Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi

Kisarawe: DC Petro Magoti ameutaka Msikiti unaotoa elimu ya dini kwa watoto 96, kuwarudisha walipowatoa sababu ya Mazingira Mabovu ya malazi

Watanzania wengi hatuko huru kwenye vichwa vyetu na mara nyingi sana fikra zetu zimefungwa either kwa ushabiki au kwa kuwa na uelewa mdogo.

Mohamed Said hapo juu amegusia jambo fulani nyeti sana ambalo watanzania wote kuna mahala tunapaswa kuwa serious nalo saana.

Shule za Serikali za msingi kawaida kwa kiasi kikubwa ndio zinazoandikiasha wanafunzi wengi sana wa kiislam na wengi sana ndio huhitimu shule hizi elimu ya msingi, kutokana na umasikini kwenye jamii kubwa ya waislamu, vijana hawa wengi huishia darasa la saba na kukosa uelekeo na hujikuta hawana namna zaidi ya kutafuta uelekeo kwenye mafundisho ya dini ambayo kwao hayana gharama zozote.

Tunapotaka kupambana na issue ya za kigaidi kwa kuamini wahusika ni vijana wa kiislam basi hatuna budi pia kuchimba mzizi wa tatizo, kama hawa vijana huachwa wakizagaa baada ya kuhitimu shule za msingi na wengi wao ndio hao waislamu hatuoni kama itakuwa rahisi kutegeka na kuingia kwenye makundi haya?
Watoto wa Kiislamu ni wengi kwenye baadhi ya mikoa kama Tanga, Pwani, na Zanzibar. Lakini kwa maeneo mengine mengi, wengi ni ama Wakristo au wapagani.

Shule ya Msingi niliyosoma kipindi chetu, katika darasa la wanafunzi 79, Waislamu wa kiume na kike walikuwa hawafiki 10.
 
Hii ni alarming kabisa, naipongeza serikal lakin jambo kama hili lisirudiwe kabisa
Huo ni utaratibu wa kawaida kabisa kwa wanafunzi wa dini wa Kiislam, labda tuseme waboreshewe mazingira ya kuishi.

Muelewe kuwa mpaka wazazi wao wameamua watoto zao wakafundishwe dini, hamfahamu ni mazingira yepi wanaishi walipotokea huko makwao. Utakuta wazazi ni duni, vishawishi vya kuwaingiza njia mbaya ni vingi ndiyo wazazi wakaamua wawapeleke wakaijuwe dini yao.

Hayo yapo miaka na miaka kwa Waislam.

Siyo huko tu, vyuo na misikiti mingi inapokea wanafunzi wa Qur'an namna hiyo.

Huyo Petro asilete mihemko yake, awasikilize kwa utuvu hao walimu, wanafunzi na wazazi wao, asikurupuke kwa sababu hawajuwi Waislam huyo.

Nashangaa hajasema "wanafundishwa ugaidi".
 
Kiongozi jenga utamaduni wa kushughulikia chanzo cha tatizo au chanzo cha uvunjifu wa sheria/utaratibu nk nani aliwaleta hapo hao watoto, kwa vibali gani..lengo ni nini? nk ili isije rudiwa tena na wale walioanzisha hili jambo wachukuliwe hatua wao binafsi. Sasa fungeni kituo, halafu baada ya muda wanakwenda kuanzisha jambo hilo hilo sehemu nyingine!
Kwani kituo kama kipo kisheria kinavunja sheria ipi?

Kinachotakiwa ifatwe sheria tu kama imekiukwa. Nyingine zote ni porojo tu.
 
Babuu,
Unajitia hofu isiyokuwa na sababu.
Waislam wamefanya makubwa katika nchi hii.

Soma historia yao.

Soma historia ya Mtwa Abdallah Mkwawa, Abushiri bin Salim, Hassan Omari Makunganya, Khadija Mkomanile, Abdulrauf Songea Mbano, Kleist Abdallah Sykes na mwanae Abdulwahid Abdallah Kleist, Hamza Mwapachu, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir, Sheikh Haidar Mwinyimvua kwa kuwataja wachache.

Soma historia za watu hawa utawajua Waislam na mafunzo yao na alama walizoacha.

