#COVID19 Kudhibiti maambukizi ya COVID-19: Wasafiri kutoka Tanzania wapigwa marufuku kuingia Uingereza

#COVID19 Kudhibiti maambukizi ya COVID-19: Wasafiri kutoka Tanzania wapigwa marufuku kuingia Uingereza

Wala sichoki kuwaelimisha
Mmesikia kuna Corona maalum imegundulika South Africa ambayo ni COVID19 lakini imebadilika na ni kali ? Inaitwa South African variant au strain? Sasa hii Corona ya Sauzi haitibiki na antibiotics etc walizotumia kupunguza makali ya Corona, pia chanjo inaonekana kutosaidia! So ni kitu kipya na inaua sana! Sasa UK wanasema Tanzania tunasambaza hiki so hawataki tuwapelekee - Nchi zilizoendelea zimelipa gharama kubwa kupata chanjo na kuwafungia raia wao wasiambukizwe - wanajiandaa kuwachanja wote warudi kwenye shughuli zao! Nyie bado mnazurura bila kujikinga mnataka kuzua balaa nyingine - hawataki masihara!
Wameanza Uingereza lakini tukiendelea kupuuza na kutochukua hatua tutafungiwa na nchi zingine pia! MATAGA waache uongo eti nchi zingine zimepigwa ban - Kenya, Rwanda, Uganda wanaruhusiwa kuingia UK bila shida! Why Tanzania na DRC? Acheni kupotosha umma!
Pili sisi wenyewe tujue Corona hii ya Sauzi ni hatari kuliko ile ya mwanzo na Afrika inaonekana kupigwa nayo ndo maana mnaona mawaziri huko Zimbabwe, South Afrika wanakwenda!
Narudia tuchukue hatua madhubuti kama Taifa dhidi ya Corona na tufanye mapema kabla hatujatengwa!
Wewe binafsi JIKINGE
#TutaelewanaTu #ChangeTanzania
Hivi Mkuu wa nchi na wataalamu wetu wana ona shida gani kutuambia tujikinge? Kama ipo isitupate. Kama haipo hatuta kuwa tume poteza chochote.
Ni heri kinga kuliko tiba..
 
Wakati mnatengeneza pesa wao watakuwa wamelala tu?The answer is this: Every country must be integrated well in the world.
Sasa Hivi tujikite kutengeneza fedha, baadaye dawa rasmi ikipatikana tutaenda. Waache waje tupate pesa, sie tujifukize tusife ili siku za usoni waone kuwa wao walikosea.
 
Kwa mawazo finyu unaweza kufikiri lockdown ni solution. Mbona haijesha huko Ulaya na Marekani? Hivi unajua kuwa wengi tumeipata na tumevuka? Siamini kupigana na zimwi lisiloonekana bali kujizatiti tu.

Najua wewe ni mpinzani ila kumbuka kwa suala hili njia tuitumiayo ndiyo njia sahihi kwa hali ya covid ilivyo. Nakuacha na rejea ya Gazeti lenu linalosema wanatibu.

A medical doctor at Aga Khan Hospital, in the city centre – who prefers not to be mentioned, without giving the exact number of those infected by Covid-19, said the number has been growing but most of them do recover after three to four days. He did not disclose the prescriptions.

Aga Khan hospital has reportedly developed a special formula for the treatment of Covid-19.

He said most of the patient comes with respiratory complications, high fever and sometimes headache, are clinically plaid and when diagnosed with Covid-19 are admitted with special supervisions – and starts treatments.

Full story Fresh Corona fears hit "Covid-free" Tanzania - Sauti Kubwa
Tatizo hata Kama Aga Khan wanatibu Ni Watanzania wangapi wanaweza kumudu gharama zao?!
 
Wala sichoki kuwaelimisha
Mmesikia kuna Corona maalum imegundulika South Africa ambayo ni COVID19 lakini imebadilika na ni kali ? Inaitwa South African variant au strain? Sasa hii Corona ya Sauzi haitibiki na antibiotics etc walizotumia kupunguza makali ya Corona, pia chanjo inaonekana kutosaidia! So ni kitu kipya na inaua sana! Sasa UK wanasema Tanzania tunasambaza hiki so hawataki tuwapelekee - Nchi zilizoendelea zimelipa gharama kubwa kupata chanjo na kuwafungia raia wao wasiambukizwe - wanajiandaa kuwachanja wote warudi kwenye shughuli zao! Nyie bado mnazurura bila kujikinga mnataka kuzua balaa nyingine - hawataki masihara!
Wameanza Uingereza lakini tukiendelea kupuuza na kutochukua hatua tutafungiwa na nchi zingine pia! MATAGA waache uongo eti nchi zingine zimepigwa ban - Kenya, Rwanda, Uganda wanaruhusiwa kuingia UK bila shida! Why Tanzania na DRC? Acheni kupotosha umma!
Pili sisi wenyewe tujue Corona hii ya Sauzi ni hatari kuliko ile ya mwanzo na Afrika inaonekana kupigwa nayo ndo maana mnaona mawaziri huko Zimbabwe, South Afrika wanakwenda!
Narudia tuchukue hatua madhubuti kama Taifa dhidi ya Corona na tufanye mapema kabla hatujatengwa!
Wewe binafsi JIKINGE
#TutaelewanaTu #ChangeTanzania
Hivi Mkuu wa nchi na wataalamu wetu wana ona shida gani kutuambia tujikinge? Kama ipo isitupate. Kama haipo hatuta kuwa tume poteza chochote.
Ni heri kinga kuliko tiba..
Ndugu achana na propaganda, ugonjwa wa COVID-19 na kujigawa kwake kwa virusi vingine vya Afrika kusini, Nigeria na Brazil upo kila nchi na kila nchi itambana nao kwa uwezo walio nao.

