Kitu gani umewahi kuona ukaamini uchawi upo?

Kitu gani umewahi kuona ukaamini uchawi upo?

Ufahamu wetu mdogo katika masuala ya roho ni sawa na falsafa ya Astria ya shimo iliyoelezwa Wayunani wa kale.

Ulielezwa hivi; wapo watu ambao maisha yao yote waliishi shimoni kwenye giza. Na kila watu walipopita nje vivuli vyao vilionekana ndani nao wakaamini vivuli vile ndio watu halisi hadi mmoja wao alipotoka nje na kuuona mwanga wa jua.

Lakini aliporudi shimoni kutokana na mwanga wa jua uliompiga usoni hakuweza kuona vizuri. Ndipo wenzie walipomwambia “sasa unaona huko nje sio kuzuri kwani huwezi kuona tena”.

Huyu Bwana akaamua kutoka mle shimoni na kuishi nje kwenye mwanga wa jua na kuacha wenzie wakiendelea na maisha ya shimoni ya kuamini vivuli kuwa watu.

Ninajaribu kukufananisha wewe na watu waishio shimoni wanaodhani dini wanazoamini na kuabudu ndio za kweli na wasioamini dini zao ni wapotevu.
Huu ni upofu na ujinga ambao hata ukitwangwa kwenye kinu hauwezi kumtoka mtu!

Niliwahi kuandika kuwa ujio wa dini hizi za mashariki ya kati yani Uislamu na Ukristo ulitokana na mchakato mzima wa ukoloni mkongwe ambao hatunabudi kupingana nao kwa nguvu zote.

Upo usemi wa kale usemao;’’Mwafrika anaenda kanisani au msikitini na msaafu kwapani lakini hawezi kusahau hirizi kiunoni.’’ Huu ni uthibitisho kuwa dini pepe hazijafua dafu mbele ya dini au imani za Kiafrika zilizoitwa ushenzi na washenzi hasa.

Tuna shuhudia viongozi wetu wa kisiasa wakikesha katika nyumba za ibada lakini kamwe hawawezi kuacha kwenda kwa sangoma kutizama upepo wa uchunguzi ujao.

Hivyo basi kunilazimisha kuamini Yehova ni mungu wa kweli nikutonitendea haki kifikra.

Sote tunapapasa kama kipofu aliegusa sikio la tembo na alipoulizwa unamjua tembo? Akasema; “ndio, tembo anafanana na beseni kubwa la kuogeshea watoto”.

Karl Max, muumini wa sosholojia alibainisha,’’dini ni ulevi, umlevya mtu kama bangi.’’ Nimelishuhudia hili pale Manzese darajani jijini Dar-es-salaam ambapo watu wana shindana kutetea dini ngeni barani Afrika kiasi cha kutokwa mapovu mdomoni mithili ya mgonjwa wa kifafa!


Dini ngeni imetumika sehemu nyingi duniani kudhoofisha jamii mbalimbali kisiasa, kiuchumi na kimahusiano.

Mwandishi Chinua Achebe anasema; “mtu mweupe ni mjanja sana, tazama aliingia kwetu, nasi tukampokea; amedhoofisha watu, hatuwezi tena kutenda kwa umoja wetu kwani hata imani zetu zimedhoofishwa”.

Haya niyasemayo yametokea nchini Ghana hivi karibuni baada ya Ghana kuwa pagumu kuingilika kwa lengo la kupora rasilimali hasa madini.

Marekani na maswahiba wao wakaamua kuanzisha madhehebu ya kilokole kila kona huku injili kuu ikiwa ni; “msihangaikie mali ya dini kwani thawabu yenu iko mbinguni ambako Yesu alienda kuandaa makao”.

Leo asilimia 90 ya vyombo vya habari nchini Ghana vinamilikiwa na madhehebu ya kiroho yenye asili ya Marekani.

Hapa ndipo kampuni ya kimataifa ya uchimbaji madini ya Barik inayomilikiwa kwa asilimia kubwa ya hisa na familia ya Rais George Walker Bush ilipoanza kuchota dhahabu hadi sasa wamehakikisha nchi ya Ghana imebaki mahandaki (sasa mapango).
Sasa Barki imehamia Tanzania sambamba na ujio wa kila aina ya kanisa inayoponya “mapepo” kwa jina la Kristo.
Hapa ndipo tunapojiuliza Ukristo wa kweli ni upi? Huu wa sasa au ule wa kihafidhina?
Ni ushahidi upi wa kitafiti unaoonyesha imani zetu za kiafrika ni ushenzi kiasi cha waamini wa hizi dini kudharau asili yao?
Tafuta kitabu kinaitwa "The Secret"

Hakihusiani na dini yoyote ile, Ila kisome tu

Siku ukija kumaliza nishtue tujadili mawili matatu.
 
