Kingunge: Mchakato wa kumpata Mgombea Urais CCM ulikuwa batili! Lowassa si fisadi kama inavyodhaniwa

Kingunge: Mchakato wa kumpata Mgombea Urais CCM ulikuwa batili! Lowassa si fisadi kama inavyodhaniwa

Mzee kingunge anajua taratibu za kuweka kiongozi wa kuwa Raisi.Mojawapo ya taratibu ni kuwa kiongozi lazima apate ridhaa ya baraza la wachawi wa utawala linalohusisha wazee walio hai na waliokufa wanaohusika na utawala wa nchi la Sogotimko linalokaa kikao chake kule Maghadeshi.Baraza hilo lilifanya kikao chake tarehe 30 may 2015 na nilitoa taarifa rasmi hapa jamii forums ya kikao hicho. Wakati mchakato unaanza mimi nilikuwa mmojawapo niliyehudhuria kama mwanafunzi (trainee) wa uchawi wa utawala.Wazee wote walikuwepo kasoro wawakilishi wa raisi aliyeko madarakani (Kikwete) walio hai na waliokufa.

Kuna mjumbe alimwuliza Kingunge mwakilishi wa Kikwete ambaye ndie mkabidhi nchi yuko wapi mbona hapa kwenye baraza haonekani? Kingunge akasema hamda haja kikao kiendelee.Mwenyekiti akasema lakini si utaratibu kwa sababu swala si wengi wanasema nani apewe swala ni kuwa lazima baraza zima la Sogotimko likubaliane kwani kwenye baraza la uchawi wa utawala mjumbe mmoja aweza kwamisha mgombea asipite.Kingunge akasema hamna haja akiwa anajiamini na waganga wake koko aliookoteza barabarani.

Walipoulizwa kundi zima wanasemaje wakasema sawa Lowasa apewe na mimi nilitoa taarifa ndani ya jamii forums tarehe 1 june 2015 kuhusu kuteuliwa kwa Lowasa na baraza la sogotimko kule maghadeshi.Moderator alifuta kabisa ile taarifa niliyotoa kwa umma muda mfupi tu baada ya kuitoa.

Dharau ya Kingunge kwa wawakilishi wa Kikwete imesababisha yote hayo.Ninaweza sema wazi kuwa Kingunge na kelele zote ndiye aliyechangia pakubwa kumwangusha Lowassa kwa ushauri mbovu na kutolipeleka swala hilo vizuri kwenye baraza la utawala kule Maghadeshi.
 
Kwa mara ya kwanza nimeshindwa kuelewa kilichoandikwa hapo juu.




Naombeni ufafanuzi.
 
Kwenye hilo baraza lenu LA wachawi na majini, magufuli alikywepo:what:
 
Nae atulie tu asilete hasira zake za kunyang'anywa tenda ya kukusanya ushuru pale Ubuno Terminal
SINA IMANI NA UKAWA
 
Mzee anatapatapa, asome alama za nyakati, wenzie hiyo chapter imeshafungwa ndio maana Sophia Simba alishiriki mapokezi ya John Magufuli.

Kwa umri wake ni vigumu kusoma alama za nyakati, ni wa kusamehewa tu.

La kumkumbusha ni moja tu, huyu aliyechaguliwa `Mgufuli` ameshindwa wapi ktk maeneo aliyopewa? Maana kamtamka Lowasa na Mradi wa maji kanda ya ziwa na wala hatuambii ya Wizara ya Ardhi.

Yote kayasema ila la msingi ni hili: "Mzee kingunge ameongeza kuwa Lowassa yupo tayari kushirikiana na Chama kusaidia Chama kupata ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi mkuu."

Na akaongeza: "......lakini mwisho wa siku watoke tukiwa wamoja ili kupambana na adui."


Hapa kajisafisha, yote mengine aliyesema futa kwani mwanzo wa safari yake ya kumuunga mkono Magufuli na maamuzi ya chama yanaanzia hapa. Kumbukeni niliwaeleza mara kwa mara wakati akimuunga mkono Lowasa, kuwa huyu mzee yupo nje ya system ya chama kwa sasa hivi ni si maarufu vile kama mnavyofikiria. Hasomi alama za nyakati kutokana na umri wake.
 
