Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana

Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana

Masikini wa akili wewe!

Kwa hiyo wewe unashabikia vifo vya wananchi vinavyosababishwa na mgomo huu,kwa vile tu wanadai maslahi?That is the very primitive approach.Kwa taarifa yako mimi namfahamu Dr Ulimboka kuliko unavyofikiri kama KENGE kuogopa matone ya mvua na kukimbilia mtoni.Nimesoma nae pale the then MUCHS.NARUDIA KUSEMA:SIUNGI MKONO UDHALILISHAJI,UNYANYASAJI NA UTEKAJI ALIOFANYIWA DR ULIMBOKA.Lakini bado serikali inatoa nafasi ya mazungumzo,wao wanataka madai yatekelezwe leo.Wakae na serikali wazungumze na ikishindikana waandamane hadi Ikulu.Mgomo ni last option.
WEWE UTAKUWA NI KILAZA UNASHABIKIA MAMBO BILA KUANGALIA IMPACT TO THE COMMUNITY.JUST COMPARE THEIR DEMANDS WITH THE IMPACT OF THE STRIKE TO THE PUBLIC.You are likely a madman
 
We acha tu MJ1...Yaani hii kitu imenikosesha raha sana. Kutaka kumuua mtu kwa kudai haki ambayo Watanzania wengi tunaona wanastahili na pia kuziboresha Hospitali zetu...Wakati mafisadi wa EPA, Rada, Kiwira n.k. wanaendelea kupeta....Nchi haina muelekeo kabisa na hawa walio madarakani hawastahili kuwepo maana kazi imewashinda sasa wanaanza kujihami kwa kuwaua Watanzania.

Watanzania wangapi wanaokufa kwa huu mgomo haramu? hilo umefikiria? au huyo kibaraka mmoja ni bora kuliko maelfu kama si malaki ya Watanzania wanaokosa huduma?

Nna uhakika waliomfanyizia hawaitakii mema Tanzania na wamemtumia huyo kama chambo, na alivyokuwa na tamaa akadhani anakwenda kupewa mlungula kumbe anakwenda kuchezea kichapo na kufanyiwa makusudi akumbuke maneno wanaotaka aje kuyasema ili kuwavuruga Watanzania.

Nakubaliana na Pasco, ma professionals huwa hawafanyi hivyo, huwa wanakumaliza au wanakupoteza tu, hawakisii. Hawa waliofanya hivi wamefanya makusudi kabisa halafu wakawapigia simu hao wanaojiita human rights na wao amma wamemezeshwa mshipi, ndoano na chubwi au wanajuwa kinachoendelea.
 
Mkubwa mimi niko pampja na wewe.Tatizo la hawa madaktari wanadhani na kujiona wao ni muhimu kuliko watumishi wengine.Halafu madai sio realistic,mshahara wa 3 million??!!!Watu wanataabika na pengine kufa wao wakishuhudia lkn wakiendelea na mgomo.Halafu hiyo Dr Ulimboka anaenda na rafiki yake kwenye issue kubwa kama hiyo tena inayohusu nchi nzima!Kwani hiyo kamati ya madaktari ni ULIMBOKA NA RAFIKI YAKE TU?Huyu
ni corrupt na hafai maana inaonekana anaweza kununuliwa na kuwasaliti wenzake.Hiyo kuitwa ili WAKAYAMALIZR yeye alijua anaitiwa dili ili akatengeneze pesa.Badala yake ndio yamempata hayo.Sishabikii itekaji na unyanyasaji aliofanyiwa Dr Ulimboka,lakini SI MTU MAKINI.

Kwenye red: Watu 6 wameficha zaidi ya Tsh 300 bn huko Uswiss, EPA, Meremeta, Deep Green, Kiwira, Misamaha ya kodi. Yote hiyo ingetosha kabisa kulipa sio tu 3 mil ila 6 million pamoja na kufanya mambo mengine. Serikali inaacha wezi wajichotee wanavyotaka huku inalalamika haiwezi kulipa madaktari!