View attachment 3039388
Kuna wa historia halafu kuna sasa yaani "the now" hawa wa sasa ni changamoto....
 
Taifa linahitaji fikra huru sana ili watanzania wote wawe/tuwe salama na tuishi kama WATANZANIA nje ya hizi dini zetu.

Watanzania wengi TUNAKUWA wanafiki sana linapofika suala la hizi dini zetu na hata kuuweka UTANZANIA wetu pembeni bila kujali athari dhidi ya watanzania wenzetu.

Elimu ya msingi katika shule za Serikali Ina hali mbaya sana na elimu hii ndio husomwa na watanzania wengi saana huku wachache wakipeleka watoto kwenye hizi International, matokeo yake ni Taifa kubaki na wapumbavu wengi ambao mwisho wa siku wanakuwa exposed kwenye mambo ya hatari kwao naa hata kwa usalama wa Taifa.

Tuboreshe elimu ya msingi na maisha ya watu kila mahala, usawa uwepo kila mahala kila wakati tuache double standards.
 
Mohamed Said & Faiza Foxy njooni mlisemee hili.

Toeni matusi yote, lakn kuna agenda ya siri ndani ya hii miskitini kwa kivuli cha imani ya dini.

Muda utaongea. Pwani, Tanga, DSm ipo siku itafahamika.

Ongezea Tabora, Dodoma , Lindi Mtwara , Arusha
 
Watoto kutoka Mtwara, Singida, Nairobi n.k wakutwa katika mazingira yasiyo rafiki ya malazi huku wakikosa elimu dunia msikitini Kiluvya wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani nchini Tanzania wakipatiwa mafunzo ya kidini.

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Petro Magoti akiwa na Kamati ya Ulinzi wamefanya ziara kwenye Msikiti huo ili kujionea mazingira ambayo watoto hao wanaishi. DC Magoti amesikitishwa na mazingira aliyoyakuta na kusema siyo salama kwa watoto hao ambao wengine walipaswa kuwa shule.

DC amemtaka Sheikh wa Msikiti huo kusitisha huduma hiyo mara moja na kuamuru watoto hao kurudishwa kwa wazazi wao mara moja kufikia Jumamosi.

Sheikh wa Msikiti huo akijitetea amesema kuwa wanawalea watoto hao kwakuwa Msikiti huo pia unafundisha Kuhifadhi Quran hivyo wamekuwa wakiondesha programu hiyo. Akijibu kuhusu wanakopata watoto hao amesema kuwa wanatoka mikoa mbalimbali nchini na wamekuwa wakiletwa na wazazi kwa baraka zao.

Kuhusu huduma ya chakula, sheikh huyo amesema kuwa wamekuwa wakipata ufadhili wa wazazi wa watoto hao ambao huchanga kwa ajili ya chakula.

Watoto wakihojiwa na DC Magoti wameonesha kuwa na baraka za wazazi wao, wengine wamedai wanasoma huko lakini wengi wao wakionesha kuishia darasa la saba na kujiunga na mafunzo hayo

DC Magoti amemtaka Sheikh huyo kufika kituo cha Polisi Kisarawe ili kuandikisha maelezo ya kina kuhusu kilichotokea na kujifunga kuwa anaondoa huduma hiyo.


Elimu ya mtoto wako unaiweka rehani kwa mtu usiyemjua? Halafu kesho kushinda kuandika jinsi mfumo kristu unavyowapendelea wakristu?
Nina hakika, huyo shekhe hana analolijua. Anawalea na kuwafundisha watoto ubabaishaji tu. If the parent does not want to hold the responsibilities of their own families, who else can bother or care?
 
Huyo mwinyi wako wengine wanaona hakuwa kiongozi mzuri na ndiye aliyeua uchumi wa Tanzania. Anyways, hilo siyo hoja hapa. Hoja ni kujua wanafundishwa nini basi. Halafu mengine ndiyo yafuate.
Auwe uchumi wa Tanzania uchumi wenyewe wa kuuza ulikuwepo!?..hata pesa ya kulipa mishahara hazina haukuwepo,watoto walikua wakifundishwa dini
Huyo mwinyi wako wengine wanaona hakuwa kiongozi mzuri na ndiye aliyeua uchumi wa Tanzania. Anyways, hilo siyo hoja hapa. Hoja ni kujua wanafundishwa nini basi. Halafu mengine ndiyo yafuate.
 
