Kuendelea kumtaja Hayati Magufuli kwa mabaya ni upuuzi wa ajabu

Kuendelea kumtaja Hayati Magufuli kwa mabaya ni upuuzi wa ajabu

Wewe unaishi wapi ambako shetani hatajwi?
Kutajwa tu sio shidamaana wapo wenye kumuabudu kabisa hivyo wanamtaja, mie nikiangalia hali ilivyo naona maovu mengi kuliko mema tafsiri yake shetani ana wafuasi wengi tunaona na kusikia mambo ya shetani kwa wingi kuliko kusikia anavyolaaniwa shetani.
 
Anaandika, Robert Heriel

Sikuwa mshabiki wa Magufuli Kutokana na namna alivyokuwa anaongoza, sisemi Kuwa Magufuli hakuwa na mambo Mema aliyoyafanya, yapo mengi mazuri Sana hasa ya miundombinu, lakini pia yapo Mabaya ambayo aidha aliyafanya au kuyafumbia macho, ambayo ndio yalinifanya nimuone kama kiongozi asiyefaa.

Ninashangazwa na kile kinachoendelea hasa Kwa upande wa Upinzani kuendelea kumtaja taja MTU ambaye tayari anasiku nyingi ameshafariki.

Wabaya Waliohai wapo wengi, Kwa nini mhangaike na Watu waliokwisha Kufa wasio na chochote cha kuchangia katika Ulimwengu wa Waliohai? Wema Waliohai pia wapo wengi.

Hatuwezi kuongoza nchi Kwa kuangalia Wafu, na hatutataka nchi yetu iongozwe na watu wenye mawazo na Matendo ya Wafu.

Tunahitaji viongozi ambao wanaongoza nchi Kwa kuangalia Maisha ya kizazi kijacho kitaishije,
Nchi inaongozwa Kwa mahitaji yajayo sio mahitaji yaliyopita. Nchi inaongozwa Kwa maslahi ya Watu wa kesho sio Kwa maslahi ya Watu wa Jana na juzi waliokwisha Kufa.

Wanaoishi Wasiwe watumwa wa Wafu, Watu waliokwisha Kufa. Hivyo ndivyo taifa hili linapaswa kujengwa na kuongozwa. Kwa sababu tunaenda Mbele na sio Nyuma.

Sijui Fulani alikuwa Nani akasema nini, hiyo haina maana yoyote Kwa wakati au kizazi kijacho, kitakachoangaliwa ni manufaa ya kizazi kijacho.

Hata Mungu tunayemuabudu ni MUNGU aliyehai na Mungu wa Waliohai sio Mungu wa Wafu.

Wanasiasa mnaomtaja taja Magufuli Kwa ubaya mnayohaja ya kujitafakari, kama mnaagenda zenu za Siri Sawa lakini eleweni kuwa haitasaidia Jambo LOLOTE lile.

Acha nipumzike SASA.

Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Makanya, Same, Kilimanjaro.
wafu hawajui neno lolote, ila marehemu atatajwa sana kwa mambo ya hovyo na mazuri aliyoyafanya ktk hii nchi
 
1). Dikteta Benito Mussolini alianza kutawala Italy tarehe 31/10/1922, karne nzima iliyopita, akapinduliwa tarehe 25/July/1943..
Hatimaye akanyongwa Kwa sababu ya uovu wake mwaka 1945.
2). Dikteta Joseph Stalin, alitawala Urusi Kwa mkono wa chuma kati ya 1924 na 1953.
3). Dikteta Vladimir Lenin alitawala kuanzia 1917 hadi 1924..
Nk..
Na kuna orodha ndeeefu ya madikteta wa Afrika ambao ni marehemu na wanaendelea kusemwa..

Wote hao wanasemwa na wataendelea kusemwa.
Ndo wewe uzibe watu midomo kumsema dikteta wa juzi hapa?!!!

Moja ya manufaa ya kuwasema waovu wa zamani ni kukumbushana na kuelimishana ili kupunguza uwezekano wa kuibuka muovu mwingine upyaaa!
Kuna tofauti ya kuzungumzia histoaria ya mtu na kumsema mtu tunakozungumzia hapa, Nyerere huwa anatajwa sana ila ni tofauti na jinsi alivyomzungumzia Tundu Lissu bungeni ikazuia maneno.
 
Hapa nilipo mie,watanzania wengi wanaoishi hapa uingereza wanamkubali sana jpm,huwa tuna club yetu ya kukutana kila jmos ya mwezi,huwez amin,wanammiss sn jpm,japo wanakili kuwa alifanya makosa kubinya upinzani,
Watu wengi walionyooka wanamkubali Magufuli.
 
Mdogo wangu Heriel humu JF hujapajua vizuri tu? Ukitaka uonekane una akili mtukane Magufuli. Kinyume chake ndio haya unayoyaona.
Watu wanaacha kupambana na maisha yao na majukumu ya kila siku wanahangaika na marehemu.
 
Kwani hakuna Marais wabaya Waliohai?
Kama lengo ni kutafutana ubaya, hatuwezi kosa ubaya WA yeyote.
Lakini kutafuta ubaya wa Wafu ni dalili ya ucheshi wa mwendawazimu.
Hakunaga Hukumu ya Wafu, wanaohukumiwa ni Waliohai.

