Kisutu: Mwendokasi na bodaboda zagongana, wawili wafariki

Kisutu: Mwendokasi na bodaboda zagongana, wawili wafariki

INAHUZUNISHA, hata hao bodaboda hapo alikuwa kwenye utafutaji, ana watoto, na pengine alimbeba mtu asiye bodaboda (abiria) aliyekuwa na haraka sana kukimbilia kipato au interest fulani. hakujua kama anaenda kufa siku hiyo, hakuna ajuaye siku wala saa ndo maana tunatakiwa kukesha, tujiweke tayari kwa kutengeneza mambo yetu na Mungu ili tukifa tufe katika Bwana twende mbinguni na kama tukiishi basi tuishi hapahapa duniani tukiwa na Mungu.

UFUNUO 14: 13 INASEMA: Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, andika, heri wafu wafao katika Bwana tangu sana. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.

wengi wa wanaosoma hata huu ujumbe hapa, aidha mtaishi au mtakufa muda wowote, leo, kesho, mwakani, au siku msiyoijua, siombei mfe, ila ukweli mchungu ndio huo, cha muhimu ni kwamba mkiishi, andaeni maisha yenu ili muishi na Mungu, ama la mkifa basi muwe mmekufa mkiwa mikononi mwa Mungu (mkiwa mmeokoka) ili mwenda mbinguni badala ya kuzimu. mwenye dhambi akifa anaenda motoni, kwasababu alishupaza shingo yake kwa mahubiri kama hayahaya ya kawaida tu haya, akagoma kuokoka. kwa sasaivi dunia yote labda kasoro North Korea tu ambako hata internet haipo, watu wachache sana hawaelewi kitu kinachoitwa "KUOKOKA" hapa Tanzania ukitaja kuokoka tu mtu anaelewa nini anatakiwa kufanya, ila anafanya shingo yake kuwa ngumu, na anakufa na dhambi zake, na anaenda motoni.

msidanganyike na mapadre na viongozi wengine wa dini wanaowadanganya na kuwaweka mateka kwamba mkifa wao watawaombea maiti zenu na mtasamehewa dhambi hukuhuko maitini. mstari nimeweka hapo juu unasema ukifa matendo yako yatafuatana nawe. utaenda na matendo yako. nafasi ya kutubu ni hii ukiwa mzima, tubo acha dhambi, okoka kwa lugha nyingine yaani, ishi, ili ukifa ufe katika Bwana, ukiishi uishi katika Bwana.

haya sasa, unajua utaishi hadi lini? kama upo kazini, utasafiri hadi kufika nyumbani bila kugongwa na gari? nani anakulinda? huyuhuyo unayemkataa? anayekuelekeza uokoke lakini unashupaza shingo yako? wengine wanakufa kwa kupiga chafya tu baada yakunywa maji. Michael jackson aliweka hadi watu watakaojitolea viongo akipata shida ili aishi miaka mingi ila alikufa kama panya tu. Nakushauri okoka. OMBA SALA HII PAMOJA NA MIMI ILI UOKOKE.

sema: BWANA YESU, MIMI NI MWENYE DHAMBI, NAAMINI YESU KRISTO ALIKUFA KUWA KAFARA LA WOKOVU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE (ZITAJE KAMA UNAZIJUA), NAOMBA UNISAMEHE, KUANZIA SASA NIWE MALI YAKO, KWA JINA LA YESU KRISTO NINAOMBA, AMEN.

kirahisi tu hivi, kama utakuwa umeomba sala hiyo kwa kumaanisha moyoni, umeshaokoka, Mungu amekusamehe, sasa ili uukulie wokovu, jiunge na wale wanaoamini wokovu kama wewe. simaanishi hao wauza mafuta au maji au keki, namaanisha walokole wa kweli. kuolokoka/kuokoka ni lazima ili umwone Mungu wala usione aibu kuamua au kuonekana umeokoka. Mungu akusaidie.
Amen, amen!
shalom!
 
