Kufanana na watu wengi hii imekaaje?

Kufanana na watu wengi hii imekaaje?

Wakati nipo mdogo mwaka 1995 au 1994 niliwahi kumfananisha mama wa watu na mama yangu.

Tulikuwa tumetoka kanisani na dada zangu wakati huo mama tulimwacha nyumbani alikuwa na safari.
Wakati tunarudi tupo njiani nikamwona huyo mama, nikamkimbilia nikamkumbatia asitembee huku nasema mama mama mama! Ikabidi na yeye anikumbatie tu. Ndio dada zangu wakamwambia amekufananisha huyu, umefanana na mama yetu.
Nilivyogundua nimeingia cha kike nikatoka nduki

Kule nyuma dada zangu wakamwelekeza nyumbani ili akamwone huyo mama wanaofana. Walivyoonana walicheka wenyewe akajisemea kuwa ni halali mwanao atufananishe. Ila mama ni mama tu, hata nilivyomkumbatia ni kama nilihisi mbona kama kuna utofauti hivi!
 
Hello JF

Nimejikuta nalazimika kuleta uzi sasa maana hii imeanza kunishangaza.

Tangu nakuwa ni kawaida kukutana na watu then wananiambia nimefanana na either ndugu yao fulani au jamaa zao. Imefika hatua now nimekuwa wengine mpaka hunipiga picha. Wakawaonyeshe wahusika. Ikafika muda nikawa nahesabu na kunote mahali, mpaka sasa ni zaidi ya watu 15 ambao nishakutana nao kisha wakanifananisha na jamaa zao.

Ingawa binafsi kihalisi nishakutana na watu watatu ukitutazama ni kama mapacha au ndugu wa tumbo moja. Uzuri mwingine nilikuwa nimemtangulia kidato shule moja.

Kiukweli inashangaza sana.
Utakuwa unafanana na mnyama flani na ni kufanana hasa.[emoji23][emoji23][emoji23]

Mtu huwezi kufanana na watu 15 wa eneo unalokaa. Yaani wilaya nzima huwezi kufanana na watu zaidi ya wawili.

Na kawaida kila mtu anafanana na mnyama flani kwa mbali. Wewe itakuwa mnyama wako kakurandisha sana. Inawezekana ni mbuzi. Si ndio wako kibao mitaani?
 
Mi nilifananishwa na watu watatu afu wa NNE nikaja onana nae mi mwenyewe airport.... Mwanamke mwenzangu ....aisee nilishtuka hata kumsimamisha niliogopa....ila tulipogongana macho tulitazamana kwa muda mrefu afu kila MTU hamwambii kitu mwenzie....Mimi mwili ulisisimka...nilijihisi upendo wa hali ya juu usioelezeka(ni kama mshtuko ulikuwa wa furaha..hata sielewi) ...njia nzima tangu tupishane ni full kugeukiana.Daaa,kumbukumbu isiyosahaulika

Hivi ukikutana na mtu uliyefanan naye unaweza kujua kama umefanana naye???
 
Utakuwa unafanana na mnyama flani na ni kufanana hasa.[emoji23][emoji23][emoji23]

Mtu huwezi kufanana na watu 15 wa eneo unalokaa. Yaani wilaya nzima huwezi kufanana na watu zaidi ya wawili.

Na kawaida kila mtu anafanana na mnyama flani kwa mbali. Wewe itakuwa mnyama wako kakurandisha sana. Inawezekana ni mbuzi. Si ndio wako kibao mitaani?
Hii ni kwa maeneo tofauti tofauti.
 
Mara nyingi watu hunifananisha na bro wangu muda mwingine hata mademu zao wakiniona hudhan mimi ndiye bro kumbe sivyo, zaidi ya hapo sijawahi kufananishwa na mtu mwingine yeyote yule.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Acha uoga!Kuna horror movie Zina huo mchezo wa jini kujifananisha sura ya mtu....Mi napenda kweli
[emoji23][emoji1787][emoji23] Sio uoga in such sipendi tu. Nakumbuka nikiwa secondary Kuna jamaa alikuwa ni km anafanana na mke kwa 80% nilikuwa sipendi Ile rafiki zangu wakinifananisha nae sometimes waniita Jina lake badala ya Jina langu. Nashukuru sijatoka na pacha[emoji23]
 
Hello JF

Nimejikuta nalazimika kuleta uzi sasa maana hii imeanza kunishangaza.

Tangu nakuwa ni kawaida kukutana na watu then wananiambia nimefanana na either ndugu yao fulani au jamaa zao. Imefika hatua now nimekuwa wengine mpaka hunipiga picha. Wakawaonyeshe wahusika. Ikafika muda nikawa nahesabu na kunote mahali, mpaka sasa ni zaidi ya watu 15 ambao nishakutana nao kisha wakanifananisha na jamaa zao.