Umaskini/ukata wa serikali ni wakati walala hoi wanadai haki zao, lakini ikija luxurious lifestyle wakubwa wana uwezo wa kununua magari ya Tsh 5 trillion! (aprox 30% ya bajeti), na kutenga Ths 3 ni kwa ajili ya mawaziri 55!
 
THE PHYSICIAN'S OATH

  • I solemnly pledge myself to consecrate my life to the service of humanity;
  • I will give to my teachers the respect and gratitude which is their due;
  • I will practice my profession with conscience and dignity;
  • The health of my patient will be my first consideration;
  • I will respect the secrets which are confided in me;
  • I will maintain by all the means in my power, the honour and the noble traditions of the medical profession;
  • My colleagues will be my brothers and sisters;
  • I will not permit considerations of religion, nationality, race, gender, politics, socioeconomic standing, or sexual orientation to intervene between my duty and my patient;
  • I will maintain the utmost respect for human life; even under threat, I will not use my medical knowledge contrary to the laws of humanity;
  • I make these promises solemnly, freely and upon my honour.
  • JIBU LAKO LIPO KWENYE BULLET ILIYOBOLD KWA WEKUNDU.
Jibu lako lipo kwenye bullet ilyobold kwa wekundu!
 
Ni bahati mbaya nimekuwa busy sijaweza kuchangia wala kupitia maoni ya wachangiaji wengine na pia kutokana na ujinga unaoendelea kujitokeza jukwaani kuona wenye mawazo tofauti kuwa wametumwa na nape nk naomba nisichangie....ila nakumbuka jumamosi iliyopita nilimuuliza mchangiaji mmoja kuwa just imagine unasafiri then yanakukuta ya kukukuta njiani halafu mgomo unaoushabikia unaendelea...fumba macho then uone hiyo picha..

At the end tulikubaliana kutokuelewana... Nachotaka kusema hapa ni kuwa bila kujali ulimboka kafanya/kafanywa nini pengine na nani bali yuko kama tunavyomuona kwenye picha...(mimi si mmojawapo wa wanaoshabikia mabaya) lakini bila huduma za madaktari (pamoja na ukweli kuwa yeye ni daktari) asilimia za kumkosa ni kubwa...je ni wangapi kuanzia kule Kintinku, Misenyi, Nguruka, Lituhi, Namanyere, Karumeli, Mbambabay Nyachabakeni, Muhoro, nk nk wanaopatwa na masahibu kama haya na wanaathirika na mgomo alouasisi yeye na hatimaye kufa kwa kukosa huduma?

Hivi maisha ya mtu yana mbadala?? serekali wanayoigomea inaathirika vipi na hili? yanini tunamalizana wenyewe kwa kudhani kuna tunayemkomoa serekalini? ...acha niwe kilaza katika hili ila bado sielewi madaktari na wanaowaunga mkono... wangetenganisha madai ya mshahara na madai ya mazingira bora ya kufanyia kazi wangeeleweka vizuri sana na tungewaunga mkono saana tu...lakini madai ya mshahara wa millioni 3 kufichwa ndani ya madai ya kuboresha huduma ...nitakuwa wa mwisho kuelewa...

Hakuna aliyelazimishwa kuwa daktari ila ukeshakuwa daktari una kiapo cha kutumikia wagonjwa...leo mzima kesho nani anajua UTAKUWA KAMA ULIMBOKA?? Alijua kuwa atakutana na alokutana nayo? Hasha...sitaki na wala sitaingika kwenye mjadala wa ama ameshughulikiwa na serekali, amefumaniwa amepata ajali...what ever the case lakini wapo watanzania wangapi ambao hawajiwezi (kama yeye) na sasa wanavuta pumzi za mwisho bila msaada kutokana na mgomo alouasisi?

Mbona wenzie hawakugoma kwake?? wamelipwa millioni 3? Nakaribisha matusi kama ilivyo kawaida ya JF nowadays ....kwamba lazima tuwaze yanayofanana.

kwa upande mkubwa nakuunga mkono kwa point 2. kwanza wana JF wao wanataka mawazo yote yaendane na kuichafua Serikali ama CCM.
Pili ni kwamba, pengine vifo na mahangaiko ya watu walioadhirika na mgomo aliouasisis unamgeukia!