Hata hivyo kuna Ile hasira ya wahanga ambayo MTU akifa humsema kutuliza hasira na chuki zao. Lakini kumchukia Na kuwa na hasira ya Marehemu Kwa zaidi ya miaka ni Jambo la kipuuzi hasa ukijua amekufa na hatorudi
mwendazake ni jinamizi lililojivika ktk vazi la uzalendo, yaani atatajwa sana, zitto kasema ambao hawataki kusikia akitajwa wamfuate kaburini
 
Kuna tofauti ya kuzungumzia histoaria ya mtu na kumsema mtu tunakozungumzia hapa, Nyerere huwa anatajwa sana ila ni tofauti na jinsi alivyomzungumzia Tundu Lissu bungeni ikazuia maneno.
Huwezi kumtenganisha mtu na matendo yake.
Kuna manabii wa Mungu walishafariki maelfu ya miaka nyuma, lakini bado wanatajwa kwa matendo yao, mazuri na mabaya
 
Anatajwa na Wajerumani? Au kina Nani?
Kutaja taja Wafu kila mara ni dalili ya kuchanganyikiwa.
Unataja Watu ambao hawana chochote chakufanyak

Magufuli nilimlaani akiwa hai lakini sinaga Laana wala baraka Kwa Watu waliokwisha Kufa.

Kila MTU MTU mpenda Haki alichukizwa na Matendo hayo, ikiwemo Mimi.
Kwa hivyo sio vibaya kukumbusha uovu wake ili wenye madaraka na watakaokua na madaraka siku zojazo wajifunze kuwa Kuna haja ya kuwatendea watu wema, Mana mabaya huambatana na mtendaji wa hayo mabaya. (Lesson)
Kizazi hiki kitayazungumzia mabaya yake wakati wote mpaka kitapotoweka kwenye uso wa dunia!!

Tusubiri miaka mingine 50 idadi ya watakaokua wanazungumzia mabaya yake itakua imeoungua Kama sio kuisha


Vivyo Kama Kama wanazungumzia mazuri yake watakwisha Ni swala la muda tu, kwahiyo Kama watu wanavyofurahia kukumbushia mazuri yake kila siku Basi wavumilie watu wanazungumzia kwa upande wa pili!
 
Anaandika, Robert Heriel

Sikuwa mshabiki wa Magufuli Kutokana na namna alivyokuwa anaongoza, sisemi Kuwa Magufuli hakuwa na mambo Mema aliyoyafanya, yapo mengi mazuri Sana hasa ya miundombinu, lakini pia yapo Mabaya ambayo aidha aliyafanya au kuyafumbia macho, ambayo ndio yalinifanya nimuone kama kiongozi asiyefaa.

Ninashangazwa na kile kinachoendelea hasa Kwa upande wa Upinzani kuendelea kumtaja taja MTU ambaye tayari anasiku nyingi ameshafariki.

Wabaya Waliohai wapo wengi, Kwa nini mhangaike na Watu waliokwisha Kufa wasio na chochote cha kuchangia katika Ulimwengu wa Waliohai? Wema Waliohai pia wapo wengi.

Hatuwezi kuongoza nchi Kwa kuangalia Wafu, na hatutataka nchi yetu iongozwe na watu wenye mawazo na Matendo ya Wafu.

Tunahitaji viongozi ambao wanaongoza nchi Kwa kuangalia Maisha ya kizazi kijacho kitaishije,
Nchi inaongozwa Kwa mahitaji yajayo sio mahitaji yaliyopita. Nchi inaongozwa Kwa maslahi ya Watu wa kesho sio Kwa maslahi ya Watu wa Jana na juzi waliokwisha Kufa.

Wanaoishi Wasiwe watumwa wa Wafu, Watu waliokwisha Kufa. Hivyo ndivyo taifa hili linapaswa kujengwa na kuongozwa. Kwa sababu tunaenda Mbele na sio Nyuma.

Sijui Fulani alikuwa Nani akasema nini, hiyo haina maana yoyote Kwa wakati au kizazi kijacho, kitakachoangaliwa ni manufaa ya kizazi kijacho.

Hata Mungu tunayemuabudu ni MUNGU aliyehai na Mungu wa Waliohai sio Mungu wa Wafu.

Wanasiasa mnaomtaja taja Magufuli Kwa ubaya mnayohaja ya kujitafakari, kama mnaagenda zenu za Siri Sawa lakini eleweni kuwa haitasaidia Jambo LOLOTE lile.

Acha nipumzike SASA.

Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Makanya, Same, Kilimanjaro.
Mpuuzi ni wewe usiyejua /usiyeweza kupima/kutafakari machungu waliyonao ya aliowaumiza! Ni upuuzi wa jabu ulio nao wewe. Mke wa azory, Ben and many many others wanajisikiaje muda huu bila kuwa na wapendwa wao? Wewe "ntu" wa ajabu!
 
