Kipi Mungu anachoweza kukifanya kikanisaidia?

Kipi Mungu anachoweza kukifanya kikanisaidia?

Tukiachana na hadithi nzuri tunazosimuliwa kuhusu nguvu za Mungu, nahitaji kufahamu ni kipi anachoweza kunisaidia maana kila kitu nafanya peke yangu.

Naamka asubuhi naenda kupambana nikipata pesa namshukuru Mungu, kwanini Mungu asinipe pesa mimi nikae? Je, hawezi? Au hataki?

Kuna kipindi niliugua sana nikaomba Mungu sikupona mpaka nilipotibiwa na wahindi. Je wahindi wanamzidi Mungu akili?

Kama ameshindwa kunipa ninachokitaka nikiwa hai, je nikifa atanipa uzima alioahidi?

SWALI: JE, NI KIPI MUNGU ANAWEZA KUNISAIDIA KIKAONEKANA?
Kupambana kwako, kuponeshwa na Wahindi, ndio jinsi alivyokusaidia kupitia uwezo aliowajaalia nyie wote. Ukijisaidia, naye atakusaidia.
 
Mariam(Bikira Maria)alikuwa ni wakufanya ibada mpaka ikafika mahali baba yake mlezi akiingia chumbani kwa Mariam anakuta Mariam Yuko na matunda na vyakula tofauti tofauti.Akimuuliza anasema Mungu ndio mmbora wa kuruzuku.Kwa ushuhuda wangu binafsi,nimekaa miezi SITA na Shekhe Salim Mbarak(Mti mkavu),huyu ni babake yule Abdul Razaq(mume wake Diva wa kipindi Cha Malavidavi pale wafasi FM radio).Kwa muda wote huo nlokaa nae haletewi pesa na mtu na ni miaka kwa miaka ni hivo,ila pakiwa na shida anatia mkono mfukoni(mfuko wa kanzu)anatoa pesa.Hii imekuwa ajabu kwa watu wengi lkn pia Kuna shekhe mwingine kama hivo hivo miaka nane nyuma amefariki kwa uzee huko Handeni lkn nae ilikuwa akihitaji pesa anafunua mkeka wake anao kalia(mana mda mwingi Yuko kwenye huo mkeka kufanya ibada)na kuchukua pesa.Katika maongezi yake huyu Shekhe mkubwa baba mkwe wake Diva alisema kwamba Kuna kiwango Cha ibada na Darja zake ukifika....basi Mungu anakupa tamanio la nafsi Yako hata kabla hujaomba.Hii miujiza ipo na itaendelea kuwepo mpaka kiama kifike.Ishu ni kuwa tu watakao kuwa na Hali hiyo watapungua wingi wao lkn wataendelea kuwepo.Kwa hiyo HATA WEWE WAWEZA KUFIKIA KIWANGO CHA IMANI AMBAPO KILE UPENDACHO NI KISEMA TU IWE NA INAKUWA NI JUHUDI TU.Huko India na china na nchi nginyine za mashariki ya mbali......mtu anaweza kuwa hoiii afya mbayaaa,lkn aka kaaa meditation wiki au mwezi tu maradhi yote yakaisha.Kama ni ngumu kwako Si na kwa wengine.
unatupoteza sasa
kuna uchawi na miujiza. tofautisha
pia kuna hadith za kutunga
 
Mungu anaweza kukusaidia na binadamu anaweza kukusaidia. You must combine the two. Usimuombe Mungu pekee na usimwombe binadamu pekee.
Mungu akiridhia ndio binadamu anakuwa na mandate ya kukusaidia.
Kuna vitu Mungu hawezi kukusaidia?
 
Mkuu hv unadhan Mungu angekuwa na nguvu tunavyoaminishwa watu wangeteseka hv!!?? Ebu angalia vipofu, vilema, viziwi, mayatima, hata waliozaliwa na virusi vya HIV je unadhan wanafurahia maisha? Yani mtu maisha yke yote ya huzuni halafu useme nguvu za Mungu zipo!!, Nashangaa watu wanaosema ushukuru kwa uzima wakati Kuna watu wanasema bora wasingezaliwa.
NB:Mungu hana maajabu mpaka Sasa maana kuna watu wengi wasio kuwa na hatia wanateseka, Au labda tuseme tunamwabudu Mungu asiye sahihi
Hasaidii watu wakiwa na uhitaji, ndo maana nikauliza ni kwa jinsi gani anatenda kazi?
 
maombi yako ndo yamefanya ukapata kukutana na hao wahindi wako kama sio Mungu usingekutana nao
Au wewe ulikua unataka uponyaji wa from nowhere
Hakukuwa na haja ya kuzunguka mahospitalini na kuuza mifugo na yeye yupo
 
Tukiachana na hadithi nzuri tunazosimuliwa kuhusu nguvu za Mungu, nahitaji kufahamu ni kipi anachoweza kunisaidia maana kila kitu nafanya peke yangu.

Naamka asubuhi naenda kupambana nikipata pesa namshukuru Mungu, kwanini Mungu asinipe pesa mimi nikae? Je, hawezi? Au hataki?

Kuna kipindi niliugua sana nikaomba Mungu sikupona mpaka nilipotibiwa na wahindi. Je wahindi wanamzidi Mungu akili?

Kama ameshindwa kunipa ninachokitaka nikiwa hai, je nikifa atanipa uzima alioahidi?

SWALI: JE, NI KIPI MUNGU ANAWEZA KUNISAIDIA KIKAONEKANA?

Kum 8:17-18​

Hapo usiseme moyoni mwako, Nguvu zangu na uwezo wa mkono wangu ndio ulionipatia utajiri huo. Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.
 

Kum 8:17-18​

Hapo usiseme moyoni mwako, Nguvu zangu na uwezo wa mkono wangu ndio ulionipatia utajiri huo. Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.
Asante kwa mstari, je hawezi kunipa utajiri bila mimi kufanya kazi?

Maana nikifanya kazi nitapata utajiri regardless
 
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa Maarifa. Ignorance is the source of suffering. In short Mungu alisha tenda..Mungu hatendi tena. Mungu ametuumba completely,jukumu letu ni kumanifest. Lakini kwa upumbavu wetu tunataka tuombe kila siku instead tunatakiwa tu Kumshukuru Mungu kila siku.
 
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa Maarifa. Ignorance is the source of suffering. In short Mungu alisha tenda..Mungu hatendi tena. Mungu ametuumba completely,jukumu letu ni kumanifest. Lakini kwa upumbavu wetu tunataka tuombe kila siku instead tunatakiwa tu Kumshukuru Mungu kila siku.
Ndio nimepata hii habari leo kutoka kwa Robert Heriel

Kumbe kazi yetu ni kupanga na kuishi sio kuomba tena
 
Back
Top Bottom