Cha msingi tusikimbilie ku conclude kwamba serikali ndio imefanya hivyo, Uwezekano ni pamoja na
1. ndugu wa mmojawapo wa aliyefariki kwa adhari ya mgomo kafanya hivyo kwa hasira
2. Watendaji walionyanganywa kitumbua chao wakaamua kufanya hivyo kwa hasira
3. Serikali ikaona usalama wa taifa unayumba kwa sababu ya msimamo wao naye kama kiongozi.
4. wanasiasa wanataka umaarufu au kuichafua seriakli kwa kutumia loop hio
5. sababu za kijamii ikiwemo madai, mapenzi, chuki etc
6. sababu tofauti na hayo

kumbuka Ulimboka ni Dr ambaye hata hatibu ila ndio kakomaa na wakati serikali inaona uwezekano ni hakuna kwani hata walimu wanahitaji chaki, madawati na kahawa kurekebisha mazingira ya kazi, nao pia wanahitahi 3M na malupulupu so 9M hapo ameanza tu kazi, je Dr bingwa inakuwaje, like-wise police, makarani, mahakimu, na wafanyakazi wote wanahitaji hata laki4 tu. why so special wakati uspecial walishapewa?

ndugu, tusikimbilie ushabiki wa kisiasa, chuki na kuharibu amani zaidi
 
kwa upande mkubwa nakuunga mkono kwa point 2. kwanza wana JF wao wanataka mawazo yote yaendane na kuichafua Serikali ama CCM.
Pili ni kwamba, pengine vifo na mahangaiko ya watu walioadhirika na mgomo aliouasisis unamgeukia!

Cha msingi tusikimbilie ku conclude kwamba serikali ndio imefanya hivyo, Uwezekano ni pamoja na
1. ndugu wa mmojawapo wa aliyefariki kwa adhari ya mgomo kafanya hivyo kwa hasira
2. Watendaji walionyanganywa kitumbua chao wakaamua kufanya hivyo kwa hasira
3. Serikali ikaona usalama wa taifa unayumba kwa sababu ya msimamo wao naye kama kiongozi.
4. wanasiasa wanataka umaarufu au kuichafua seriakli kwa kutumia loop hio
5. sababu za kijamii ikiwemo madai, mapenzi, chuki etc
6. sababu tofauti na hayo

kumbuka Ulimboka ni Dr ambaye hata hatibu ila ndio kakomaa na wakati serikali inaona uwezekano ni hakuna kwani hata walimu wanahitaji chaki, madawati na kahawa kurekebisha mazingira ya kazi, nao pia wanahitahi 3M na malupulupu so 9M hapo ameanza tu kazi, je Dr bingwa inakuwaje, like-wise police, makarani, mahakimu, na wafanyakazi wote wanahitaji hata laki4 tu. why so special wakati uspecial walishapewa?

ndugu, tusikimbilie ushabiki wa kisiasa, chuki na kuharibu amani zaidi
wewe ni ******
 
Kwenye red: Watu 6 wameficha zaidi ya Tsh 300 bn huko Uswiss, EPA, Meremeta, Deep Green, Kiwira, Misamaha ya kodi. Yote hiyo ingetosha kabisa kulipa sio tu 3 mil ila 6 million pamoja na kufanya mambo mengine. Serikali inaacha wezi wajichotee wanavyotaka huku inalalamika haiwezi kulipa madaktari!

Umaskini/ukata wa serikali ni wakati walala hoi wanadai haki zao, lakini ikija luxurious lifestyle wakubwa wana uwezo wa kununua magari ya Tsh 5 trillion! (aprox 30% ya bajeti), na kutenga Ths 3 ni kwa ajili ya mawaziri 55!