My brother!! Upo sahihi asilimia 100% and mybe nasema haya coz naamin in Astheism na pia nipo in Religion.

Kaka kuna vitu omba sana visikupate! Havielezeki kwa Philosophy wala Science, ni very complicated! Niamini mimi brother ikikutokea inakuvurugwa hard enough kiasi kwamba unashindwa hata kutoa Reference ya either utumie Dini ku define au Astheism!!
Hamna mtu amefanikiwa kisa uchawi...Kama unafanikiwa nenda na wewe uwe mchawi...acheni wivu wa maendeleo jamani
 
Yaani wewe unataka watu waamini tu kuna mungu au unataka waamini kuna mungu unaemwamini wewe? Elezea vizuri hapa, maana kuna majitu mengine yanaweza kukuambia yehova ndio mungu wengine wanaweza kukuambia allah ndio mungu wengine wanaweza kukuambia shinto ndio mungu wengine budha ndio ukweli, wengine yesu ndio mungu, sasa unataka watu waamini tu katika mungu au waamini katika mungu yupi ndio ujue kuwa uchawi haupo baada ya kujiunga nawewe.?
Samahani, unaishi DSM?
 
My brother!! Upo sahihi asilimia 100% and mybe nasema haya coz naamin in Astheism na pia nipo in Religion.

Kaka kuna vitu omba sana visikupate! Havielezeki kwa Philosophy wala Science, ni very complicated! Niamini mimi brother ikikutokea inakuvurugwa hard enough kiasi kwamba unashindwa hata kutoa Reference ya either utumie Dini ku define au Astheism!!
😂😂😂Ni Vitisho...if u don't understand kitu fuatilia usipopata jibu bac it's u don't know... tatizo watu washaweka conclusion if kitu hukielewi it's magic I don't think that way...ndo maana naishi huru..I don't have to know everything in the world na bado najifunza kitu..ila I refuse kuamini kitu out of ignorance n fear Tena without evidence ya kuaminika..eyes n ears can lie ndo maana hizi story tu ni za watu ila no verifiable evidence coz ni personal mental issues tu..najua watu hawapendi kuambiwa ila ndo hivyo
 
[emoji23][emoji23][emoji23]Ni Vitisho...if u don't understand kitu fuatilia usipopata jibu bac it's u don't know... tatizo watu washaweka conclusion if kitu hukielewi it's magic I don't think that way...ndo maana naishi huru..I don't have to know everything in the world na bado najifunza kitu..ila I refuse kuamini kitu out of ignorance n fear Tena without evidence ya kuaminika..eyes n ears can lie ndo maana hizi story tu ni za watu ila no verifiable evidence coz ni personal mental issues tu..najua watu hawapendi kuambiwa ila ndo hivyo
Ukisema unajifunza nakataa, wewe ulishajilimit kujifunza,, Vitisho vya watu vikuzuie wewe kujifunza jambo ? Mbona ni sababu ya kitoto sana

Kwa mtu mwenye utimamu wa akili anaependa kujua au kujifunza mambo tofauti, angejifunza kwanza ndio ajue anakubali au anakataa kuwa hilo jambo lipo..
Lakini atheist wengi huwa mnapinga tu yani hamna sababu ya kwanini mnapinga ila mnaamua tu kupinga kuwa Mungu hayupo..

Kama unazo sababu za msingi kabisa ambazo haziachi shaka yoyote kuwa kwanini unapinga kuwa Mungu yupo naomba utujibu hapa....Wenda tutajifunza jambo kutoka kwako
 
Dah! Uchawi upo jamani..!

2002 huko shule ya Bulyaga ya msingi, Wilaya ya Rungwe mkoani mbeya ilikuwa hivi ….
Nikiwa std five pale aisee nilisoma na jamaa anaitwa Baraka nani sijui jina la mwisho nimesahau, ilikuwa ikifika jumatano na ijumaa jamaa anateswa sana na mapepo sasa kuna siku ilikuwa ni kivumbii alikuwa yakiamsha siku hiyo anawatembezea kichapo balaaa alikuwa anakuwa na nguvu za ajabu yaani… baadae nilihama ile shule nkarud town sijui iliishiaje yule mwamba halafu alikuwaga na akili kinomaa yaan
Bulyaga kwa mwakwilusya si ndio
 
Back
Top Bottom