Bodaboda unampa masharti? Labda kama un ampa na mzigo mwengine ila si hawa "maafisa usafirishaji wa UVCCM"
Mzigo mwingine upi ww bibie?.funguka..nikipanda boda yyt namwambia sitaki anikimbize hilo ni la kwanza kabisa kabla sijapanda..mm ndo natoa nauli...shida nyie mkipandishwa mnaona raha anavyochomekea mbele ya magari na vigauni vyenu vinapepea..
 
Vizuri sana,,, hiyo nayo huwa inasaidia na unatakiwa kumwambia mi sina haraka

Hlf madam Kalpana hivi ujasiri wa kuchati juu ya boda nyie wadada huwa mnautoa wapi?
Nilisahau kugusia hili..yani ukipanda boda weka simu ndani ya mkoba au kipima joto chako..bana kwapani na ww uwe dereva wa pili kuangalia hatari yyt ili uweze kumshtua..maana ukute yuko anaendesha ila mawazo hayako hapo..
Mm sichati naogopa kuangusha simu yangu na siwezi kuona hatari mbele..ila naona kama wanaume wamezidi Bey...
 
Mzigo mwingine upi ww bibie?.funguka..nikipanda boda yyt namwambia sitaki anikimbize hilo ni la kwanza kabisa kabla sijapanda..mm ndo natoa nauli...shida nyie mkipandishwa mnaona raha anavyochomekea mbele ya magari na vigauni vyenu vinapepea..
Unamzuia kukatisha katikati ya magari?
Unamzuia kupita with red lights ?
Unamzuia kuchomekea na kupita service road ambazo hujui nini kitatokea?
 
Unamzuia kukatisha katikati ya magari?
Unamzuia kupita with red lights ?
Unamzuia kuchomekea na kupita service road ambazo hujui nini kitatokea?
zamani nilikuwa nawachukia sana boda, nilikuwa nikiendesha gari nawazuia wasinibugudhi, nilikuwa nawaona ni kadhia. siku nilienda mkoa usio nyumbani kwangu, nikalazimika kupanda boda, inikimbize sehemu moja ya muhimu mno, ilikuwa lazima nikimbizwe. hapo ndio niliona umuhimu wao. siku hizi hata nikiona anataka kunichomekea namwacha tu apite, kwasababu sijui yule aliyepakizwa anakimbizwa wapi,wengine wanaenda hospitali, wengine wanaenda kuokoa maisha ya watu, wengine wanaenda airport, wengine wanaenda sehemu muhimu mno. yafaa tuishi kwa kuvumiliana, na Mungu anataka hivyo.
 
Unamzuia kukatisha katikati ya magari?
Unamzuia kupita with red lights ?
Unamzuia kuchomekea na kupita service road ambazo hujui nini kitatokea?
Mbona unaona kama ni ngumu? Kuna boda wastaarabu au ww unakutana na boda mcharuko hakusikilizi? Kuna boda hizo njia hawazipiti na wanaangalia na mteja..kama uko hoya hoya utapitishwa mpka kwny reli..
 
Mbona unaona kama ni ngumu? Kuna boda wastaarabu au ww unakutana na boda mcharuko hakusikilizi? Kuna boda hizo njia hawazipiti na wanaangalia na mteja..kama uko hoya hoya utapitishwa mpka kwny reli..
hivi mtu akiwa anaenda airport, foleni imesimama, zimebaki dakika chache tu checking in ifungwe, hautamwambia boda apite izo njia mnazoona sio halali yao? umepigiwa simu nyumbani mtoto kaungua moto, au kapata shida ambayo unatakiwa kufika haraka mno, una gari, ila kuna foleni haitembei kabisa, hautapita izo njia uwahi kwenda kwa mtoto wako? tuwavumilie hawa boda hata kama wanavunja sheria. wengine wanakuwa na sababu za msingi.
 
