Tetesi: Kuelekea Mkutano Mkuu wa CCM: Mbunge, Wajumbe na Katibu wa Mikoa wa Upinzani kujiunga CCM

Tetesi: Kuelekea Mkutano Mkuu wa CCM: Mbunge, Wajumbe na Katibu wa Mikoa wa Upinzani kujiunga CCM

Kuelekea Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) unaotarajia kufanyika tarehe 23th July 2016 mjini Dodoma, tayari zipo taarifa za kuaminika juu ya Viongozi wakubwa wa Vyama vya Upinzani kuazimia kujiunga na CCM katika siku hiyo.

Taarifa iliyotufikia inamtaja Mbunge mmoja maarufu wa CHADEMA ambae mpaka jana alikuwa anamaliza mazungumzo ya mwisho na viongozi waandamizi wa CCM juu ya utaratibu wa mapokezi yake na hatma yake kisiasa.

Wengine ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Pia yupo Mgombea Uenyekiti wa BAVICHA na mgombea Ubunge wa Moja ya Majimbo ya Kaskazini. Pamoja nao yupo aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, pamoja na Makatibu kadhaa wa Mikoa wa Chama cha ACT.

Ukiachilia mbali Viongozi hao wa wapinzani ambao idadi yao kwa ujumla inakaribia 18, wapo waliokuwa wa CCM na wakahama na kumfuata LOWASSA upinzani, Viongozi hao nao wameendelea kubembeleza ili waweze kupokelewa tena ndani ya CCM. Watatu kati yao tayari wako Dodoma wakiongozwa na aliyekuwa "Mtoto na Msiri" wa Lowassa ambae pia alikuwa ni KATIBU wa CCM Wilaya ya Monduli.

Wakati Viongozi hao wakijiandaa kujiunga na CCM, maandalizi ya Mkutano Mkuu yameendelea kukamilika na kufikia hatua nzuri, ambapo jana Katibu Mkuu wa CCM alikagua hatua ya maandalizi na kujiridhisha kuwa Mkutano Mkuu utakuwa wa mafanikio makubwa kutokana na kukamilika kwa maandalizi ya Mkutano huo kwa sehemu kubwa.
Mheshimiwa waziri huyo mbunge mnakubaliana kumpa cheo gani??
 
Duh! Hii lugha imekuwa ngumu kwangu.
mm huwa naotaota, ndio maana lugha zangu hazueleweki ila tuijenge nchi wote kama watz. tukikopa deni ni letu kama watz. ukija uchaguzi ndio ccm,cuf nk. deni la taifa tunalipa wote na huu mkopo wa reli ni wa watz. sio ukawa wala ccm
 
Wakati ccm wakitalajia kuwapokea hao 18 tarehe 23/7 ....tarehe 25 upinzani utapokea vigogo kutoka ccm 180 ...hii inaitwa kampa , kampa tena ...
Hahaaa ndoto za alinacha. Kuhamia upinzani wafuate nini. Hakuna kitu kama hicho. Poleni VVU
 
Huu ni uongo una uzushi! Tetesi halafu uthibitisha mmana ake nini? Hivi unafikiri JJ Mnyika hata kama kuna mambo hayafurahii Chadema unafikiri anapelekwa na bongo za CCM?
Ccm unaweza kuwaita jina jepesi tu kuwa WAMEFULIA KISIASA
 
mm huwa naotaota, ndio maana lugha zangu hazueleweki ila tuijenge nchi wote kama watz. tukikopa deni ni letu kama watz. ukija uchaguzi ndio ccm,cuf nk. deni la taifa tunalipa wote na huu mkopo wa reli ni wa watz. sio ukawa wala ccm
Hakika. Na maendeleo yakiletwa na CCM tunaenjoy wote. Ona lile daraja ya Mwalimu Nyerere pale Kigamboni. Ona barabara za mabasi ya Mwendokasi. Imeanzia Kimara Uchagani hadi Ferry. Hakuna kubagua.
 
Ccm unaweza kuwaita jina jepesi tu kuwa WAMEFULIA KISIASA
Duh! Aisee mipasho yako nimeipenda sana. Yaani chama kinaongoza Dola bado unasema kimefulia kisiasa! Na Mzee Lowasa utamuitaje?
 
Aiseeeeeea, hii sasa kali. Tafsdhali Mwenyekiti wangu Magufuli. Utatuulia upinzani. Unafikiri wataishije ikiwa SACCOS zao zitapungua mapato?
 
Ndoto kwako kwa kuwa wewe ndio mwanachama unayeomba kurudi ccm jukwaani umesharudi zito unamwacha mwenyewe baada ya kudai demokrasia
Huyo jamaa MOTOCHINI amethibitisha pasipo shaka kuwa ni chumia tumbo tu kamuwacha kabwe pekee yake
 
Back
Top Bottom