Kufanana na watu wengi hii imekaaje?

Kufanana na watu wengi hii imekaaje?

Nilivyokua 1st yr nilifananishwa na mdada wa 3rd year, nilikutana na watu kama wa4 wananiambia unafanana na fulani, ni dada yako?Me nashangaa tu na kucheka, nikawa na hamu ya kumuona.
Hiyo siku huyo mdada akanitafuta tukaonana nilifurahi sana

Kilichonishangaza zaidi kumbe tumetoka mkoa mmoja na huko tulikua chama kimoja cha kitume ila Parokia tofauti, so baada ya mimi kumaliza tulikua tunakutana sana hadi leo hii amekua rafiki yangu mzuri sana na kipenzi 🥰
 
Hata mimi nimeshafananishwa sana tena wengine naambiwa hadi tabia na ucheshi tunafanana

Kuna mmoja huyo aliwah nishangaza anasema nafanana na kaka ake sana mpaka jina lilikuwa linafanana,majina ya baba nayo yalitofautiana herufi chache tu
 
Hello JF

Nimejikuta nalazimika kuleta uzi sasa maana hii imeanza kunishangaza.

Tangu nakuwa ni kawaida kukutana na watu then wananiambia nimefanana na either ndugu yao fulani au jamaa zao. Imefika hatua now nimekuwa wengine mpaka hunipiga picha. Wakawaonyeshe wahusika. Ikafika muda nikawa nahesabu na kunote mahali, mpaka sasa ni zaidi ya watu 15 ambao nishakutana nao kisha wakanifananisha na jamaa zao.

Ingawa binafsi kihalisi nishakutana na watu watatu ukitutazama ni kama mapacha au ndugu wa tumbo moja. Uzuri mwingine nilikuwa nimemtangulia kidato shule moja.

Kiukweli inashangaza sana.
Kuna shoga mmoja wa Tandale Uzuri umefanana naye kinyamaaaa.
 
Kuna siku nilikuwa naperuzi facebook, nikiangalia machapisho mbalimbali. Aisee, nilishtuka baada ya kuona mtu kapost picha najiona mimi kabisa. Nikajiuliza maswali mengi, huyu ni mimi nimepostiwa ? Lakini mbona sijawahi kuwa na mavazi haya ? Itoshe kusema kuna watu hufanana saana
 
Ni kwamba upo plain (not in a bad way) sababu hauna distinctive features ni rahisi mtu kuchora taswira yake kutoka kwako (yaani kama vile karatasi) ndio maana wachina na wajapan tunaona wanafanana sana wapo plain hawana features nyingi ni kama uweke karai uchore tumacho tudogo na ka-mdomo
 
[emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] Hata wao wakituona wanasema tunafanana sana....
anhaa! ndiyo maana nilimwambia To yeye kwamba kujigundua wewe mwenyewe kwamba unafanana na fulani, mmh wachache sana.
...kumbe na sisi kwa wadhungu tunafanana?! aloo
 
Mwaka 2011 kuna jamaa aliendaga Mwanza hotel saa 12 alfajiri akasema kaagizwa na meneja aje achukue sound system kwa ajili ya kuifanyia matengenezo, meneja akaelezewa na mlinzi muonekano wa huyo aliyekuja kuchukua vitu vyao.......moja kwa moja akajua ni mimi, akaniita pale ile kufika mlinzi akakazia kuwa ni mimi, ilibaki kidogo sana Gachuma aniweke ndani kwa ishu hiyo.

Wiki mbili baadae yule jamaa akataka kufanya jaribio la ivo sehemu nyingine akadakwa tukaitana wadau wote kwenda kumuona, nilienda na hasira huku nimepanga kwenda kumfanyia kitu mbaya sana......lakini kufika eneo la tukio mwili ulinisisimka na damu yote mwilini ikajikusanya sehemu moja, yani nilikuwa najiangalia mimi halisi kupitia kwa yule jamaa mwizi, yule mwizi alikuwa ni mimi copy kabisa
 
Mi nilifananishwa na watu watatu afu wa NNE nikaja onana nae mi mwenyewe airport.... Mwanamke mwenzangu ....aisee nilishtuka hata kumsimamisha niliogopa....ila tulipogongana macho tulitazamana kwa muda mrefu afu kila MTU hamwambii kitu mwenzie....Mimi mwili ulisisimka...nilijihisi upendo wa hali ya juu usioelezeka(ni kama mshtuko ulikuwa wa furaha..hata sielewi) ...njia nzima tangu tupishane ni full kugeukiana.Daaa,kumbukumbu isiyosahaulika
Ilibidi muongee huenda ni ndugu yako
 
Back
Top Bottom