Kocha Mwinyi Zahera aachia ngazi Yanga. Mkwasa kuinoa kwa muda

Kocha Mwinyi Zahera aachia ngazi Yanga. Mkwasa kuinoa kwa muda

Kweli kabisa umeongea vema lakini mi nihoji kidogo hivi kweli tatizo la yanga ni kocha kabisa?mi nadhani hapana tatizo nadhni bado safu nzuri ya uongozi kwa haijapatikana
Yanga siku nyingine muwe mnaiga ukomavu wa Simba. Maana Simba ilifungwa 5:0 na waarabu wala haikufukuza kocha. Pia mwaka huu tuliaminishwa kuwa Simba itatinga tena Group stage ya CAF na ikaishia round ya awali na wala haikufukuza Kocha. Pia Simba imefungwa na Mwadui wala hakuna anaemtukana Kocha. Yanga kuna kitu mnapaswa kujifunza.
 
Tunamshukuru kwa yote aliyotufanyia. Kwa usajili wa wacheza wa msimu huu acha tuseme inatosha. Bhoo
 
Yanga siku nyingine muwe mnaiga ukomavu wa Simba. Maana Simba ilifungwa 5:0 na waarabu wala haikufukuza kocha. Pia mwaka huu tuliaminishwa kuwa Simba itatinga tena Group stage ya CAF na ikaishia round ya awali na wala haikufukuza Kocha. Pia Simba imefungwa na Mwadui wala hakuna anaemtukana Kocha. Yanga kuna kitu mnapaswa kujifunza.
Ni suala la muda tu uyo mcheza mieleka atarudi kwao
 
Kweli fadhila mfadhili mbuzi utakunywa mchuzi wanadamu anamaudhi ,jamani huyu Zahera kawapa posho wachezaji ,amekaa nao kwa wakati mgumu ,wakati huu wamemtimua
Kwa hiyo aachwe tu hata kama ameshindwa kisa aliifadhili timu wakati wa shida, hiyo itakuwa ni "Blackmail".

Yeye aondoke tu uwezo wake umefikia upeo, hata kwenye hii ligi asingeweza kuifikisha timu popote na hata kwenye usajili pia alisajili hovyo sana.
Let him go and nobody will cry after him for he has done the club a great disservice.
 
Waswahili wana misemo mingi kuhusu tahadhari juu ya matumizi ya ulimi. Upo msemo kwamba "Chunga ulimi" , upo pia unaotwambia "Ulimi hauna mfupa" vile vile upo unaosema " bora ujikwae kidole lakini si ulimi" Misemo yote hiyo aghalabu ilikusudia kutupa tahadhari juu ya matumizi ya kiungo ulimi.Ulimi unaweza kukupandisha mpaka ukashangaa lakini ulimi huo huo unawez ukakushusha ghafla mpaka ukakufuru. Haya yote mawili yametokea katika maisha ya paapaaa Mwinyi Zahera ndani ya Yanga. Ulimi ulimpandisha na ulimi huo huo umemshusha.

Zahera labda hakuambiwa Yanga ni timu ya namna gani. Timu iliyoshind makombe mengi ya ligi kuu kuliko zote nchini hauwezi kusema imesajili kwa ajili ya ligi kuu. Yanga hakuna ilichobakiza katika ligi kuu.. Yanga imetwaa kombe hili mara nyingi zaidi , Yanga imemfunga mpinzani wake wa jadi mara nyingi zaidi. Iweje leo useme timu kama Yanga imesajili kwa ajili ya ligi kuu pekee? Kama ndivyo basi si kocha tu bali mpaka kamati ya usajili ingepaswa kufutwa kazi.

Yanga timu iliyoanzishwa miaka mingi zaidi kuliko nyingine yoyote katika ligi kuu haipaswi kuendelea kufikiria ligi kuu au michuano mingine yoyote ya ndani. Kushinda vikombe vya ndani si jambo kubwa ndani ya Yanga hivyo nadhani Zahera hakuambiwa hili.

Unaposema umesajili kwa ajili ya ligi ya ndani hapo hapo tutakuuliza. kuna timu kama Simba na Azam zimesajili kw ajili ya michuano ya Afrika je wewe unayejinasibu kwamba umesajili kwa ajili ya michuano y ndani utacheza nazo vipi hizi timu? jibu ni rahis tu kwamba hautakuwa kwenye kiwango sawa na hawa na automatic ni kwamba hutaweza kuchukua ubingwa wala nafasi ya pili mbele ya hawa . Je huoni kwamba utaendelea kusajili kwa ajili ya michuano ya ndani? maana ili ufuzu kimataifa inabidi uwe mbele Ya Simba na Azam kimatokeo , uwe mbele ya timu zote Tanzania bara.

Lakini pia huwezi kusajili wachezaji nane wa kigeni halafu wawe ni kwa ajili ya ligi za ndani tu. Hiyo ni hasara na ni hesabu kichaa. wachezaji nane wa kimataifa kwa ligi zipi hap bongo? kwa zawadi zipi?

Unaposema umesajili wachezaji kwa ajili ya michuano ya ndani tu , maana yake umma wa wapenda soka wafaham kwamba umesajili wachezaji wa viwango vya kawaida kama sio vidogo. Je hufaham kwamba maneno hayo yanaenda kuwaathiri kisaikolojia wachezaji wako?

Wazungu wanasema its better later than never. Zahera alipaswa kufukuzw kazi Yanga ndani ya masaa 24 tangu azungumze kwamba wachezaji waliosajiliwa ni kw malengo ya michuano ya ndani tu.
 
Lakini pia huwezi kusajili wachezaji nane wa kigeni halafu wawe ni kwa ajili ya ligi za ndani tu. Hiyo ni hasara na ni hesabu kichaa. wachezaji nane wa kimataifa kwa ligi zipi hap bongo? kwa zawadi zipi?
 
Kombe kile chakula kinacholiwa na Bwana Harusi na watu wake harusini

Rage alikuwa sahihi kuwaita nyinyi ni mbumbumbu! Yaani hamuelewi hata kidogo ni kwa nini timu ya Wananchi inatambulika pia kama Mabingwa wa Kihistoria!
 
Unamfukuza kocha bila kujiandaa kama wameshtukizwa au ndo wanawaiga tff haraka ya nini kama huna wa kuziba pengo wa uhakika
 
Itakuwa jambo la busara sana iwapo viongozi walikaa na Zahera na Mwandila wakakubalina kuachana kiungwana kama nilivyoshauri hapa jamvini wiki iliyopita. Lakini iwapo wamekurupuka ili kuwafurahisha wanachama kwa kweli itakuwa shida sana kwa Yanga kwani hawa makocha watadai pesa nyingi kutokana na kuvunjiwa mikataba yao hasa ukizingatia Mwandila alibakiza wiki tatu tu kwenye mkataba wake. Nasubiri kuona je viongozi walitumia busara au walitumia mihemuko?
 
Back
Top Bottom