Wale wote 38 waliokatwa majina Yao wanalalamika chini chini lakini wengi ni wanafiki sana, wanaogopa kulalamika Kwa uwazi wakihofia kukosa Vyeo , Ubunge na Uwaziri kwenye Serikali ijayo ya magufuli , Unafiki ni sumu kubwa na cha Ajabu hapa Tanzania Msema Ukweli huwa Adui lakini Msema uongo na mpenda magumashi huwa rafiki wa wengi, Mzee kingunge kasema Ukweli na habari ndiyo hiyoo asiyekubali atabakia kuwa Mnafiki milele.

Alitakiwa mtu mmoja kati ya 38 kwa nini Lowasa ndiye analia sana kuna nini uvunguni?
 
Maandishi yako yooootee hayawez kuondoa ukweli wa alichokisema mzee Kingunge. Hayo mambo ya kiimla ya China hayatuhusu hapa kwetu. Sisi tuna sheria zetu tofauti na za China. China ukila rushwa unatwangwa risasi, hapa kwetu unafungwa, fine au hata kudunda mitaani. Hivyo hayo mambo ya Kichina hayatuhusu, ukweli wa mzee Kingunge hakuna hata mmoja ataweza kuukanusha. Mzee huyu anakuwa mtu wa Tano katika watu waliopinga mchakato ulivyoendeshwa:-
1.Dr Nchimbi
2.Mama Sophie Simba
3.Kimbisa
4.Dr Kakokola
5.Mzee Kingunge

Watu hawa wote hawawez kuwa waongo!

Kwa nini yeye tu analalamika kuna nini? wenye chama wamefanya mchakato umeisha, angeshawishi awe mgombea pekee lakini walikua 42 na 38 walirudisha fomu.
Ghalibu kakatwa, Pinda kakatwa, Sumaye kakatwa kwanini Lowasa tuambiwe!!!!
 
Hajuia Antendalo kivipi ? Kwani kusema kweli ni Dhambi? Wenye Akili zao wanajua Ukweli sasa upo wazi , Tatizo la watanzania wengi ni kupenda Uongo kuliko Ukweli ndiyo maana wasema uongo huonekana bora kuliko wasema Ukweli. Sasa kingunge kaanika ukweli atapata maadui wengi sana na huenda akaundiwa zengwe pia .

Wajumbe wa NEC waliambiwa kazi yao ni kupitisha majina 3 kwenda mkutano mkuu asiye afiki atoke nje sasa kanuni gani ilivunjwa ikiwa wote walishiriki kupiga kura.
 
Aindoi similarities zilizopo baina ya hivyo vyama viwili kwenye umuhimu wa sura ya chama na kuangalia integrity ya mwanachama anaye gombea anasura gani kwenye jamii na kama ndio mtu anaefaa kushika uongozi wa chama kama kinavyojinadi.

Uwezi kutembea na watu wenye kila aina ya kashfa halafu utake kuwa kiongozi wa chama ambacho kinapinga aina ya watu hao the 'iron law of oligarch' will apply from the party elites of the time iwe wanajiita CC kama CCM au Pelitrubo Committee ya China.

Anyway argument yangu ni kwamba kutokana na support aliyokuwa nayo Lowassa ndani ya chama na kuachwa mpaka wakati wa uchaguzi wa ndani ilikuwa makosa na matokeo yake kutolewa kwa kuvunja kanuni ili kuzuia support yake na democracy processes za chama sio njia sahihi na hapa nakubaliana na argument ya Kingunge 'dont shoot the messenger' alichokisema ni ukweli mchungu wa uvunjifu wa taratibu kufikia malengo ambayo yanaweza onekana sio sahihi kwa supporters wa mwanachama aliye enguliwa.

Kwa hivyo wala sishangai watu kutoka hadharani na kupinga kwa kile kilichotokea kwa sababu kushinda uchaguzi wa ndani ya chama chochote cha siasa lazima uwe na support on all levels of party structure kuelekea uchaguzi, kwa hivyo kama waliamini hafai walikuwa na muda mrefu sana wakuimaliza safari yake prior to changing of guards procedure na kutumia mbinu chafu zinazo vunja taratibu kama waliyoifanya Dodoma sivyo watu wanavyofanya.

