KKKT ni kanisa kubwa kuliko mtu, Kiburi kimemponza Mchungaji Kimaro

KKKT ni kanisa kubwa kuliko mtu, Kiburi kimemponza Mchungaji Kimaro

Alionywa kwa kosa lipi?

Waliogopa tu kuwa siku akisimama kugombeya U Askofu atawabwaga wote.

Yupo huyo mkuu wa jimbo naamini ana lenga kuwa Askofu, anadhoofisha wengine nguvu.

Je mmesahau huyu mkuu wa jimbo kufikia hapo alifanya kitu gani?

Na hapa wanajiandaa kumdhoofisha pia Matsai
Taratibu za kupata uaskofu au kitu chochote Cha uongozi Mara nyingi Ni vurugu na umafia ufanyika ndio tunazita siasa za kanisa

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Kanisa ka Kiinjili, la Kilutheri Tanzania, KKKT ina hstoria na ni taasisi ya muda mrefu.
Ina taratibu na kanuni zake , mchungaji au mtumishi atafanya mbwembwe zake zoote lakini lazima awe ndani ya utaratibu wa Kanisa.

Mtumishi akiwa na Karama au upako lazima aongozwe na hekima na siyo jeuri na kiburi cha kufanya na kusema atakavyo kwa kujiona yuko juu ya taratibu zilizowekwa .
Hakuna Mtumishi aliye juu ya KKKT kama taasisi , KKKT ni kubwa kiasi kwamba hata askofu hayupo juu ya KKKT.
Sasa hivi tunsona watumishi wanao lipatia kanisa au usharika mafanikio, cha kushangaza mafanikii yao yanawapanda kichwani na kuanza jeuri, dharau na kiburi.
Sbabu kubwa ni ukubwa wa wafuasi binafsi walionao.

Mwaka jana Dayosisi ya Konde Askofu wake Dr Mwaikali alivuliwa uaskofu.
Wengi wa tulioifuatilia ile ibada ya kumvua Uaskofu tulisononeshwa na uksidi wa Askofu Mwaikali.

Leo, Dayosisi ya KKKT Konde na kanisa linaendelea.

Kama mtumishi anajiona ana karama na unapendwa na watu wengi, bado una wiwa kufuata taratibu za Kanisa.

Kinyume na hapo kwa karama zako anzisha taasisi yako,

Jeuri na kiburi alichoanza kuonyesha hadharani huyu Dr Rev I Kimaro ni upungufu wa maono ya kutoona mbali.
Kuna fununubkuwa Kimaro alionywa mara kadhaa juu ya tabia yake binafsi kujiona yuko juu ya utaratubu, akakaidi, na wakati mwingine anajibu hadharani, na clips zipo.

Sasa inaelekea anavuna alichopanda.
Na hizi Phd magumashi wanapeana zinawatia kiburi cha bure baadhi ya watumishi wa kiroho. Ingekua vema kuona watumishi wale tu waliyosoma mafunzo yawe ya dini au elimu zingine hadi kupata shahada ya Phd kutumia tittle ya Dr.
 
Kilicho mponza mchungaji wa watu ni kusema kweli mbele ya watu wasiopenda ukweli... Hata ccm ukiwaambia ukweli wanaona unawakosea heshima [emoji23][emoji23] ... Nimemsikiliza mchungaji Tena na Tena, yaani kaongea ukweli mtupuuuu kbs...nilivyo muelewa yule jamaa ni kuwa , wakristo tujisahihishe
 
Kilicho mponza mchungaji wa watu ni kusema kweli mbele ya watu wasiopenda ukweli... Hata ccm ukiwaambia ukweli wanaona unawakosea heshima [emoji23][emoji23] ... Nimemsikiliza mchungaji Tena na Tena, yaani kaongea ukweli mtupuuuu kbs...nilivyo muelewa yule jamaa ni kuwa , wakristo tujisahihishe
Ukiwa na hekima ndio utaona kwamba jamaa ametumia lugha flani hivi ya picha ili kuwakumbusha kuwa watu tubadilike tuone wenzetu wamewezaje ili nasisi tunyooke.

Ila kama kawaida Tanzania ukiongea fact uwe hujafungamana na taasisi yeyote ile maana hata kama hujaisema taasisi lazma ikuvagae kwamba kwanini umeongea kitu cha namna hio.
 
Alionywa kwa kosa lipi?

Waliogopa tu kuwa siku akisimama kugombeya U Askofu atawabwaga wote.

Yupo huyo mkuu wa jimbo naamini ana lenga kuwa Askofu, anadhoofisha wengine nguvu.

