Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,743
- 25,564
Mwaka flani wageni walikuja nyumbani mtoto akamuomba mama ake simu acheze game mama yake akamwambi imezima chaji na hapakuwa na umeme toka asubuhi
Mama wa huyo mtoto akanambia mpe Basi simu yako acheze game maana ataanza sumbua hapa..nikamjibu haina ilioko ni ya kutumia akili sana sio game last kitoto ..mama yake akasema kuliko Alie we mpe ashindwe[emoji848]
Au mpe a download anajua kutafuta game zake...nikamjibu mwache Alie hii sio PS
πππππhaya banaDuh ataichomoaje? Angekula kofi moja ashangae
Yaani kama ulikafinya,hio safiiii mtoto mdg ahui hata maisha hio tv ajui hata bei yake...Nilienda kwa kaka yangu wa tumbo moja.
Nipo sebuleni naangalia TV, mtoto wa bro alitoka shule. Alipofika hata hakunisalimia.
Kakasimama katika ya TV, nikamwambia toka hapo, bado tu. Nikamwambia tena. Kakazima TV kakaingia chumbani.
Nikawasha, nikasubiri kanatoka chumban. Nikakashika, nikakapa kifinyo.
Usiku bro anakuja, kanamwambia. Nimempiga. Bro akasema, huyu akileta ujinga piga.
Wazazi wa sasa, jitahidini kuwalewa watoto wenu katika tabia njema ndiyo maana hata ndoa za siku hizi zinavunjika kwa sababu ya malezi.
Namshukuru sana mama yangu, ametulea katika maadili mema. Sisi nyumbani ukimkuta mgeni lazima umsalimie halafu unaenda kucheza nje. Mgeni aletewe hata soda halafu nawe unataka unywe naye kipigo utakachopata.
Kumbe wewe ni wa kike..!Nikiona Mtoto anaedeka au mtundu mtundu hua najitenga nae mbali maana najua sitakawia kumbonda. Nawachukia watoto watundu na mideko, Sikulelewa kimideko so napenda na watoto wengine wawe hivo.
Siku moja nilijisahau nikampa maji Mgeni nikiwa nimesimama baada ya hapo nilikula kichapo sana. Baada ya ya hapo mpaka leo hii na ndevu zangu kama nampa kitu mtu mzima lazima nifanye kama napiga goti moja. Kama ni baba nampa kitu lazima nipige magoti...mwili ushazoea wenyewe unajua nini ufanye nikimpa kitu mtu.
Hahaaa aiseeNilienda kutembelea ndugu jijini dar es salaam sasa katoto ka sister kakaja tukawa tunapakua msosi nilivyomaliza kukapakulia.nikajipakulia na mimi wacha kashtuke eti khee njomba unakula sana naenda kusema kwa mama[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Kuna ka aibu flani nilijiskia ila nikasema potelea mbali...Hahaaa aisee
Hapo likipigwa bomu linaua basi zima kwa mchanganyiko huo.Malezi ya kulea watoto kwapani siwafichi ndugu zangu ndio yanayosababisha kuwe na ongezeko kubwa sana la mashoga siku hizi,hizi tabia za kufumbia macho kila wanachofanya kina Junia ipo siku huko mbeleni tutakuja kujuta..Hii nimewachana jana tu kwenye basi wakati natoka Dodoma kwenda Dar kuna vitoto viwili vilikuwa na wazazi wao basi walikuwa hawatulii kelele wao,mara wapande juu ya siti gari ikiwa mwendo kasi,mara wavute nywele wakubwa halafu wazazi wao wanawaangalia tu nilikaa siti tatu kwa nyuma kutoka kwao si ndio mmoja akajitela bwana kujifanya kuja kwangu ananiuliza maswali kuhusu screen zile zilizopo kwenye siti za Shabiby nikawa namjibu fresh tu huku nikichukua tahadhari maana niligundua ni mtundu,eh!!! si akabonyeza ghafla kitufe kimojawapo cha cha screen nikamsukumia ghafla kuelekea uelekeo wa wazazi wao na mineno juu watu wakaniunga mkono "hawa watoto watundu kweli" hapo ndipo nikaanza kupiga madongo kuhusu malezi ya watoto wazazi wao wakisikia..Sema niligundua hata mzazi wake wa kike pia hana malezi mazuri maana mtu mwenye malezi mazuri hawezi kula hovyohovyo alikuwa na rundo la mivyakula mara miwa,zabibu,mayai,tambi,biscuti,juice,sambusa na vyote alikuwa anakula kwa wakati mmoja
ππππππ ila wee jamaa ππ»ππ»ππ»ππ»ππ»Huyu mtoto wa binamu yangu bwana nacheza cheza nae sii akaanza kunichapa ngumi kwenye de libolo. Sasa ilibidi nijikaze tuu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] acha ukauzu mkuuKwangu angekufa njaa huyu, au la mama ake ndo amtumie hizo hela za chips.
Mkuu we acha tu, kuna anti yangu mmoja ni kauzu kwelikweli kwa sisi wengine ila watoto wake anavyowalea ni kichefuchefuIla haya malezi ya sasa haki vile wengI wetu tutakuja kujibu mbele za Mungu.
Na wengi tunaojikosha hapa ukute ndo sisi sisi tunawalea akina junya huko nyumban sema tu ni vile hatujuani
Mungu aturehemu kiukweli
Hili swali lilinishangaza maana sijawahi kula kwenye huo mji.Sasa na weye unaendaga kula kwa watu ili iweje?
Hujui kama mafuta yamepanda bei?
Sometimes baadhi ya wazazi humtuma mtoto akaropoke maneno kwa mgeni ili ajiongeze maisha magumu mjini[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Amekua na tabia zile zile za ushakunaku. Kaanzia toka utotoni hizo tabia zake kichefu chefu humjui tu. Hata akiolewa sichangi.[emoji1787][emoji1787][emoji1787] mkuu msamehe mtoto