Kozi gani umesoma ambayo huwezi kumshauri mtu mwingine aisome?

Sijasomea hizo kozi ila wahitimu wa hizo kozi wanalilia kila mwaka mtandaoni wanaandika hadi mashairi, na kiukweli kazi zake mtandaoni zikitangazwa huwa hazizidi 4 kwa mwaka mzima.
Mkuu ukiona kazi zinatangazwa nne usifikiri kwamba hilo eneo halilipi hapana linalipa sana sema watu hawajajua hizo kazi zinapatikana wapi.Ukiwa na utaalam kama huo unaweza kufanya kazi kwenye hata makampuni local yanayohusika na mafuta na gas,unachotakiwa tu na kujiongezea ujuzi wa ziada.

Sio lazima ukisoma GEOLOGY uwe mchimba madini.Unaweza kuwa mtafiti(Free lance)Unaweza kuwa Broker,unaweza kuwa mshauri(consultant) unaweza kuwa anything kwenye sekta ya madini mradi uwe na utayari na uelewa.Iwapo unahitaji ushauri wa namna ya kubadili eneo lako la usomi kuwa fursa basi tuwasiliane kwa email au pm.Maisha ni kupambana
 
Nikurekebishe boss Geology sio mchimba madini boss,kazi ya geology ni kufanya utafiti wa rasirimali zilizo chini ya ardhi (Exploration ) ,Reserve Estimation ,kuplan na kufanya survey ya mineral resources.

Mtu anayehusika katika kuchimba ni mining engineer mzigo ukishatoka ardhini kazi ya kuusafisha na kuuweka katika hali nzuri ni ya Mineral Processing Engineer/Chemical and Processing/Chemistry
 
Acha uongo, Watu wenye hii elimu wanalindwa sana
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu wewe unasema kwa nadharia tu, hizo petroleum ni siasa tu kaka
 
Mkuu wewe unasema kwa nadharia tu, hizo petroleum ni siasa tu kaka
Mkuu ni jukumu la msomi kubadili nadharia kuwa uhalisia,huwezi kupewa elimu na kazi pia upewe.Ikitokea umepata kazi ni sawa ila kama hujapata ni lazima uwe na uwezo wa kutumia elimu yako kufanya jambo vinginevyo ni sawa na ulipoteza muda kwenda shuleni bora ungechunga kuku tu.
 
Ila accounting ukiotea pande pazuri umetoka! Hamna kitu najutia kama kutosoma uhasibu, sidhani kama ningekuwa uraiani mpaka leo.
Plan ni kutafuta hata ka Postgraduate diploma kake baadae.
Yeah uhasibu ni kozi ambayo siku zote iko sokoni
Nadhani kajiongeze ata kapostgraduate openi university kama siyo account basi business administration nao hawakai sana kitaa
Hizi ni kozi zenye uhitaji miaka yote
 
Duuuu aisee
 
MUNGU asaidie muendelee kuwa na utu hivyo kulikoni siku al shabashi wakiwapa mualiko wa kutoa mafunzo ya milipuko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Write your reply...Course ya kuchat kwenye social media sishauri kabisa watu waisome
 
Then tushirikishane..professional short courses upande wa Environmental sciences..ukiachilia mbali hizi.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
bingwa mtu aliyesomea microfinance ushauri wa short course pls
Microfinance wale kwa uelewa wangu hawana tofauti saaana na watu wa finance hapo unalazimika kujua Financial Management Tools (eg Excel,Power Point,Quick Book,SAP, BR net,Tally etc).

Kama unataka kufanya kazi kwny ma bank kachukue Banking Certificate I &II then kuna kitu inaitwa Certified Proffessional Banker (CPB).

Kama unataka kujiweka kwny nafasi nzuri ya ajira nenda kagonge MBA ,CPA(T) au ACCA.

Umeshindwa kabisa kasome hata ka Certificate cha sheria bila shaka ni mwaka mmoja,maana kuna kazi za Microfinance zinahitaji mtu mwny ujuzi wa sheria maana kudeal na wadaiwa legal matters zinahusika,mtu ambaye ni mdaiwa sugu (Bad Debtor) mahakama inamuhusu.
 
[emoji23][emoji23][emoji23] wadaiwa sugu..wanatia hasara kampuni.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii huwezi itumia kwenye coz ya renewable energy engineering?
 
Telecommunications Eng kwakwel hapana....ka degree kameisha vzr pale mlimani, ee game linanilazimu nisome tena CCNA, CCNP na ni mpunga mlefu balaa...ka sio ujinga ni nini huu




Sent using Jamii Forums mobile app
Hiv ccna na ccnp ni sh ngapi? Nawaza kujisomea tu mwenyewe home nilipie hio mitihani nifanye!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…