Tatizo hujanielewa,NCHI HII SIYO MADAKTARI TU,KUNA WATUMISHI KIBAO NA WOTE NI MUHIMU KILA MTU KWA NAFASI YAKE.NA KILA MTUMISHI AKIGOMA ANA ATHARI ZAKE KWA WANANCHI.Tatizo hii kauli ya kusema HAKUNA ALIYE MUHIMU KAMA DAKTARI NI ya kijinga.Pia kumbuka mafisadi kufocha fedha nje ya nchi hakuwezi kuhalalisha madai ya milioni 3na zaidi kwa daktari.Wanataka kugeuza fani ya udaktari kama sehemu ya kupatia utajiri?MIMI PIA NIKO NAO IDARA MOJA,nahitaji maslahi mazuri mazingira bora ya kazi lakini tudai huku tukiangalia na idara zingine na pia TUTUMIE APPROACH YA KUIBANA SERIKALI AMBAYO HAITAKUWA NA MADHALA KWA WANANCHI KAMA ILIVYO SASA.Hapo hatuibani serikali badala yake tunaumiza wananchi.WANANCHI WANAHUSIKA VIPI NA MADAI YETU MPAKA TUWAADHIBU KWA KUWANYIMA HUDUMA NA PIA KUWASABABISHIA VIFO??
 
Inaelekea wewe ni mtoto wa fisadi ulisomea nje............. Wenzako kunji tulishazoea toka enzi zile!!

Mr Z, Umenisoma vibaya na Hilo ndio Tatizo la washiriki wengi hapa JF hawawezi/hawajui kukaa na kubaki ndani ya Mada inayojadiliwa. Hawakawii kupandisha Jazba na kuugeuza mjadala kuwa wa Mafisadi, Posho za Wabunge nk. Naomba tubaki kwenye mada tuwe wa kweli kwa fikira za kibinadamu kwa uwezo wa Akili tulizopewa. (Kwanza mm si mtoto wa Fisadi, nimesoma nje na pia nimeishi nje kwa muda mzuri tu).
Nikupe mfano jirani na Nyumba yako pana Duka Mmezoeana vizuri na mwenye duka pamja na ujirani mmekuwa marafiki. siku moja akakuomba umsaidie pesa aongeze Mtaji wake, ukampa bila kusita bila kuandikiana nae na wala hukumwuliza Atarudisha lini! Muda ukapita hukumuulizi mnacheka na kutabasamu. siku moja ghafla akakuita akarudishaile pesa kama alivyoazima. Urafiki ukashamiri baada ya miezi kadhaa Rafiki yako akawa anauza gari lake ukapenda ulinunue, alipokupa bei ukaona pesa uliyonayo imepungua kidogo, ukamwomba achukue hizo na iliyobaki ummalizie bada ya wiki tatu hivi. yeye akasema hapana bila kufika bei yake haachii gari. Ukambembeleza sana jamaa haelewi. Ukamtuma mama watoto wako aende kwa shogake, mke wa rafiki yako ajaribu kumsomesha ili amsomeshe Mumewe likafanyika na haikusaidia. mkaenda wewe na mkeo mkamuomba jamaa achukue hiyo pesa na abaki na gari mpaka mtakapommalizia, pia akakataa.
Rafiki uliemsaidia leo amekudhalilisha na kukufedhehesha, Utajisikia vipi? Baada ya siku mbili za matokeo hayo ukisikia hilo gari limeibiwa au limepata Ajali, utaenda kumpa pole? Isitoshe anaweza akadai kuwa wewe Umefanya njama ili hayo yatokee (au Umemloga). Sasa kwa Madaktari ni zaidi ya hayo hawa Ndugu zetu wamechukua Dhamana ya Roho/Maisha ya wananchi wenzao kujaribu kuwaokoa wanapofikwa na Maradhi. Mwanao na Apate Tatizo la kuhitaji Tabibu saa mgomo unaendelea ufuke nae Muhimbili, Bugando, Bombo, Mt Meru au popote wewe ulipo, ukose huduma kwa sababu wataalam wamegoma MTOTO ANAKUFIA MIKONONI!! Nani atakuwa Mpumbavu hapo? WEWE uliyemfikisha mtoto hospitali kwa wakati? MADAKTARI waliogoma kutekeleza wajibu wao? au SEREKALI iliyoahidi kutekeleza madai yao kwa awamu?
 