Ndio maana leo usikii watu wakilalama kukatwa kwa Nyalandu au Kingwang'ala kwa sababu they just dint have that internal support hila kukiwa na mgombea mwenye support to ensure mambo kama haya ayatokei its simple badala ya kusubiri uchaguzi na uvunje kanuni, peleka ushahidi wa tuhuma mtoe kwenye mbio mapema ndio watu wanavyoendesha vyama vya siasa nchi zilizoendelea na kuzuia mipasuko hizi ndio sababu sisi waafrika tunaishia kuvuruga mataifa yetu kwa kufanya mambo kiholela holela.

cc moshdar

Taratibu kwa mujibu wa kanuni za CCM zimezingatiwa wao huamua hivyo mambo yao, kumbuka Nyerere alimwambia Kawawa simtaki John na akatolewa katika kinyanga'nyiro hiyo ni kanuni iliheshimiwa John alikubali.

Mara hii tena kanuni ni zile zile Lowasa katolewa na siyo peke yake pamoja na Vigogo wenzie, NEC imekaa ubishi ukaanza wakaambiwa kazi yao siyo kuhoji Bali kupokea majina 5 na kupigia kura majina 3 yaende mkutano mkuu, ubishi ulipozidi Ben akasimama kuwaambia wajumbe tumepokea majina 5 tupige kura asiyetaka mlango uko wazi hakuna hata mmoja aliyetoka kura zimepigwa mshindi kapatikana.

Shida kubwa ipo kwenye Katiba ya vyama vyote vya siasa Tz kuna wenye turufu, Maalim Seif alimfukuza mwanzilishi wa CUF watu kimya, tumeona Katiba zinabadilishwa ili watu waendelee kuongoza watu kimya, watu wananyanga'nywa uanachama wao watu kimya!!!

Kwa nini Lowasa????
 
Last edited by a moderator:
Ndugu wana jamvi,

Nachukua wana fursa hii kuwasalimu wana CCM na wasio wana CCM, Nichukue fursa hii kuwapongeza wasio wana CCM kwa kulaumu jinsi mchakato ulivyokwenda ndani ya vikio vya chama. Nawapongeza sio kwa sababu wapo sahihi, hapana, ila nawapongeza kwa nia yao nzuri ya kutotaka uvunjifu wa taratibu, kanuni na sheria katika ufanyaji wa maamuzi mbalimbali.

Nawashangaa wana CCM ambao leo ndio wanajua umuhimu wa kufuata taratibu, kanuni na sheria zilizotungwa? Kwa mheshimiwa Kingunge, heshima kwake, napata shida kumuelewa; hivi hakuwepo kwenye Bunge la Katiba?

Kuna watu walisingiziwa wamepiga kura ya ndio na huku hawakupiga, kwa Kingunge ilikuwa sawa! Kumbukumbu zangu zinanipeleka kwenye maneno yaliyowahi kusemwa na kiongozi mmoja "Ukishakula nyama ya mtu hauwezi kuacha"

Sasa kwa kumsaidia mzee wetu, kila mwanajamvi mwenye kumbukumbu ya uvunjifu wa sheria na kanuni wa serikali ya CCM aandike, lengo sio kushangilia kilichotokea Dododma, la hasha, bali kuwakumbusha wana CCM umuhimu wa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu mlizojiwekea.

Nawakumbusha tena wanajamvi, lengo sio kupongeza kukatwa kwa mtu fulani hapa,
 
Me mwenyewe ninawashanga ccm walivyo majuha kwakujuwa kabisa ccm hawakufuata kanuni lakini bado yakazidi kutulia kama majuha kweli ccm ni janga na kuwa ccm lazima uwe juha!
 
Aindoi similarities zilizopo baina ya hivyo vyama viwili kwenye umuhimu wa sura ya chama na kuangalia integrity ya mwanachama anaye gombea anasura gani kwenye jamii na kama ndio mtu anaefaa kushika uongozi wa chama kama kinavyojinadi.

Uwezi kutembea na watu wenye kila aina ya kashfa halafu utake kuwa kiongozi wa chama ambacho kinapinga aina ya watu hao the 'iron law of oligarch' will apply from the party elites of the time iwe wanajiita CC kama CCM au Pelitrubo Committee ya China.

