Ambition plus
JF-Expert Member
- Feb 23, 2018
- 6,101
- 11,381
Mungu ni mwema litapita kwa amani.Mkuu unahisi hakuna dunia bila wayahudi...?
Hii mada umeipamba na ushabiki mwingi.
Hizi sio mambo za kushabikia kabisa...
Lipite kwa amani hope watafikia muafaka mzuri kwa pande zote.
Putin sio mwenye tatizo peke yake. Rafiki wa adui yako ni adui yako, hizi sababu za military expansion na alliances ndio zilileta WW1 na WW2. Russia inataka buffer zone na imefanya hivi kila ikiona maslahi yake yanapotea, Nikita Khrushchev alivyoondoa makombora Cuba wale Soviet politburo walimuona mzembe na pacifist. Ni interest za Russians kuwa mbali na NATO, Finland imezingatia hilo, Ukraine ilizingatia hilo ila mwishowe ikataka kuwa member.Putin ndio tatizo lenyewe. Mbona Ukraine iliyoongozwa na kina Kuchma au Yanukovich ilikuwa na uhusiano mwema na Russia?.
USA kuikaribia Ukraine haijaanza jana wala juzi, lakini hatukuwahi kuona Kremlin wakifikia maamuzi ya kuipiga nchi na kutangaza majimbo yake kuwa ni sehemu ya Russia.
Enzi za Yeltsin hatukuwahi kusikia hizi habari za kibabe zikiongelewa, waliijua diplomasia na ujanja wake.
Hamna ubunifu miongoni mwa wenye kufanya diplomasia ndani ya serikali ya Russia.
Wajue mustakabali wa nchi yao unapoishia ndipo mstakabali wa nchi nyingine unapoanzia.
Hitaji lao kubwa wajiunge na NATO. Hii Atlantic organization mpaka mpakani mwa Russia haina hata mantiki.
Fikiria Russia leo akisema anapeleka zana za kijeshi zikiwemo za nyuklia kwa rafiki yake Venezuela au Cuba, patakalika?!
Tatizo ni US kujifanya yeye ndie mmiliki wa hii dunia.
Sasa masuala ya kimataifa kutofautiana yana uzito. Southern Ossetia na Abkhazia ilikuwa hivi, Crimea imekuwa annexed Russia wakawekewa vikwazo. Bado ukirudi kwenye chanzo chenyewe Ukraine haikufanya vizuri calculations za kuwa karibu na NATO, kina Poland waliwahi kipindi Russia haijatengamaa. Finland waliochelewa tena ambao USSR ilishawahi kuwavamia wakaamua kuwa neutral kwa sababu wanapakana na Russia. Ukraine ndio doorstep ya kuingia Russia alafu anataka NATO waweke bases zake. Mbona US hawezi kukubali bases za Russia kuwepo Venezuela au Cuba.
Ushasema mambo ya kimataifa hutofautiana. Ndio tofauti zenyewe hizi
Udikteta wa marekani kwa dunia ya leo ni mara 20 zaidi ya ule wa Hitler miaka ile. Si kwamba unavumiliwa, pengine Putin anaionyesha dunia kwamba ipo namna ya kuweza kuuondosha udikteta huo.Mkuu
Kuvamia nchi nyingine kwa sababu zisizoingia kichwani ni ngumu sana. Ni kweli si Saddam lakini udikteta wa Hitler kwa karne hakuna atakayeuvumilia.
Putin ameanza kuishambulia Ukraine muda huu tunavyoongea.Udikteta wa marekani kwa dunia ya leo ni mara 20 zaidi ya ule wa Hitler miaka ile. Si kwamba unavumiliwa, pengine Putin anaionyesha dunia kwamba ipo namna ya kuweza kuuondosha udikteta huo.
Jambo jema sana. Russia na China wanasaidia kuweka balance kwenye geopolitics.Putin ameanza kuishambulia Ukraine muda huu tunavyoongea.
Unaongelea geopolitics wakati kuna watu wanakufa na wengine wanageuka mayatima!!?.Jambo jema sana. Russia na China wanasaidia kuweka balance kwenye geopolitics.
Unajua idadi ya waliokufa Iran au Korea kaskazini kutokana na vikwazo walivyowekewa na Marekani?!Unaongelea geopolitics wakati kuna watu wanakufa na wengine wanageuka mayatima!!?.
Mkuu kuna watoto wa kitanzania wanaosoma vyuo vikuu vya Ukraine, sasa hivi jiulize wapo katika hali gani.Unajua idadi ya waliokufa Iran au Korea kaskazini kutokana na vikwazo walivyowekewa na Marekani?!
Au hiyo haikugusi!
Hata Iran na North Korea wapo watanzania. Acha ubinafsi.Mkuu kuna watoto wa kitanzania wanaosoma vyuo vikuu vya Ukraine, sasa hivi jiulize wapo katika hali gani.
Biden unamsingizia hana ndoto hizo. Hiyo Russia inayozidiwa uchumi na South Korea ndio unasema iwekeze Eastern Europe? Kwa hela ipi waliyonayo..Russia wawekeze Eastern Europe ili kuinua standard of living za raia wa nchi hizo.
..USA iwekeze South America ambako wananchi wake wana hali mbaya kwelikweli na wanalazimika kukimbilia USA.
