Mtu kuwa CCM sio ndio kiumbe wa CCM!. Binadamu wote ni viumbe wa Mungu, hakuna kiumbe wa chama chochote!.
Wana CCM tuko wa aina nyingi, kuna washabiki, wafuasi, wanachama, makada, wakereketwa, wafurukutwa na siku hizi kuna machawa!, mimi ni CCM wa Nyerere type CCM sio baba yangu, sio mama yangu!.
Hiki ni kipindi cha kujadili issues za kisiasa, kiuchumi na kijamii, na kwenye issues za kijamii, kwa vile mimi ni wakili, pia nitaelimisha umma kuhusu katiba, sheria na haki, sasa hapa what has u CCM wangu got to do with this program?
View: https://youtu.be/VZlHxInJWfI?si=jpu7EpmZDAj6CBff
Composition
CCM ni mmoja tuu Rais Samia !.
- Rais Samia- CCM
- Prof. Lipumba -CUF
- Askofu Mwamakula - Dini
- Wallece Mayunga- ADC
- Ali Omar Juma - Chauma
- Juma Duni - ACT Wazalendo
- Abdul Nondo- ACT Wazalendo
Leo saa 3 usiku, angalia kipindi,
Manguli wa Siasa, Zitto Kabwe, Stephen Wasira, John Cheyo, Kuunguruma Kwenye Kipindi cha KMT cha Channel Ten, Kila Jumapili Saa 3:00 Usiku, Usikose!
Lineup ni hii
CCM ni mmoja tuu Mzee Stephen Wasira!, sasa huo u CCM wangu unaoupigia kelele ni upi?
- Mwenyekiti wa Chama cha DP, Mzee John Memosa Cheyo, " Mzee wa Mapesa",
- Mwanasiasa Mkongwe wa CCM toka enzi za Nyerere, Mzee Stephen Wasira,
- Mwanasiasa Kijana Machachari, na Kiongozi Mkuu, wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe
- Dorothy Semu wa ACT Wazalendo,
- Mrajis Azasi Zanzibar, Ahmed Khalid Abdullah,
- Profesa wa Siasa, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Bernadeta Killian
- Pascal Mayalla
P
Hizo ni mbinu za ccm kukwepa kuwa na Katiba ya wananchi mpaka hapo uchaguzi utakapowadia 2025 ili wawatumie tena maDED kusimamia uchaguzi!!
Elimu mnayosema mnawapa wananchi, wangapi wana television huko vijijini hata wapate hiyo elimu yenu?Hata hao wenye tv wangapi wa naangalia hiyo channel ya ccm?
Acheni hayo mazingaombwe ya kutaka kuihalalisha haramu!