Mimi hata sielewi wapi hapaeleweki. Ni wazi hatuupendi mgomo wa madaktari kwa sababu unatuumiza lakini pia hatupendi namna serikali inavyolichukulia suala zima la mgomo na madai ya madaktari. Malumbano ya mafahari hawa wawili yanatuumiza sie wagonjwa, yanapoteza maisha ya wapendwa wetu kila kukicha. Inatufaidia nini basi tukikesha na kupiga kelele hapa JF. Kelele ambazo hazizuii vifo na mateso ya wapendwa wetu mahospitalini? TUINGIE MITAANI TUDAI HAKI ZETU. HAKI YETU YA KUPATA HUDUMA YA AFYA. Sisi tukiingia mtaani na kuidai kwa vitendo haki hii, hawa mafahari wawili watajua watakavyomalizana wenyewe lakini watupe haki zetu maana sie malumbano yao hayatuhusu kwa sababu wakati wanapeana mikataba ya kazi sie hatukuwepo kwa nini wanihusishe kwenye kuammend mikataba hiyo? Tena wanaiammend on the expense of our sisters, brothers, mothers, fathers, sons and daughters' lives!

Pole Dr. Ulimboka.
 
Tatizo hujanielewa,NCHI HII SIYO MADAKTARI TU,KUNA WATUMISHI KIBAO NA WOTE NI MUHIMU KILA MTU KWA NAFASI YAKE.NA KILA MTUMISHI AKIGOMA ANA ATHARI ZAKE KWA WANANCHI.Tatizo hii kauli ya kusema HAKUNA ALIYE MUHIMU KAMA DAKTARI NI ya kijinga.Pia kumbuka mafisadi kufocha fedha nje ya nchi hakuwezi kuhalalisha madai ya milioni 3na zaidi kwa daktari.Wanataka kugeuza fani ya udaktari kama sehemu ya kupatia utajiri?MIMI PIA NIKO NAO IDARA MOJA,nahitaji maslahi mazuri mazingira bora ya kazi lakini tudai huku tukiangalia na idara zingine na pia TUTUMIE APPROACH YA KUIBANA SERIKALI AMBAYO HAITAKUWA NA MADHALA KWA WANANCHI KAMA ILIVYO SASA.Hapo hatuibani serikali badala yake tunaumiza wananchi.WANANCHI WANAHUSIKA VIPI NA MADAI YETU MPAKA TUWAADHIBU KWA KUWANYIMA HUDUMA NA PIA KUWASABABISHIA VIFO??

Sasa ungetanabaisha kuwa madaktari watumie njia gani tofouti na hii yakugoma na wewe ni kibaraka wa magamba tu manake kama hii njia tu ambayo ina direct effect kwa raia serkali bado haiwaskilizi basi hata wafanye njia gani nyingine kamwe serikali yenu ya magamba haito waskiliza.
 
I am ready be in the front line in the battle against the current regime when time comes; I cannot withstand this.
 
