Kituko kingine Wizara ya Afya, Waziri abariki uteuzi wa AMO kuwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu

Kituko kingine Wizara ya Afya, Waziri abariki uteuzi wa AMO kuwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu

kama issue ni experience basi tuna ma DMO ambao ni MD MPH wenye experience kuliko yeye kwa nini wasipewe cheo hiko?punguzeni ujuaji.

Wamefanya nini kipya kwenye mikoa yao kila siku ni semina tu zakutengeneza hasa mwishoni mwa mwaka na mademu zao manesi baadhi ya maeneo hospital hazina hata syringe na fedha za makusanyo ya uchangiaji wa wananchi wanakula na wahasibu.
 
RMO ni cheo cha uongozi/ utawala sio cheo cha kitaaluma. RMO mara nyingi hatibu anashinda kwenye vikao vya kiutawala vya RAS au mahala pengine hupitisha likizo za watumishi.
Tatizo ni kuwa cadre ya madaktari kila mtu anajiona yeye binafsi ndiyo nshomile kuliko hata mwenzake. Daktari wa madawa ( internal medicine) hujiona bora kuliko wa upasuaji, wa meno bora kuliko wa magonjwa ya watoto mlolongo ni mrefu ili mradi kila mmoja hataki mwenzake aonekane anafaa.
Madaktari husoma udaktari kwa taabu na kwa muda mrefu lakini kama nafasi ya kukwepa kufanya udaktari wangependa sana kuukwepa wakaenda maofisini kupitisha likizo, kazi isiyohusiana kabisa na udaktari. Madaktari Bingwa wanakwepa kufanya kazi daktari Bingwa wanakimbilia kwenye tu NGOs ambako hata 1/8 ya utaalam wao hautumiki.
Ukiangalia kwa makini utaona uongozi halina uhusiano wa moja kwa moja na taluma. Kama ingalikuwa hivyo Profesa Mkandala wa chuo kikuu cha DSM angekuwa Rais, Dr. Lwaitama angelikuwa Waziri Mkuu, Prof. Lipumba angalikuwa waziri wa uchumi. Lakini mambo sio hivyo. Jemadari huchaguliwa vitani, madaktari waache kulalama wafanye kazi wataonekana na watateuliwa tu. Nafasi ya RMO katika mkoa ni moja tu hata wakigombania ni daktari mmoja tu atakayeteuliwa.
Katika mataifa mengine watawala katika sekta za Afya sio madaktari ni watawala, madaktari wako katika hospitali kushughulika na wagonjwa wao. Madaktari wa Tanzania hawapendi kukaa hospitalini wanawakimbia wagonjwa. Ukitaka ushahidi neda wizarani, utakuta madaktari vijana hawajatumikia fani ya udaktari hata mwaka mmoja wapo wizarani kufanya kazi za ukarani huku tuna acute shortage ya madaktari.
Ukifuatilia kwa makini atajiuliza " Hivi mtaala wa fani hii ya udaktari wanafundisha pia kulalamika? Utajiuliza swali hili kwa sababu wanatumia muda mwingi kulalamika kuliko kutibu. Katika hali ya kawaida watu wenye maneno mengi ya kuchunguza hiki au kile hawana kazi za kutosha, kinyume chake hawana muda kuchunguza nani kapata nini au kakosa nini.

Mkuu unaeleza kana kwamba it is an offense kwa daktari kuwa mtawala..lakini nikukumbushe pamoja na kazi za Administration jukumu la DMO na RMO ana kazi ya kitaaluma, Proffesional..nikupe mfano;mfano kazi za kusimamia hospitali kama mtaalamu (na sio kama mtawala), utokeaji wa magonjwa ya mlipuko, magonjwa hatari ya kutokwa damu.mf. Ebola n.k..kote kunahotaji expertise kama daktari na SIO kama mtawala!
 
Acha kudanganya watu kwa taarifa yako tofauti ni ndogo sana wote wanareason nimesoma co,amo na sasa ni MD sijawa ona vitabu mfano cha medicine davidson tofauti kuanzia co mpaka MD the same book suala hapa ni kujituma tu tunaona ma MD hapa wanachemka hata kuandika dose tu Doctor gani unareason watu wanakufa tunao hapa hata kumanage pph wanashindwa AMO wanapiga kazi ile mbaya maisha ya watanzania wengi yanaokolewa na AMO na CO.