Kuna kitu kinaitwa "closure". Kwa kiswahili cha mtaani tunaweza kuita "kufunga mafaili" ya jambo au suala. Katika utawala wa Magufuli kuna mambo mengi mabaya sana yaliyofanyika ambayo hadi leo hayajapatiwa majibu au tuseme bado yako gizani. Kwa mfano, mauaji ya Akwilina, Lwajabe, miili iliyookotwa kwenye viroba, kupotea kwa Azori, Ben Saanane, risasi za Lissu, kutekwa kwa Mo, Roma, Magoti, wizi wa uchaguzi 2019, 2020. kuzima vyombo vya habari, vyama vya upinzani, ukwapuaji wa fedha za watu benki, bureau de change, n.k. Na majuzi Rais wa sasa kaongezea ufisadi kwenye pesa za "plea bargain" zisizojulikana zilipo.

Yote hayo bado yako gizani. Serikali ya CCM bado haionyeshi utashi wa kuleta CLOSURE kwenye kadhia hizi.

Lazima mkondo wa sheria ufanye kazi, ukweli ujulikane, hukumu sahihi itolewe (hata posthumously ikibidi) na hatua zichukuliwe kwa wahusika waliopo. MUHIMU ZAIDI kwa amani na utulivu wa nchi ni vyema kuwa na mchakato wa maridhiano ya kitaifa (truth and reconcilliation process). Hiyo ndiyo namna bora ya kupata CLOSURE. Maridhiano yanayoendelea ni hatua nzuri lakini haitoshi. Kinachosikitisha sana ni kwamba miaka ya karibuni serikali ya CCM imezidi kuendesha propaganda hatarishi za kuwagawa wananchi.

Kwa wale watakaodai hata awamu zilizopita zina matatizo ya aina hiyo wako sawa ingawa ni wazi kuwa Rais wa awamu ya tano aliyafikisha kwenye kiwango cha kutisha. Yaliyotokea kwa Mwangosi, Zona, Ulimboka na Kibanda awamu ya nne nayo bado "yananing'inia". Hayajapata CLOSURE. Ni doa kubwa kwa serikali ya CCM. Wahenga hawakukosea waliposema "damu ya mtu haipotei bure". Yote haya yataendelea kulitesa taifa kwa miaka mingi ijayo.

Walio na shauku kubwa kutaka Magufuli asisemwe au asitajwe basi waiombe serikali yao ya CCM ichukue hatua kuleta CLOSURE na UTANGAMANO kwa wananchi wote nchini. NA pia wajue wakianzisha mada za kumsifu Magufuli katika mazingira haya ambapo kadhia nyingi za utawla wake hajipata CLOSURE basi wasishangae kujibiwa na wenye kero zao. Waingereza wanaita kujibiwa "in kind".
Maelezo kuntu..
Hii post inafaa kufanyiwa lamination na kuwasilishwa pale Lumumba!
Ionwe na Robert Heriel, ccm
 
Tunamtaje jpm kama sehemu ya mktaba wa maridhiano na mama,japo hata sisi hatupendi kumtaja,lkn maelekezo ni lazima tumnange na kumkashifi na kimxushua mambo mabaya,lengo ni kupunguza nguvu kubwa ya ushawishi alionao kwa watanzania na dunia nzima,Na nikili kuwa tunao wakati mgumu sana mbele ta watanzania,kwani tunaxomewa na kutukanwa,
Ona tutusa hili.
 
Ingekuwa wewe ndiye uliyepigwa Risasi thealthini,Mtoto wako alipotezwa, Ndugu zako waliuawa(Baba au mama yako) ulibomolewa nyumba yako Morogoro Road bila kulipwa hata mia nazani ungekuwa unamlaani milele hata kama amekufa
Haisaidiii....
 
  • Thanks
Reactions: nao
Hebu jifunze kunyamaza, Hujui wala hufeel pain ambazo watu wamezipata kutoka Kwa huyo ibilisi unayemtetea, labda angeuwawa baba yako mzazi na mama yako mzazi ndio ungejuwa uchungu wake.

Huyo hata ipite miaka 50 ni lazima atashtakiwa tu ili haki itendeke haijarishi yupo kaburini cha msingi ni ile hukumu itakayotolewa ili ikae kwenye kumbukumbu.
Una uthibitisho gani kwamba Magufuli aliua mtu? Alimuua nani? Thibitisha...
 
  • Thanks
Reactions: nao
Wayahudi wanaomlaani Hitler mpaka Leo unadhani niwajinga wewe ndio mwerevu! Mjinga kabisa wewe!
Sawa, wewe endelea kulialia kama juha uone kama kunakitakacho badilika.
Magufuli alisha waumbua wajombazenu walamba asali na wapinzani wachumia tumbo, akikuambia hataki ujinga kwenye rasilimali za nchi he was not joking.

Mnajitia mastress ya kijinga bila kujua.
Wengine mnatumwatu,mjitoe akili 24/7 muwe mna pambana na Marehemu.

Saazingine muwe mnawalaumu wazaziwenu kwa kuzembea kuwapeleka shule,maisha hayana short cut, cheti feki unajuwa ninacho maanisha.
 
  • Thanks
Reactions: nao
Back
Top Bottom