Mr Z, Umenisoma vibaya na Hilo ndio Tatizo la washiriki wengi hapa JF hawawezi/hawajui kukaa na kubaki ndani ya Mada inayojadiliwa. Hawakawii kupandisha Jazba na kuugeuza mjadala kuwa wa Mafisadi, Posho za Wabunge nk. Naomba tubaki kwenye mada tuwe wa kweli kwa fikira za kibinadamu kwa uwezo wa Akili tulizopewa. (Kwanza mm si mtoto wa Fisadi, nimesoma nje na pia nimeishi nje kwa muda mzuri tu).
Nikupe mfano jirani na Nyumba yako pana Duka Mmezoeana vizuri na mwenye duka pamja na ujirani mmekuwa marafiki. siku moja akakuomba umsaidie pesa aongeze Mtaji wake, ukampa bila kusita bila kuandikiana nae na wala hukumwuliza Atarudisha lini! Muda ukapita hukumuulizi mnacheka na kutabasamu. siku moja ghafla akakuita akarudishaile pesa kama alivyoazima. Urafiki ukashamiri baada ya miezi kadhaa Rafiki yako akawa anauza gari lake ukapenda ulinunue, alipokupa bei ukaona pesa uliyonayo imepungua kidogo, ukamwomba achukue hizo na iliyobaki ummalizie bada ya wiki tatu hivi. yeye akasema hapana bila kufika bei yake haachii gari. Ukambembeleza sana jamaa haelewi. Ukamtuma mama watoto wako aende kwa shogake, mke wa rafiki yako ajaribu kumsomesha ili amsomeshe Mumewe likafanyika na haikusaidia. mkaenda wewe na mkeo mkamuomba jamaa achukue hiyo pesa na abaki na gari mpaka mtakapommalizia, pia akakataa.
Rafiki uliemsaidia leo amekudhalilisha na kukufedhehesha, Utajisikia vipi? Baada ya siku mbili za matokeo hayo ukisikia hilo gari limeibiwa au limepata Ajali, utaenda kumpa pole? Isitoshe anaweza akadai kuwa wewe Umefanya njama ili hayo yatokee (au Umemloga). Sasa kwa Madaktari ni zaidi ya hayo hawa Ndugu zetu wamechukua Dhamana ya Roho/Maisha ya wananchi wenzao kujaribu kuwaokoa wanapofikwa na Maradhi. Mwanao na Apate Tatizo la kuhitaji Tabibu saa mgomo unaendelea ufuke nae Muhimbili, Bugando, Bombo, Mt Meru au popote wewe ulipo, ukose huduma kwa sababu wataalam wamegoma MTOTO ANAKUFIA MIKONONI!! Nani atakuwa Mpumbavu hapo? WEWE uliyemfikisha mtoto hospitali kwa wakati? MADAKTARI waliogoma kutekeleza wajibu wao? au SEREKALI iliyoahidi kutekeleza madai yao kwa awamu?

serikali ndio inamakosa hapo kwani hata kipofu anaona na kwanini wasiwatekelezee madai yao?fedha ndio hazipo?wakati huo wao wanajilipa mishahara mikubwa na hawana elimu zaidi ya hao madaktari.
 
Leo hii serikali ya wauuaji sijui wataamka la lipi hospitali zote sasa ni complete tools down anguko kubwa la serikali ya Dhaifu Kikwete
 
Haiingii akilini kwa binaadam yeyote mwenye fikra japo kidogo, eti Serikali wakuchukuwe, wakupige, wakutupe Mabwepande halafu waje haki za binaadam kukuota.
haiwezi kukuingia hata puani maana wewe ni dhaifu kama unayemfanyia kazi,
 
wamempeleka MOI kumtibu.......... Tena kwa taarifa yako matibabu anayopewa hata rais wako hajawahi kupewa; under specialists care for 24hrs tumepeana shifts.

Sawa "dk" nimekusoma...Kwahiyo ninyi ni wabaguzi?? Hao mnaowarudisha kwenye machela wamewakosea nini?? Ndo wanaowanyima millioni tatu?? Tatizo lenu (if at all u are one of them) hamjui adui mnayepaswa kupambana nae na mbinu mnazopaswa kutumia....Haya mengine ni laana tu kwasababu malipo ni hapa hapa duniani.
 
THE PHYSICIAN'S OATH

  • I solemnly pledge myself to consecrate my life to the service of humanity;
  • I will give to my teachers the respect and gratitude which is their due;
  • I will practice my profession with conscience and dignity;
  • The health of my patient will be my first consideration;
  • I will respect the secrets which are confided in me;
  • I will maintain by all the means in my power, the honour and the noble traditions of the medical profession;
  • My colleagues will be my brothers and sisters;
  • I will not permit considerations of religion, nationality, race, gender, politics, socioeconomic standing, or sexual orientation to intervene between my duty and my patient;
  • I will maintain the utmost respect for human life; even under threat, I will not use my medical knowledge contrary to the laws of humanity;
  • I make these promises solemnly, freely and upon my honour.
  • JIBU LAKO LIPO KWENYE BULLET ILIYOBOLD KWA WEKUNDU.
Vipi hapo kwenye blue je??
 
Back
Top Bottom