Sasa, km ulikuwa na AMO tayari, na kitabu ni kile kile, ilikuwaje ukaenda kupoteza miaka 6 ili kuwa registered MD(MO)?

Km kigezo ni MD, apewe MD, si AMO, acheni ujanja ujanja.
 
mwalimu mkuu diploma..... mwalimu wa kawaida MASTERS this is how we do!

Haohao wenye degree na masters ndio wametufikisha hapa tulipo na elimu zao hazizalishi kitu mikoani hawataki kuja na ndio wengi viongozi huko wizarani hospitali hazina hata panadol siwabunifu acha na AMO tuwaone nao.
 
Sasa, km ulikuwa na AMO tayari, na kitabu ni kile kile, ilikuwaje ukaenda kupoteza miaka 6 ili kuwa registered MD(MO)?

Km kigezo ni MD, apewe MD, si AMO, acheni ujanja ujanja.

Mbona kwenye mahospitali ya wilaya kwenye wananchi wengi hatuwaoni kama sio kutaka vyeo tu na kutembea mikono mifukoni hamtaki kuwasaidia watu.
 
Acha kudanganya watu kwa taarifa yako tofauti ni ndogo sana wote wanareason nimesoma co,amo na sasa ni MD sijawa ona vitabu mfano cha medicine davidson tofauti kuanzia co mpaka MD the same book suala hapa ni kujituma tu tunaona ma MD hapa wanachemka hata kuandika dose tu Doctor gani unareason watu wanakufa tunao hapa hata kumanage pph wanashindwa AMO wanapiga kazi ile mbaya maisha ya watanzania wengi yanaokolewa na AMO na CO.

Kweli we ndo maana ulianzia u CO, u AMO!
Kwamba kwa vile kitabu ni hicho hicho i.e Davidson, na kinatumiwa na hadi Specialist, basi rank za elimu hazina tofauti kubwa!
Hukawii kusema kwa vile Das inatumiwa na MD na Surgeons wkt wa shule, basi MD ni equivalent na surgeon!
 
Ata mi na hivi viwango butu kielimu bado ninamatumaini ya kula post la ukweli ilimradi gamba libaki magogoni.
 
pumba tupu degree is equivalent to advanced diploma au we shida yako n nn?

Mkuu mambo hayako rahisi hivyo, (na kama yako hivyo siyo katika taaluma ya udaktari)..AMO pamoja na countless years he might have, akitaka kuwa DAKTARI (MD) bado atasoma tena miaka mitano, mkuu.!!
 
huyo ana experience, Advanced Diploma is equivalent to a Bachelor. acheni ujinga, inamaana watamteua mtu aliye na bachelor amemaliza chuo juzi kuwa RMO wamuache mtu mwenye 10 years working experience katika field hiyo? kwani elimu ni cheti pekee? wakuteue wewe ukaendeleze migomo ya kitoto watu waendelee kufa?

Hahaha..mkuu,
I wish ungejua AMO wanasoma nini na MD wanasoma nini!
Then ulete experience!!
Haijalishi amemaliza chuo leo au atamaliza chuo kesho..is eligibility ndiyo suala la msingi hapa!
 
Kanuni inamtaka mteule wa nafasi hyo ya mganga mkuu awe na digrii na vigezo vingne vya ziada ikiwa ni pamoja na uzoefu na kaz ya utabibu. Kama kigezo cha msing ingekuwa ni uzoefu basi kuna manesi wana miaka 30 kazini wangeteuliwa hao.
 
hiyo haijalishi, hata mlie vipi hamuwezi kupewa. wakati mwingine bora kuangalia maslahi ya taifa, kuliko kuwapa ninyi mnaojifanya wajuaji na kuacha watu wafe tu.

Hata tulie vipi hatupewi??..mkuu suala hapa si kulilia madaraka..you're really missing the point here! Kwani mikoa yenyewe iko mingapi hadi watu "walilie" hayo madaraka?!..Suala ni management in health system...I would understand kama MDs wangekuwa hakuna kiasi cha kwamba AMOs should take the place!!Not for governing sake but for health management's.
 
Kweli we ndo maana ulianzia u CO, u AMO!
Kwamba kwa vile kitabu ni hicho hicho i.e Davidson, na kinatumiwa na hadi Specialist, basi rank za elimu hazina tofauti kubwa!
Hukawii kusema kwa vile Das inatumiwa na MD na Surgeons wkt wa shule, basi MD ni equivalent na surgeon!

