vinagawiwa kulingana na idadi ya wakazi katika eneo la uchaguzi. Hii ni kama House of Representatives Marekani. Bunge la pili ni Council of States ambapo kila Canton inatoa wawakilishi wawili. Hii ni kama Senate ya Marekani.

Mimi nitatoa mfano wa United Kingdom ambayo nadhani kidogo inafanana na mfumo wetu wa Muungano. UK ni muungano wa nchi nne ambazo ni England, Scotland, Wales na Ireland ya Kaskazini. Nchi zote hizo zina mabunge yao isipokuwa England. Bunge la UK linaitwa House of Commons ( kuna lingine linaloitwa House of Lords). Katika House of Commons yenye viti 650 England ina wabunge 543, Scotland 57, Wales 37 na Ireland ya Kaskazini 18. Jimbo la uchaguzi katika House of Commons linatakiwa kuwa na watu wasiopungua 69,724 na wasiozidi 77,062 isipokuwa kwenye visiwa vya Orkney na Shetland. Ni dhahiri kuwa idadi ya wabunge inatokana na idadi ya watu wanaoishi katika jimbo la uchaguzi na sio idadi ya watu wanaoishi katika nchi husika. Hii ni kwa sababu wabunge ni wawakilishi wa jimbo lao na sio nchi yao.

Tukiangalia mifano hii, idadi ya wabunge katika Bunge letu ilitakiwa kuendana na idadi ya watu wanaoishi katika jimbo bila kujali jimbo liko upande upi wa Muungano.

Kwa mantik hii wabunge kutoka Zanzibar ni wawakilishi wa majimbo yao na sio nchi ya Zanzibar katika Bunge la JMT. Kama tunataka uwakilishi wa Zanzibar basi liundwe Bunge lingine ambalo litakuwa na wawakilishi sawa sawa kutoka kila upande wa Muungano. Kwa mfano, Tanzania Bara inaweza kuwa na wawakilishi 20 na Zanzibar 20 ( Pemba 10 na Unguja 10).

Lissu hakukosea kwenye hili.

Amandla....

JokaKuu
 
We nae unaona eti umeandiiiika na halafu ukaridhika kabisa kwamba umemjibu sawa sawa mh Kinana!! Machagadema mkiambiwa akili zenu ni sawa na nyumbu mnakasirika!
Mimi nitakuwa refa wenu; kati yako na mleta mada.
Hadi hapa tulipo, mleta mada anayo akili safi kabisa mara mia ya hiyo yako, tukitazama tu uandishi wenu.

Watu wa aina yako, ndio mliojazana CCM siku hizi. Hamna uwezo kabisa juu ya jambo lolote. Kilichobaki ni kukaa madarakani kwa nguvu.
 
Kwa mantik hii wabunge kutoka Zanzibar ni wawakilishi wa majimbo yao na sio nchi ya Zanzibar katika Bunge la JMT. Kama tunataka uwakilishi wa Zanzibar basi liundwe Bunge lingine ambalo litakuwa na wawakilishi sawa sawa kutoka kila upande wa Muungano. Kwa mfano, Tanzania Bara inaweza kuwa na wawakilishi 20 na Zanzibar 20 ( Pemba 10 na Unguja 10).
Umetoa maelezo na mifano mizuri kabisa, hasa hiyo la UK na US
Ireland ni ya Kaskazini.
 
Uko sahihi. Northern Ireland ni Ireland ya Kaskazini. Nimesahihisha nilicho andika.

Amandla...
Ninavyozidi kusoma yanayodaiwa yalisemwa na Kinana, nazidi kuwa na wasiwasi juu ya hawa watu wa CCM.

Hivi kweli Kinana anaweza kusema maneno kama haya yaliyowekwa kwenye kichwa cha mada; kwamba:"Rais Samia wanayemsema ndio ameleta uhuru uliopo sasa hivi; akisema kuanzia leo hakuna maandamano....ITAKUWA NIN"I?

Hajui kwamba watu wanaonyimwa uhuru wanayo haki ya kuutafuta uhuru huo? Kasahau kwamba mikutano na maandamano ni haki inayoruhusiwa na katiba ya nchi? Hajui kwamba ni ukiukwaji wa katiba kiongozi anapozuia uhuru wa watu unaotokana na katiba ambayo ndiyo imewaweka madarakani na kuapa kuilinda katiba hiyo?

Kwa mtu kama Kinana kuwa na mawazo ya aina hii, inaonyesha wazi huko ndani ya chama kuna matatizo makubwa zaidi
 
Nani ameleta uhuru nchini?? Hamuoni aibu mwanaume MZIMA unadai uhuru umeletewa na mwanamama toka nchi nyingine??
LISSU anachotuambia tunahitaji kuirekebisha katiba na tuunde muungano wetu vyema na kilanchi iwe na serikali au serikali iwe moja
 
Ninavyozidi kusoma yanayodaiwa yalisemwa na Kinana, nazidi kuwa na wasiwasi juu ya hawa watu wa CCM.

Hivi kweli Kinana anaweza kusema maneno kama haya yaliyowekwa kwenye kichwa cha mada; kwamba:"Rais Samia wanayemsema ndio ameleta uhuru uliopo sasa hivi; akisema kuanzia leo hakuna maandamano....ITAKUWA NIN"I?

Hajui kwamba watu wanaonyimwa uhuru wanayo haki ya kuutafuta uhuru huo? Kasahau kwamba mikutano na maandamano ni haki inayoruhusiwa na katiba ya nchi? Hajui kwamba ni ukiukwaji wa katiba kiongozi anapozuia uhuru wa watu unaotokana na katiba ambayo ndiyo imewaweka madarakani na kuapa kuilinda katiba hiyo?

Kwa mtu kama Kinana kuwa na mawazo ya aina hii, inaonyesha wazi huko ndani ya chama kuna matatizo makubwa zaidi
Hata mimi ndio maana nina wasiwasi kama kweli kayasema. Ukisema Samia kaleta uhuru unamaanisha kuwa kabla yake hapakuwa na uhuru. Sasa kwa vile huo uhuru ni haki ya msingi ya kikatiba ya raia wa JMT ni kuwa anakiri kuwa chama chake (ambapo Rais wa sasa alikuwa Makamu wa Rais wa awamu iliyopita) kimekuwa kikikiuka Katiba katika awamu zote mpaka hii ya sasa! Na kwa vile Kinana amekuwa katika nafasi za juu katika Chama au serikali iliyoundwa na chama chake basi nae alishiriki katika ukiukwaji huo uliowanyima uhuru watanzania!

Amandla...
 
Kumbe hakunaga namna Rais wa Nchi ataweza kujiweka kando na Uteuzi wa viongozi wakuu wa Tume Huru ya Uchaguzi

Hata Kenya na Africa Kusini ambako makamu Mwenyekiti wa Chadema mh Tundu Lisu anaona Tume Huru ya Uchaguzi ni Bora Bado Mwenyekiti anachaguliwa na Rais

Nasubiri majibu ya Tundu Antipas Lisu kwa makamu Mwenyekiti wa CCM komredi Kinana

Nawatakieni Dominica Njema
Kwanini hawataki kusema mifano ya nchi ya US, Canada na UK?! Wanaleta mifano ya nchi za ajabuajabu?; uchina?! Kenya?!
 
Back
Top Bottom