Sitafuti kuaminiwa nimechangia mada kuwa hizo madrasa zinazolea watoto zipo sio hiyo ya kisarawe tu huenda hiyo ikawa na idadi kubwa ya watoto tu, lakini hizo madrasa zipo sehemu nyingi tu tatizo ni usiri unaoendelea ndani ya hizo madrasa!

Habari za ugaidi umezileta wewe kumbe ndo kinachofundishwa?
Aliyekwambia kuna usiri ni nani? Nani alienda kuuliza kinachoendelea hakujibiwa? Wazazi hawana uwezo wa kupeleka watoto shule binafsi za sekondari mlitaka wafanye nini? Mtoto asijue dini yake kisa mzazi hana uwezo? Acheni chuki za kipumbavu nyie
 
Binafsi naungana na Mkuu wa wilaya. kituo kama hicho kinatakiwa kiwe kimetimiza matakwa yote ya sheria.

Waislam tunatakiwa tuwe Makhalifa na mfano bora kwa jamii, Waislam kama hao wanaoendesha hicho kituo ndiyo wanautukanisha Uislam.
 
Wanaweza kusafirishwa kimya kimya kupelekwa Somalia kwa njia za Majahazi usiku wa manane ili kwenda kupewa mafunzo ya Kigaidi halafu kurejeshwa kimya kimya.

Kana Yule wa Dodoma mberesero aliekamatwa Kenya chuo cha Garisa , Kwani imeshawahi kujulikana sligikaje pale kwenye uharifu mkubwa ule wa wasomali?
 
Watoto kutoka Mtwara, Singida, Nairobi n.k wakutwa katika mazingira yasiyo rafiki ya malazi huku wakikosa elimu dunia msikitini Kiluvya wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani nchini Tanzania wakipatiwa mafunzo ya kidini.

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Petro Magoti akiwa na Kamati ya Ulinzi wamefanya ziara kwenye Msikiti huo ili kujionea mazingira ambayo watoto hao wanaishi. DC Magoti amesikitishwa na mazingira aliyoyakuta na kusema siyo salama kwa watoto hao ambao wengine walipaswa kuwa shule.

DC amemtaka Sheikh wa Msikiti huo kusitisha huduma hiyo mara moja na kuamuru watoto hao kurudishwa kwa wazazi wao mara moja kufikia Jumamosi.

Sheikh wa Msikiti huo akijitetea amesema kuwa wanawalea watoto hao kwakuwa Msikiti huo pia unafundisha Kuhifadhi Quran hivyo wamekuwa wakiondesha programu hiyo. Akijibu kuhusu wanakopata watoto hao amesema kuwa wanatoka mikoa mbalimbali nchini na wamekuwa wakiletwa na wazazi kwa baraka zao.

Kuhusu huduma ya chakula, sheikh huyo amesema kuwa wamekuwa wakipata ufadhili wa wazazi wa watoto hao ambao huchanga kwa ajili ya chakula.

Watoto wakihojiwa na DC Magoti wameonesha kuwa na baraka za wazazi wao, wengine wamedai wanasoma huko lakini wengi wao wakionesha kuishia darasa la saba na kujiunga na mafunzo hayo

DC Magoti amemtaka Sheikh huyo kufika kituo cha Polisi Kisarawe ili kuandikisha maelezo ya kina kuhusu kilichotokea na kujifunga kuwa anaondoa huduma hiyo.

Shule za kawaida kusoma ni bure hadi form four, Kwanini hawasomi elimu ya kawaida?
Halafu mje kusema mfumo Kristo na blah blah ?
Pelekeni watoto Shule wasijekuwalaumu.
 
Ya Nigeria ni real example ya Boko Haram ilivyo anza ilianza hivi hivi,tatizo wao hawa kuyakemea na gundua mapema.

Kweli kiimani ni mkrisho,ila ukiniambia nichague amani ya nchi yangu na dini yangu,nitachagua amani ya nchi yangu,sababu kwenye amani hata ule utulivu wa kusali unaupata.