Hembu nipe tofauti ya AMO na MD Kiutendaji kwa hapa kwetu Tanzania acheni kutishatisha watu nasema sioni kipya na kutaja kitabu ni Mfano tu na hiyo Das kubwa sijui ndogo sijui bailey and love ni vitabu tu sijawahi kuona tofauti ya mgonjwa aliyetibiwa na MD na AMO wakapona tofauti,hembu nambie hao ma MD tangu timeanza kuwapa uongozi wa URMO mpaka DMO wamefanyanini kama sio uoza tu.
 
Nimeshatibiwa na MD hawajawahi kunishauri nifanye nini ili nisipate tena malaria. Leave that aside this, it is shocking kwa MDs kugombea nafasi ya kiutawala kama hiyo.

Why would a reasonable and a well qualified MD agree to be responsible and accountable to the RAS on a day to day basis on administrative and technical issues? Khaa!

Be directly responsible and accountable to your patients, not to the dam RAS.
pole sana kwa kukosa huduma hiyo ya ki-MD .Rudi kwenye suala la msingi.... Je walioweka vigezo vya kuwa RMO walikosea?anacholalamikia mleta thread ni ukiukwaji wa taratibu zilizopo!

Kuna post yangu nimeeleza wazi kuwa most of RMOs ni makada wa ccm
 
Hembu nipe tofauti ya AMO na MD Kiutendaji kwa hapa kwetu Tanzania acheni kutishatisha watu nasema sioni kipya na kutaja kitabu ni Mfano tu na hiyo Das kubwa sijui ndogo sijui bailey and love ni vitabu tu sijawahi kuona tofauti ya mgonjwa aliyetibiwa na MD na AMO wakapona tofauti,hembu nambie hao ma MD tangu timeanza kuwapa uongozi wa URMO mpaka DMO wamefanyanini kama sio uoza tu.
huwezi kuona hizo tofauti kama kila siku unatibiwa na AMO na anakuambia una malaria,uti na sti
 
AMO sio Daktari, ni Daktari msaidizi, na hicho cheo kipo Bongo tu, ila taaluma yao inayotambulika kimataifa ni ile ya U Clinical Officer.
Narudia tena, akitaka udaktari, anaenda kuanza MD 5 yrs, kisha Internship.
Hakuna Equivalency hapo. Na MD si Bachelor's degree tu, ni muunganiko wa Bachelor of Medicine&Bachelor of Surgery, kule Makerere huitwa MBChB, na huku huitwa Degree of Doctor of Medicine(MD).
Na vigezo vya uchaguzi wa RMO, vinasema awe MD(mwenye MPH na uzoefu wa UDMO miaka 7), na hawasemi MD au AMO au Nurse, ila ni MD tu. MPH yeyote aweza soma, ht wenye B. A. Ed wanafanya MPH!
Sasa iweje apewe AMO mwenye MPH na uzoefu, wkt kuna MD wenye MPH na uzoefu wa u DMO?
Vigezo na masharti lzm kuzingatiwa, msitetee uvunjaji kanuni na taratibu, kwa vile tu mna chuki na MD, hivyo ht penye ukweli mnafumba macho.
Wambieni wabadilisha vigezo, waseme RMO anaweza kuwa MD au AMO plus vigezo vingne. Hamtaona mtu analalamika hapa.

Maelezo mazuri haya mkuu...na SAHIHI.
 
Sikiliza wewe, unafaham majukumu ya DMO/RMO?
Kwa taarifa tu, wana kazi kuu 5:
1. Professional
2. Public health
3. Political
4. Training
5. Nimeisahau

Hapo kwenye professional na training, taaluma inahusika, huwezi ukafanya kazi ya ku supervise ma Dr kitaaluma wkt huna taaluma husika.
Mwisho utasema Engeneer wa mkoa/wilaya awe fundi Sanifu/fundi mchundo mwenye FTC, wkt wenye shahada na sifa za ziada wapo. Au Mwl wa cheti awe DEO/REO wkt wenye B. Ed na B.A. Ed na sifa za ziada wapo.
Hapa suala ni vigezo, km vinataja MD, apewe mwenye MD, usichoelewa kipi?
Unless wabadili vigezo.

Msendekwa, unanikumusha ile issue ya Mhe. Tundu Lissu na majaji wasio kuwa na degree ya sheria. It is very important to meet the required qualifications as recommended. Unless you change them otherwise adherence to agreed and documented qualifications must be followed.
Queen Esther
 
Back
Top Bottom