Anyway argument yangu ni kwamba kutokana na support aliyokuwa nayo Lowassa ndani ya chama na kuachwa mpaka wakati wa uchaguzi wa ndani ilikuwa makosa na matokeo yake kutolewa kwa kuvunja kanuni ili kuzuia support yake na democracy processes za chama sio njia sahihi na hapa nakubaliana na argument ya Kingunge 'dont shoot the messenger' alichokisema ni ukweli mchungu wa uvunjifu wa taratibu kufikia malengo ambayo yanaweza onekana sio sahihi kwa supporters wa mwanachama aliye enguliwa.

Kwa hivyo wala sishangai watu kutoka hadharani na kupinga kwa kile kilichotokea kwa sababu kushinda uchaguzi wa ndani ya chama chochote cha siasa lazima uwe na support on all levels of party structure kuelekea uchaguzi, kwa hivyo kama waliamini hafai walikuwa na muda mrefu sana wakuimaliza safari yake prior to changing of guards procedure na kutumia mbinu chafu zinazo vunja taratibu kama waliyoifanya Dodoma sivyo watu wanavyofanya.

Ndio maana leo usikii watu wakilalama kukatwa kwa Nyalandu au Kingwang'ala kwa sababu they just dint have that internal support hila kukiwa na mgombea mwenye support to ensure mambo kama haya ayatokei its simple badala ya kusubiri uchaguzi na uvunje kanuni, peleka ushahidi wa tuhuma mtoe kwenye mbio mapema ndio watu wanavyoendesha vyama vya siasa nchi zilizoendelea na kuzuia mipasuko hizi ndio sababu sisi waafrika tunaishia kuvuruga mataifa yetu kwa kufanya mambo kiholela holela.

cc moshdar
ccm played the game and beat kingunge on his own style. kwa muda mrefu kazee kamekuwa ndo kocha wa mbinu chafu, na za kidhulma, za ccm dhidi ya wasio wana ccm. Sasa mchezaji (ccm) amehitimu vizuri, katumia mbinu za kocha (kingunge) kushinda mchezo dhidi ya kocha mwenyewe, cha ajabu kocha analalamika tena!!! hivi hakujua matokeo ya mwanafunzi kufuzwa ni mwanafunzi huyo kufuzu kwa maana ya kumudu maarifa na mbinu za medani alizopewa na kocha?!!!!

kwenye matamshi haya ya kingunge hakuna la maana zaidi tu ya lile la yeye mwenyewe kingunge, kama mwanaccm, kuwadhibitishia watanzania kuwa, kumbe ni kweli kuwa, kwa miaka karibu yote ya siasa za vyama vingi, ccm huwa inashinda uchaguzi si kihalali bali kwa mbinu chafu na za kijanjakijanja. Mzee aliua kwa upanga na, uzuri ni kuwa, kanuni zipo wazi...ukiua kwa upanga na wewe utauwawa kwa upanga, malipo ni hapa hapa duniani. Machozi ya Salim Ahmed Salim hayatopotea bure.

tulishasema muda mrefu ccm ilifanya makosa makubwa sana kuzitosa fikra za Nyerere na kukimbilia kuwekeza na kujijenga juu ya msingi wa ufisadi. ccm haikusikia. imejijenga kiufisadi na itaangushwa na ufisadi huohuo na muda ndo umefika sasa. Baada ya wajumbe watatu wa CC kutoka nje, na kumwaga hadharani siri za mazingaumbwe ya cc, basi ccm will never be the same anymore. ccm haitokaa iwe kama ilivyokuwa tena na dalili la anguko lii kila mahali....Mene Mene Tekeli na Peresi...Maandishi yapo ukutani.
 