Je mmesahau huyu mkuu wa jimbo kufikia hapo alifanya kitu gani?

Na hapa wanajiandaa kumdhoofisha pia Matsai
Kwani huko kkkt uaskofu huwa unagombaniwa kwa kuomba kura?
 
Inawezekana sasa haya makanisa yameanza kutumiwa na wachungaji kama vijiwe vya kutafuta umaarufu ili wajipatie wafuasi, siku wakitoka nje ya hapo wahame na wafuasi wao waende kwenye makanisa watakayoanzisha..

Waumini wanatumika bila kujua dhamira za ndani za hao wachungaji, kwasababu kama nia ya mchungaji ni kuihubiri injili, ujuaji hauwezi kupata nafasi mahala hapo, lakini kama mtu ana sababu zake zilizojificha, lazima awe mjuaji ili mwisho wa siku atimize malengo yake.
 
Freemason ufanya Kazi kupitia maaskofu wengi Ili kufifisha injili.
Hata yule askofu aliyeleta mgogoro TAG ni member wa freemason batani 3 hata sasa,na anashiriki vikao vya freemason hata kesho.
Shetani ana hasira sana na Moses Kulola sababu kamgaragaza Sana shetani alipokuwa duniani. Thus ana hasira sana na wafuasi wa Moses Kulola,bila Mch Mwaisabila yule askofu dr alishaliuza kanisa kwa freemason.
So huwa hatushangai ya Kimaro sio mapya, shetani kazini.
 
Ninachofurahi mchungaji Kimaro yeye ameaga tu kondoo wake. Mengine yote ni ya sisi tunaoongea pasipokujua sababu ya likizo ya lazima. Ameshaanza likizo yake ya siku 60. Hebu tumwache apumzike.
 
Inawezekana sasa haya makanisa yameanza kutumiwa na wachungaji kama vijiwe vya kutafuta umaarufu ili wajipatie wafuasi, siku wakitoka nje ya hapo wahame na wafuasi wao waende kwenye makanisa watakayoanzisha..

Waumini wanatumika bila kujua dhamira za ndani za hao wachungaji, kwasababu kama nia ya mchungaji ni kuihubiri injili, ujuaji hauwezi kupata nafasi mahala hapo, lakini kama mtu ana sababu zake zilizojificha, lazima awe mjuaji ili mwisho wa siku atimize malengo yake.
Sababu zilizojificha ndio zipi hizo, mtu kuongea ukweli ndio ujuaji? Pathetic Tanzanians like you deserve to be bombed.
 
Freemason ufanya Kazi kupitia maaskofu wengi Ili kufifisha injili.
Hata yule askofu aliyeleta mgogoro TAG ni member wa freemason hata sasa.
Shetani ana hasira sana na Moses Kulola sababu kamgaragaza Sana shetani alipokuwa duniani. Thus ana hasira sana na wafuasi wa Moses Kulola,bila Mch Mwaisabila yule askofu dr alishaliuza kanisa kwa freemason.
So huwa hatushangai ya Kimaro sio mapya, shetani kazini.
Kwamba Kimaro anatumika na shetani
 
Freemason ufanya Kazi kupitia maaskofu wengi Ili kufifisha injili.
Hata yule askofu aliyeleta mgogoro TAG ni member wa freemason hata sasa na anashiriki vikao vya freemason hata kesho.
Shetani ana hasira sana na Moses Kulola sababu kamgaragaza Sana shetani alipokuwa duniani. Thus ana hasira sana na wafuasi wa Moses Kulola,bila Mch Mwaisabila yule askofu dr alishaliuza kanisa kwa freemason.
So huwa hatushangai ya Kimaro sio mapya, shetani kazini.

Sijui hata unajua umeandika nini
 
Rubbish tupu. Kwa taarifa yako tu, kanisa hai lenye kumwabudu Mungu katika roho na kweli huwa halizuiliwi na mipaka, mapokeo ya kibinadamu. Refer kina Petro na Yohana baada ya kumponya yule kiwete pale kwenye mlango mzuri wakati wanakwenda kusali.

Viongozi wa dini wakawaita na kuwapiga biti mbaya kabisa, unajua walichosema? Walijibu "IMETUPASA KUMTII MUNGU, KULIKO WANADAMU". Wachungaji wa kweli husimama na kweli, no matter what.
KKKT inaongozwa na katiba mkuu. Ile ni taasisi kuwa muelewa. Kimaro analipwa mshahara kila mwisho wa mwezi, muajiriwa wa KKKT
 
Back
Top Bottom