..dunia imebadilika sasa hivi wakati Biden na Putin bado wanaota ndoto za kizamani za wakati wa cold war. Yaani wanabishania kitu na masuala ambayo hayana manufaa yoyote kwa wananchi wa nchi zao, na dunia kwa ujumla.
Mimi nilikuwa kule na nimeacha watanzania ninaowafahamu. Unaongea North Korea na Iran ukiwa unajenga hoja tu, ni vitu viwili tofauti.Hata Iran na North Korea wapo watanzania. Acha ubinafsi.
Ukitanguliza utanzania kwenye masuala kama haya unakuwa unaweka mbele ubinafsi. Waone wote wanaoteseka duniani kwa kadhia hizi kama ndugu zako, itakuweka huru.Mimi nilikuwa kule na nimeacha watanzania ninaowafahamu. Unaongea North Korea na Iran ukiwa unajenga hoja tu, ni vitu viwili tofauti.
Inasikitisha sana.Ukitanguliza utanzania kwenye masuala kama haya unakuwa unaweka mbele ubinafsi. Waone wote wanaoteseka duniani kwa kadhia hizi kama ndugu zako, itakuweka huru.
Jumuia ya kimataifa imeishachelewa kuchukua hatua,kama ilivyochelewa kwa Adolf Hitler mpaka akaua wayahudi milioni moja.Wanasiasa hufanya makosa mengi sana wakiwa madarakani. Wanapoyafanya huwa hawana uwezo wa kupima ukubwa na madhara ya wanachokusudia kukifanya. Ni pale wanapokuwa wanapokea lawama nyingi ndio hujisumbua kuangalia kwa kina namna ambavyo wangeweza kuzuia kile walichokifanya, wangefanya hivi na wakafanya vile ndio huwa ni wazo lililochelewa wakati wake. Wanapokuwa wakiamua kufanya maamuzi yanayoongozwa na upofu au ulevi wa madaraka huwa wamezungukwa na wapambe wanaosema kitu wanachotaka kukisikia. Wao kuwa na maamuzi ya mwisho wakati mwingine huwanyima ile busara ya kuwa mawazo yao sio kila wakati huwa ndio ya kutekelezwa na yakaja na jibu lililokusudiwa na lenye faida.
Rais wa Russia Vladmir Putin anataka kufanya kosa litakalompa umaarufu mbovu kama ule aliokuwa nao Adolph Hitler mwaka 1939. Putin anataka kufanya kosa kama lile alilolifanya Idd Amin mwaka 1978 kwa kuivamia sehemu ya mkoa wa Kagera, kipigo alichokipata kilimpoteza kabisa miongoni mwa viongozi wa mataifa waliostahili heshima kila walipokatiza. Putin ameiangalia Ukraine katika udogo wake kwa kuilinganisha na Russia hivyo anaamini kwamba anaweza kufanya lolote na dunia ya sasa ikatulia tu na kumtazama. Kitakachompata kitakuwa ni fedheha kama ile iliyomkuta Hitler ambaye aliishia kujinyonga baada ya vita kumalizika akiwa ameshindwa vibaya.
Anatakiwa kukumbushwa kuwa Volodymyr Zelensky licha ya kuwa ni rais wa Ukraine taifa huru lenye maamuzi huru kama ilivyo Russia pia ni myahudi. Kwa asili ya wayahudi huwa ni watu wenye mtandao ulio hai na makini siku zote. Wayahudi wanajuana popote walipo, na mwanasiasa ambaye hata kama upande wa Mama ndio wayahudi huwa wanamchukulia kama ni mtoto wao. Wayahudi wanalinda ushawishi walionao duniani kote. Na ni rahisi kwao kumpachika jina la 'anti semitic' yoyote yule anayekwenda kinyume na falsafa zao au anayewakejeli.
Sembuse maamuzi ya Putin kuivamia nchi huru ya Ukraine inayoongozwa na myahudi mwenzao!!. Putin anakosa washauri wenye kutazama mbali, wenye ushawishi wa kidunia. Atumie busara sana kwani anachofikiria dhidi ya Ukraine kinaweza kumpoteza kabisa na yale yote aliyokwisha kuyafanya tangu 1999 alipoanza kuongoza Russia yakafunikwa na huu 'ujinga' anaouwazia kwa sauti ya juu.
Ulimwengu wa 1939 wakati Hitler akiivamia Austria sio huu wa 2022. Zimetungwa sheria nyingi za kimataifa zinazolinda uhuru wa kila taifa. Wamezaliwa wanasiasa wenye maarifa mazito ya kuongoza. Sayansi haijabaki nyuma zimeundwa silaha za hatari zenye kuweza kuangamiza kila kilichopo juu ya uso wa dunia ndani ya saa chache tu. Anaumizwa sana na ushawishi wa USA kwa jirani yake wa karibu, lakini nguvu nyingi hutumiwa na mwenye maarifa madogo ya uongozi.
Putin katoa onyo mapema; wakiweka pua zao kwenye huu mzozo anazing'oa.NATO na USA zile nguvu walizotumia kuisambaratisha Libya na Ghadafi,wanashindwa nini kuzitumia sasa hv.
Hizo sheria zimetungwa kwa kuzidhoofisha inchi zingine lakn US yy yupo juu yahizo sheria.Us alipoingia Libya, Iraq, Afghan na kuua mamilion ya watu ilikua sawa?