zamani nilikuwa nawachukia sana boda, nilikuwa nikiendesha gari nawazuia wasinibugudhi, nilikuwa nawaona ni kadhia. siku nilienda mkoa usio nyumbani kwangu, nikalazimika kupanda boda, inikimbize sehemu moja ya muhimu mno, ilikuwa lazima nikimbizwe. hapo ndio niliona umuhimu wao. siku hizi hata nikiona anataka kunichomekea namwacha tu apite, kwasababu sijui yule aliyepakizwa anakimbizwa wapi,wengine wanaenda hospitali, wengine wanaenda kuokoa maisha ya watu, wengine wanaenda airport, wengine wanaenda sehemu muhimu mno. yafaa tuishi kwa kuvumiliana, na Mungu anataka hivyo.
Wangefuata utaratibu kusingekuwa na foleni.
Kila mtu akiwa na haraka ndio foleni inaanza.
Kila mtu akiwa na kimgora wasio nachoi wanakesha barabarani.
Ukiwa na haraka wahi kabla ya muda.
 
hivi mtu akiwa anaenda airport, foleni imesimama, zimebaki dakika chache tu checking in ifungwe, hautamwambia boda apite izo njia mnazoona sio halali yao? umepigiwa simu nyumbani mtoto kaungua moto, au kapata shida ambayo unatakiwa kufika haraka mno, una gari, ila kuna foleni haitembei kabisa, hautapita izo njia uwahi kwenda kwa mtoto wako? tuwavumilie hawa boda hata kama wanavunja sheria. wengine wanakuwa na sababu za msingi.
Kwanini uchelewe airport, huo ni uzembe uliopitiliza na ndio unaopingwa.
Time management and smartness inaanzia na unavyojipanga.
 
hivi mtu akiwa anaenda airport, foleni imesimama, zimebaki dakika chache tu checking in ifungwe, hautamwambia boda apite izo njia mnazoona sio halali yao? umepigiwa simu nyumbani mtoto kaungua moto, au kapata shida ambayo unatakiwa kufika haraka mno, una gari, ila kuna foleni haitembei kabisa, hautapita izo njia uwahi kwenda kwa mtoto wako? tuwavumilie hawa boda hata kama wanavunja sheria. wengine wanakuwa na sababu za msingi.
Bado tunarudi pale pale..ni ww unavyotaka ndivyo utakavyopata...sasa umeshasema unataka uwahishwe ndo hivyo sasa utawahishwa..ila kama unataka mwendo wa kistaarabu wahi mapema unakoenda nenda na muda ili uende kwa mwendo wa kistaarabu utakaomwelekeza..
 
Kubwa ni kujihadhari kupanda boda boda maeneo ya mjini kwenye purukushani nyingi

Pili ukitaka kupanda boda angalia wenye kujielewa kwa mwonekano tu waeza hisi huyu anajielewa,,,,we unamuona mtu kageuza kofia, kiduku kikubwa, mziki mkubwa hao watu ni hatar sana
Ikiwa unataka kupanda bodaboda chagua boda ambaye ni mtu mzima. Unajua ni kwa nini?

Mtu mzima tayari ana majukumu. Anajua kuna watu wanamtegemea. Ameoa ana familia na familia inamtegemea na bodaboda ndiyo kazi yake.

Hivyo wakiwa barabarani wanakuwa wapo makini zaidi kwa sababu anajua nikivunjika mguu miezi mitatu au minne familia yangu itaishi vipi? Watoto wanahitajika kwenda shule na nyumbani kila siku wale na mahitaji mengineyo muhimu. Wanakuwa makini sana.

Au ukimuona kijana ambaye anaendesha kiustaarabu kuna mawili. Mosi, alipata ajali na kunusurika. Pili, hiyo ndiyo kazi inayomwezesha aendesha familia. Hivyo tutarudi palepale kwenye majukumu.

Ila kwa hawa mayanki habari ni tofauti. Yeye anajiona yupo peke yake hivyo inamjengea kujiona yupo huru kwani hana hatia kuona kuna watu wanamtegemea. Umakini kwake unakuwa mdogo sana.
 
Back
Top Bottom