Ingawa binafsi kihalisi nishakutana na watu watatu ukitutazama ni kama mapacha au ndugu wa tumbo moja. Uzuri mwingine nilikuwa nimemtangulia kidato shule moja.

Kiukweli inashangaza sana.
Kweli bro !! Unafanana na panyaroad [emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
 
[emoji23][emoji1787][emoji23] Sio uoga in such sipendi tu. Nakumbuka nikiwa secondary Kuna jamaa alikuwa ni km anafanana na mke kwa 80% nilikuwa sipendi Ile rafiki zangu wakinifananisha nae sometimes waniita Jina lake badala ya Jina langu. Nashukuru sijatoka na pacha[emoji23]
😂😂😂We jamaa mbinafsi sana
 
Hiyo ni kawaida me jana tu nimekutana na mbaba anasema kanifundisha O level
Mara nimeonekana Arusha mwingine ndio rafik yangu yaani tunafanana kama korosho [emoji1787]watu wanatuchanganya hatari wengine wanadai nimesoma nao sahiv nimewambia mkiniona popote nipigeni picha nimechoka mie
 
Mi nilifananishwa na watu watatu afu wa NNE nikaja onana nae mi mwenyewe airport.... Mwanamke mwenzangu ....aisee nilishtuka hata kumsimamisha niliogopa....ila tulipogongana macho tulitazamana kwa muda mrefu afu kila MTU hamwambii kitu mwenzie....Mimi mwili ulisisimka...nilijihisi upendo wa hali ya juu usioelezeka(ni kama mshtuko ulikuwa wa furaha..hata sielewi) ...njia nzima tangu tupishane ni full kugeukiana.Daaa,kumbukumbu isiyosahaulika
Nimewahi kukutana na mtu kama huyu
 
Me nafananishwa sana na watu wengi kisa ubanaji wa nywele hizi wanaita natural hair sijui.... Si na mm ninazo bhn.
Basi full kupata offer, sema naogopa nisije fananishwa na mke wa mtu bure ndy maana saizi nasuka sanaaa.
 
Zamani nilikua nafananishwa na watu wengi mara huyu aseme kaniona Dodoma mwingine Kigoma mara hivi mara vile...

Ila maisha yalivyochanganya na kunichapa sura yangu asili ikapatikana. Sasa hivi nina miaka 12+ sijawahi sikia hiyo kauli.

Nikwambie tu bado una sura ya maziwa ya mama, maisha hayajachanganya... Huoni watoto wachanga wengi wanafanana?
Hii ina ukweli... me pia ni hivyohivyo
 
Ishu ya kufanana aisee...

Mimi ni mwalimu wa primary aka "fom foo feliya"

Kuna mwanafunzi wangu (alishamaliza shule mwaka jana) nilikuta binti mwingine kijiji jirani wanafanana sana ikanibidi nimuulize yule binti kama anamjua huyo mwanafunzi akasema hamjui

Darasani nikamuuliza yule mwanafunzi naye akasema hamtambui huyo binti. Mara wenzake wakamchambulia na kumuelekeza zaidi (kulingana na maelezo niliyotoa) akasema ameshamjua huyo binti ninayemzungumzia lakini hawana uhusiano wowote

Basi nikajiropokea tu kumwambia yule mwanafunzi wangu "yule lazima ni dada yako tu hebu muulize mama yako vizuri" na kauli hiyo nikawa nairudia rudia. Sasa bwana siku hiyo nashangaa yule mwanafunzi akanambia amekuwa akimuuliza mama yake na mama akakataa kumjua huyo binti lakini baadae akamwambia "ni kweli huyo binti na wewe baba yenu ni mmoja" lakini haikuwa open hata siku moja hivyo alishangaa na kumuuliza "huyo mwalimu wako amejuaje?"
 
Nikiwa shule nimeshafananishwa sana na msanii mmoja from chuga.

Kipindi nimeingia shule kuna dada alikua darasa la juu. Sekondari iyo. Sasa mi nikawa nasoma na mdogo wake darasa moja. Hiyo siku yule dada akamwambia mdogo wake huyu mtoto kafanana na mama yetu.

Ndo yule nlokua nasoma nae kuniambia yeye hakuwahi kumfahamu mama yao kwa sababu aliondoka akiwa mdogo sana. Nadhan ni mambo ya kutengana kwa wazazi. Wakawa wanapenda tu kunitazama wakiwa pamoja mtu na dada ake.

Nasikia kipindi cha kifo cha Kanumba na ile kesi ya lulu akawekwa ndani, kuna mdada goba alikua anafanana sana na lulu. Akapanda daladala siku moja, watz tulivyo na mihemko sasa. Yule dada ilikua apigwe aumizwe kisa yy lulu eti. Ndo wachache kumtetea hapana huyu sio lulu...walikua wanaishi nae eneo moja. Wabongo sisi..smh
 
Back
Top Bottom