Mtu wake kakatwa na pesa amekula Mzee wa watu! Ha ha ha
 
Kwa namna yoyote ambayo Mzee Kingunge ataongea, bado ataonekana anatetea maslahi yake hasa kutokana na Lowassa kuwa na mpango wa kutengania kofia za Rais na Uenyekiti wa CCM baada ya kuingia madarakani. Hatujui huyu mzee kama aliahidiwa chochote kutokana na mpango huo.
Hakuona jinsi CCM ambavyo ingepata shida kuiba hela za serikali kwa matumizi ya chama, kama ilivyoiba hela za TANAPA za kujengea ule ukumbi wao mpya wa mikutano, uliofungwa vifaa vya gharama kubwa vya ulinzi. Ina maana hakuona hilo na ukongwe wake wote ndani ya CCM?
Bado najiuliza kwanini hakumshauri kuachana na mpango wake wa kulirudisha nyuma suala la Katiba Mpya badala ya kwenda moja kwa moja kwenye upigaji kura? Wenyewe Maccm wanaamini uamuzi huo ni sawa na kutoa ushindi kwa Ukawa, sasa Kingunge hakuona kama Lowassa wake atalazimishwa kukatika kutokana na hilo?
Vilevile, kwanini hakumshauri kuachana na mpango wake wa kuivunja Bakwata na kuundwa upya chombo hicho pamoja na vyombo vingine vya Kiislam vinavyoilalamikia Bakwata, na kuundwa chombo hicho maridhiano yatakayofanya chombo hicho kikubalike kwa Waislam wote?
Ina maana hakujua kama kuna vigogo wenzei wa chama kama Shamim Khan wamejificha huko na kushiriki kuuza na kujikodisha mali za Bakwata? Hakujua kama hayo yote yangewaumbua vigogo wa chama waliojiuzia na kujikodisha mali za Bakwata na akaacha aendelee kujipanga kwa mpango wake huo? Sasa anamlaumu nani?
Na hivi hakujua kauli na mambo yake wakati alipokuwa atafuta wadhamini zilikuwa zinamfanya akiuke sheria za uchaguzi na ndizo Jaji alizozitumia kwa kuandika ule waraka uliotishia kwamba, endapo atapitishwa kuna uwezekano wa kuwekewa pingamizi na wapinzani wake na likapita, hivyo CCM kukosa mgombea kwenye kiti cha Urais? Kwanini hakumkataza?
Kingunge, anapaswa kupumzika sasa amalize maisha yake salama kwani vile vitalu vya Utalii alivyopewa kwa upendeleo vinamtosha sana kuishi bila kelele hata kama Pinda alimpora kituo cha mabasi Ubungo na parking za mjini na kujipa yeye kwa mgongo wa yule mshikaji wake wa Msasani Club.
Kuna kitu kimoja mzee Kingunge ambacho hakijui, ni kwamba hidi ni dalili za mwaka wa mwisho wa CCM kuwa kama chama tawala, kwa kawaida anayekaribia kufa huweweseka na kupoteza mwelekeo. Kwa ukongwe wake anashindwa kusoma alama za nyakati? Hajui kama CCM imekosa mgombea kabisa katika list nzima ya wagombea wao 42? Poleni sana Maccm.

Ova
 
Source:ITV saa 2.Mambao yanaanza noga.CCM wakumbushana kufanya maridhiano ya ndani ili waweze pata ushindi..NI wazi moto ndnai ya CCM ni mkubwa kuliko akili ya CCM..ni muda tuu kila pembe ya nchi itasema yao,na mwishowe hata akina PInda na wengine nao watawasha moto kwa siri na mwisho wazi
 
Ngoja waumizane washenzi walikuwa wanadanganya ulimwengu kwamba wametoka Dodoma wakiwa wamoja na sasa yamewafika!
 
Maridhiano baada ya mchakato ni hila za kutaka kutumiana baada ya ku abyusiana. Ni sawa na Sita kutaka maridhiano na ukawa baada ya kutoa li rasimu ili tu kwamba Ukawa waliunge mkono.

Mitafarku walioona tangu mwanzo. Ukiukwaji wa taratibu waliouona hata kabla ya kuanza kwa mchakato. Kama ndivyo walitakiwa wadhibiti hali ile kama kuziba ufa badala ya kuacha nyumba imeanguka sasa wanaanza kujenga ukuta.

Kwa sasa waitane waombane misamaha bila unafiki ili wakubaliane kumpa aliyewazidi kete na waliopoteza milele wakubali wamepoteza.

Lakini sidhani kama ccm itasimama tena kwa sababu Kakobe alishatamka na neno like halirudi bure!.
 
Back
Top Bottom