Sasa nikishaujua huo mchango wa dini yako,then .......... then inahusiana nini na hiki kikicho tokea Kisarawe.
Hatari ya kisarawe ni nini? Huyo mkuu wa wilaya angekuwa na akili asingeweka udini kama wewe, angetaka kujua mafundisho yanayotolewa ya athari gani kwa amani yetu basi,
 
DC Magoti amemtaka Sheikh huyo kufika kituo cha Polisi Kisarawe ili kuandikisha maelezo ya kina kuhusu kilichotokea na kujifunga kuwa anaondoa huduma hiyo.
Petro kuuzungumzia Msikiti!!!
😷😷
 
Mzee, ungetafuta kwanza ufafanuzi wa wa mafundisho wanayopewa humo msikitini kabla hujaamisha mjadala kwenda NECTA. Litakapotokea la kutokea utasema uislam hautufundishi hivyo. Sasa hivi kun jukumu la kujua mafundshilo hayo yanalenga nini na wanagungldishwa nini? Isije kuwa wanafundishwa vitu tofauti kwa mhongo wa elimu ya dini. Najua wewe ni msomi, Sasa wasomi hufanya utafiti kabla ya kuzungumza. Tafuta kwanza mafundisho yao Yana msingi gani.
Mbona DC hakulalamikia mafunzo? DC kasema mazingira ya kulala ndio tatizo na si elimu itolewayo hapo, au bando mzozo?
 
Hatari ya kisarawe ni nini? Huyo mkuu wa wilaya angekuwa na akili asingeweka udini kama wewe, angetaka kujua mafundisho yanayotolewa ya athari gani kwa amani yetu basi,
Kuna sehemu nimeongea udini? nimeongea according to reference nilicho kiona kupitia documentary ya Boko Haram,sababu road map yake ilianza kwa style kama hii ya Kisarawe au unazani Boko Haram iliibuka tu from no where?

Vp unajua content wanazofundishwa?
Vp silabasi wanayo itumia?
Walimu je wanauelewa na wanacho kifundisha kina impact gani kwenye makuzi ya akili ya mtoto?
Vp mzingira ni salama kwa makuzi ya mtoto?
Vp afya zao kimwili na kiakili?

DC anataka kujua zaidi na ndio maana kamwabia aende kituoni kwa maelezo zaidi,ili apaje majibu ya undani zaidi juu ya hayo maswali ya hapo juu.
 
Watoto kutoka Mtwara, Singida, Nairobi n.k wakutwa katika mazingira yasiyo rafiki ya malazi huku wakikosa elimu dunia msikitini Kiluvya wilaya ya Kisarawe mkoa wa Pwani nchini Tanzania wakipatiwa mafunzo ya kidini.

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Petro Magoti akiwa na Kamati ya Ulinzi wamefanya ziara kwenye Msikiti huo ili kujionea mazingira ambayo watoto hao wanaishi. DC Magoti amesikitishwa na mazingira aliyoyakuta na kusema siyo salama kwa watoto hao ambao wengine walipaswa kuwa shule.

DC amemtaka Sheikh wa Msikiti huo kusitisha huduma hiyo mara moja na kuamuru watoto hao kurudishwa kwa wazazi wao mara moja kufikia Jumamosi.

Sheikh wa Msikiti huo akijitetea amesema kuwa wanawalea watoto hao kwakuwa Msikiti huo pia unafundisha Kuhifadhi Quran hivyo wamekuwa wakiondesha programu hiyo. Akijibu kuhusu wanakopata watoto hao amesema kuwa wanatoka mikoa mbalimbali nchini na wamekuwa wakiletwa na wazazi kwa baraka zao.

Kuhusu huduma ya chakula, sheikh huyo amesema kuwa wamekuwa wakipata ufadhili wa wazazi wa watoto hao ambao huchanga kwa ajili ya chakula.

Watoto wakihojiwa na DC Magoti wameonesha kuwa na baraka za wazazi wao, wengine wamedai wanasoma huko lakini wengi wao wakionesha kuishia darasa la saba na kujiunga na mafunzo hayo

DC Magoti amemtaka Sheikh huyo kufika kituo cha Polisi Kisarawe ili kuandikisha maelezo ya kina kuhusu kilichotokea na kujifunga kuwa anaondoa huduma hiyo.

Hata kile cha ukerewe Huwa sielewi dhamira yake
 
Back
Top Bottom