Hizi variants za ugonjwa pia zimegundulika Ujerumani na baadhi ya nchi zinazitokeza kusema zimegundua hizi variants.

Variants ni jinsi kirusi kinavyojibadili kulingana na mazingira ya sehemu na aina ya watu waliopo hapo.

Hivyo hata umoja wa Ulaya nao wanapanga kuwazuia raia na wakazi wa Uingereza kuingia kwenye hizo nchi kama Ujerumani.

Kama hufahamu mwezi December mwaka jana nchi nyingi za jumuiya ya Ulaya zilizuia ndege za kutoka UK kuingia katika nchi hizo.

Hivi sasa wanapanga hatua zaidi na wanawalenga Uingereza.

Soma hapa:

Individual EU countries could temporarily ban all UK residents - the new proposal explained (msn.com)

Tusiwe wajinga wa kukumbatia kila propaganda.
 
Yule balozi wao aliyeambiwa na jiwe awaonye wale wengine badala yake naye kawa mshirika wa kutufungia mlango?

Kama shere dunia kweli imetupata.

Twachezwa shere kila upande.
JPM anafikiria wazungu ni watu wa mchezo....na bado..huwezi kumdanganya mtu mwenye akili...aendelee kutoa watanzania sadaka tu.
 
Lakini hii sirikali yetu inachekesha sana, ni kweli maambukizi ya korona sio makubwa nchini. Kuna ubaya gani wa kutoa data za hao wagonjwa?

Nchi yetu sio kisiwa ina muingiliano na mataifa mengine yaliyoathirika sana na wala ugonjwa huu sio wa aibu haujaanzia kwetu...kuna tatizo gani kusema hali yetu nchini kuhusu korona ikoje.

Yaani li sirikali lipo kimya japo hata kuendelea kuhamasisha raia wake kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa ambao dhahiri bado ni tishio duniani.
Kwenu kuna Nimonia tu
 
Kama hukwenda darasani huwezi kujua umuhumu wa data.
ulienda darasani na unatizama data kama mkombozi wa ugonjwa wa mlipuko usio na tiba!!!

tofauti yako na tofali la kukalia ni nini????
 
This is stupid sana.
Hii ndo sababu, hata siku moja, shangaa mapungufu ya nchi yangu, siwezi ku-support mataifa mageni kuingilia maswala ya ndani ya nchi za Africa.

Mbona kwao wanakufa wakiangahika na UK variant. Wamefanya lockdown na kila aina intervention na wameshindwa.

Ja AFRICA tumewatenga? NO!
AFRICA tumezuia watu wao? NO!
Tumewauliza maswali kuhusu sera zao za afya? NO!

Ila ndungu zetu hawaishiwi kutuwekea vizuizi
Mara wanataka lockdown
Mara wanataka Data

Kwani mkimpima mtu kuna Tatizo gani?!
Kwani hao residents wana resistance ya virus?!!


Hizi ndo siasa za mabeberu, uonevu na dhalau
Baki kwenu kwani ni lazima uende kwa mabeberu?
 
ulienda darasani na unatizama data kama mkombozi wa ugonjwa wa mlipuko usio na tiba!!!

tofauti yako na tofali la kukalia ni nini????
Unafikiri dawa zinapatikana kwa kuokotwa barabarani watu wamefanya research nyingi kabla na huwezi kufanya research bila data.
 
Kirusi kimegunduliwa Afrika Kusini lakini wanaozuiwa ni Watanzania na Wakongo,,,,,,sielewi.
 
Kuna wakati tuseme ukweli zaidi kuliko kusema siasa zaid,laiti kama Corona ingekuwepo kama inavyoonekana kuwepo katika mataifa mengine,na laiti kama wazee tungekuwa tunaishi kama tunavyoishi sasa na Corona ikawa kama ilivyo kwingine,basi Tanzania nzima hadi sasa maiti zingekuwa zikiliwa na kunguru barabarani,itoshe tu kusema Corona ipo na tahadhari zichukuliwe.
Kama watanzania watakataliwa kwenda sehemu nyingine kwa sababu kuna Corona,kwanini tung'ang'ani nchi za watu,hata bila COorna tungezuiana tu kuingia kwenye za watu maana yapo mengi ya kusababisha tuzuiane ila siyo kuja na kusingizia Corona,ajabu sana kuona watu wanadanganyika kwa kugeuzwa uongo kuwa ukweli.
 
Back
Top Bottom